Ni uongo gani unaoenezwa duniani kuhusu Tanzania?

Ni uongo gani unaoenezwa duniani kuhusu Tanzania?

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
1,968
Reaction score
2,957
Nilimsikia Rais akisema filamu tunayoitengeneza inakwenda kufuta uongo unaoenezwa duniani kuhusu Tanzania.

Niwaombe wadau mnisaidie kujua ni uongo gani hip? Ni nani wanaeneza? Je, filamu pekee inatosha kufuta huo uongo?
 
Kuufuta uongo ni kutumia mbinu ya Russia, na Uingereza kwa kuwezesha mashirika yao ya habari kujitanua ulimwenguni. Wengi mnazijua RT na BBC ni vyombo vilivyochini ya serikali ya nchi hizo tajwa. Vyombo hivi vimesaidiwa kupata vibali vya kurusha matangazo kwenye maeneo ambayo nchi hizo zinadhani zinachafuliwa ama masalahi yake yaweza kuhatarishwa. Vyombo hivi vimefanya kazi kubwa sana kutimiza azma ya serikali hizo.

Ni kwa mtaji huu, binafsi nafikiri Serikali ya Tanzania iliwezeshe shirika la utangazaji la taifa TBC kupata leseni za matangazo huko huko kwenye mataifa tunapodhani tunahujumiwa kwa uongo. Shirika liwezeshwe kuboresha viwango vya watangazaji wake na hata kwa kupata watangazaji bora kutoka kwenye mashirika mengine makubwa ili kukidhi vigezo vya kuimarisha mbinu za kufuta uongo.

Hii itasaidia sana kumuwezesha rais wetu mpendwa Mama Samia KUENDELEA kufanya Kazi nyingine za kuboresha uchumi wa Taifa hili kwa ujumla.
 
kwamba tanzania hakuna uhuru wa habari na demokrasia.

huu unduza hata wanaoambiwa wameukataa.
 
Nilimsikia Rais akisema filamu tunayoitengeneza inakwenda kufuta uongo unaoenezwa duniani kuhusu Tanzania.

Niwaombe wadau mnisaidie kujua ni uongo gani hip? Ni nani wanaeneza? Je, filamu pekee inatosha kufuta huo uongo?
Dunia ni kijiji hakuna anayeweza kusingizia uwongo mwanakijiji jirani maana yeye ndo ataonekana kuwa mwongo Kwa sababu wanakijiji wote wanajua ukweli. Mwakajana tu Mkuu wa Mbuga za Utalii nchini alikiri kuwa Watalii wanaotembelea Mbuga zetu huwa hawarudi tena kama wanavyofanya nchi nyingine za kitalii. Miaka miwili/mitatu iliyopita ndege 5 zilileta Watalii wengi sana toka Australia na nyingine nyingi toka Urusi na Jamhuri ya Czech lakini hawakurudi tena. Barani Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara ni Kisiwa cha Mauritius ambacho ni kidogo kuliko Wilaya zetu nyingi ndo kinapokea Watalii wengi ingawa hawana big five hata mmoja. Kenya nchi ndogo na vivutio vichache inatembelewa na Watalii wengi kuliko Tanzania lakini viongozi wetu hawajiulizi kulikoni wao ni kujisifu kila kivutio kinapatikana kwetu tu. Kivutio kikubwa kuliko vyote vya Watalii nchi yoyote duniani ni watu wake!
 
Nilimsikia Rais akisema filamu tunayoitengeneza inakwenda kufuta uongo unaoenezwa duniani kuhusu Tanzania.

Niwaombe wadau mnisaidie kujua ni uongo gani hip? Ni nani wanaeneza? Je, filamu pekee inatosha kufuta huo uongo?
That they are Uneducated, Lazy, Drunkers, Useless, Short Sighted and best Gossipers Worldwide.
 
Kuufuta uongo ni kutumia mbinu ya Russia, na Uingereza kwa kuwezesha mashirika yao ya habari kujitanua ulimwenguni. Wengi mnazijua RT na BBC ni vyombo vilivyochini ya serikali ya nchi hizo tajwa. Vyombo hivi vimesaidiwa kupata vibali vya kurusha matangazo kwenye maeneo ambayo nchi hizo zinadhani zinachafuliwa ama masalahi yake yaweza kuhatarishwa. Vyombo hivi vimefanya kazi kubwa sana kutimiza azma ya serikali hizo.

Ni kwa mtaji huu, binafsi nafikiri Serikali ya Tanzania iliwezeshe shirika la utangazaji la taifa TBC kupata leseni za matangazo huko huko kwenye mataifa tunapodhani tunahujumiwa kwa uongo. Shirika liwezeshwe kuboresha viwango vya watangazaji wake na hata kwa kupata watangazaji bora kutoka kwenye mashirika mengine makubwa ili kukidhi vigezo vya kuimarisha mbinu za kufuta uongo.

Hii itasaidia sana kumuwezesha rais wetu mpendwa Mama Samia KUENDELEA kufanya Kazi nyingine za kuboresha uchumi wa Taifa hili kwa ujumla.
Unaota mchana dogo
 
Nilimsikia Rais akisema filamu tunayoitengeneza inakwenda kufuta uongo unaoenezwa duniani kuhusu Tanzania.

Niwaombe wadau mnisaidie kujua ni uongo gani hip? Ni nani wanaeneza? Je, filamu pekee inatosha kufuta huo uongo?
Mama yenu amishapotezwa mwelekeo na mahafidhina ya ccm, Kwisha kabisa, siku hizi anaongea vitu horojo sana
 
kwamba tanzania hakuna uhuru wa habari na demokrasia.

huu unduza hata wanaoambiwa wameukataa.

Kwamba; Upelelezi sakata la Ndugai kumpiga mgombea wakamilika

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime alisema jana kuwa kinachosubiriwa ni ripoti ya daktari aliyemhudumia mgombea huyo ili kuendelea na hatua nyingine za kisheria. Mwananchi; Habari Zaidi; Kitaifa FRIDAY JULY 31 2015

 
Back
Top Bottom