Jamani kumbe tulikuwa tunadanganyana sana kuwa samaki aina ya nguva ana umbo kama msichana mrembo sehemu ya kukatia kiunoni kwenda juu na kwenda chini samaki.
Huu ni uongo mtupu wa hadithi, ukweli ni kwamba nguva ni samaki mkubwa mwenye umbo la samaki ila sehemu ya kichwani hasa mdomoni anafanana kila kitu na ng'ombe na kitaalam anaitwa NG'OMBE BAHARI.
Huu ndio ukweli wa nguva, ukitaka ushahidi kamili nenda pale posta makumbusho ya taifa utamuona huyu samaki nguva na utakubaliana nami.
hizi story za nguva uongo uongo mwingi kweliHahaaa Nguva anaongea English, nao wanatechnol ya kutengeneza sidilia?
nguva mbona wapo wakuu, mimi mvuvi kila siku nakutana nao baharini
Wapo wengi tu jamani, kuna mmoja huyo huwa anajiuza kabisa kwa wanaume
Kweli? Au unatutania ?
ni uzushi...google..mermaid uoneWanabodi,
Kwa Mwenye elimu juu ya viumbe hawa karibu utupe somo
Viumbe hawa wana uhusiano gani maana huyu nguva kwa mjibu wa taarifa anasura nzuri ya msichana tena mpole chini anatisha sana na mazingira yake ni sawa na majini
Nawasilisha.