Ni wakati muafaka sasa Mifugo itozwe kodi. Msukuma au Mmasai anamiliki zaidi ya ng’ombe 1,000 na hachangii chochote! It is not fair

Kuna mdau kajibu vizuri. Shida sio kodi je serikali iko tayari kuwekeza. Maana hata sasa kinachowatia watu uvivu kulipa kodi ni hawaoni kodi wanayolipa inawasaidiaje kurahisisha shughuli yao.
Nakubaliana na wewe, lakini ni busara kuchagua kipi kianze. Ikisanywe kodi ili uwekeze au kinyume chake? Kwa vile tiyari mifugo ipo, lakini hela ya kuwekeza ndiyo shida, basi tukusanye kodi then tuwekeze zaidi.
 
Happy umenena vyema kunauonezi mkubwa Sana kwa wafanyabiashara
 
Hivi nani kakudanganya wafugaji hawalipi kodi ?

Kwa taarifa yako wafugaji tunazipa halamashauri mapato makubwa kuliko hata hako kaduka kako kachupi za mitumba.
 
Hivi nani kakudanganya wafugaji hawalipi kodi ?

Kwa taarifa yako wafugaji tunazipa halamashauri mapato makubwa kuliko hata hako kaduka kako kachupi za mitumba.
Tofautisha rushwa na kodi.
 
Nakubaliana na wewe, lakini ni busara kuchagua kipi kianze. Ikisanywe kodi ili uwekeze au kinyume chake? Kwa vile tiyari mifugo ipo, lakini hela ya kuwekeza ndiyo shida, basi tukusanye kodi then tuwekeze zaidi.

Unatoza Kodi mfugaji ambaye asaidiwi chochote na serikali hii haiko sawa...

Serikali itatue migogoro ya wakulima na wafugaji... Kwa kuwapa maeneo rasmi yenye malisho ya mifugo...

Serikali itoe huduma za majosho, ruzuku ya chanjo na elimu ya ufugaji wa kisasa...

Waboreshe na sera zinazohusu mifugo... Kupata mkopo na bima kupitia mifugo...

Serikali haiwezi kufanya hivyo kwa Sasa maana wafugaji wengi wanafuga kienyeji...

Serikali ilikuwa na mpango wa kila mwaka mifugo kuwekewa alama na kuchukua takwimu... Jiulize kwa Nini ilo zoezi halikuwa endelevu? Sababu kubwa Ni serikali kutothamini mifugo na sekta ya uvuvi...
 
Utaratibu huwa ni kukusanya kodi ili fedha itakayopatikana, itumike kuleta unavyohitaji! Tunakusanya kodi ili kujenga miundombinu shule nk. Huwezi kuiambia serikali ijenge kwanza miundombinu ndo ikusanye kodi! Vivyo hivyo, huwezi kuiambia serikali ijenge majosho ya mifugo ndo mifugo walipishwe kodi! Hiyo fedha itoke kwa nani?
 
Kuna sehemu nimetaja rushwa ?
Unaposema H/shauri zinatoza kodi ya mifugo,hiyo kodi ni ipi na inatozwa kwa kila mifugo kwa idadi na muda sawa?
 
Kweli kabisa,jibu sahihi kabisa
Ilipopanda bei ya sukari,kulitokana na ongezeko gani la kodi? Mkuu, hutegemea madhara ya kodi kwenye ongezeko au punguzo la faida pia sera za nchi.
Tukuogopa kutoza kodi kwa kuhofia kupanda bei bidhaa siyo sawa maana yake tutarudi nyuma kimaendeleo.
 
Ikitozwa kodi bei ya nyama itapanda hutaweza kununua! Kila kitu kina impact! Vyanzo vya kodi ni vingi lakini lazima uangaloe na uwezo wa vyanzo vyenyewe! Na mbona hujataja rasilimali kibao zilizopo unakimbilia Mifugo
 
Naunga mkono hoja
 
bonge la wazo nadhani ni muda sasa serikali kutambua kwamba siyo pekee wenye akili watafakari kuwa na member anayefahamika kuchukua maoni ya hii platform then kuifanyia kazi manake Kama idea hii mtu anakuwa na ng'ombe 2000 anaharibu mazingira,mto na Bado serikali hainufaiki na chochote na wakati ile ni asset
 
Unafikiri wakitozwa kodi utamudu kununua nyama buchani?. Watu wa mazao ya kilimo na mifugo ni wa kupewa ruzuku si kuwaundia kodi
Mbona wenye maduka wanatozwa kodi na tunanunua sukari mchele mafuta unga kila siku na tunaimudu na chakula bei poa kwa mama ntilie
 
Kuku nao watozwe kodi
 
Mwenye ngombe mfano
Ushuru wa kila ngombe kwa mfugaji+ushuru wa ngombe pale unapouza huyo ngombe+ushuru ngombe kusafirisha mfano mikoani+ushuru wa machinjio+ushuru wa bucha hapo= alafu nyama shingapi hapo

Bei lazima iwe juu...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…