Ni wakati sasa wa kuhalalisha matumizi ya bangi

Ni wakati sasa wa kuhalalisha matumizi ya bangi

Bangi inafaida kuliko inavyozungumzwa na wala haina madhara kama inavyozungumzwa. Ndani ya bangi kuna kemikali moja nzuri sana ambayo inasaidia kuongeza hamu ya kula. Baada ya wataalamu kuona faida hiyo, wakaiga kemikali hiyo na kutengeneza dawa ya kusaidia kuongeza hamu ya kula. Dawa hiyo hupewa sana wagonjwa wakansa ambao hutumia madawa makali. Madawa makali ya kansa husababisha ukosefu wa hamu ya kula.

Bangi ni dawa nzuri sana ya hangover. Kuvuta au kupata supu ya bangi ni tiba bora sana ya hangover. Licha ya hivyo wakati huohuo ni mboga pia. Pia mbegu zake zina mafuta na mashina yake yanaweza kutoa nkamba na nyuzi. Faida ninyingi sana. Hizo hapo ni chahce tu.
View attachment 3018390


Pia bangi haina madhara kama inavyosemwa. Ujerumani imehalalisha matumizi ya bangi. Juzi wakati wa kuanza kwa mashindano ya Euro imewashauri mashabiki kutumia bangi badala ya pombe ili kupunguza vurugu viwanjani.

Nchi nyingi zimeishaona umuhimu wa bangi.
View attachment 3018391

Nchi za Bluu zimehalalisha. Nchi za njano hazijahalalisha lakini si kosa kuvuta bangi. Nchi za pinki ni kosa kuvuta bangi lakini mara nyingi haushtakiwi. Nchi nyekundu zimepiga marufuku
Tanzania bangi imepigwa ban lakini inatumiwa na karibu na kila mwananchi toka viongozi wa dini na watu serikalini
 
Bongo ushamba umekua mwingi. Labda siku kije kizazi kinachojielewa ndio kitaruhusu
 
Mkuu hujatoa fununu kuhusu kiasi na umri wa watu ambao wanaweza kutumia katika jamii. Nasema hivyo kwa kuwa matumizi ya vilevi kuna tahadhari inatolewa kuhusu wale wenye umri zaidi ya miaka 18, kutokunywa kwa kupitiliza na pia unywaji uwe wenye kumtaka mnywaji kuwajibika mwenyewe endapo matokeo ya unywaji wake yatakapo leta taflani fulani.

Aidha katika matumizi ya mazao ya tumbaku, tunaona tahadhari ikitolewa kwa kuzingatia umri pia kuhusu adhari za kiafya kwa mtumiaji. Sasa hii kitu hii 👉BANGE 👈 tahadhari gani itatolewa kuhusu matumizi yake kwa kuzingatia umri unaokulabilika, sehemu rasmi za uvutaji wake (kwa wale wavutaji), athari zake za kiafya (natambua zipo kwa kuwa bange inaorodheshwa kama mojawapo ya madawa ya kulevya hapa nchini),, harufu (kwa maana kitu huwa kinatema! 😩), ikiwa katika hali yake uasilia, yaani, "crude form" ama "processed" n.k.

Mtoa mada jaribu kudadavua zaidi ili tupime kwa nini nchi chache sana zimehalalisha matumizi yake, wakati nchi nyingi zikiwa zimepiga marufuku matumizi yake. Ukizichunguza kwa umakini baadhi ya haki za binadamu zinakwenda kinyume kabisa na maadili ya Mwafrika, na imani zake za kiroho. Agenda nyingi zenye nia mbaya zinapenyezwa "overtly or covertly" zikiwa na nia mbaya ya kumfanya Mwafrika awe "derailed and brainwashed par excellence"!


Tumbaku sio asili ya mwafrika lakini imehalalishwa na ililetwa na Wakaloni wakawafundisha wazee wetu kuvuta kiko na wengine kutumia Ugoro. Tumbaku inatengeneza Siagari ambayo pia sio asili yetu.

Pombe zote za viwandani zililetwa na Wazungu sio asili yetu.
Pombe za kienyeji zinapigwa vita sana na serikali kwa sababu serikali ni matokeo ya Ukoloni.
.Bangi ni zao la asili linaloota kwenye misiti na Mbuga zetu kama ilivyo pia Mirungi. Haya mazao yanaota yenyewe na kiasili ni dawa na sehemu nyingine ni mboga

nyungu inavyofanyika.

Mimea au mazao yaliyoletwa na Wakaloni kama vile tumbaku hayawezi kuota kwenye mapori yetu bila kulimwa na kuhudumiwa kitaalam . Bangi ni mbaya kwa sababu imepewa jina baya kutokana na ushindani wa kibiashara.

Madhara yanayotakana na ulevi wa pombe na uvutaji wa sigara wenye jamii ni makubwa kuliko yale yanayotokana na bangi.

Zao la Bangi linatumika kutengeneza bidhaa nyingi kuliko tumbaku inayotengeneza sigara na ugoro pekee.

Iko hivi ;biashara zote duniani zenye soko kubwa la kuvuka mipaka ya nchi ambazo zinapatikana kirahisi zinadhibitiwa na watawala wa Dunia na familia zao na marafiki zao ndio wanaoweza kuzifanya.

Biashara za Pembe za ndovu.
Biashara za dhahabu.
Biashara za wanyama hai.
Biashara ya bangi kwenye makontena kwenda nje ya nchi.
Biashara ya Mafuta .
Biashara za mirungi
Biashara za madawa kama unga wa kokeini.
Biashara ya kutakatisha fedha.
Mikataba hewa n.k.

Hizi ni biashara za watawala wa dunia . Hakuna mtu anayeweza kuzifanya akatoboa kama hana koneksheni na watawala wa dunia hii.
Ndio maana zikawekewa sheria kali ili watu maskini wasije wakapata fedha kirahisi rahisi .

Tujiulize kwa nini mara nyingi watoto wa wakubwa au marafiki zao kote duniani ndio wanaozifanya!?

Kuna wakati Dr.Slaa alimtuhumu Mtoto wa Zakaya ,Lithione kuwa alikamatwa China.
Alipojitambulisha kuwa ni mtoto wa mkubwa ,kilichofanyika ni wakubwa kutaka kuhakiki tu kuwa ni kweli ni mtoto wa mkubwa mwenzao ili aendelee na biashara yake .

Kwa Mujibu wa Dr. Slaa Inasemekana walipopata uhakika kuwa ni mtoto wa mkubwa walimuachia huru bila kunyongwa kwa mujibu wa sheria ya China.
Kwa nini walimwachia mpaka sasa hatujawekwa wazi lakini,ukweli ni kwamba hizo ndizo biashara zinazofanywa na watawala wengi wa Dunia na familia zao hasa wa nchi za Magharibi na Asia na sasa Afrika ndio maana familia zao zinaibuka kwa utajiri mkubwa sana na kwa Muda mfupi.

Hii inasaidia wao kupata pesa nyingi sana mbali na pesa za umma za madafu .

Akitokea mtawala kama JPM atapingwa sana kila kona ya dunia lakini sababu kubwa ni kuzuia biashara hizo nilizozotaja ambazo ni dili kubwa kwa watawala wa dunia lakini kwa wananchi wa kawaida ni marufuku kuzifanya au hata kufikiria kuzifanya.

Mfano tu kukutwa na Gunua la bangi ni kosa kuwa kuliko kuhamishia malipo ya serikali kwenye Akaunti ya mtu na kujaza pesa nyumbani kwenye gunia mana anaweza akazirudisha na mambo yakaisha, na baadae akateuliwa tena kwenda kwenye ofisi nyingine ya kusimamia mapato.
 
Mbona akili za watoto wa A City zinatupa shaka kdg kama wako race, sio madhara ya majani yale makavu?!😂, naskia Tarime pia zinawaka sana.😃
 
Halafu kama hujawahi vuta ndumu usichangie Uzi maaña wengi hawajui hata wanaongea nn.Bangi sio drugs it's the gateway to drugs,na Sio kwamba inakufanya uwe na tabia mbaya ila inakufanya ww uwe ww.So kama tabia yako ya kimbuzi ukila ndumu itazidi kuwa ya kimbuzi ila kama ni mstaarabu basi mtu atakuwa mstaarabu kupita zaidi.
 
Halafu kama hujawahi vuta ndumu usichangie Uzi maaña wengi hawajui hata wanaongea nn.Bangi sio drugs it's the gateway to drugs,na Sio kwamba inakufanya uwe na tabia mbaya ila inakufanya ww uwe ww.So kama tabia yako ya kimbuzi ukila ndumu itazidi kuwa ya kimbuzi ila kama ni mstaarabu basi mtu atakuwa mstaarabu kupita zaidi.
Kwa huu uzi mjomba umefunguliwa kwa ajili ya watumiaji tu kuchangia?!
 
Uwe unanunua unampelekea Baba ako na Mama ako wawe vizuri kama wajerumani.
 
Mtoa mada watu wa R chuga ukienda kugombea ubunge kule unapita bila kupingwa
Sasa ni hiviiii kitaalamu active ingredient ya bangi inaitwa tetra hydrocanabinol

Bangi iko kwenye group la dawa linaitwa trangulizer ambazo hata mahosipitali zinatumika hasa kwa wagonjwa wa mivunjiko ya mifupa.Kuna dawa inaitwa PETHIDINE hii dawa hata manesi wanapokabidhiana shift wanakabidhiana hii dawa kwa maandishi.
Hii soda mnayokunywa inatengenezwa kwa mimea inayoitwa Coca ambayo ni jamii ya bangi lakini iliyo poa ndiio maana wasabato wameshtukia coca cola inasisimua mwili.

Kitabibu bangi ni dawa wanayopewa wagonjwa wa akili lakini ni ile iliyohuishwa na kufanyiwa marekebisho.

Medicinal uses for oil obtained from hemp seeds first appeared in Arabic literature by al-Razi (857 AD), who proposed its use for the ear, dissolving flatulence, and to cure epilepsy. Hashish is the Arabic name for the cannabis extract used in the Middle East.

it may provide greater symptom relief for people who use marijuana to treat medical conditions, such as chronic pain or cancer.

Duuhh mtoa mada katika ramani yako ningeshangaa sana kutokuona nchi ya kiduku wa Korea ya kaskazini hawaruhusu bangi.

Mazao maarufu duniani kwa mpangilio ni yafuatayo
1.Bangi
2.Tumbaku
3.Aloe Vera
4.Muarubaini
5.????????????
6.?????????????
7.?????????????
8.?????????????
9.Nafaka zikiwepo Mahindi,Mchele n.k

Ajabu sasa namba tisa ni muhimu kuliko vyote lakini sio maarufu
Kuna kitu kwenye somo la development studies Karl Max alisema kuna value na use value
Mfano almasi value yake ni kubwa sana lakini use value yake ni ndogo
Tanzanite value yake ni kubwa sana lakini use value yake ni ndogo sana
Madini ya chuma value yake ni ndogo mno lakini use value yake ni kubwa mno
Mkate value yake ni ndogo sana lakini use value yake ni kubwa
hapo nimeweka mkate kama mfano wa namba tisa
Haya tena kiberiti ni kitu muhimu ajabu sana hivyo use value yake ni ndogo mno kinauzwa shillingi 100 tu lakini use value yake asikwambie mtu ni kubwa mno kikosekane watu hawali.
 
Faida zinazowezekana za bangi hutegemea matumizi ya aina fulani ya bangi kama tiba ya magonjwa au hali fulani za kiafya. Baadhi ya faida zinazojulikana za bangi katika matibabu ni pamoja na:

1. Kupunguza maumivu: Bangi hutumiwa kupunguza maumivu sugu, kama vile maumivu yanayosababishwa na saratani, arthritis, au ugonjwa wa neva.

2. Kudhibiti kichefuchefu na kutapika: Hasa kwa wagonjwa wa saratani wanaopokea tiba ya mionzi au chemotherapy, bangi inaweza kusaidia kudhibiti kichefuchefu na kutapika.

3. Kuongeza hamu ya chakula: Bangi inaweza kusaidia watu wenye matatizo ya kula, kama vile wale wanaougua UKIMWI au saratani, kuongeza hamu yao ya kula.

4. Kutuliza misuli inayokakamaa: Bangi hutumiwa katika baadhi ya matibabu ya ugonjwa wa sclerosis nyingi (MS) ili kupunguza kukakamaa kwa misuli.

5. Matibabu ya wasiwasi na unyogovu: Watu wengine hutumia bangi ili kupunguza hisia za wasiwasi au unyogovu, ingawa hii inapaswa kufanywa kwa tahadhari.

6. Matibabu ya kifafa: Baadhi ya utafiti unaonyesha kuwa bangi au CBD (ambayo ni kiungo ndani ya bangi) inaweza kusaidia katika kudhibiti kifafa kisichodhibitiwa kwa njia za kawaida.

Ni muhimu kutambua kwamba faida hizi zinapatikana zaidi kwa matumizi ya tiba na chini ya uangalizi wa kitaalam. Matumizi ya bangi kiholela au bila uangalizi yanaweza kuleta madhara mbalimbali kiafya na kisheria.
 
Back
Top Bottom