Ni wakati turuhusu New Breed CHADEMA

Ni wakati turuhusu New Breed CHADEMA

econonist

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
20,189
Reaction score
29,663
Kutokana na sintofahamu kwenye chama Cha CHADEMA inayoendelea sasa hivi ndani ya chama hasa Viongozi kuhongwa na suala la akina Halima Mdee kurudishwa kwenye chama huko mbeleni, nina ushauri maalumu.

Ushauri wangu ni kwamba CHADEMA ijikite kwenye damu changa na siyo kuendelea kuhangaika na majina ya Viongozi waliohudumu CHADEMA Kwa muda mrefu. Hii Hali ya kuwa na Viongozi wa muda mrefu kwenye chama ndio inasababisha mgawanyiko. Maana Kuna Viongozi wengine wanajiona wao ndio Bora kwenye chama bila wao chama hakiendi, hivyo kuleta vitisho vya kuhama.

Mimi nadhani tukiwekeza kwa vijana na kuachana na haya majina makubwa hicho kiburi kitapungua. Kwa mfano kiongozi ndani ya CHADEMA anagombea cheo Fulani , asipokipata anahama chama. Hili tumeliona kwa Katibu Mkuu wa zamani Dr Mashinji aliyeondoka CHADEMA na kuhamia CCM baada ya kutoteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA. kwa Msigwa pia baada ya kuanguka uenyekiti wa Kanda ya Nyasa na hata kwa Selasini baada ya kushindwa uchaguzi wa Kanda ya Kaskazini akahamia NCCR. Hii ni hatari Sana. Hivi karibuni Wenje katangaza kugombea umakamu wenyekiti, je akianguka atabaki kwenye chama? au atahama Kama Msigwa. Je John Mnyika asipoteuliwa Tena kwenye Ukatibu Mkuu atabaki kwenye chama? Ila tungekubali kuwapa nafasi vijana ndani ya chama haya mambo ya Kiongozi kugombea nafasi kisa anataka kuhama yasingekuwepo maana anajua akiondoka wapo wengi wa kujaza nafasi yake.

Pia Kuna ujinga Fulani ndani ya CHADEMA ya kwamba kiongozi Fulani akipata ubunge anaanza kuota mapembe na kukidharau chama. Tumeona hili kwa Nassari ambaye alidiriki hata kukacha vikao vya bunge ili afukuzwe ahamie CCM, tumeona kwenye bunge la 2015 kwa akina Silinde, Lwakatare, Kubenea, nk wengi waliohama chama na kukidharau baada ya kupata ubunge, maana walijiona wao Wana majina makubwa hivyo chama kinawahitaji kuliko wao kukihitaji chama. Ila tungewekeza kwa vijana haya maujinga yasingekuwepo.

Mwisho CHADEMA imeshakuwa brand, Sasa tuiuze hiyo brand watu wailewe ili tupate vijana wengi wanachama. Tuje na strategies ya kupata vijana wengi.
 
Imetiririka vzr. Lkn hujazitoa strategy.
Ili kina Lema wanaohisi ni wakubwa kuliko chama waondolewe.

Nilikuwa ndani ya chadema na nililiona hilo, nimeamua kuwa pembeni lkn kwa sasa namsapoti Lissu.

Ni yeye ndie mwenye strategy ya kureform chadema.

Kwa matamko aliyotoa siku mbili hizi zilizopita
 
Kutokana na sintofahamu kwenye chama Cha CHADEMA inayoendelea sasa hivi ndani ya chama hasa Viongozi kuhongwa na suala la akina Halima Mdee kurudishwa kwenye chama huko mbeleni, nina ushauri maalumu.

Ushauri wangu ni kwamba CHADEMA ijikite kwenye damu changa na siyo kuendelea kuhangaika na majina ya Viongozi waliohudumu CHADEMA Kwa muda mrefu. Hii Hali ya kuwa na Viongozi wa muda mrefu kwenye chama ndio inasababisha mgawanyiko. Maana Kuna Viongozi wengine wanajiona wao ndio Bora kwenye chama bila wao chama hakiendi, hivyo kuleta vitisho vya kuhama.

Mimi nadhani tukiwekeza kwa vijana na kuachana na haya majina makubwa hicho kiburi kitapungua. Kwa mfano kiongozi ndani ya CHADEMA anagombea cheo Fulani , asipokipata anahama chama. Hili tumeliona kwa Katibu Mkuu wa zamani Dr Mashinji aliyeondoka CHADEMA na kuhamia CCM baada ya kutoteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA. kwa Msigwa pia baada ya kuanguka uenyekiti wa Kanda ya Nyasa na hata kwa Selasini baada ya kushindwa uchaguzi wa Kanda ya Kaskazini akahamia NCCR. Hii ni hatari Sana. Hivi karibuni Wenje katangaza kugombea umakamu wenyekiti, je akianguka atabaki kwenye chama? au atahama Kama Msigwa. Je John Mnyika asipoteuliwa Tena kwenye Ukatibu Mkuu atabaki kwenye chama? Ila tungekubali kuwapa nafasi vijana ndani ya chama haya mambo ya Kiongozi kugombea nafasi kisa anataka kuhama yasingekuwepo maana anajua akiondoka wapo wengi wa kujaza nafasi yake.

Pia Kuna ujinga Fulani ndani ya CHADEMA ya kwamba kiongozi Fulani akipata ubunge anaanza kuota mapembe na kukidharau chama. Tumeona hili kwa Nassari ambaye alidiriki hata kukacha vikao vya bunge ili afukuzwe ahamie CCM, tumeona kwenye bunge la 2015 kwa akina Silinde, Lwakatare, Kubenea, nk wengi waliohama chama na kukidharau baada ya kupata ubunge, maana walijiona wao Wana majina makubwa hivyo chama kinawahitaji kuliko wao kukihitaji chama. Ila tungewekeza kwa vijana haya maujinga yasingekuwepo.

Mwisho CHADEMA imeshakuwa brand, Sasa tuiuze hiyo brand watu wailewe ili tupate vijana wengi wanachama. Tuje na strategies ya kupata vijana wengi.
Mkuu. Kwenye siasa za Afrika, na hususani Tanzania, kuhama vyama ni suala endelevu. Hii ni kwa sababu watu wengi wako kwenye siasa kwa kutanguliza maslahi yao kwanza. Hili ni kwa vyama vyote. Kwa hiyo hata ukiwekeza kwa vijana, nao watahongwa. Cha kupigania ni kuwa na katiba nzuri ili viongozi wapatikane kwa matakwa ya wananchi na siyo rais wa nchi. Yes, katiba yetu inampa rais nguvu ya kuamua viongozi wa upinzani wawe kina nani na akishindwa, anapenyeza fedha na nguvu za dola kuwaharibu. Mwarabu kamwaga fedha nyingi sana sana ili kulinda maslahi yake. Usidhani anaingia mikataba kijinga bila kujua ana uwezo wa ku-influence ni nani awe rais wa Tanzania. Bahati mbaya sana katiba yetu haitoi haki ya viongozi kuungana na kuunda chama cha dharura cha kushiriki kwenye uchaguzi kama Kenya.
 
Hakuna mwenye dhamira ya dhati kwenye hivi vyama, new breed huwa inatokana na succession plans, na kama sio succession plan basi mapinduzi yafanyike.

Hivi vyama vyote ni mali ya watu fulani na wao ndio wenye maamuzi ya Kila kitu.
 
Kutokana na sintofahamu kwenye chama Cha CHADEMA inayoendelea sasa hivi ndani ya chama hasa Viongozi kuhongwa na suala la akina Halima Mdee kurudishwa kwenye chama huko mbeleni, nina ushauri maalumu.

Ushauri wangu ni kwamba CHADEMA ijikite kwenye damu changa na siyo kuendelea kuhangaika na majina ya Viongozi waliohudumu CHADEMA Kwa muda mrefu. Hii Hali ya kuwa na Viongozi wa muda mrefu kwenye chama ndio inasababisha mgawanyiko. Maana Kuna Viongozi wengine wanajiona wao ndio Bora kwenye chama bila wao chama hakiendi, hivyo kuleta vitisho vya kuhama.

Mimi nadhani tukiwekeza kwa vijana na kuachana na haya majina makubwa hicho kiburi kitapungua. Kwa mfano kiongozi ndani ya CHADEMA anagombea cheo Fulani , asipokipata anahama chama. Hili tumeliona kwa Katibu Mkuu wa zamani Dr Mashinji aliyeondoka CHADEMA na kuhamia CCM baada ya kutoteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA. kwa Msigwa pia baada ya kuanguka uenyekiti wa Kanda ya Nyasa na hata kwa Selasini baada ya kushindwa uchaguzi wa Kanda ya Kaskazini akahamia NCCR. Hii ni hatari Sana. Hivi karibuni Wenje katangaza kugombea umakamu wenyekiti, je akianguka atabaki kwenye chama? au atahama Kama Msigwa. Je John Mnyika asipoteuliwa Tena kwenye Ukatibu Mkuu atabaki kwenye chama? Ila tungekubali kuwapa nafasi vijana ndani ya chama haya mambo ya Kiongozi kugombea nafasi kisa anataka kuhama yasingekuwepo maana anajua akiondoka wapo wengi wa kujaza nafasi yake.

Pia Kuna ujinga Fulani ndani ya CHADEMA ya kwamba kiongozi Fulani akipata ubunge anaanza kuota mapembe na kukidharau chama. Tumeona hili kwa Nassari ambaye alidiriki hata kukacha vikao vya bunge ili afukuzwe ahamie CCM, tumeona kwenye bunge la 2015 kwa akina Silinde, Lwakatare, Kubenea, nk wengi waliohama chama na kukidharau baada ya kupata ubunge, maana walijiona wao Wana majina makubwa hivyo chama kinawahitaji kuliko wao kukihitaji chama. Ila tungewekeza kwa vijana haya maujinga yasingekuwepo.

Mwisho CHADEMA imeshakuwa brand, Sasa tuiuze hiyo brand watu wailewe ili tupate vijana wengi wanachama. Tuje na strategies ya kupata vijana wengi.
niliona na nikashauri kibobevu jambo hili mapema, nafurahi kamanda umeliona na kulieleza kwa kina kwa namna nyingine....

mie bado nashauri na kusisitiza, lisu na mbowe waondoke kwa pamoja chamani kwasabb akibaki moja wapo vita baridi ya maneno itaendelea kua pale pale na kuzidisha migawanyiko chamani....

sasa kuondokana na kasumba hiyo hakuna budi kukaribisha mawazo, mtazamo na fikra mapya, mipango mipya, uelekeo na pumzi mpya chadema...

wangwana hao wapewe thank you, lakini pia hawana budi kuachia ngazi au kutoswa wakidinda...
migawanyiko na mipasuko wanayosababisha dah, imetosha ndrugu zango 🐒

Lissu na Mbowe waking'atuka, CHADEMA itaimarika sana na kuwa chama cha upinzani chenye ushawishi na nguvu sana Tanzania
 
Imetiririka vzr. Lkn hujazitoa strategy.
Ili kina Lema wanaohisi ni wakubwa kuliko chama waondolewe.

Nilikuwa ndani ya chadema na nililiona hilo, nimeamua kuwa pembeni lkn kwa sasa namsapoti Lissu.

Ni yeye ndie mwenye strategy ya kureform chadema.

Kwa matamko aliyotoa siku mbili hizi zilizopita
Ni kweli kabisa. Tunahitaji reforms ndani ya CHADEMA. Na Lissu ndiye kiongozi anayeweza kufanikisha Hilo.
 
Kwasasa Lissu ndo mpinzani pekee anayeaminika kwa wananchi, Chadema wakitaka kuendelea kushika mioyo ya watanganyika wamshikirie Lissu kinyume na hivyo litakuwa anguko kuu.
Ni kweli, nje ya Lissu labda Heche. Tunamuhitaji Lissu pale juu kama mwenyekiti.
 
Mkuu. Kwenye siasa za Afrika, na hususani Tanzania, kuhama vyama ni suala endelevu. Hii ni kwa sababu watu wengi wako kwenye siasa kwa kutanguliza maslahi yao kwanza. Hili ni kwa vyama vyote. Kwa hiyo hata ukiwekeza kwa vijana, nao watahongwa. Cha kupigania ni kuwa na katiba nzuri ili viongozi wapatikane kwa matakwa ya wananchi na siyo rais wa nchi. Yes, katiba yetu inampa rais nguvu ya kuamua viongozi wa upinzani wawe kina nani na akishindwa, anapenyeza fedha na nguvu za dola kuwaharibu. Mwarabu kamwaga fedha nyingi sana sana ili kulinda maslahi yake. Usidhani anaingia mikataba kijinga bila kujua ana uwezo wa ku-influence ni nani awe rais wa Tanzania. Bahati mbaya sana katiba yetu haitoi haki ya viongozi kuungana na kuunda chama cha dharura cha kushiriki kwenye uchaguzi kama Kenya.
Kweli kabisa mkuu.
 
Hakuna mwenye dhamira ya dhati kwenye hivi vyama, new breed huwa inatokana na succession plans, na kama sio succession plan basi mapinduzi yafanyike.

Hivi vyama vyote ni mali ya watu fulani na wao ndio wenye maamuzi ya Kila kitu.
Ni kweli, ingawa CHADEMA tumefanya kosa la kutokuwa na succession plan. Kila ikifika uchaguzi wa mwenyekiti tunadai mwamba tuvushe.
 
niliona na nikashauri kibobevu jambo hili mapema, nafurahi kamanda umeliona na kulieleza kwa kina kwa namna nyingine....

mie bado nashauri na kusisitiza, lisu na mbowe waondoke kwa pamoja chamani kwasabb akibaki moja wapo vita baridi ya maneno itaendelea kua pale pale na kuzidisha migawanyiko chamani....

sasa kuondokana na kasumba hiyo hakuna budi kukaribisha mawazo, mtazamo na fikra mapya, mipango mipya, uelekeo na pumzi mpya chadema...

wangwana hao wapewe thank you, lakini pia hawana budi kuachia ngazi au kutoswa wakidinda...
migawanyiko na mipasuko wanayosababisha dah, imetosha ndrugu zango 🐒

Lissu na Mbowe waking'atuka, CHADEMA itaimarika sana na kuwa chama cha upinzani chenye ushawishi na nguvu sana Tanzania
Nakubaliana na wewe. Ila Lissu bado anahitajika pale kwenye uenyekiti.
 
Hao damu changa nayo unayosema ikishapata umaarufu kupitia chama nao watajiona ni wakubwa kuliko chama.
Bora damu changa inaweza kuthibitiwa tofauti na kiongozi mwandamizi ambaye ana kundi la watu nyuma yake.
 
Ili mada iwe tamu zaid ungemzungumzia na Lowassa baada ya kukatwa akahamia Chadema
 
Hakuna mwenye dhamira ya dhati kwenye hivi vyama, new breed huwa inatokana na succession plans, na kama sio succession plan basi mapinduzi yafanyike.

Hivi vyama vyote ni mali ya watu fulani na wao ndio wenye maamuzi ya Kila kitu.
Umepatia sana! Ndio maana sio mwana ccm Wala mwana cdm
 
Back
Top Bottom