Ni wakati turuhusu New Breed CHADEMA

Ni wakati turuhusu New Breed CHADEMA

Kutokana na sintofahamu kwenye chama Cha CHADEMA inayoendelea sasa hivi ndani ya chama hasa Viongozi kuhongwa na suala la akina Halima Mdee kurudishwa kwenye chama huko mbeleni, nina ushauri maalumu.

Ushauri wangu ni kwamba CHADEMA ijikite kwenye damu changa na siyo kuendelea kuhangaika na majina ya Viongozi waliohudumu CHADEMA Kwa muda mrefu. Hii Hali ya kuwa na Viongozi wa muda mrefu kwenye chama ndio inasababisha mgawanyiko. Maana Kuna Viongozi wengine wanajiona wao ndio Bora kwenye chama bila wao chama hakiendi, hivyo kuleta vitisho vya kuhama.

Mimi nadhani tukiwekeza kwa vijana na kuachana na haya majina makubwa hicho kiburi kitapungua. Kwa mfano kiongozi ndani ya CHADEMA anagombea cheo Fulani , asipokipata anahama chama. Hili tumeliona kwa Katibu Mkuu wa zamani Dr Mashinji aliyeondoka CHADEMA na kuhamia CCM baada ya kutoteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA. kwa Msigwa pia baada ya kuanguka uenyekiti wa Kanda ya Nyasa na hata kwa Selasini baada ya kushindwa uchaguzi wa Kanda ya Kaskazini akahamia NCCR. Hii ni hatari Sana. Hivi karibuni Wenje katangaza kugombea umakamu wenyekiti, je akianguka atabaki kwenye chama? au atahama Kama Msigwa. Je John Mnyika asipoteuliwa Tena kwenye Ukatibu Mkuu atabaki kwenye chama? Ila tungekubali kuwapa nafasi vijana ndani ya chama haya mambo ya Kiongozi kugombea nafasi kisa anataka kuhama yasingekuwepo maana anajua akiondoka wapo wengi wa kujaza nafasi yake.

Pia Kuna ujinga Fulani ndani ya CHADEMA ya kwamba kiongozi Fulani akipata ubunge anaanza kuota mapembe na kukidharau chama. Tumeona hili kwa Nassari ambaye alidiriki hata kukacha vikao vya bunge ili afukuzwe ahamie CCM, tumeona kwenye bunge la 2015 kwa akina Silinde, Lwakatare, Kubenea, nk wengi waliohama chama na kukidharau baada ya kupata ubunge, maana walijiona wao Wana majina makubwa hivyo chama kinawahitaji kuliko wao kukihitaji chama. Ila tungewekeza kwa vijana haya maujinga yasingekuwepo.

Mwisho CHADEMA imeshakuwa brand, Sasa tuiuze hiyo brand watu wailewe ili tupate vijana wengi wanachama. Tuje na strategies ya kupata vijana wengi.

Toka ujio wa Lowassa nilisema Mbowe hastahili tena kuendelea kuwa mwenyekiti wa cdm. Kinachoendelea sasa ndani ya cdm ni madhara ya uongozi wa muda mrefu wa Mbowe kama mwenyekiti wa cdm.
 
Viongozi wa chama wasiwe wabunge Wala madiwani. Na uongozi wa chama, ubunge,udiwani uwe na ukomo at least miaka 10 mpaka 15. Ukishatumikia chama kwenye ubunge,udiwani au nafasi ya juu ya chama ukimaliza muda wako unapisha wengine. Hii itatoa furusa kupata mawazo mapya. Lakini pia kiongozi mmoja asishike nafasi mbili kwa wakati mmoja, hii itasaidia mgawanyo wa madaraka nakutoa nafasi kwa vipaji vipya.

Ingawa sidhani kama itawezekana.
 
Nakubaliana na wewe. Ila Lissu bado anahitajika pale kwenye uenyekiti.
huoni kwamba hiyo itaendeleza cold war baina ya huyo atakae ng'atuka na atakae baki uongozini na kuchochea migawanyiko zaidi, lakini na mipasuko isiyoisha ndani ya Chadema?

hali ya kisiasa inayoendelea hivi sasa ndani ya Chadema, inasemekana ni kuhujumiana katika azma za mafahali hawa wa wawili yaani chairman na vice chairman kufikia ndoto, malengo na matarajio yao ya siku za usoni....

kwa mfano,
chairman ana uhakika 100% wa kukiongoza chama uchaguzi mkuu ujao na kikapata wabunge at least wa5 wa kuchaguliwa na kujihakikishia ruzuku na wingi wa wabunge wa viti maalumu kulingana na wingi wa kura za mgombea urasi ambae, kwa kumtazama body language, tone na facial expressions za mwenyekiti ni dhahiri anapendelea awe Dr.wilbroad Peter slaa na sio huyu naibu wake chamani kama siyo yeye mwenyewe kugombea 🐒

nadhani fresh blood ni muhimu zaidi kwa uhai wa sasa, na kwa mustakabali mwema wa Chadema ya baadae 🐒
 
Viongozi wa chama wasiwe wabunge Wala madiwani. Na uongozi wa chama, ubunge,udiwani uwe na ukomo at least miaka 10 mpaka 15. Ukishatumikia chama kwenye ubunge,udiwani au nafasi ya juu ya chama ukimaliza muda wako unapisha wengine. Hii itatoa furusa kupata mawazo mapya. Lakini pia kiongozi mmoja asishike nafasi mbili kwa wakati mmoja, hii itasaidia mgawanyo wa madaraka nakutoa nafasi kwa vipaji vipya.

Ingawa sidhani kama itawezekana.
Asante sana Kwa maoni yako mkuu.
 
huoni kwamba hiyo itaendeleza cold war baina ya huyo atakae ng'atuka na atakae baki uongozini na kuchochea migawanyiko zaidi, lakini na mipasuko isiyoisha ndani ya Chadema?

hali ya kisiasa inayoendelea hivi sasa ndani ya Chadema, inasemekana ni kuhujumiana katika azma za mafahali hawa wa wawili yaani chairman na vice chairman kufikia ndoto, malengo na matarajio yao ya siku za usoni....

kwa mfano,
chairman ana uhakika 100% wa kukiongoza chama uchaguzi mkuu ujao na kikapata wabunge at least wa5 wa kuchaguliwa na kujihakikishia ruzuku na wingi wa wabunge wa viti maalumu kulingana na wingi wa kura za mgombea urasi ambae, kwa kumtazama body language, tone na facial expressions za mwenyekiti ni dhahiri anapendelea awe Dr.wilbroad Peter slaa na sio huyu naibu wake chamani kama siyo yeye mwenyewe kugombea 🐒

nadhani fresh blood ni muhimu zaidi kwa uhai wa sasa, na kwa mustakabali mwema wa Chadema ya baadae 🐒
Hakutatokea cold war, maana mwenyekiti alishatangaza anastaafu Sasa sijui ni pesa za Abdul ndio zimemfanya aghairi kustaafu.

Kwa succession plan Lissu alistahili kuwa Mwenyekiti kwa wakati huu kutokana kuaminika na kusimamia ukweli na kuwa mwanaharakati ambayo ndio tradition ya CHADEMA. Mbowe ameshamaliza muda wake makalio yake yameisha.
 
Toka ujio wa Lowassa nilisema Mbowe hastahili tena kuendelea kuwa mwenyekiti wa cdm. Kinachoendelea sasa ndani ya cdm ni madhara ya uongozi wa muda mrefu wa Mbowe kama mwenyekiti wa cdm.
Kweli mkuu, Mbowe hastahili kuendelea kuwa Mwenyekiti. Na akilazimisha kuendelea CHADEMA itaingia kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 ukiwa dhaifu kupindukia na hata CCM haitakuwa na haja ya kuiba kura.
 
Kutokana na sintofahamu kwenye chama Cha CHADEMA inayoendelea sasa hivi ndani ya chama hasa Viongozi kuhongwa na suala la akina Halima Mdee kurudishwa kwenye chama huko mbeleni, nina ushauri maalumu.

Ushauri wangu ni kwamba CHADEMA ijikite kwenye damu changa na siyo kuendelea kuhangaika na majina ya Viongozi waliohudumu CHADEMA Kwa muda mrefu. Hii Hali ya kuwa na Viongozi wa muda mrefu kwenye chama ndio inasababisha mgawanyiko. Maana Kuna Viongozi wengine wanajiona wao ndio Bora kwenye chama bila wao chama hakiendi, hivyo kuleta vitisho vya kuhama.

Mimi nadhani tukiwekeza kwa vijana na kuachana na haya majina makubwa hicho kiburi kitapungua. Kwa mfano kiongozi ndani ya CHADEMA anagombea cheo Fulani , asipokipata anahama chama. Hili tumeliona kwa Katibu Mkuu wa zamani Dr Mashinji aliyeondoka CHADEMA na kuhamia CCM baada ya kutoteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA. kwa Msigwa pia baada ya kuanguka uenyekiti wa Kanda ya Nyasa na hata kwa Selasini baada ya kushindwa uchaguzi wa Kanda ya Kaskazini akahamia NCCR. Hii ni hatari Sana. Hivi karibuni Wenje katangaza kugombea umakamu wenyekiti, je akianguka atabaki kwenye chama? au atahama Kama Msigwa. Je John Mnyika asipoteuliwa Tena kwenye Ukatibu Mkuu atabaki kwenye chama? Ila tungekubali kuwapa nafasi vijana ndani ya chama haya mambo ya Kiongozi kugombea nafasi kisa anataka kuhama yasingekuwepo maana anajua akiondoka wapo wengi wa kujaza nafasi yake.

Pia Kuna ujinga Fulani ndani ya CHADEMA ya kwamba kiongozi Fulani akipata ubunge anaanza kuota mapembe na kukidharau chama. Tumeona hili kwa Nassari ambaye alidiriki hata kukacha vikao vya bunge ili afukuzwe ahamie CCM, tumeona kwenye bunge la 2015 kwa akina Silinde, Lwakatare, Kubenea, nk wengi waliohama chama na kukidharau baada ya kupata ubunge, maana walijiona wao Wana majina makubwa hivyo chama kinawahitaji kuliko wao kukihitaji chama. Ila tungewekeza kwa vijana haya maujinga yasingekuwepo.

Mwisho CHADEMA imeshakuwa brand, Sasa tuiuze hiyo brand watu wailewe ili tupate vijana wengi wanachama. Tuje na strategies ya kupata vijana wengi.
Ni Too late nadhani soln ni kupata katiba mpya ili raisi asiwe na nguvu ya kuhonga Kila mtu au kumshawishi Kila mtu

Wapambe wa raisi Wana hela nyingi za rushwa wanaweza kuhonga Kila mtu
 
Mlikubali ushindi wa sugu bila kujua pesa zilipotoka
Msigwa aliyehama anaweza asiwe threat kwa chama kuliko sugu aliyebaki. Amepokea rushwa, imemsaidia kuwa kiongozi mkubwa ndani ya chama. Mmekwisha
 
Hakutatokea cold war, maana mwenyekiti alishatangaza anastaafu Sasa sijui ni pesa za Abdul ndio zimemfanya aghairi kustaafu.

Kwa succession plan Lissu alistahili kuwa Mwenyekiti kwa wakati huu kutokana kuaminika na kusimamia ukweli na kuwa mwanaharakati ambayo ndio tradition ya CHADEMA. Mbowe ameshamaliza muda wake makalio yake yameisha.
disrespect na loyalty yenye shaka ya vice chairman inatambakiza chairman chadema mpaka ahakikishe chadema iko mikononi mwa mtu ambae ni loyal na amemuandaa but for sure, not the shouting gentleman 🐒
 
Back
Top Bottom