Ni wakati wa Musonda kuondoka Yanga

Ni wakati wa Musonda kuondoka Yanga

Binafsi naona atoke
1: skudu
2: lomalisa


Kwa wazawa waanze na kibabage, dogo sijui kwann anapata namba lakini hafai kabisa
Uondoe wachezaji wanacheza nafasi moja kwa wakati moja? replacement yao iki fail unafanyaje?
 
Yanga isitarajie kufanya cha ajabu kimataifa kama itakuwa na washambuliaji Musonda na Mzize.
 
Yanga inapaswa kufikiria kuachana na Kennedy Musonda.

Tokea aje hapa nchini, Musonda hajatoa kile kilichotegemewa kwa 100%. Ni mchezaji mzuri sana, lakini yapo yanayofikirisha juu yake.

Musonda hana muendelezo mzuri. Ni michezo michache sana amecheza kwa kiwango cha juu, iliyosalia anakuwa wa kawaida tu au kushindwa kutoa kitu chenye tija.

Nadhani, Yanga SC inapaswa kufikiria kumleta mchezaji bora zaidi yake. Ili timu kama timu ipige hatua kwenda mbele. Sio dhambi. Al Ahly iliwasajili Ahmed Kendouci, Walter Bwalya, na wakawaondoa haraka.. baada ya kuonekana hawaisaidii timu kwenda mbele zaidi.

Yanga SC wanapaswa waangalie mchezaji bora zaidi ya Musonda. Ili aje akisogeze mbele kikosi kutoka hapa kilipo na kuwa tishio zaidi hapa AFRIKA.
Abakie mmoja tu kati ya Musonda, Guede na Mzize. Yanga watafute mshambuliaji wa kueleweka, kuna mechi tulipoteza kutokana na ushambuliaji kuwa nyoro nyoro.
 
Binafsi naona atoke
1: skudu
2: lomalisa


Kwa wazawa waanze na kibabage, dogo sijui kwann anapata namba lakini hafai kabisa
Lomalisa ni mchezaji mzuri sana, Kibabage zaidi ya mbio hana akili za mpira. Kuna mechi anakuwa uchochoro sana, kwani zaidi ya kupanda kushambulia hana uwezo wa kukaba.
 
Kama unamtazama Musonda kwa jicho la kumtazama namba Tisa,ambapo kwa mujibu wa usajili wake tuliambiwa ni mfungaji,, utapata jibu AONDOKE,,,kama utamtazama kwa jicho la mchango wake kwenye timu jibu ni ABAKI na kama mkataba wake unakaribia mwisho uongezwe.

Sijawahi kusikia kwenye mechi yoyote ya yanga, kutoka kwa mashabiki au wanahabari wakisema mechi fulani yanga inatakiwa SKUDU na GIFT FREAD waanze. Lakini kwa MUSONDA ni mechi nyingi anatajwa uwepo wake.
 
Daah washabiki bhana mchezaji akikosa goli tu atoke aisee...juzi mlikua mnasema Gwede hafai leo mmegeuka Musonda hafai yaani mnataka Yanga iwe kama Madrid kwa siku moja kazi kweli kweli...
 
Hapo kwa kibabage sikuungi mkono. Dogo anaupiga mwingi.
Kibabage kwenye defense akili Hana kabisa, Jana kibu angehamia namba 7 Kule alivyoingia kibabage tungepata shida sana, kampa kazi sana Ibrahim bacca, maana dogo hajui tofauti kati ya namba 3 na 11 Kila saa alikua out of position ashukuru maxi defensively anajua sana kumsaidia left back
 
Mimi ninachotamani kutoka Yanga ni kuona tu inapiga hatua kubwa zaidi ya hii iliyopo sasa.

Kama benchi la ufundi litaona kuna umuhimu wa kupunguza baadhi ya wachezaji, na kuongeza wengine! Sioni kama kuna tatizo.

 
Back
Top Bottom