Ni wakati wa wanachadema kumuelewa Dr. Slaa na kumuwajibisha Mbowe!

Ni wakati wa wanachadema kumuelewa Dr. Slaa na kumuwajibisha Mbowe!

Ina maana hawakoseani, mbona wahajafukuzana? Acha matamshi ya hvyo! Kama kuna wakati Mbowe anahitajika ni sasa. Risasi , mabomu, jela kesi kibao buila uongozi imara, CDM itasambaratika.
Kama umetumwa, kafie kaburini
Awachane na uenyekiti apishe wengine, kwani chadema yupo yeye tu?
Akiwa si mwenyekiti uhitajika wake unakua umekoma?
 
WADAU CCM kupitia UVCCM wanahangaika sana kujifanya ni Bavicha eti hawamtaki Mh.Feeeman MBOWE kuwa Mwenyekiti Wa Chadema.Najiuliza ni kwanini CCM haimtaki Mh.Mbowe? Ana madhara gani kwao?
 
Pale wema Sepetu atakapo teuliwa kugombea urais kupitia Chadema hapo ndipo Red brigade watakapo stuka.
 
Kadri siku zinavyokwenda ndio ninazidi kutambua kumbe Mbowe yuko strong sana ktk medani ya siasa kulinganisha na wenyeviti wengine. Mawe yamekuwa mengi sana kwake.... Hii ni baada ya kila jitihada za kumtikisa kushindikana!
 
Na mugabe wa chadema ni nani?
Nikuelimishe kuhusu sheria ya uchochezi ambayo wewe unaupractice humu. Ni kosa kubwa kushawishi watu au kikundi cha watu kufanya au kuvunja sheria. Hili unalolishawishi tena kwa kutumia mfano wa rais halali wa nchi huru utakuwa tayari kupambana na Kibatala? Dogo ishi maisha yako na iache ccm inayokutumia kinyume na maumbile!
 
WADAU CCM kupitia UVCCM wanahangaika sana kujifanya ni Bavicha eti hawamtaki Mh.Feeeman MBOWE kuwa Mwenyekiti Wa Chadema.Najiuliza ni kwanini CCM haimtaki Mh.Mbowe? Ana madhara gani kwao?
Chacha wangwe na Zitto walivyohitaki kile kiti na kukiona cha moto kumbe ni UVCCM, kama upeo wako umeishia hapo hongera mjomba
 
Freeman Aikael Mbowe mwenyekiti wa CHADEMA Taifa anapaswa kupata somo kutoka kwa Rais Robert Mugabe hii inatokana na ukweli kwamba kaminya sana democracy ndani ya chama chake kiasi kwamba asipopata funzo kutoka kwa mwenzake Robert Mugabe nae yatamkuta kama yaliyomkuta Mugabe na nitatoa mifano michache

1.Freeman Mbowe kama mwenyekiti wa CHADEMA Taifa chini ya Uongozi wake kafuta ukomo wa madaraka ambapo mtu anaweza kuwa kiongozi maisha yake yote cha msingi achaguliwe na wanachama wake Mbowe sasa takribani yupo madarakani kwa miaka 14 aina hii ya democracy ndio alikua akiifanya Mugabe kwani pia Zimbabwe haikua na ukomo wa madaraka na Mugabe siku zote alikua akichaguliwa kama rais na wananchi wake so hapa Mbowe ni kama Mugabe ana kitu cha kujifunza.

2.Utawala unaoamini katika chaguo lake na maamuzi yake tunaona mwaka 2015 Mbowe alimleta Lowasa kugombea urais na alipitishwa kwa kura za NDIO na HAPANA watu hawakupiga kura za siri kama msingi wa demokrasia inavyotaka aina hii ya upigaji kura ilifanyika ili chaguo la mwenyekiti lipite na kweli lowasa alipita kwa kura nyingi za NDIO kwa upande wa Mugabe tunaona alivokua akiminya demokrasia kwa kutaka chaguo lake mkewe aje kumlithi kwa vile alikua akimtaka yeye so hapa Mbowe ana kitu cha kujifunza ili yasije kumpata yaliyompata mwenzake Mugabe

3.Kuminya watu wenye mawazo mbadala Freeman Mbowe kama alivyo Mugabe anatabia ya kuminya watu ndani ya chama chake wanaoona wanataka kuleta mabadiliko alianza Chacha Wangwe kutaka kugombea uenyekiti CHADEMA akafukuzwa uanachama akaja Zitto Kabwe kutaka kugombea uenyekiti akafukuzwa uanachama hii tabia ni sawa na ya Mugabe alipoona Makamu wake wa Rais anaweza kum challenge akaamua kumfukuza katika nafasi yake so hapa Mbowe ni kama Mugabe

Kwa yaliyotokea Zimbabwe Mbowe unasomo kubwa la kujifunza kutoka kwa mwenzako Robert Mugabe
 
Mbowe kama akakutuma we kula hela zake tu. Mugabe wetu yule.
tapatalk_1485892146512.jpeg
 
Kumbuka mwenyekiti na mgombea Rais ni watu wawili tofauti, hebu nyinyi jitafakarini kama mnaweza kumrudisha JK awe chairman halafu huyu mhenga aendelee na nafasi aliyonayo!
 
  1. Askofu Shao amfananisha Rais Magufuli na Robert Mugabe wa Zimbabwe... ataka watanzania tumuunge mkono!
 
Kumbuka mwenyekiti na mgombea Rais ni watu wawili tofauti, hebu nyinyi jitafakarini kama mnaweza kumrudisha JK awe chairman halafu huyu mhenga aendelee na nafasi aliyonayo!
Soma uelewe
 
Kama wewe ni mwanachama wa chadema kweli sepa zako tu,Tuachie mwenyekiti wetu jombaa.
 
Back
Top Bottom