#COVID19 Ni Watanzania gani wanaohitaji chanjo?

#COVID19 Ni Watanzania gani wanaohitaji chanjo?

Nimesikia baadhi ya viongozi na watendaji wa serikali wakisema kuwa Watanzania wanasubiri chanjo ili nao waungane na dunia katika mapambano dhidi ya Corona, Leo ningependa kujua hao Watanzania wanaohitaji chanjo wanapatikana wapi?

Maana ukweli ni kuwa majority wameonesha kutotaka chanjo, au sikuhizi mambo yanakwenda kinyume?

Viongozi wetu mkikosea kwenye hili mtakuja kujuta sana, huu uzi utakuwa shahidi siku hizo.

Hii inaonyesha nchi yetu bado ni masikini. Hata sehemu ambazo chanjo ni bure Mfano USA majimbo masikini kuliko yote ndiyo wamepiga chanjo wachache maana elimu ni ndogo kwa watu. Masikini ndiyo wakwanza kuamini uvumi na uongo na hawaamini sayansi. Hiki ni kipimo kizuri kujua mtu au watu wako kundi lipi. Na kama unasema hamna watu unathibitisha kabisa umezungukwa na hao walala hoi. Kule Uninio najua mimi wazee karibu wote wanasubiri chanjo! kuna watu kibao wengine mpaka waandishi wa habari na wanasiasa wanaenda nje kupata chanjo
 
Nimesikia baadhi ya viongozi na watendaji wa serikali wakisema kuwa Watanzania wanasubiri chanjo ili nao waungane na dunia katika mapambano dhidi ya Corona, Leo ningependa kujua hao Watanzania wanaohitaji chanjo wanapatikana wapi?

Maana ukweli ni kuwa majority wameonesha kutotaka chanjo, au sikuhizi mambo yanakwenda kinyume?

Viongozi wetu mkikosea kwenye hili mtakuja kujuta sana, huu uzi utakuwa shahidi siku hizo.

Hao watanzania umewasikia wapi? Maana siku hizi kuna viongozi walioko madarakani bila ridhaa ya umma, wamepora sauti za wananchi, kisha mitazamo yao wanawawekea wananchi mdomoni na kusema ni matakwa ya watanzania.
 
Hiyo chanjo haiondoi ugonjwa, maana siyo tiba....

Kweli mkuu.....

CHANJO ni KINGA....ni sawa na kufunga milango ya nyumba nyakati za usiku kule KEKO....haina maana WEZI hawawezi kuingia na kuvunja milango....

Wataalam wanatuambia ya kwamba ukichomwa chanjo na kukutana na hivyo vidudu unaweza kuugua ila si kufikia kuwa na HALI TETE....
 
Basi usiende kasi sana, kabla hujachanja utahitaji kutusainia fomu yetu......ili tusigeukane mbele ya safari.
Sawa mkuu....

Nitatoka huku kwa Mkunduge kuja kuisaini hiyo fomu mkuu wangu....

Niko radhi na tayari kusaini mkuu wangu....masela wangu Zwande ,Bozu ,Ally Meza na Philimon Chenje nao wamekubali kuchomwa hizo chanjo....nitakuja nao mkuu wangu!!
 
Kweli mkuu.....

CHANJO ni KINGA....ni sawa na kufunga milango ya nyumba nyakati za usiku kule KEKO....haina maana WEZI hawawezi kuingia na kuvunja milango....

Wataalam wanatuambia ya kwamba ukichomwa chanjo na kukutana na hivyo vidudu unaweza kuugua ila si kufikia kuwa na HALI TETE....
Kuna watu wengi wanapata infection bila kuonyesha dalili, lakini hawajachoma hizo takataka...
 
Chanjo ni hiari hakuna atakayekulazimisha lakini kwa maoni yangu madaktari, manesi na wote wanaofanya kazi hospitalini na vituo vya afya inabidi iwe lazima. Pia Kuna hili la COVID-19 passport kwa wale wasafiri wa nchi za nje nchi nyingi zitatumia hii kitu ili kuruhusu wageni kuingia kwenye nchi zao. Kama wewe si msafiri wa nchi za nje basi HALIKUHUSU.

Nimesikia baadhi ya viongozi na watendaji wa serikali wakisema kuwa Watanzania wanasubiri chanjo ili nao waungane na dunia katika mapambano dhidi ya Corona, Leo ningependa kujua hao Watanzania wanaohitaji chanjo wanapatikana wapi?

Maana ukweli ni kuwa majority wameonesha kutotaka chanjo, au sikuhizi mambo yanakwenda kinyume?

Viongozi wetu mkikosea kwenye hili mtakuja kujuta sana, huu uzi utakuwa shahidi siku hizo.
 
Kuna watu wengi wanapata infection bila kuonyesha dalili, lakini hawajachoma hizo takataka...
Kwani kung'atwa na mbu ndio kupata ugonjwa wa malaria?!!

Mkuu wangu unadhani sote tuna KINGA madhubuti dhidi ya magonjwa ya milipuko ?!!

Kwa hizi chumi zetu za kupitisha mchana kwa pasi ndefu...kahawa vikombe 3 na kashata ili vitoto vyetu viende SKONGA.....

Kwa hizi tamaduni zetu huku uswazi ambako mboga za majani na matunda ni mwiko na anasa ?!!

Mkuu ni bora tu tuchanjwe halafu ukija kutuchapa basi hatua stahiki zitakuwa zimeshachukuliwa.....
 
Nimesikia baadhi ya viongozi na watendaji wa serikali wakisema kuwa Watanzania wanasubiri chanjo ili nao waungane na dunia katika mapambano dhidi ya Corona, Leo ningependa kujua hao Watanzania wanaohitaji chanjo wanapatikana wapi?

Maana ukweli ni kuwa majority wameonesha kutotaka chanjo, au sikuhizi mambo yanakwenda kinyume?

Viongozi wetu mkikosea kwenye hili mtakuja kujuta sana, huu uzi utakuwa shahidi siku hizo.
Usiwasemee watu, subiri chanjo zifike halafu tutashuhudia kwa macho na tutajua uhalisia wa mioyo ya watanzania. Ni mapema sana kuanza kusema chochote kuhusuuhitaji wa hii chanjo ila ninachojua watu wengi watachoma chanjo, ni suala la muda tu
 
Ninapendekeza hilo.

Nchi za wenzetu hakuna hiyari kwa hao watoa huduma mahospitalini.

HEBU TUFIKIRIE:
Mtaalamu wetu wa HOSPITALI anarudi nyumbani kwa mumewe/mkewe na wanawe...hajachanjwa, anaupeleka ugonjwa nyumbani kwa wapendwa wake....tusisahau wao ndio rahisi mno kuambukizwa "DOZI KUBWA" kuliko wengine.

#ChanjoIweLazimaKwaWataalamWaAfya
#MieMlalahoiNinaisubiriKwaHamuHiyoChanjo
Nakubaliana na hili kwa 100% kwa sababu wapo kwenye risk kubwa ya kuoata maambukizi tofauti na watu wengine
 
Nakubaliana na hili kwa 100% kwa sababu wapo kwenye risk kubwa ya kuoata maambukizi tofauti na watu wengine
Hakika mkuu wangu Abrianna....

Ni bora tuwalinde wao ,wapendwa wao majumbani na sisi walalahoi wa Kiburugwa na Kwa Mtogole!👍
 
Usiwasemee watu, subiri chanjo zifike halafu tutashuhudia kwa macho na tutajua uhalisia wa mioyo ya watanzania. Ni mapema sana kuanza kusema chochote kuhusuuhitaji wa hii chanjo ila ninachojua watu wengi watachoma chanjo, ni suala la muda tu
Vibaraka ndo mtachoma, wazalendo tulisha malizana na corona kitambo sana.
 
Kwani kung'atwa na mbu ndio kupata ugonjwa wa malaria?!!

Mkuu wangu unadhani sote tuna KINGA madhubuti dhidi ya magonjwa ya milipuko ?!!

Kwa hizi chumi zetu za kupitisha mchana kwa pasi ndefu...kahawa vikombe 3 na kashata ili vitoto vyetu viende SKONGA.....

Kwa hizi tamaduni zetu huku uswazi ambako mboga za majani na matunda ni mwiko na anasa ?!!

Mkuu ni bora tu tuchanjwe halafu ukija kutuchapa basi hatua stahiki zitakuwa zimeshachukuliwa.....
Utaishia kupata vaccination failures, korona ikipita inatambaa tu kama inanawa.....
 
Nimesikia baadhi ya viongozi na watendaji wa serikali wakisema kuwa Watanzania wanasubiri chanjo ili nao waungane na dunia katika mapambano dhidi ya Corona, Leo ningependa kujua hao Watanzania wanaohitaji chanjo wanapatikana wapi?

Maana ukweli ni kuwa majority wameonesha kutotaka chanjo, au sikuhizi mambo yanakwenda kinyume?

Viongozi wetu mkikosea kwenye hili mtakuja kujuta sana, huu uzi utakuwa shahidi siku hizo.
Hiyo ya majority kutotaka chanjo, huo utafiti ulifanyia wapi? Mimi binafsi sina shida na chanjo. Sijawahi kukosa chanjo yoyote, nina sababu gani ya kuikataa hii ya sasa?

Kazini pangu, kila mmoja anazungumzia kuwa tayari kuchanjwa, sidhani kama yupo hata mmoja ambaye hataki.

Kwanza chanjo haziwezi kutosha kwa watu wote, itakuwa kwa awamu. Kama watakuwepo wasiotaka itakuwa ahueni kwa tunaotaka na kwa Serikali. Hao wasiotaka watakuja kupewa mwishoni kabisa, ikiwezekana hata mwakani, kwa wale ambao watakuwa hai.
 
Back
Top Bottom