#COVID19 Ni Watanzania gani wanaohitaji chanjo?

#COVID19 Ni Watanzania gani wanaohitaji chanjo?

itakuwa ndo chanjo ya maisha au wanazi update kila baada ya muda flani kama software
Chanjo ya maisha dhidi ya hiyo CORONA....zitakuwa ni zaidi ya moja kama chanjo nyinginezo tu.....

Mbona tunachomwa chanjo 5 kwa ajili ya kuzuia PEPOPUNDA?!!!
 
🤣🤣

Mimi ni wa BABA....(Hapa kazi tu)

Mimi ni wa MAMA...(Kazi Inaendelea)

Kama Raia kila siku inabidi tuwe bora zaidi ya "Jana"....

Mh.SSH ndiye kiongozi mkuu wa taifa letu pendwa ,kumuunga mkono ni wajibu wetu wa kila mmoja ukiacha baadhi ya wale wenye "mbango"....ni "mbango tu" mkuu....MBANGO TU 🤣

#KaziInaendelea
#ChanjoIjeTu

Kuna tofauti kubwa baina ya kumwunga mkono mtu na kuwa chawa wake. Ninamwuunga mkono mama, lakini siyo chawa wake.

Unaona chawa wa baba na Corona? Unadhani hawaelewi hatari yake? Unaona chawa wa mama na katiba? Unadhani hawauoni umuhimu wake?

Sioni andiko bora kabisa kuhusu vyawa kuliko hili:

IMG_20210711_205649_038.jpg


Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Hivi kuamini sayansi ni kupi ni kukubali kila unachoambiwa ilimradi kimehuaiahwa na sayansi au ni vp? maana sielewi hii kauli, hao unaosema hawaamini sayansi ndio hao hao wanatibiwa hospitali endapo wakiumwa na hospitali wanatumia sayansi. Wengine wanadharau matunda na kuita uganga wa kienyeji ila jawajui kuwa sayansi hiyo hiyo ndio inatuambia faida zilizopo kwenye hayo matunda(kama malimao vitunguu tangawizi) na madhara yake, ila mtu anaona kula hayo matunda ni kinyume na sayansi na ni sawa na matunguri.

Wengine humu unakuta hata matumizi sahihi ya barakoa hayajui ila nae anavaa tu na kupoga kelele humu ili tu asionekane mjinga asiyeelimika kama sie wengine, hata hawa wanaotaka chanjo si kwamba wanauelewa wengine hawana uelewa wotewote ni kufuata mkumbo tu nae aonekane anaamini sayansi.

Mtu ambaye hataki chanjo kiukweli sio mwelewa. Mimi naishi US hapa watu 200 Milioni wamepata chanjo mimi nikiwa mojawapo na ndugu zangu wengine zaidi ya kumi wote tuko salama na tuna kinga. Kwasasa wasiwasi wa Watanzania wengi ni wazee wetu ambao wako 70's ni hatari sana kwao kupata Corona. Tunavyosema sayansi kuna wasomi wameshakaa na kuja na report ya kila kitu kuhusu chanjo.

Lakini ukweli ni kwamba kuna uhusiano mkubwa wa umasikini na kuamini chanjo mfano hapa US chanjo ni bure lakini majimbo masikini kuliko yote ndiyo kuna watu wengi ambao ni waoga wamechanja 36% hivi lakini nchi nzima ni karibu 67%. Inaelekea ukiwa na fikra za kimasikini vilevile unakuwa mtu wa kuamini uvumi. Hapa nasema fikra za kimasikini maana leo ukiwa masikini ukaenda kuiba bank na kuwa tajiri kwa wizi bado fikra zako ni za kimasikini.
 
Tafuta asilimia ya kifo kwa korona na asilimia ya kifo kwa chanjo. Ukipata jibu utaamua mwenyewe cha kufanya hakuna wa kukulazimisha maana kuna fomu ya kujaza.
Hiyo ni fomu ya ridhaa kushiriki kwenye majaribio ya chanjo, mnafanywa panya wa majaribio maana hakuna fidia yoyote mnayolipwa na mtafiti hausiki na madhara yatakayojitokeza.......huu ni uzumbukuku...
 
Askari wetu walio mstari wa mbele kutupatia HUDUMA ZA AFYA;

1) Manesi(nurses)

2) Madaktari (Doctors)

3) Wataalam wa maabara

4) Wataalam wa mionzi ,mashine za hospitali

5) Makatibu wa hospitali

6) Wahasibu wa hospitali

7) Watoa ushauri nasaha

8) Wataalamu wa viungo cheza

9) Wafamasia

10) Wahifadhi maiti

11) Wahudumu (nurses attendants)

12) Wahudumu wa usafi hospitalini

13) Wafanyakazi wa BANK za malipo zilizopo ndani ya Hospitali

14) Walinzi wakiwemo maaskari wa SUMA JKT/magrupu ya Ulinzi

WOTE HAWA NI LAZIMA WACHANJWE..

Upande wetu RAIA ,mathalani binafsi nitakuwa wa mwanzomwanzo kuitikia wito wa KUCHANJWA CHANJO HIYO DHIDI YA CORONA.

Hapa nimeshaanza kuliandaa bega langu kwa ajili ya hizo SINDANO....[emoji123]

#TuchanjweNduguZangu
#TuwalindeWengine
#NchiKwanza
#ChanjoNiMuhimu
#KaziIendelee
"...WOTE HAWA NI LAZIMA WACHANJWE..."

Huoni kama hujatoa jibu sahihi bado?

By the way, chanjo ni hiari wala siyo hiyo sentence yako
 
Askari wetu walio mstari wa mbele kutupatia HUDUMA ZA AFYA;

1) Manesi(nurses)

2) Madaktari (Doctors)

3) Wataalam wa maabara

4) Wataalam wa mionzi ,mashine za hospitali

5) Makatibu wa hospitali

6) Wahasibu wa hospitali

7) Watoa ushauri nasaha

8) Wataalamu wa viungo cheza

9) Wafamasia

10) Wahifadhi maiti

11) Wahudumu (nurses attendants)

12) Wahudumu wa usafi hospitalini

13) Wafanyakazi wa BANK za malipo zilizopo ndani ya Hospitali

14) Walinzi wakiwemo maaskari wa SUMA JKT/magrupu ya Ulinzi

WOTE HAWA NI LAZIMA WACHANJWE..

Upande wetu RAIA ,mathalani binafsi nitakuwa wa mwanzomwanzo kuitikia wito wa KUCHANJWA CHANJO HIYO DHIDI YA CORONA.

Hapa nimeshaanza kuliandaa bega langu kwa ajili ya hizo SINDANO....💪

#TuchanjweNduguZangu
#TuwalindeWengine
#NchiKwanza
#ChanjoNiMuhimu
#KaziIendelee
Majority ya Health care workers hawako tayari kuchanjwa. Anyway, tutegemee wengi kufoji vyeti vya Chanjo ili tuu waweze kupata vibali vya kufanya kazi na Taasisi za Kimataifa.
 
Back
Top Bottom