Ni zipi mbinu za kudhibiti wizi kwenye duka la jumla?

Ni zipi mbinu za kudhibiti wizi kwenye duka la jumla?

Hakuna haja ya camera, ujiwa na software ya inventory management, camera ni kujiongezea gharama. Maana hata ikiondoka carton moja ya item moja hesabu zinagoma . Cha kufanya kila item moja iwe displayed kwenye ngazi halaf zingine zote zinabakia store. Kwa hiyo mteja akija ataangalia sample kwenye item ambayo ipo kwenye ngszi then muuzaji ataangalia hiyo item kama ipo kwa kiasi gani kwenye system na kujulisha mteja kama ipo ama imeisha sasa kule store kutakuwa na store keeper naye ana comouter ilounganishwa kwenye system yeye kazi yake nikuregister vitu vinavyotoka na kuingia na bei za kununulia na kuuzia, na kutakuwa na watu wanaobeba vitu kutoa store kuleta kwa mteja, sasa ikipotea hata item moja wale wabebaji na mtu wa store kata kwenye mishahara yao. Wewe utabaki sehem tu kuangalia report tu . Na kwa vile una maduka mengi system inakuwa vizuri ikiwa online.
Ahsante kwa ushauri wako kuu

Ngoja niwatafute jamaa wa IT naamini hii itakua issue simple kwao...
 
Hapo software itafanya kila kitu
Stock inayoingia na jinsi wafanyakazi wanavyo uza. Kila kitu kirekodiwe kwenye software
sawa mkuu ngoja nianze kuifatilia hi issue

Nitaweka mrejesho hapa...
 
Mkuu samahani nje ya mada. Hivi duka kama lako hilo la jumla linacost kiasi gani cha pesa?
nimeanza na mtaji mdogo then kila biashara inavyo zidi kuwa na wateja wengi naongeza mtaji


Minimum niliyoanza nayo milion 10.700.000
 
Hello JF,

Moja kwa moja kwenye bandiko

Mimi nimmoja ya wamiliki wa Duka la Jumla kiukweli hi biashara inalipa sana hasa inalipa faida ya milion 1.5 kwa mwezi kabla ya kutoa malipo ya wafanyakazi na Kodi ya pango nabaki na 600k au 700k Kama faida, kwa Duka moja.

Hivyo kutokana nabiashara kukua nimefungua zaidi ya maduka 4 ya jumla katika mikoa ya Tanga Arusha Mwanza

Dar ndio mean Office ilipo

Biashara ambazo nazi-manege

Tomato, pemepers biscuits, kalamu, Super Grue, madaftari, pipi Big G, nk.

Changamoto ipo kwenye kulinda wafanyakazi wasiibia sana hadi kupelekea biashara kufa

Je, ni mifumo gani ya ulinzi niiweke ili kulinda Mahesabu pamoja na store?

Pia nawaomba Moderator huu uzi msiuunganishe wala kuuwamisha Active nimeuweka hapa ili niweze kupata Great thinks
Mkuu una ID ya kibabe sana.
Tupe siri ya mafanikio katika biashara yako
 
Hello JF,

Moja kwa moja kwenye bandiko

Mimi nimmoja ya wamiliki wa Duka la Jumla kiukweli hi biashara inalipa sana hasa inalipa faida ya milion 1.5 kwa mwezi kabla ya kutoa malipo ya wafanyakazi na Kodi ya pango nabaki na 600k au 700k Kama faida, kwa Duka moja.

Hivyo kutokana nabiashara kukua nimefungua zaidi ya maduka 4 ya jumla katika mikoa ya Tanga Arusha Mwanza

Dar ndio mean Office ilipo

Biashara ambazo nazi-manege

Tomato, pemepers biscuits, kalamu, Super Grue, madaftari, pipi Big G, nk.

Changamoto ipo kwenye kulinda wafanyakazi wasiibia sana hadi kupelekea biashara kufa

Je, ni mifumo gani ya ulinzi niiweke ili kulinda Mahesabu pamoja na store?

Pia nawaomba Moderator huu uzi msiuunganishe wala kuuwamisha Active nimeuweka hapa ili niweze kupata Great thinks

Kuna system sijui ndo app unaingiza stock yako yote
Akiuza anaingiza inadeduct pale,bidhaa ikikaribia kuisha inaonyesha pale

App inabeba idadi ya bidhaa pamoja na mauzo

Utaona turnover ya mwezi na pia unaweza kuregister wanunuzi wa mara Kwa mara ukaona turnover yao.
 
Ahsante kwa ushauri wako kuu

Ngoja niwatafute jamaa wa IT naamini hii itakua issue simple kwao...

Kuna jamaa anafanya hii ndo wauzaji wa kariakoo wanatumia
Ukihitaji kesho naweza kukutafutia mawasiliano
 
Unahitaji CCTV kwa ajili ya kufuatilia yanayoendelea katika maduka yako. Unahitaji well thought interconnection ya hizo CCTV na internet ili uwe na access popote.

Pili unahitaji accounting software ambayo inaweza kufanya inventory management ili kufanya tracking ya purchase, sales, profit and loss na kujua financial position yako.

Kwa upande wa Software kama unataka serious consultant unaweza kunicheck inbox. Ni kama tu uko serious. Yale mambo ya kupotezeana muda huwa sina muda nayo.
Kwa picha ya Duka lake inaonekana Ni biashara changa bado na kumuambia sijui CCTV sijui Software unamuongezea gharama bila sababu. Wabongo anakuja na vitu vyake anauza kwanza baadae ndio anauza vyako. Hizo Software hazigusi utakuta hesabu zipo sawa always
 
Kwa picha ya Duka lake inaonekana Ni biashara changa bado na kumuambia sijui CCTV sijui Software unamuongezea gharama bila sababu. Wabongo anakuja na vitu vyake anauza kwanza baadae ndio anauza vyako. Hizo Software hazigusi utakuta hesabu zipo sawa always
hi ndio inaniumiza sana siku nitakayo tembelea mfano Mwanza nikaa Dukanii mweyewe siku nzima basi mauzo yanaongezeka mara mbili ya mauzo ya wafanyakazi....
 
All in all huwezi kuzuia mianya ya kupigwa hata ufunge nn
Chamsingi walipe vizur wafanyakazi ishi nao kwà amani na upendo Jenga Imani kwako

Cha mwisho kama unapata faida hicho ndo chamsingi hayo mengine ni kujipa gharama bure

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mastermind wanajua kusoma ramani jinsi ya kupiga na mda gani jambo litokee huenda wakachagua siku upo ñdo wanapiga vizur tuu hata ufunge nn wabongo hawashindwi jambo


Ilikujaga mashine ya kukamata wezi bongo mbona iliibiwa hiyo mashine

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Weka mfumo wa computer, kuna kiapplication kinaitwa aleco kiko poa, au app nying tu za ivyo zipo ukitafta
 
Hahaha kumbe ndivyo ilivyo
Mkuu usiombee!

Nilikuwa nafanya kazi na dogo mmoja nauza spare na oils,sasa siku moja akaja jamaa nilikumbuka kumuona sana akija kufanya manunuzi pale dukani so nikawa nimekariri bidhaa anazopenda kuchukua mara kwa mara ila siku hiyo akaja akataka bidhaa tofauti na alizozoea,(kwangu halikuwa tatizo)tatizo ni bidhaa aliyoagiza mbona carton yake ikaonekana nzito sana isivyo kawaida?

Normally,carton ya oil zile litre moja moja uzito wake hauzidi Kg10/12 but nikashangaa mbona hili boksi alilotoa huyu dogo linaonekana zito ameinua hadi mishipa ya shingo imemtoka na amelifunga kamba katikati?siyo kawaida kabisa box jepesi kufungwa kamba(ukweli sikuelewa na ilikuwa ni bahati yangu tu kama ningekuwa bize ningeshaisha)nikamwambia weka hilo box chini,akashtuka ohh bro unajua jamaa ana haraka sana nikamuuliza ana haraka mbona unamsemea wewe yeye hajasema mwenyewe?kuinua macho namuona jamaa yule mteja anavuka mtaa anakimbia na hela yake kaacha,nikajiuliza inakuwaje hapa?sijakaa sawa yule dogo akatoka mle ndani speed alikoswa koswa kugongwa na pikipiki.

Kwa ufupi,alikuwa amejaza spare battery terminals zile za gari kubwa zenye thamani ya Tsh 680,000/= kwenye boksi ya oil yenye thamani ya Tsh 56,000/= ambayo ndo nilikuwa nimelipwa mkononi!!utauwa mtu!!!mimi sasa hivi kama sipo office haifunguliwi acha nipate hasara ya siku kuliko kuamini tena mtu.
 
Back
Top Bottom