Nia ya mheshimiwa Rais ni njema, turekebishe mapungufu yaliyoonekana ili DPW aanze kazi haraka hapo bandarini.

Nia ya mheshimiwa Rais ni njema, turekebishe mapungufu yaliyoonekana ili DPW aanze kazi haraka hapo bandarini.

Manunuzi ya umma yanaruhusu single source ukiwa na justification. Haina tatizo kabisa, kwenye tenda huko hakufai sometimes.

Hao wanajaribu kung'olewa pale bandarini watakuja na makampuni yenye majina tofauti tofauti na watapenyeza rupia mpaka washinde tenda. Kisha business as usual.

Turekebishe tu ule mkataba usikae ki 'Mangungo', uwe na muda naalumu na kuwe na mechanism ya kuhakikisha pande zote zinawajibika.
Sheria za manunuzi ya umma hairuhusu kampuni kutoa ushawishi wowote ikiwemo rushwa ili kupewa tender, kuna taarifa hawa watu wamemwaga asali kwa baadhi ya wanasiasa na watendaji.

Kinachotakiwa ni hiyo kampuni kuwa blacklisted na siyo kuweka viraka kwenye mkataba wa kitapeli.​
 
Sheria za manunuzi ya umma hairuhusu kampuni kutoa ushawishi wowote ikiwemo rushwa ili kupewa tender, kuna taarifa hawa watu wamemwaga asali kwa baadhi ya wanasiasa na watendaji.

Kinachotakiwa ni hiyo kampuni kuwa blacklisted na siyo kuweka viraka kwenye mkataba wa kitapeli.​
Ni kweli. Hao jamaa ni wajanja sana, sio wao tu bali wawekezaji wote. Iliyokoukwa ni sheria ya maadili ya viongozi wa umma. Mwekezaji hana kosa, yes, kutoa zawadi nzito nzito kwa viongozi wa nchi fulani ili kurahisisha mchakato it's immoral but not illegal! kosa ni la waliopokea zawadi na kushindwa kuziwasilisha mahala husika.

Hako ka utaratibu ka wawekezaji kuwapeleka watendaji nje kapo sana nchini. Hata TRC bila shaka walikwenda Korea kabla ya kuwapa tenda ya kutengeneza mabehewa. Watu waserikalini huwaambii kitu kwenye hizo safari za nje.
 
Peleka huko uzwazwa wako!
Sisi tunasubiri hukumu ya Mahakama Kuu ya tarehe 7/8.
Kungekuwa na nia njema Watanzania wangejulishwa mapema na si kwenda kisiri Siri ughaibuni kusaini mkataba wa Kimangungo!
 
Mkuu uko sahihi lkn tatizo kubwa la nchi hii ni kuto kuwa na maadili na uzalendo kwa nchi yetu na kwa wa Tz wenzetu, hii imepekea kuwa kuwa wabinafsi tulio kubuhu.
Watu hatujali kabisa shida za wezetu hata kidogo, hatudhamini kabisa naisha ya watu wengine.
Na chukizwa sana na hii tabia ya ubinafsi
Hao wabinafsi na wezi wanawekwa na viongozi kwa nepotism. Viongozi wanaweka watu wao kwenye kila shirika linaloingiza pesa nyingi, hapo usitegemee ufanisi bali upigaji.
Katiba mpya iweka vigezo mahususi za kuongoza hayo mashirika, vijana wenye vipaji ndo washikirie mashirika yetu uone kama hayatasonga.
 
Ataweza kuwafukuza watoto wapendwa Mbarawa, Aisha na Johari! Sidhani na sitarajii.

Hivi kweli wewe unategemea Mbarawa, Ausha na Johari wanaweza kuwa maadui wa ndani ya chama wa mama?

Ufahamu kuwa inner circle yote ya kushughulikia jambo hili ilikuwa ya Wazanzibari. Unataka kuwaaminisha watu kuwa maadui wa mama ni Wazanzibari?
Wazanzibari wote hautaki muungano by nature. Kwa hiyo wakipata upenyo wa kuiumiza Tanganyika wanaiumiza kweli kweli. Hapo walikuwa hawafanyi kumkomoa mama bali kuikomoa Tanganyika. Matokeo yake sasa watanganyika wameamka, soon watarudi kwao wasubiri kisiwa chao kumezwa na bahari kama ilivyotabiriwa kwenye Qur'an
 
Kwani wenye mamlaka ya kurekebisha mkataba ni nani? Gharama na usumbufu wa kurekebisha mkataba DPW Hawatakubari kirahisi. Frame ya mkataba wa DPW haukuwa hivi ila mikataba ya namna hii ni kama kubet tu kadri unavyoongeza mechi odd zinaongezeka i.e mpunga unapanda kwa kasi wenye bonas. Sababu ya mikataba kuliumiza taifa ni hyo ya kutaka pakubwa kwa haraka
 
Nchi hii ina mambo jamani, yaani kuna vita zinaendelea chini chini huko ndani ya chama Mungu amsaidie mama yetu SSH.

Nia ya uwekezaji pale bandarini ni njema kabisa, dhamira safi kabisa. Ni uwekezaji unaokwenda kukata mirija wa watoto wa mjini ambao wamekuwa wakinyonya pale kwa raha zao.

Sasa nashindwa kuelewa, kwamba wahusika walipaswa kumsaidia Mh. Rais kwenye ule mkataba/ makubaliano ni vilaza au wamefanya makusudi kusaini yale madudu ili kumchafua Mheshimiwa?? Kwamba miongoni mwao wapo watu wa ile kambi nyingine ya chama ambao wameamua kumhujumu Rais kwa makusudi kabisa??

Mama SSH usiwe mnyonge, rekebisha mapungufu machche yaliyopo kisha wawajibishe wote waliosababisha taharuki hii kwa kutokutimiza wajibu wao na kupitisha mkataba ukiwa hovyo kiasi kile. Baada ya hapo kazi iendelee, tunahitaji uwekezaji wenye tija pale bandarini. Kama DPW anaiweza hiyo kazi na watafanya kwa uaminifu na kuhakikisha wale wahuni hawaigeuzi bandari kuwa shamba la bibi, why NOT? Tuwape wapige kazi.

Usisahau kuiweka mikataba wazi, itakusaidia usichomekewe madudu na wapinzani wako wa ndani ya chama. Inaonekana mtandao wao ni mpana.
Hata kwakutumia mikataba mibovu? ambayo jiwe allikataa
 
Samia ndo wa kwanza kusign, mkataba una sahihi yake, kwa mara ya kwanza Tanzania Rais ana sign mkataba hewa, lakini cha msingi ni kurekebisha, kuondoa vile vipengele tata na kuendelea na uwekezaji, shida kubwa ni ccm , badala ya kurekebisha wako busy kusomba watu waje kwenye mikutano kusikiliza makosa ambayo hawataki kukubali, unaona walivyo wajinga?

Kama Rais sio mjanja CCM ni raihisi sana kukuingiza King, mimi nashauri Samia asisikilize mapambio ya CCM angesikiliza watalaam wa sheria ambao hawa fungamani na chama , hapo ndo atajua ukweli.
 
Hakuna rahisi mbovu kama huyu.
Hakuna anachojua zaidi ya kusema na hili nalo mkaliangalie.
Serekale imekuwa ya kipigaji na wizi wa wazi wazi.
 
Peleka huko uzwazwa wako!
Sisi tunasubiri hukumu ya Mahakama Kuu ya tarehe 7/8.
Kungekuwa na nia njema Watanzania wangejulishwa mapema na si kwenda kisiri Siri ughaibuni kusaini mkataba wa Kimangungo!
😁😁😁
Ndugu yangu unaimani kubwa sana juu ya uwezo wa mahakama zetu kuitikisa serikali. Historia inaonesha mara nyingi waheshimiwa majaji hawana huo ujasiri.
 
Kwani wenye mamlaka ya kurekebisha mkataba ni nani? Gharama na usumbufu wa kurekebisha mkataba DPW Hawatakubari kirahisi. Frame ya mkataba wa DPW haukuwa hivi ila mikataba ya namna hii ni kama kubet tu kadri unavyoongeza mechi odd zinaongezeka i.e mpunga unapanda kwa kasi wenye bonas. Sababu ya mikataba kuliumiza taifa ni hyo ya kutaka pakubwa kwa haraka
Bado tuko hatua za awali, hawajawekeza fedha yoyote pale bandarini. Tunaweza kurekebisha au hata kuuvunja kama tutakuwa tayari kusema ukweli mahakamani juu wa viongozi wetu waliopewa 'zawadi' kule Dubai.

Kuomba mazungumzo na kurekebisha ni njia nzuri zaidi.
 
Back
Top Bottom