Nichague ipi kati ya Nissan Fuga New model au Toyota Crown new model

Nichague ipi kati ya Nissan Fuga New model au Toyota Crown new model

Inaonekana gari umeijulia ukubwani...kuna kitu kinaitwa "HKS Speed Limit Defencer" google halafu njoo usome hii post yake...tena...
Nisome nini kwamba ni uongo ? au unajifanya unajua sana tafuta hiyo ya kwako inayovuka ambayo siyo kubwa jinga
 
Nisome nini kwamba ni uongo ? au unajifanya unajua sana tafuta hiyo ya kwako inayovuka ambayo siyo kubwa jinga
Zipo zinazovuka mkuu... hii ni mark x ina 260kph
Screenshot_20220408-143327_Chrome.jpg
 
Haha, majesta ni habari nyingine mzee. Ila ile imekaa ki-don sana.

Inafaa kuendeshwa nasio uendeshe mwenyewe

Athlete, iko fresh pia , fuga ni moja kati ya gari kali sana, kuanzia interior etc

Naona tatizo kubwa ni sio "Toyota" tuu , hivyo hata mafundi nao ni kichomi.

Ila ni gari moja tamu sana. Kwa mwendo na kutulia barabarani, ndio yenyewe.
Kuna mdau humu anamiliki Fuga.

Sijawahi ona analalamika kuhusu hiyo gari.

Yeye fundi anatoa wapi? Spea nazo anatoa wapi?
 
Yani kuna watu bado wananunua magari ili washindane na watu wasiowajua barabarani??
Ni kituko sana. Barabara zenyewe za kukimbizana sijui ni zipi [emoji28][emoji28][emoji28]. Unakutana na mtu barabarani kakomaa akupite kumbe mwenyewe unaishia hapo mbele tu.. Mtu wa namna hii ukikutana nae either ana kiduku, kavaa suruali ya kubana kama za dada zake na zimechanika magotini.

Sent from my FIG-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Kuna mdau humu anamiliki Fuga.

Sijawahi ona analalamika kuhusu hiyo gari.

Yeye fundi anatoa wapi? Spea nazo anatoa wapi?
Mzee,

Binafsi siwezi kumsemea mtu, nimeongelea wingi na sio uchache.

Tukubaliane kwamba,

Ile kwamba wengi wanalalamikia jambo fulani, haina maana kwamba ni wote wanapaswa kulalamikia.
( Ama kinyume chake )

Ni sawa na kusema, kipindi vijana wengi wanalalamikia ukosekanaji wa ajira, haina maana kwamba wote hawana ajira, wapo baadhi ambao wanazo.

Kwahiyo, ukweli unabakia pale pale kwamba, "Watu tumetofautiana"

Naamini umenielewa,

ahsante.
 
Back
Top Bottom