Nifanye biashara gani ambayo naweza kuingiza laki moja kila siku

Nifanye biashara gani ambayo naweza kuingiza laki moja kila siku

Chukua milioni 10 fungua fixed akaunti NMB.
Milioni 10 iliyobakia nenda Silverland Tanzania/Silverland Dar nunua vifaranga aina y SASSO 1000 kila mmoja ni 1400, wafuge ndani ya miezi minne watakuwa wamekuwa wakubwa kweli kweli utauza kwa 15,000 au 20,000 kwa mmoja.
NB: SASSO ni kuku chotara wanaovumilia magonjwa na hali ngumu zote.

Gharama ya kuwahudumia SASSO 1000 pamoja na banda, madawa n.k havitazidi hata milioni 5.
Pia jifunze formula ya kutengeneza chakula cha kuku wewe mwenyewe ili kupunguza gharama.


Babu ufugaji wa kuku sio mwepesi kama ulivyoandika, tena vifaranga wanahitaji matunzo ya hali ya juu ukiwazembea hata masaa manne unaweza kuta wamekufa kama robo ya idadi uliyonunua, mpaka wanakua unakuta umekuza robo ya idadi ya uliyonunua mpaka hapo unakuwa ushaingia hasara bado hatujapigia gharama ya chakula na dawa ulizonunua, ikumbukwe hao ni vifaranga hivyo hakuna mayai hapo yaliyotagwa useme utauza mayai urudishe hela.

Kwa nadharia ni rahisi kweli ila ukiingia mzigoni utaona mziki wake, mbaya zaidi ukute mtu ndo mara ya kwanza umemshauri hivyo na hajawahi kufuga, hajui changamoto zake atajikuta anaua vifaranga vyote na kuanza kukuachia laana wewe uliyemshauri. Ukitaka kuamini ingia mtaani ufanye research kuhusiana na hilo ulilomshauri. It is not a win to win situation 100%
 
Babu ufugaji wa kuku sio mwepesi kama ulivyoandika, tena vifaranga wanahitaji matunzo ya hali ya juu ukiwazembea hata masaa manne unaweza kuta wamekufa kama robo ya idadi uliyonunua, mpaka wanakua unakuta umekuza robo ya idadi ya uliyonunua mpaka hapo unakuwa ushaingia hasara bado hatujapigia gharama ya chakula na dawa ulizonunua, ikumbukwe hao ni vifaranga hivyo hakuna mayai hapo yaliyotagwa useme utauza mayai urudishe hela.

Kwa nadharia ni rahisi kweli ila ukiingia mzigoni utaona mziki wake, mbaya zaidi ukute mtu ndo mara ya kwanza umemshauri hivyo na hajawahi kufuga, hajui changamoto zake atajikuta anaua vifaranga vyote na kuanza kukuachia laana wewe uliyemshauri. Ukitaka kuamini ingia mtaani ufanye research kuhusiana na hilo ulilomshauri. It is not a win to win situation 100%
Unajifanya 'pingapinga' wa kila kitu.

Mshikaji ameandika vizuri tu hapo juu kuwa, hao SASSO ni aina ya kuku chotara wanaovumilia hali ngumu na Magonjwa.
 
Unajifanya 'pingapinga' wa kila kitu.

Mshikaji ameandika vizuri tu hapo juu kuwa, hao SASSO ni aina ya kuku chotara wanaovumilia hali ngumu na Magonjwa.

Umewahi kuwafuga? Tupe mrejesho, ila kama hujawafuga huna evidence ukae kwa kutulia.
 
Umewahi kuwafuga? Tupe mrejesho, ila kama hujawafuga huna evidence ukae kwa kutulia.
Evidence ni maneno kutoka kwa mfugaji mwenye experience yake hapo juu. Amesha sema. Wewe ni nani upingepinge
 
"Nifanye biashara gani"
Ni swali gumu sana

Swali hili linaweza kujibiwa na
1. Unachopenda (Hobby yako)
2. Mazingira ulipo (Location)
3.Uzoefu (Experience)*
4.connection (network yako)
5.Mtaji
6.Muda (management) na
7.Watu (wasaidizi waaminifu)

Tafakari mambo haya 7 kwa kina.
Namba 4 na 7 nimuhimu sana kwani mtaji anao
 
Daah
Kuwa mpole sana kufanya maamuzi usije angamiza hela yako.

enewei nilikuwa najua mtu akikuita dear anakupenda nashangaa wewe unawaita watu dear, kumbe kishkaji tuu
nimetongoza wengi kisa kuniita dear tuu.
[emoji23][emoji23][emoji23] umenikumbisha mbali kidogo; kuna mdada moja wa kizungu niliwahi kufanya nae Kazi alikuja kama task force sasa kila saa tukikutana ananikonyeza; nikajisemea yes mtoto kanizimikia. Baada ya sikunkadhaa nikaamua kumtolea uvivu akachomoa nikamwambie sasa kwanini huwa unanikonyeza akasema kwo huko ni jambo la kawaida.
 
Uza samaki wabichi jumla jumla, kwenye masoko ya samaki,
Mfano niliwahi kufanya kaz jamaa mmjo, anachukua samaki wabichi ziwani kilo 250kg kwa 625k afu anaangiza mm nmuuzia soko LA samaki
Napata 1m au 900k ukitoa ushuru pamoja na nauri ya mzigo 150k

Faida unapata 100k hadi 150 na samaki wanaisha kwa usiku mmja maana soko linafunguliwa SAA nane usiku, na samaki huuzwa kwa kilo 1kg= 7k 5k 4k wadogo 2k


Changamoto kubwa upatikanaji wa samaki maziwani (hutumia hadi siki mbili kupata kg 250), kuhifadhi wasiharibike pamoja usafiri ndo shida
 
Uza samaki wabichi jumla jumla, kwenye masoko ya samaki,
Mfano niliwahi kufanya kaz jamaa mmjo, anachukua samaki wabichi ziwani kilo 250kg kwa 625k afu anaangiza mm nmuuzia soko LA samaki
Napata 1m au 900k ukitoa ushuru pamoja na nauri ya mzigo 150k

Faida unapata 100k hadi 150 na samaki wanaisha kwa usiku mmja maana soko linafunguliwa SAA nane usiku, na samaki huuzwa kwa kilo 1kg= 7k 5k 4k wadogo 2k


Changamoto kubwa upatikanaji wa samaki maziwani (hutumia hadi siki mbili kupata kg 250), kuhifadhi wasiharibike pamoja usafiri ndo shida
Ulkuwa unauzia wapi
I mean mkoa gani?
 
Uko wapi, una mtaji gani? Maana waweza kuwa Misigiri ukashauriwa vitu vya kufanya oysterbay Dar es salaam vya mitaji ya mamilioni wakati wewe una 150k tsh.
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hello nifanye biashara gani, lengo langu nipate angalau laki moja kila siku.

Binafsi napenda saloon ya kike lakini sina uhakika kama nitaingiza laki moja kwa siku.

Naomba Ushauri wenu tafadhali.
nitoe ushauri au ninyamase?? nijipuni bhasi nyie wana jf
 
Ukitoa milioni 2 na nusu tu na hiyo nyingine baki nayo nakupa biashara itakayokuingizia laki na elfu 20 kila siku. Uhakika Ni 💯 isiporudi nakurudishia hiyo hela. Nipm kwa maelezo zaidi na kujua hiyo biashara.
Nb Mimi pia nafanya hiyo biashara
 
Njoo inbox nikupe madini ya uhakika...

Ila inahusiana saana na kilimo, ufugaji, biashara za mobile money eg tigo pesa,

Uje unipe detail flani tupeane ushaur
 
Do not dare kuzika pesa yoote! Kuwa na back up pembeni ili awe mkombozi wako na mfariji baada ya busines kufail.

Ni Million 10 pekee ndani ya biashara tatu tofauti zenye usimamizi wa kina, kwa umakini uliotukuka unaweza kulaza 100K kwa siku.

Amini.
 
Back
Top Bottom