Nifanye ibada kwa njia ipi ili Mungu wangu ajibu maombi yangu kwa haraka?

Nifanye ibada kwa njia ipi ili Mungu wangu ajibu maombi yangu kwa haraka?

Huba imani ndio maana unataka kumuwahisha Mungu kukujibu. Kama unataka kujibiwa kwa muda uutakao wewe nenda kwa shetani
Mkuu wewe maishani mwako haujawahi kujibiwa jambo lolote lile na mwenyezi Mungu kwa wakati ule ule uliohitaji kujibiwa? Mbona wengi tu hii imetutokea.
 
Hakika utajua hujui, na utajuta kuzaliwa kama mpaka sasa hujui maombi yako yanatakiwa yaweje na Umuombe Mungu yupi ama MUUMBA.

Nasemaje Muumba hataki rushwa wala kupelekeshwa labda kama unataka short-cut ni kwa waganga na wapiga ramli, ama jibiidishe haswa.

Huyo Mungu wa makanisan na misikitin utaomba kwa kila style mpka utapiga goti hewan kamwe hatojibu maombi yako ng'oo labda umpe rushwa[emoji23][emoji23].

Target ya maombi yako ukiyaelekeza kwa Muumba wa kweli anayekujua na anaepaswa kuombwa basi shida yako itatatulika kwa wakati.

Jibiidishe kutatua hilo tatizo, fungua akili yako ione fursa ama njia mbadala wa kusolve na ikishindikana hamia kwenye maombi, na maombi simaanishi haya ya wapiga makelele walokole wa wavaa kobazi, i mean maombi yanapotakiwa.

Babu zetu wakifufuka leo hii watatupiga fimbo za kutosha maana mambo madogo tumekuwa tukishindwa kuyatatua either kwa kukosa imani ama kuabudu sehem zisizo sahihi.

Na hii ni kwa wote mnaopoteza muda wenu makanisan na misikitin, huko kamwe hakuna majibu zaid ya utapeli na mazingaombwe[emoji23][emoji23].

Ukweli mchungu
 
Mwenzenu nina shida ya haraka, ambayo nikiweza kutatua ndani ya siku 3, maisha yangu yatakuwa yamefunguliwa upya. Kila nikiwaza binadamu gani wa kunisaidia simuoni. Tumaini ninaloliona ni kupata msaada toka kwa Mwenyezi Mungu. Wana bodi, Nifanye ibada gani Ili Mungu anisaidie kwa uharaka?
Maombi ambayo hujibiwa haraka sana bila kuchelewa ni maombi ya dhati ya toba ya kweli ( yaani maombi ya kutubu dhambi uovu na makosa full stop) lkn haya ya kufanikiwa sijui kazi sijui laan au ajali na mengneyo MUNGU hajui kuchelewa au kuwah hapangiwi anaweza akujibj au asikujibu kabisa , au ajibu kwa kuchelewa au kuwah...........1☺😊😇😋
 
1.OKOKA, MPE YESU MAISHA YAKO

2.TUBU DHAMBI NA KUZIACHA

3.SOMA NENO LA MUNGU

4.KUWA MTU WA MAOMBI KILA SIKU

5.TAFUTA KANISA LA WATU WALIOKOKA UJUMUIKE NAO
Umemaliza mkuu, hapa ndio nilipomuona YESU KRISTO katika maisha yangu.

Ninafura ninafuraha ninafuraha...

Nimeonja Utamu wa YESU KRISTO
Rose Muhando
 
Ndiyo. Unataka nikupe connection ya wajenzi huru?
Halafu inaonekana wewe ni customer care kwenye kampuni ya simu. Mzee wa kufowadi sms za matangazo hata kama ni usiku wa manane, wewe ni kubonyeza tu kitufe cha kufowadi
 
Mwenzenu nina shida ya haraka, ambayo nikiweza kutatua ndani ya siku 3, maisha yangu yatakuwa yamefunguliwa upya. Kila nikiwaza binadamu gani wa kunisaidia simuoni. Tumaini ninaloliona ni kupata msaada toka kwa Mwenyezi Mungu. Wana bodi, Nifanye ibada gani Ili Mungu anisaidie kwa uharaka?
Kwanza ni vizuri unatambua kuwa Mwenyezi Mungu ni muweza wa yote.

Pili, tambua vile vile usikome kumuomba Mungu wakati wote. Mungu hakawii wala hawahi, kwake muda ni irrelevant.

Wengine sisi tulimuomba kwa miaka 25 na tukafanikiwa.
 
Funga na kuomba masaa kumi na mbili tu , ukiomba usiombe tu ukitakacho pia uombe mapenzi ya Mungu yatimizwe katika hilo uombalo .

Baada ya hapo endelea na mambo yako
 
(Anyone can) TRY THIS!!

1 Asubuhi kabla jua halijachomoza nenda njia panda (sehem ambapo njia/barabara zinatengeneza +.

2 Simama kwa kuangalia mashariki (jua linapochomoza)

3 Fumba macho, Sali ile sala ya BABA YETU ULIE JUU MBINGUNI....(ukimaliza hii sala)...

4 Muombe Mungu (unaemwamini wewe binafsi) ukimuelezea shida yako.

Baada ya hapo rudi nyumbani/ endelea na siku yako kama kawaida.

Ni kitendo cha dakika 1-2
Anaekukuta hapo njiapanda ndo shida itaanzia kuwa mchawi
 
Kwaiyo wewe ni mjenzi ambaye ulikuwa umefungwa na sasa upo huru(freemasons). Je ulifanya kosa gani kwenye icho chama mpaka ukafungwa, ulipindisha nyumba ya watu, uliiba cement au uliiba matofali au nondo, au ulikula posho ya mafundi wenzako?

Acha ngonjera, unataka connection uuage ufukara au hutaki?
 
Acha ngonjera, unataka connection uuage ufukara au hutaki?
mzee wa customer care kwenye kampuni ya simu. We endelea tu na kazi yako ya kufowadi hizo sms za wajenzi huru mpaka usiku wa manane fowadi tu mzee maana ndiyo kazi uliyoichagua. Usiishie tu kufowadi hizo sms sasa inakupasa ujiunge nao ili na wewe utoke hapo kwenye hiyo kampuni uwe elon musk wa bongo
 
Kuwa na Tabia ya kutoa sadaka na kusaidia maskini na yatima. Kwa kipindi hiki ungeshangaa Tu kuna kitu kinatokea. Mungu akusimamie ushinde jaribu lako unalopitia.
 
Acha ngonjera, unataka connection uuage ufukara au hutaki?
Wewe tangia umejiunga hatujawai kukusikia umekua bill gates wa bongo umebaki palepale ulipokuepo mwanzoni kufowadi sms. Hizo connections wape rafiki zako, hawara zako, wake zako pamoja na mitoto yako shwain wewe
 
Mwenzenu nina shida ya haraka, ambayo nikiweza kutatua ndani ya siku 3, maisha yangu yatakuwa yamefunguliwa upya. Kila nikiwaza binadamu gani wa kunisaidia simuoni. Tumaini ninaloliona ni kupata msaada toka kwa Mwenyezi Mungu. Wana bodi, nifanye ibada gani Ili Mungu anisaidie kwa uharaka?
kuna siri moja wengi hawaijui. nayo ni hii; MAOMBI YENYE UHAKIKA KWAMBA YAMEFIKA KWA MUNGU NA MUNGU ATAJIBU, NI MAOMBI KWA ROHO MTAKATIFU, YAANI YA KUNENA KWA LUGHA. achana na lugha za kuiga, na lugha ambazo sheteni anawajaza watu ili wajione kama wamejazwa kumbe sio, ile inayotokea kwa hakika, baada ya mtu kuokoka, ametakaswa akajazwa Roho Mtakatifu na kunena kwa lugha, na moyoni unashuhudiwa hivyo. maombi hayo ni 100% yanajibiwa yote. why? kwasababu ni Mungu mwenyewe anakusaidia kuomba (Roho Mtakatifu) na utaomba sawasawa na mapenzi yake.

Warumi 8:26 - 27 INASEMA; Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa. na yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho ilivyo, kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu.

Wagalatia 4:6 Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba.

hii inaweza kuleta discussion ndefu sana kwasasbabu wapo wanaopinga kabisa ujazo wa Roho Mtakatifu, wapo wanaomkataa kabisa kama wakatoliki na wengine. wanaamini wao wanaweza peke yao, na kujazwa wanasema sio lazima kwasababu wanamini hicho ni kipawa mtu mmoja aweza kupewa na mwingine asipewe, wakati Yesu alisema bila huyo hatuwezi kufanya lolote.

kwa ushauri, unaweza kuomba kwa akili, na unaweza kuomba kwa Roho Mtakatifu (kunena). ila maombi ya Roho ni asilimia mia yamefika na yatajibiwa, ya akili ni machache hata yakifika yatajibiwa kwasababu akili yako utaomba kwa tamaa za mwili wako na hauwezi kuomba sawasawa na mapenzi ya Mungu. Okoka, mpe Yesu maisha yako, omba akujaze Roho Mtakatifu, naye atakusaidia kuomba na atakuwa Mungu wako.

Waefeso 2:20-21
inasema, Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yale tuyaombayo au tuyawazayo kwa kadiri ya Nguvu itendayo kazi ndani yetu. (hiyo nguvu itendayo kazi ndani yetu sio ya kibinadamu ni Nguvu ya Roho, hapa anaongelea watu waliookoka na kuishi na Roho Mtakatifu, sio watu wote, kwasababu ni wale waliookoka na kuongozwa na Roho tu ndio wana hiyo nguvu).
 
Back
Top Bottom