RESILIENT KATO
JF-Expert Member
- Aug 21, 2024
- 1,472
- 2,766
Uzuri mimi sina kupimo cha kujua kama K imetumika je wewe mwenzangu ila hizo video zina shawishi kutumika, hahaaaKitu kixito kimeshatua ila naona hakijakujeruhi sana na unayo nafasi ya kutoka japo kitakuachia majeraha madogo.
Muhoji haya maswali kuweka mambo sawa.
Ni kazi ndio ilimpeleka Dar au ni hilo jambo?
Nini kilipelekea akaacha kazi baada ya miezi 9?
Nini kilifanya akafuta hizo picha (ipo motive mpaka akafuta)
Kwakua aliindoka kama mchumba wako unayo haki ya msingi kujua kila kitu kuhusiana na hizo picha.
Kutumika tunajua wanatumika wakiwa mbali na sisi lakini linapokuja swala la kupata ushahidi ndio unajihakikishia hapa mali imeliwa kweli. Hapo kwa hizo picha unataka kusema waliishia kushikana shikana tu?Uzuri mimi sina kupimo cha kujua kama K imetumika je wewe mwenzangu ila hizo video zina shawishi kutumika, hahaaa
Apotezee ila hizo picha zinatosha kumu disciplineNyakati zenu zimeisha!
Mwambie hivyo,muonyeshe na picha kwamba Kwa hizi sitokua na imani na wewe Tena maishani tuachane kistaarabu!
Au potezea muishi kisamaria tu!
Duu ila hapo patamu kwa maana hilo jambo nilahisia za muda mfupi tuKutumika tunajua wanatumika wakiwa mbali na sisi lakini linapokuja swala la kupata ushahidi ndio unajihakikishia hapa mali imeliwa kweli. Hapo kwa hizo picha unataka kusema waliishia kushikana shikana tu?
Naamin kakaHawa wanawake bhana duuh kuna jamaa ni ticha juzi kati kakosa kufa na BP sababu ya mke yaani mke alikuwa anatoka na kishikaji ambacho kilikuwa kihawala cha binti wa huyo mama tena kimempa had mimba binti yake daah Yan ni hatareee ticha BP ilipanda had akawa anatoka had damu puani ikabidi serkal ifanye mpango wa kumhamisha ticha kwenda mko mwingine akae mbali na mke wake binti Nae katoroka hajulikani aliko..........kiufupi tu baharia mwenzangu piga chini huyo hiyo ni alama ya check ingine ogopa sana
Amehisi jua baada ya mwamvuli kuondolewa!Sasa kwann simu za plz n nyingi baada ya kumrudisha kwao?
Hapo jua la milele na limuangazie tu. Nmejarb kufikiria namna ya ku cope na hali lkn nmeshndwa. Aende kwa kwelAmehisi jua baada ya mwamvuli kuondolewa!
Hawa viumbe ukiwa nao wanakula na kishiba plus kulala na mahitaji yanapatikana Huwa wanaona si kitu kabisa hawaridhiki Hadi wapate MTU Bora zaidi ndio huondoka au wakiachika ndio wanajua umuhimu was MMe!
Inapendeza kwamba tumebadilishana uzoefu, (life learning experience), hawa wanyama wako wengi sana unahitaji subira tuImepitishwa hii mkuu
Hii nzuri...Kwanza kabisa,
Wewe na huyo mchumba wako mna mikakati gani kuhusu zoezi muhimu kabisa la uchaguzi wa serikali za mitaa?
Tuanzie hapo kwanza mkuu.
Nimeipenda hii,huwa napenda kusema usitafute mambo ambayo ukiyajua yatakuhuzunishaMkuu una uhakika umepekua vizuri Kwenye hiyo trash ya simu yake?
Mbona Kama hujaangalia picha zote zilizomo Kwenye trash ama umeamua kufanya Siri sisi tusijue Kila kitu?
Enewei, wanasemaga mwana kulitafuta mwana kulipata.Wewe wakati uliingia Kwenye trash ya simu ya mwenzio ulitegemea kukutana na Mambo gani tofauti na hayo uliyoyakuta?
Masikitiko.Habarini wadau.
Niende moja kwa moja kwenye mada...
Huyu mrembo wangu nimekuwa naye kwa zaidi ya miaka mitatu. Kabla hatujaanza kuishi pamoja alipata kazi mkoa wa mbali kidogo (dar) na hapa ninapoishi mimi (Arusha). Alienda na alifanya kazi hio kwa miezi 9 tu kisha akaachana nayo na kurudi nilipo mimi na kuendelea na shughuli alizokuwa akifanya kipindi cha nyuma.
Kwa vile tulishatambulishana na mahari nimemtolea sikuona vibaya kuanza kuishi nae kabla ya ndoa. Alibeba kila kilicho chake na kuhamia kwangu rasmi.
Juzi wakati tukiwa kwny stori za hapa na pale, aliomba kuangalia simu yangu ninayoitumia. Sikuona tabu nikampatia, cha ajabu hakuhangaika na vilivyomo ndani, badala yake alitoa kava na kuikagua jinsi ilivyo kwa nje kisha akatabasamu na kusema kuwa ameipenda, na kama haitakuwa noma tubadilishane simu.
Sikuwa na neno coz namjua anapenda sana show offs. Japo yake pia n simu kali ila nilimkubalia. Tukahamisha details muhimu then tukabalilishana simu.
Jana nlipotoka job sikuwa na la kufanya, nikaona si mbaya nipitepite kwa simu hii niizoee mkononi.
Nlijikuta nmefika kwny trash (zinapohifadhiwa picha na video zilizofutwa kabla ya kufutika mazima).
Nilikutana na picha nyingi sana za mwanamke wangu akiwa ktk moja ya fukwe maarufu sana dar na alipiga kipindi ambacho alienda huko alipopata kazi aloifanya kwa muda mdogo na kurejea mkoani. Amevalia nguo ambazo hata mimi sijawah kuziona.
Pia zipo video akiwa na jamaa flan hv wakibebana na kucheza kwenye mchanga wa Beach wakiwa nusu uchi.
Hapa nimepigwa butwaa sielew nichukue maamuzi yapi kwa sasa. Bado sijamwambia chochote had sasa.
Maoni yenu n muhimu wakuu.