Nifanye nini Mume wangu aache pombe na sigara? Hakuwa hivyo zamani

Nifanye nini Mume wangu aache pombe na sigara? Hakuwa hivyo zamani

images (2).jpeg
feelings
 
Siku akiamua kuacha pombe ataacha mwenyewe bila shuruti.

Kuna muda mimi nilikuwa naagiza pombe nanywea nyumbani nalewa hadi siku ya pili nakuwa mgonjwa, hata kuongea nakuwa naongea huku natetemeka, yaani hata nikipigiwa simu sipokei kwa kuhofia kugundulika sauti. Lakini siku hizi nakaa hata siku tatu bila kunywa.
 
Amevurugwa kisaikolojia huyo;jitahidi kuzungumza naye kabla hajalewa,ili uweze kugundua tatizo ni nini
 
Mna ndoa ya kanisani, msikitini au selikarini? Na chanzo cha kuanza kulewa na kivuta sigara ni nini? Isije kua wewe ndo chanzo.
 
Yaaani zamani hakua hivyo alikua naakunywa kistaarabu ila sasa amekua mlevi ambae hataki hata kuoga yaana kama karogwa vile msaada nipate dawa au mawazo nijue chakufanya maana ndoa imekua ngumu
Nunua pombe anayoipenda nyumbani kisha tia maziwa mabichi/fresh kwa pombe hakikisha hakuoni! Akinywa hatorudia kabisa..
 
Yaaani zamani hakua hivyo alikua naakunywa kistaarabu ila sasa amekua mlevi ambae hataki hata kuoga yaana kama karogwa vile msaada nipate dawa au mawazo nijue chakufanya maana ndoa imekua ngumu

Unavumilia vipi kuwa na mpenzi ambaye kuoga tu ni shida?.
 
Nunua pombe anayoipenda nyumbani kisha tia maziwa mabichi/fresh kwa pombe hakikisha hakuoni! Akinywa hatorudia kabisa..

Mdanganye tu mwenzako,mimi hua tunatoka ulevini nikifika home wife ananipa nusu lita ya kikombe cha maziwa(tukijipa moyo yanaenda kuondoa sumu) nayagonga naenda zangu kulala.Hakuna cha kutapika wala kujisikia vibaya.
 
Pole sana kwa changamoto jaribu kukaa naye muongee kwa kina ili mpate kujua tatizo liko wapi, pia muweke kwenye maombi Mungu akusaidie katika changamoto unayopitia.
 
“Zamani hakuwa hivyo alikuwa anakunywa kistaarabu”

Hapo ndio kuna dosari, je kuna nini baina yenu najua ni ngumu sana baadhi ya watu kusema ukweli hebu funguka
Ina maana zamani mlikuwa hamna tatizo ila limekuwa zito kwake na kaamua kujipumbaza kwa ulevi wa ziada
Kutokuoga ni msongo wa mawazo
Hapo labda kipato chake hakutoshi kwa demand zako kubwa
Huenda umekuwa na matumizi mengi ambayo anashindwa kukupa kwa kutokana na kipato

Matatizo mengi huwa ni finance hebu kuwa mkweli na ubadilike
Au labda kuna watu wa karibu yako wanaishi na nyie na hayupo Radhi ila anakuheshimu sana

Kwa kweli mpaka tusukie ukweli wako hatuwezi kuamua bali assumptions tu

Msaidie sana na kama ni wewe jirekebishe
I wish ningekua na hizo demand bt sina coz namsupport kwa kila kitu toka ameyumba kiuchumi
 
Back
Top Bottom