Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Huyu anatupangaHii ni jinsia gani?? Utakuwa na matatizo ya akili!
Hivi huyu mwanamke ananichukuliaje?
Wakuuu hivi binti ananionaje? Kwamba ameniona mie zuzu? Au yaani aisee kila siku matusi na vipigo kutoka kwa mke wangu bila sababu yoyote ile na pia maneno ya kashfa kila siku eti kwamba mimi ni mwanaume suruali aisee nimechoka kabisa aisee Yaani kuna siku alikuwa anataka kuondoka hapa nyumbani...www.jamiiforums.com
Nina tattoo makalioni, mume wangu kuniambia nitafute mwanaume mwingine
Wakati niko chuo nilikuwa na rafiki zangu wawili ambao tulikuwa tunaaka chumba kimoja. Ni watu wa kujirusha, na kipindi hicho tulikuwa wazuri sana. Mambo yalikuwa mengi na tulifanya ujinga mwingi. Kuna mambo mengi nilifanya kipindi hicho ambayo mpaka leo najutia, lakini kuna hili moja ambalo...www.jamiiforums.com
Alinisaliti nimebeba mimba ya mwanaume mwingine ananiambia niitoe ili anioe
Wakuu naombeni ushauri wako, sijui nifanye nini. Mimi ni binti wa miaka 23, nipo chuo mwaka wa pili naingia watatu. Naomba ushauri wako, mwaka jana nilikuwa na mpenzi wangu, ni mwanafunzi mwenzangu, lakini tukagombana tukaachana, na yeye akamchukua rafiki yangu. Nikiwa katika maumivu, nilikutana...www.jamiiforums.com
Nimeibiwa pesa zangu milioni 5 asubuhi hii Stendi ya Singida
Hii ni mara ya pili naibiwa pesa kwenye stendi hii ya singida mara ya kwanza niliibiwa laki tatu stendi hii ya singida aisee sasa naona watu wa singida mmenizoea sana aisee na mniibia kwa style ile ile tu sijui nyie watu niwafanyia nini aisee Kuna siku mmwamenivunjia kioo cha gari langu crown...www.jamiiforums.com
Sina furaha na ajira yangu, natamani kuacha. Je, nitaachaje?
Wadau, kusema za ukweli sina hisia na furaha kwenye ajira yangu japo nipo muda mchache tokea nimeajiriwa ila hisia na ile furaha ya ajira haipo tena yaani nafanya kazi tu ili siku ziende tu nachukia kufanya kazi labda ni sababu ni wilaya niliyokuwepo. Nilikuwa kwenye shirika x mkoa x baada ya...www.jamiiforums.com
Ushindwe. Tafuta mwanaume mwenye hela na anayejali kama huyoNJIAPANDA; NIFANYE NINI NAMTAMANI KAKA YANGU!
Nina miaka 33, sijaolewa na sasa hivi siko kwenye mahusiano, iko hivi, mimi nafanya kazi na kipato changu ni kizuri tu. Naishi kwa Kaka yangu, si Kaka wa tumbo moja bali ni mtoto wa Mama Mkubwa ila tunaishi kama ndugu.
Huyu Kaka ana kampuni yake, kipato kikubwa na yeye na mke wake wote ni wafanyakazi wakubwa sana serikalini. Sababu ya kuishi hapa nikuwa ndugu hawampendi huyu mwanamke, ni mbinafsi na si wale watu wa kujichanganya, yaani kwa kifupi ana dharau.
Anatudharau sisi ndugu wamume wake, ni kama mume wake kazaliwa peke yake, yaani hata Mama mkwe anmdharau, hata mimi ninayeishi hapa hatupatani kila siku nikugombana.
Shida nikuwa, nikitaka kuondoka ndugu wananikatalia kwa madai kuwa nilinde mali za Kaka kwani nikiondoka anaweza kumuua. Kaka ni mtu wa kumsikiliza sana mke wake, huwezi kumuambia kitu atakuamini, yaani kila kitu anafanya na mke wake, huwezi amini haata nyumba kaandika majina yao wote.
Hali hiyo inawafanya ndugu kuona siku Kaka akifa basi kila kitu atachukua wifi. Mwanzo nilikua najisikia vizuri kukaa hapa nikiamini wataachana lakini sasa hivi naona kama napoteza muda, kila mahusiano ninayoingia yanafutika kwakua sina uhuru na mwanaume wangu.
Nakua bize kazini an weekend natoka na Kaka sasa mwanaume labda nikumuambia tuongozane mimi na Kaka na wifi hataki. Tunagombana tunaachana, sasa nimechoka hii hali ila nawaza hivi nikiondoka hizi mali zitaishia wapi.
Kitu kingine ambacho kinanisumbua nikuwa nsihaanza kumpenda Kaka yangu kimapenzi, yeye hajui ila nikimuona namna anavyoishi na mkewe, anamjali natamani anijali mimi, natamani kuishi kama yeye hivyo nikipata mwanaume hajali kam kaka nakua na hasira sijui nifanye nini hii hali iishe!