Nifanye nini nipate hati ya kusafiria baada ya haya mazingira kujitokeza?

Kama mmoja wa mzazi ni Mtanzania kuzaliwa Tanzania Kuna kupa haki ya kuwa Mtanzania.
Raia wa nchi mbili hadi ukifika mwisho miaka 18 unabaki na uraia wa nchi utakayo chagua.
Wote wamezaliwa hapa na Mimi nimezaliwa Moro
 
Pia na kuangalia usalama wa nchi pia kutotoa pasipoti kwa wasio watanzania.
Kama upo chini ya miaka 18 hata zaidi still mzazi au mtoto yeyeto anaweza akakublock usipate passport hata uchunguzi ukithibitika.
 
Jamaa haelewi
Cheti Cha kuzaliwa
NIDA number anayo ? N so forth
Km hana mwambie alipie magendo apewe passport
✍️
Kama kakamalika magendo ya nini kulipia haki yake.
Magumashi ngumu siku hizi mifumo inasomana
 
Kama kakamalika magendo ya nini kulipia haki yake.
Magumashi ngumu siku hizi mifumo inasomana
Mzee mwenzangu hawa wadau watakupa haki yako lakini wataichelewesha lengo ni uilipie tu ukilipia tu unaipata chapchap usipolipia unajifanya kichwa ngumu nenda rudi zitakua nyingi
✍️
 
Kuna Mzee Mmoja wa Kihaya Ghorofa ya Pili ( BMC ) anaitwa Afande Katema au Katemo kama sijakosea huyu hana tu Roho Mbaya ila ana Wivu mno na Maendeleo ya Watanzania wanaotafuta au wanaopata Kazi nje ya nchi.

CGI Dkt. Anna Makakala amuondoe hapo.
 
Mkuu tayari nishakata nikapigwa na picha yani kila kitu nimefanya .lkn jamaa ndo kaishikilia
Ukijaribu kuangalia maombi yako kwenye mfumo kupitia reference number inaonesha jibu gani?

Pili, Baada ya kupiga picha waliandika tarehe gani utegemee kukamilika kwa hati yako ya kusafiria?

Na ikiwa ofisa mmoja ananongwa, inawezekena ofisa mwingine akaifanyia kazi ombi lako. Tafuta ofisa mwingine mpatie application number ya ombi lako anaweza kukusaidia.

Kwa wadau wa hapa, ukijibu swali la kwanza na pili tunaweza kukupa namna ya kutatua changamoto yako.
 
Niliambiwa nikachukue 24/5/2023
Pia kwenye system aliyeshikilia ni yule afisa aliyenihoji.sabab yeye anadai Mimi siyo raia kwahyo anampelekea taalfa pco na pco hawezi kufanya maamuzi sabab taalifa anapokea kwa yule jamaa wa mwanzoni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…