Nifanyeje ili mbwa wangu wawe wakali?

Ni jamii gani ya mbwa. Watakuja watu hapa watakudanganya uwalishe pilipili au bangi au kila aina ya nadharia. Wadharau. Kuna jamii ya mbwa hawawi wakali. Chukuwa breed nzuri hao ni koko. Ukiwachanganya inaweza kusaidia.
 
Kwa hawa wa kibongo bongo rahisi sana kwanza mchana afungiwe na ahudumiwe na watu wasiozidi watatu alafu usimzoeshe kula kila saa ale mara moja kwa siku ule muda unaomfungulia aanze ulinzi ndo uumpe chakula ale ashibe.

Ukimzoesha hivyo huwa hataki mazoea na kiumbe yoyote zaidi ya wale wanao muhudumia
 
Fanya yafuatayo mbwa awe mkali.

1.Asionane wa watu ,na harufu za watu mbwa anafunguliwa saa 4 usiku sio saa 12.

2.Mnunulie mbwa mpira(Raba) ya kuchezea Au wanaita mswaki wa mbwa.

3.Mbwa analiashwa Mara moja lakini chakula cha kutosha. Usiku.

.Usisahau chanjo na madini ya vitamu I vya mbwa.
 
Wanakula na kushiba?, sio wanashindia jalalani na kula pampaz zenye vinyesi.
 
Wapambanie
 
Asante kwa ushauri
 
Inasikitisha sana! Tafuta mbwa mkali japo mmoja, hao wengine wataiga tabia kwake na kuwa wakali pia.
Mimi ninao sita na hawauzwi ni wa ulinzi katika himaya yangu na hapatiliki mguu, wameshang'ata watu kadhaa ila ni kwa makosa yao wenyewe.
 
Kabla sija kushauri hao mbwaa ni breed gani kwanza pia mbwaa afundishwi ukali iyo ni natural kwa aina ya mbwaa sasa chagua ubaki na ao mbwaa wako wa mtaani kwenu au nikuuzie rottweiler pure bread acheki na kima
 
Wafungie kwenye chumba hakina mwanga tafuta bangi weka kwenye kifuu kisha washa wakiwa ndani ya hiko chumba. Utakuja kunishukuru
 
Walishe mchanganyiko wa bange mbichi na Mavi makavu ya binadamu hasa wale wanaokunyaga porini
 
Mimi naona tatizo la mbwa wako sio ukali ila tatizo lao hawana ujasiri. Sasa angalia njia utazotumia usijetengeneza tatizo zaidi maana mbwa mkali asiyejihisi salama ni hatari zaidi anakuwa ni useless mbwa kichaa.

Kitendo cha wao kuogopa watu ni kumaanisha wana historia mbaya na watu inawezekana walishapitia mateso huko nyuma, je uliwafuga tangu wadogo?

Vipi kuhusu historia ya wazazi wao nao walikuwa waoga?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…