Nifanyeje nizoeane na majirani?

Nifanyeje nizoeane na majirani?

Dah hio phobia hata mie ndio inanitesa ila mkiwa na watoto wakawa wamejenga urafiki inaboost mahusiano yenu
Hakuna kurogana so unaweka mipaka binafsi Kuna mmama mmoja nilimkataa live Mana Tabia yake sikupenda. Anaongea majirani walivyo na Tabia zao. Nikajua na huyu namie atawaambia wengine nilivyo. Na ndiye aliyenifanyia usafi wa nyumba wakati nimekamilisha.akataka ukaribu Sana nikamkataa. Saivi nasikia ananisema kuwa natembea na jirani mmoja ivi kisa wakati anafanya usafi aliona Nampa ndio moja ya rangi tupu.yeye aliomba nikamtolea nje nikamwambia ndo naanzia maisha jamani.
Huku hajui huyo mdada yeye aliniokoa na nini
 
Mkuu watu ambao hatuna mazoea na wengine huwa tunadhani hawa wengine hawatuoni kumbe wanatuchora tuuu.

Ulichosimulia kimenikuta na mimi...


Kuna siku nilienda dukani kuulizia kitu flani hapa ahpa mtaani,sasa nikaambiwa kile kitu hakipo,

yule muuzaduka kumbuka kuwa simjui jina ila tunajuana kwa sura tu

Basi wife akaenda baadae kuulizia tena kile kitu alafu alikuwa amevaa nikabu(ninja) katika duka lile lile.

Muuza duka akamuambia "hiki kitu sina na mumeo katoka kuulizia muda sio mrefu"

Wife alichoka akasema wamejuaje kuwa mimi na wewe ni wanandoa wakati ni mara chache mno huwa tunafuatana tena tukifuatana basi tunaenda safari na sio kuzunguka hapa mtaani na ajabu zaidi wife huwa anavaa ninja mara nyingi lakini bado wakamjua kwamba huyu ni mke wa safuher.

Hivyo mtaani watu wanakuchora tuu unaweza dhani hawana deta zako zozote vile wanavyojikausha ukiwa umekutana nao.
Binadamu lazima amjue binadamu mwenzake hata Kupitia kwa wengine.kuna muda watu wanakujua mpaka uvunguni mwako
 
Dah hio phobia hata mie ndio inanitesa ila mkiwa na watoto wakawa wamejenga urafiki inaboost mahusiano yenu
Kabisaa mkuu mimi nina fomula yangu moja naiita "acha nature ichukue nafasi"

Nature ya kwanza ambayo itachukua nafasi ni kusalimiana.

Nature ya pili ni kuzungumza kwa mujibu wa muktadha wa nyakati hizo.

Nature ya tatu ni kuongea pale inapobidi,mimi suala la kusema nnatoka naenda kwa mtu kwa lengo la kupiga stori alafu hatuna miadi ya kukutana siwezi aisee.
 
Nadhani watu wengi hawajagundua hili au hawajijui.
Nilichogundua ni watu wengi wabinafsi na wanataka kunyenyekewa.

Mfano wewe unasuffer na roho yako pia kuhangaika kutengeza ujirani na salamu.
Je umejiuliza kwanini wao mpaka leo hii hawajaja kukusalimia?
Kwanini wao ndani ya muda wote wasianze wao uanze wewe?

Majibu yako mengi ila kukusaidia ni labda kwa sababu hawagive a damn about ujirani wala salamu.

Mfano mimi kwenye shida naweza kusaidia mtu yoyote ambaye simjui ila shida ikitokea kwako kwa sababu hawakujui trust me hakuna mtu atakusaidia.

Majirani sio solution ya matatizo unayoyafikiria.
Ni kama Murphy's law.

Murphy's law inamaanisha "anything that can go wrong will go wrong".
Lakini hiyo siyo maana pekee bali pia inamaanisha"chochote kinachoweza kutokea lazima kitatokea" na hutoweza kukizuia.

Strange thing ni watu wengi wanadhani kuwa na majirani ndio itaweza kuprevent bad things au kusaidiwa pale kitu kibaya kitakapotokea, which is wrong and impossible.

Na hiyo inapelekea ile definition ya "Uoga wa Maisha" kuwa applied on this circumstance. It's like the act of seeking security.

Na hiyo ndio sababu kubwa ya watu wengi kutafuta majirani kwa ulazima.
Na wengine wakishauri hivyo kwenye hii thread

Naamini ujirani hauwezi kuwa created deliberately bali ni kama nature's coincidence.
Na kulazimisha itepeleka baadae kukosana au kuonekana mnafiki na kero kwa wengine na hali itakuwa mbaya zaidi.

Personally mtu huyo ningemuona irritative.
Lakini sisi binadamu ni tumetofautiana so it depends.

Sidhani kama umewahi kuishi nje ya africa lakini ungepata tabu kuishi USA sababu asilimia kubwa ya watu ni minding your own business.

Bytheway hiyo ilikuwa opinion yangu even though it's a Fact.
 
Eeh tabia ya kufunga vioo nayo sio hio! Mie huwa napenda kusalimia tu majirani ila sipendi mazoea nao 😅😅😅
Kweli mkuu muhimu sana kuwasalimia, ila ukishawasalimia ni ngumu kukwepa mazoea pia.
Ngumu sana kuishi kishua kwenye mtaa wa kiswahili, ukishindwa hamia ushuani. Kule no time for bullshit mnapishana kwa ma-indicator tu na mahoni 😂
 
Hakuna kurogana so unaweka mipaka binafsi Kuna mmama mmoja nilimkataa live Mana Tabia yake sikupenda. Anaongea majirani walivyo na Tabia zao. Nikajua na huyu namie atawaambia wengine nilivyo. Na ndiye aliyenifanyia usafi wa

inamaanisha"chochote kinachoweza kutokea lazima kitatokea" na hutoweza kukizuia.
Unanikumbusha kauli ya mtume muhammad inayosema "lililokupata halikuwa likukose,na ambalo limekukosa halikuwa likupate "

Hiyo law inaendana na maneno ya mtume muhammad kabisa kabisa.

Na ndio naishi katika msingi huoo.

Ilinikamata homa kali sana hakuna jurani ambaye alijua,baada ya kupata afadhali ndo watu wanashangaa nna vidonda mdomoni.

Sihitaji mazoea na watu hata kama nikiumwa.
 
Majirani sio solution ya matatizo unayoyafikiria.
Ni kama Murphy's law.

Murphy's law inamaanisha "anything that can go wrong will go wrong".
Lakini hiyo siyo maana pekee bali pia inamaanisha"chochote kinachoweza kutokea lazima kitatokea" na hutoweza kukizuia.

Strange thing ni watu wengi wanadhani kuwa na majirani ndio itaweza kuprevent bad things au kusaidiwa pale kitu kibaya kitakapotokea, which is wrong and impossible.

Na hiyo inapelekea ile definition ya "Uoga wa Maisha" kuwa applied on this circumstance. It's like the act of seeking security.

Na hiyo ndio sababu kubwa ya watu wengi kutafuta majirani kwa ulazima.
Na wengine wakishauri hivyo kwenye hii thread.

Naamini ujirani hauwezi kuwa created deliberately bali ni kama nature's coincidence.
Na kulazimisha itepeleka baadae kukosana au kuonekana mnafiki na kero kwa wengine na hali itakuwa mbaya zaidi.

Personally mtu huyo ningemuona irritative.
Lakini sisi binadamu ni tumetofautiana so it depends.

Sidhani kama umewahi kuishi nje ya africa lakini ungepata tabu kuishi USA sababu asilimia kubwa ya watu ni minding your own business.

Bytheway hiyo ilikuwa opinion yangu even though it's a Fact.
Haitakiwi kulazimisha mazoea ama ujirani,hata urafiki ama love ishu kuwa inatokea automatically. Salamu inatosha sana.pia mkizoeana kuchorana,stori zikizidi Sana baadaye umbeya.
So salamu na maneno mawili matatu inatosha,sema usifunge Sana vioo.
Huko USA ama Africa kunajulikana kila mtu Ana adapt mazingira mkuu.
Sema watu ni muhimu,huko USA Kuna zile park ama beach ama night club mbona watu wanaenda ili ku socialize na wengine ama nimekosea.
 
Tangu nimehamia hapa mtaani ni takribani mwaka sasa umekatika. Mtaa ninaoishi ni nje kidogo ya mji ambapo watu wamejenga nyumba zao wamezungusha fensi na mageti. Pia wengi (pamoja na mimi) ni wafanyakazi ambapo mara nyingi ni watu wa kutoka asubuhi na kirudi jioni wakiwa ndani ya magari yao.

Sasa leo nimekaa nikatafakari, nikagundua kuwa zaidi ya majirani niliopakana nao upande wa kushoto na kulia, hakuna jirani mwingine ambaye walau hata namjua kwa jina. Hakuna mawasiliano ya aina yoyote kati yangu na majirani zangu, hakuna tukio lolote linalotukutanisha, na hata ikitokea mtu akapata tatizo, sidhani kama kuna mtu atajitokeza kusaidia.

Mimi naona kama hii hali sio nzuri ila nashindwa kujua nifanyeje ili kujenga ujirani mwema, hasa kwa hawa majirani wa mbali kidogo nyumba ya tatu ya nne huko?
Tenga holiday moja au weekend nenda Gonga jitambulishe kuwa wewe ni mkazi wa eneo hilo, (onesha nyumba) na mweleze mkuu w boma husika ulipoenda kuwa umependa kuwafahamu majirani maana kuna leo na kesho, mbadilishane Namba fanya hivyo kwa majirani kadhaa ikiwezekana muunde Whatapp group.

Ipo siku watakushukuru kwa wazo lako.
 
Wewe sijui ni wangapi.. Unatoa ushauri huu wa jumuiya.. Upo sahihi kabisa kabisa.. Jumuiya ni kitu muhimu sana sana.. Nimepitia situation za kuhamia mitaa ya vigogo aisee kabla sijajiunga jumuiya nilijuta kuishi huko. Ila baada ya kujiunga mimi ndie m.kiti wao.. Haijalishi mavyeo yao Serikalini au wapi? Maisha yamekuwa mazuri yenye amani na mshikamano mkubwa.

Walioanzisha jumuiya aisee. Mungu asiwasahau katika ufalme wake.
Mimi nilikaa miezi sita ni mute tu na siku moja nilenda kanisani nako mute tu hakuna niliyekua namfahamu.Baada ya kuanza jumuiya na siku nyingine wakaja kusali kwangu yaani saizi nikienda kanisani najikuta watu kibao nafahamiana nao baada ya ibada tunasalimiana na kutaniana mtaani ndo usiseme kwa sasa
 
Unanikumbusha kauli ya mtume muhammad inayosema "lililokupata halikuwa likukose,na ambalo limekukosa halikuwa likupate "

Hiyo law inaendana na maneno ya mtume muhammad kabisa kabisa.

Na ndio naishi katika msingi huoo.

Ilinikamata homa kali sana hakuna jurani ambaye alijua,baada ya kupata afadhali ndo watu wanashangaa nna vidonda mdomoni.

Sihitaji mazoea na watu hata kama nikiumwa.
Yes Mana hawawezi kubadilisha uhalisia,hata Kama unakufa hawawezi kuzuia.sema maisha ni maamuzi yako.kile unachotoa ndicho utakachopata ama kuvuna.
Ninajua mie sio muhimu kuliko wewe na wewe pia sio muhimu kuliko mie.ukijifungia namie najifungia Mana hakuna anayempa mwingine pumzi ama kulipa bills zake za kila siku
 
Kweli mkuu muhimu sana kuwasalimia, ila ukishawasalimia ni ngumu kukwepa mazoea pia.
Ngumu sana kuishi kishua kwenye mtaa wa kiswahili, ukishindwa hamia ushuani. Kule no time for bullshit mnapishana kwa ma-indicator tu na mahoni 😂
Mazoea labda na ma shawty niwatanie tanie ila wahuni tunaishia kwenye salamu tu 😅😅😅
 
Mimi nilikaa miezi sita ni mute tu na siku moja nilenda kanisani nako mute tu hakuna niliyekua namfahamu.Baada ya kuanza jumuiya na siku nyingine wakaja kusali kwangu yaani saizi nikienda kanisani najikuta watu kibao nafahamiana nao baada ya ibada tunasalimiana na kutaniana mtaani ndo usiseme kwa sasa
Heheheh mtumishi habari ya sahizii😅
 
Haitakiwi kulazimisha mazoea ama ujirani,hata urafiki ama love ishu kuwa inatokea automatically. Salamu inatosha sana.pia mkizoeana kuchorana,stori zikizidi Sana baadaye umbeya.
So salamu na maneno mawili matatu inatosha,sema usifunge Sana vioo.
Huko USA ama Africa kunajulikana kila mtu Ana adapt mazingira mkuu.
Sema watu ni muhimu,huko USA Kuna zile park ama beach ama night club mbona watu wanaenda ili ku socialize na wengine ama nimekosea.
Mazoea ni ngumu kama watu hamna interests zinazoendana!

Mfano majirani mnapiga mtonji hapo mtakuwa mnaitana au kupitiana kwenda bar za mtaani ila hata wake zenu na watoto watazoeana thats how you network kitaani!

Mnaweza kuwa mnacheza mpira weekend ile mnapitiana kwenda ground thats how you manage to network na majirani kupitia social interests.
 
Unavyotaka kujenga au kuhamia sehemu inafaa uchunguze tabia za wakazi.

Ili usije kwenda ukaona ugumu na kubadilisha wanavyotaka wakazi uliowakuta.

Pengine wenyewe ndivyo wanavyopenda.
 
Huko USA ama Africa kunajulikana kila mtu Ana adapt mazingira mkuu.
Sema watu ni muhimu,huko USA Kuna zile park ama beach ama night club mbona watu wanaenda ili ku socialize na wengine ama nimekosea.
Kama yalivyo majina ya sehemu ulizozitaja.
Ni sehemu maalum unaenda kusocialize na rafiki zako.

Hapo'hapo pia unaweza kuwa lonely kama huna rafiki.
Again kila mtu atakuwa anamind their own business.

Lakini sehemu hizo ndio nzuri kwa kutengeneza marafiki so it depends.
 
Tangu nimehamia hapa mtaani ni takribani mwaka sasa umekatika. Mtaa ninaoishi ni nje kidogo ya mji ambapo watu wamejenga nyumba zao wamezungusha fensi na mageti. Pia wengi (pamoja na mimi) ni wafanyakazi ambapo mara nyingi ni watu wa kutoka asubuhi na kirudi jioni wakiwa ndani ya magari yao.

Sasa leo nimekaa nikatafakari, nikagundua kuwa zaidi ya majirani niliopakana nao upande wa kushoto na kulia, hakuna jirani mwingine ambaye walau hata namjua kwa jina. Hakuna mawasiliano ya aina yoyote kati yangu na majirani zangu, hakuna tukio lolote linalotukutanisha, na hata ikitokea mtu akapata tatizo, sidhani kama kuna mtu atajitokeza kusaidia.

Mimi naona kama hii hali sio nzuri ila nashindwa kujua nifanyeje ili kujenga ujirani mwema, hasa kwa hawa majirani wa mbali kidogo nyumba ya tatu ya nne huko?
Mimi nilihamia sehemu sina jirani wa karibu kabsa. Nipo kama kisiwa yani nmezungukwa kulia kushoto mbele nyuma ni viwanja tupu na jirani wa karibu yupo mita 30 halafu nipo ndani ya ukuta....
Nikawa nikichomoka asubuhi narudi saa 4 mpaka 6 usiku.
Kumbe wajuba wananichora....
Nikapigwa tukio la kwanza nikachomoa....
Nikapigwa la pili nikachomoa....
Nikapigwa la tatu wakaniweza wakaniibia laptop na vitu vingine vidogo....

Baada ya hapo nikatafakari maisha nayoishi nikaona ni ubatili mtupu....

Hatua nilizochukua.

1. Nikaongeza kuhudhuria jumuiya yani hata nirudi home chakari saa 10 asubuhi saa 12 nipo jumuiya ..
2. Siku moja moja nikawa nakunywa mtaani na hata nisipokunywa nikawa nakaa kwa mangi nanunulia hata watu vichungu...
3. Kuhudhuria shughuli za kijamii misiba sherehe n.k
4. Vuta demu home... Wanawake wana nguvu za kuvuta majirani acha tu mzee...

5. Jua boda boda kadhaa .....

Baada ya hapo nina miaka miwili sijawahi vamiwa tena....
Na sasa nina majirani watatu wa karibu kabsa.....
Na mtaani najua almost kila mtu atleast kwa jina....

Kuishi kivyakovyako sio kabsa... Utajifia gheto watu wasijue.
 
Back
Top Bottom