Ni genetics kwa asilimia chache sana. Sababu kama ni kweli genetics zingekuwa ndio zina-determine intelligence ya kiumbe kwa 100%. Then it means kuna familia na vizazi ambavyo ni wajinga milele. Kitu ambacho ni kinyume na sheria kuu ya nature, Development and specific adaptability to certain environments. So usiwasikilize waliosema Genetics kama kichocheo kikuu cha akilia za binadamu.
Bali kwa kiasi kikubwa intelligence ya binadamu inachochewa na Malezi na Mazingira. Hivyo kumlea mtoto kwa kukuza curiosity yake ya utoto na kumjibu kila swali lake na kumsukuma ili aendelee kuwa hivyo ni njia mojawapo. Badala ya kumfokea kwa kumuona msumbufu. Kwani kufanya hivyo kutam-discourage na kudumaza uwezo wake milele. Ukilinganisha watoto huona wazazi wao kama miungu na kuamini kila walisemalo.
Hapo utaupa nafasi ubongo wake kukua kwa haraka, wanaita brain-plasticity na ku-strengthen neurotransmitters. Hivyo kuzidisha ufikiri na kasi yake, ikiwemo kuongezeka kwa curiosity. Hapo lazima apasue masomo ya darasani ambayo kwa wakati huo wa miaka 6-7 yatakuwa chini yake sababu tayari ubongo umekomaa kupitiliza. Ni kama vile wewe upewe maswali ya 5+5. Vilevile kumfunza lugha za kigeni kama English au Kifaransa zinasaidia kukuza uwezo wake wa kufikiri na kusolve vitu.
Kama kweli unataka kukuza an absolute thinking machine basi, kwenye kipengele cha mazingira itabidi uwe strickt kupitiliza. Ikiwemo kuangalia marafiki anaocheza nao kila siku ni watoto wa aina gani kutoka familia gani ya watu wa aina gani ili kutomchanganya wako na wao na kupelekea kudumaa kwa ufikiri, curiosity, utambuzi na brain-plasticity inayochochewa na new informations.
Hapo bado hujachelewa kama bado ni wadogo. Kujibu maswali, kujifunza na udadisi isiwe shule tu. Bali maisha yao ya kila siku.
Vilevile fimbo hazisaidii kitu bali hubomoa tu kwa kumpa mtoto uoga na kumuaminisha yeye hawezi kufanya ulichomwambia kwani njia pekee ni kuelewa. Kitu ambacho sio kweli, sababu mara nyingi mzazi na mwalimu ndio wenye makosa yanayosababisha mtoto kutokuelewa.
Na vilevile mazoea ya mzazi na mtoto. Kama mwanao unamlea kama mbwa kazi yako ni kumpa chakula na kumkaririsha kanuni za hisabati. Basi usitegemee huyo mtoto kuwa na uwezo mkubwa wa kufikiri.
Kukaa nae muda mwingi, kucheza nae, kuongea nae kama mtu mzima, na kuwa na mazoea naye kama rafiki ndiyo njia pekee ya kujua akili ya kweli ya mtoto na kujua utaikuza vipi. Matter of fact, watoto wenye uwezo mkubwa wa kufikiri na ufaulu mkubwa darasani, wengi ndivyo walivyolelewa hivyo. Otherwise ni kazi bure.
Dogo langu anapasua 100% kwenye kila mtihani bila hata kutumia nguvu. Na hata mimi nilikuwa nafaulu mitihani bila hata ya kusoma na kukesha usiku kucha kama wale mabaharia wa mabeseni.
Simply sababu uwezo wa kufikiri na uwezo wa kusolve makubwa ulikuwa mkubwa, hivyo viswali vya mitihani ni kama kumuuliza mtu mzima 1+1.
Kuna thread niliandika a few years back inahusu why Africa haina maendeleo, nenda kaicheck. Nimeelezea baadhi ya haya mambo.
Mkuu haukukosea kujiita andrew tate maana umeelezea hii inshu kwa undani kabisa na uhalisia wake kama ambavyo the Top G alivyo.
Wazazi ndio watu wa kutupiwa lawama pale ambapo mtoto anakuwa ni kilaza shuleni,hakuna mwingine.
Binafsi nilipoigundua hii siri ya kwamba akili ya mtoto inakuwa kwa mujibu wa mazingora na malezi basi nikawa makini sana na kijana wangu.
Nikaanza kumshirikisha kwenye kazi ninazofanya nyumbani kama vile kung'oa majani na kuyaweka kwenye mifuko na kwenda kutupa.
Au kufua nguo naye huwa namuwekea beseni lake na nguo huku akifua na niasema kabisa "baba tufue nguo" ili misamiati hiyo iingie kichwani mwake na kutengeneza uwezo mpya katika ubongo.
Hata kama kazi inanzofanya hatofanya kama mimi ila lengo ni kumuongezea uwezo na kulanua ubongo wa mtoto ili ije kumsaidia huko mbeleni.
Watu wengi hawafahamu kwamba kila jambo analojifunza mtoto kwa kufanya ama kuongea basi jambo hilo linaenda kufungua milango fulani kwenye ubongo na hatimae sasa mlango unakuwa wazi na linapotokea jambo fulani ambolo linafanana kidogo ama sana na jambo lileee ambalo lilifungua mlango basi unakuta mtoto ni rahisi kuelewa kwa sababu mlango ulishafunguka.
Siku moj nilimkuta mwanangu amefungua bomba la maji anachezea yale maji yanayochuruzika hiku akipitisha mkono kana kwamba alitarajia yale maji yatakwamisha mkono wake kama ilivyo kamba,lakini haikuwa hivyo na aliendelea na mchezo huo,binafsi nilijua kwamba hapo kuna kitu anatafiti japokuwa mwenyewe hajui kama anatafiti na hawezi kusema kwamba baba ee hapa nafanya utafiti ila unconsciously anatafiti(curiosity)na utafiti huo unaenda kufungua milango mlango wa ufahamu katika ubongo wake.
Imagine leo mzazi anamkuta mtoto anachezea maji eti anampiga na kumkataza,ukatili ulioje huu.
Lakini pia kazi ndogondogo ambazo utamshirikisha mtoto naye azifanye alaafu akawa anazifanya hata kama sio kwa ukamilifu,hapo maana yake unamtengeneza mtoto awe na tabia ya kuelewa yaani kule kufanya kwake hizo kazi basi kazi hizo zinaenda kufungua milango ya kuwa muelewa kwenye akili yake.
Yaani maanayake ni kusema kwamba kama ameelewa task nyingi anazopewa nyumbani vipi atashindwa kuelewa task za shule ?
Hapo sasa tunamtengeneza mtoto awe na tabia ya kuelewa na mimi huu ndio msemo wangu kwa watoto kwamba KUELEWA NI TABIA,hivyo tabia hiyo inatakiwa ianzie nyumbani.
Na ili tabia hiyo ianze nyumbani basi lazima mzazi awe anamfundisha mwanawe mambo mbalimbali nyumbani na ashirikiane nae kufanya kazi za nyumbani.
Kama mama anamenya vitunguu swaumu basi mpe na mtoto naye amenye hata kama hatofanya kwa usahihi ila unamtengeneza akili iwe komavu kuhandle tasks anazopewa.
Kama inaosha vyombo mpe chombo naye ashikeshike hata kama ni vya kuvunjika mpe hata akivunja kimoja atajua kwamba kumbe vinavunjika,hiyo itakuza akili.
Haya yote yanachangia katikabkukuza uelewa wa mtoto na kumfanya awe na akili njema.
Wazazi wanaogopa kuwapa task watoto nyumbani kwa kudhani hawastahili lakini ndio wanawauwa vibaya sana na kuwafanya wawe na akili iliyojifunga ambayo haina experience na vitu vingi.
hAta kwenye kula mtoto wa miaka mi3 utakuta analishwa eti kisa yeye hawezi kula vizuri,muache ale hata akimwaga chakula chini mwache aenjoy utoto wake na muda sio mrefu ataweza kula vizuri.
Yapo mengi ya kuandika kwa kuwaelimisha wazazi,nikushukuru sana bwana
Andrew Tate ate kwa mchango wako murua ambao nilikuwa nautafuta kwenye comment karibia zote.