Niffer atoa majibu baada ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kutaka akamatwe kwa uchangishaji wa fedha kwa ajali ya maafa Kariakoo

Niffer atoa majibu baada ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kutaka akamatwe kwa uchangishaji wa fedha kwa ajali ya maafa Kariakoo

Kungekuwa na sheria za wazi na zinazojulikana kuhusu fundraising.

Mfano, kuna nchi zinataka mtu anayechangisha awe na foundation na awe anaripoti mapato na matumizi wazi kwa taasisi ya kukusanya kodi na kwa wananchi.

Ni kweli kwamba kutojua sheria si excuse ya kuvunja sheria, lakini pia, sheria isiyojulikana ikivunjwa ni rahisi kwa wananchi kumuonea huruma aliyevunja sheria.

Zaidi, jamii yetu imekaa kuhukumiana zaidi ya kusaidiana. Mtu kama Niffer angeunganishwa tu katika efforts za serikali za kukusanya michango.
Nakubaliana na wewe ila pia Niffer kujitwisha hiyo kazi kwenye account zinazosoma jina lake alitakiwa ajiulize mara mbili.
 
Akili za kuambiwa changanya na zako.

Wabongo tunakasumba ya kumchukia mtu pasipo sababu yeyote ya msingi. Na hasa akiwa amepiga hatua flani hua tunatamani kumrudisha alikotoka

TRA kutwa Kila siku wanazunguka madukani wewe unavyohisi hawajawahi mfikia dukani kwake?

Ishu ilikua anavunja bei, baadhi ya washindani wake wakaona anaharibu soko ndo wakatoa na izo shtuma.
Kwa hiyo wewe una akili za kujionea na siyo za kuambiwa?

Rudisheni hela za watu na huyo dada yako daaaddeki
 
Chizi huyo wamfundishe adabu anaaibisha kitengo cha maafa
Mosa lake hasa ni lipi? Mbona kila mara mnatangaza michango mbalimbali na watu wanatoa ikiwemo mchango wa gari la LISU.
Serikali inashindwa nini kiasi halisi atakachokiwa amekusanya kidigitali?

Kinachotakiwa ni kuelekezwa namna ya michango yake kuwafikia waathirika.
 
Watesi wake ndiyo akina nani? Wako wapi?

Mtandaoni
Wakiongozwa na Mdada mmoja Jina nimesahau, walitaka asichangishe yeye achangishe mwingine na ndio ikawa hivi kumshitaki alipoona chini sijui ya saa moja(kama sijakosea ila muda mfupi sana) amepokea 30m jana. Nao watesi hawajui biashara tangu zamani wanataka kumshusha Niffer binti mdogo mchapa kazi. Sio wa pauda kama wao.
 
Mosa lake hasa ni lipi? Mbona kila mara mnatangaza michango mbalimbali na watu wanatoa ikiwemo mchango wa gari la LISU.
Serikali inashindwa nini kiasi halisi atakachokiwa amekusanya kidigitali?

Kinachotakiwa ni kuelekezwa namna ya michango yake kuwafikia waathirika.
Ipo sheria kuna kanuni imekataza I hope kesho utaona kwenye groups za WhatsApp
 
Nakubaliana na wewe ila pia Niffer kujitwisha hiyo kazi kwenye account zinazosoma jina lake alitakiwa ajiulize mara mbili.
Alitakiwa ajiulize mara mbili lakini pia ujue huu ni wakati ambao watu wapo emotional sana hawafikirii vizuri. Wengine wanaweza kufikiri tu kwamba mimi nina network kubwa ya watu wanaoweza kuchangia, natumia network yangu kusaidia hapa.

Halafu paap, wanakutana na mkono wa Kassim Majaliwa.
 
Back
Top Bottom