Nifungue project/biashara gani kwa mtaji wa milion 12

Nifungue project/biashara gani kwa mtaji wa milion 12

Wekeza kwa mkataba na kampuni ya vegrab.co.tz utafunga mashine za kukaushia pilipili na utalipwa na kampuni mpaka 2M Kwa mwezi

Na mradi ni mpaka 20years
Woow, hii ni nzuri sana. wacha nitembelee website yao kuona masharti na vigezo
 
Hapo ndio wengi tunafeli, tuna mitaji ya fedha, ila hatuna mtaji wa mda. Nikushauri, usianzishe biashara ambayo huna mda nayo.
Sasa mkuu, ili ku-avoid hizi risks nishauri hii pesa niiweke kwenye eneo gani ili iendelee kuwa salama na itengeneze returns kiasi
 
Kama upo kanda ya ziwa hasahasa mwanza nitafute nikupeleke kwa vijana uwanunulie pikipiki za mkataba na ili.kuweka commitment Siku hizi wanatanguliza laki nne ili ikitokea akashidwa mkataba hiyo pesa aliyotoa inakuwa ni hasara kwake maana pesa hairudishwi na pikipiki anairudisha kwa mmliki ikiwa nzima kabisa.


Hii biashara ni nzuri maana unaingiza faida huku unafanya mambo yako mengine.
 
Milioni 12, halafu upate faida ya milioni 2 kwa mwezi!! Ukifanikiwa kupata hiyo biashara unishirikishe na mimi niifanye aisee!!

Hiyo faida siyo ya mchezo hata kidogo!!
Hivi huwa mnafanya biashara gani zinazofanya muone ugumu hivyo? Yani wewe ukioewa 12 huwezi kupata faida ya 2M kwa mwezi? Aiseeeh, kazi ipo.

Faida hiyo inapatikana tu,itategemeana na umeamua kuwekeza kwenye kitu gani.Kwa mfano, mtu anaweza kuwekeza 200 kupitia bonds za Serikali Ili apate 8M kwa mwaka, wakati huohuo mtaji ukimpa mtu makini baada ya miaka 5 utamkuta na 400-500M.

Ukishindwa wewe kuitengeneza faida fulani kwenye mtaji fulani kupitia biashara fulani, haimaanishi kuwa haiwezekani.
 
Tupe na gharama za usafirishaji toka shamba mpk Dar pamoja na ushuru na mengineyo ili tupge hesabu ya net profit
Zifuatazo ni gharama za usafirishaji pamoja na ushuru kutoka Mbeya usangu hadi Dar es Salaam

Tone 1 ya gunia za mpunga gharama yake ni Tsh. 50,000/= katika usafiri wa malori makubwa.

Hivyo basi katika gunia 240 za mpunga nilizozungumzia hapo juu ni tone 34 za mpunga, hivyo jumla ya gharama za usafiri kwa tone zote ni Tsh. 1,700,000/=

Ushuru kwa kila gunia ni Tsh. 2000,hivyo kwa gunia zote 240 jumla ya ushuru ni Tsh. 480,000/=

Jumla ya gharama za ushuru na usafirishaji itakuwa ni Tsh. 2,180,000/=

Pia gharama za kuhifadhi mpunga kama ikatokea ukapata mashine ya kukobolea, yule mwenye mashine yuko tayari afanye kuhifadhi mzigo wako bure kwa sharti la kukoboa mzigo wako Ukisha kuwa tayari na mipango yako.

Pia na wanunuzi wengi wa mchele huwa wanapatikana palepale kwenye zile mashine za kukobolea kwa mfano hapa Dar kuna watu kutoka commoro, Kenya, Uganda na Zanzibar wanakuja kwaajili ya kuja kununua mchele

Pia unaweza kufanya maamuzi ya kuweka mchele wako katika store yako na kuuza taratibu kwa kilo kwani utaweza kupata faida maradufu zaidi

Na ndio maana katika ile faida ya TSH. 15,000,000/=,tulifanya approximation ya TSH. 5,000,000/= tunaitoa kwasababu ya gharama ya usafiri, ushuru na gharama za kukoboa na kufanya grading ya mchele wako

Ila lazima profit itabaki zaidi ya TSH. 10,000,000/= kama net profit yako

Watu wanakula na kuupenda sana wali katika nchi hii na nchi za jirani uhitaji ni mkubwa sana, ukiweza kuliona hili basi utaona na kunusa pesa faida ya Pesa ndefu hasa ukiwa na Mtaji

Try this, and thanks me later
 
Kutokana na mtoa mada anahitaji pesa au faida ya haraka basi ushauri wangu hautamfaa san ila kama anahitaji kam kuweka akiba ya faida kubwa hata miaka 5 mbele unaweza kumfaa.

Wazo n kwamba aje Kilombero anaweza kukodi shamba kwa bei ya 500k kwa kila heka na akapat heka 6 na kulihudumia na kulima kwa kila heka ni bajeti ya 1.5M

Na kilimo atakachokifanya ni cha miwa ambapo kila mvuno wa heka moja kam amehudumia vzur anaweza kupata mpk 3M kwa heka moja

Na bei io ya kukodi shamba n kwa makato 5 ndio unarudisha shamba yan kuvuniwa muwa mara 5 kwa hyo io n akiba nzuri tu ya miaka 5 mpk 10 ya kula matunda ya investment uliyofanya maan muwa ukivunwa unaota tena ww n kuweka mbolea kwa wakati na kupalilia tu

Sasa hapo piga faida yake 3M × 6 heka × mivuno 5 hapo utatoa hela ya kuhudumia shamba kdg iliyobaki n faida na ni zaid ya investment for future.
 
Au study forex exchange market for 6 months,. Utafute na mentor mzuri wa kukuelekeza,
Milioni mbili itakua n ndogo Sana, kwa mwezi
Aaah hay mambo ya forex sikushaur mkuu
Yan forex nayo n probability na biashara yake n volatile san unaweza pata Ml 20 leo kesho ukapoteza mpk mtaji na kudaiwa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hata ikiwa kila ki2 humo sawa na zitatosha kwa kianzio ila profit utayopata ni kubwa sana kaa uwekezaji wa hiyo mil8 kikubwa UZA jumla na rejareja utamaliza mzigo haraka na utawahi kuchukua mzigo mwingine na ukienda kwa mara ya pili dubai unaweza pata mzigo kwa discount kubwa mno yaniii kiufupiii spare parts used haimuangushiii mtuuu tuishiii humu
Nauli ya kwenda na kurudi dubai n shngap kwa experience yako mkuu??
 
Kama ni mirathi basi nunua boda mbili harafu nyingine zipige fixed account

Achana na pisi utakua lia balaa ukiishiwa tu wanaachana nawewe.

Mungu akutangulie

Sent from my TECNO F2 using JamiiForums mobile app
[emoji1787][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Aweke mzigo fixed then aachane na pisi kabisa
 
Tafuta sehemu ambayo ni upcoming fungua day care & nursery ya kisasa haswa, itangaze vizuri then anza kupokea mil 2 kila mwezi kama faida [emoji1550][emoji1550][emoji1550]
Naijua hii biashara... Uwe tayari kwamba mwaka wa kwanza na wa pili ni wa kujenga jina na kuaminiwa na wazazi, hii siyo kama kufungua Bar mpya ambapo from day one wateja hujazana na huanza kupungua wakishapazoea. Hii ni kinyume chake... Ukifungua uanze kufanya lobbying na kuchukua walimu wazuri, ambao pia watakuwa wanakuletea wanafunzi from other schools.
 
Mkuu tuliza akili ...kupitia haya mawazo uliyopewa hapa chagua moja unaloona litakufaa ..lakini Usisahau kui invest muda wako katika project au biashara utakayoamua kuifanya na uifuatilie kwa karibu ...usiwe mtu wa kupewa report tuu .....na muhimu katika biashara au project ikiwa ktk introduction stage ni muhimu sana kuisimamia mwenyewe na sio kumuachia mtu
 
Back
Top Bottom