Nifute kwenye kitabu cha kuzimu, niandike kwenye kitabu cha uzima" Hivi vitabu vikoje na uhalisia wake?

Nifute kwenye kitabu cha kuzimu, niandike kwenye kitabu cha uzima" Hivi vitabu vikoje na uhalisia wake?

Rudi nyuma kidogo.
Kupitia hizo kanuni ndizo tunazozitumia kumuelezea Mungu
Kama ambavyo unazozitumia kumpinga Mungu.
Sawa.

Kanuni gani? Umezitaja wapi tuzichambue?

Mimi nimekupa kanuni za kimantiki.

Kwamba, kimantiki, Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote kuumba ulimwengu ambao unaruhusu mabaya kuwepo kuna contradiction.

Contradiction hiyo inaonesha Mungu huyo hayupo.

Naweza kuonesha hilo kimantiki kama ninavyoweza kukuonesha kwamba wewe mwanamme mwenyewe miaka 30 leo huna mama mzazi ambaye ana miezi 6 leo, kwa sababu wewe kuwa na mama mzazi huyo inaleta contradiction kwenye timeline.

Sasa mimi nakwambia hivyo (Mungu huyo hayupo, binti wa miezi 6 ambaye ni mama yako hayupo) wewe unaniuliza chanzo cha binadamu ni nini (unaniuliza kama huyo binti si mama yako, mama yako nani?).

Mimi sijawahi kusema najua chanzo cha binadamu ni nini. Nimesema huyo Mungu hayupo.

Mimi sijawahi kusema namjua mama yako mzazi ni nani. Nimekwambia tu kuwa huyo binti wa miezi 6 hawezi kuwa mama yako mzazi wewe mwanamme mwenye miaka 30.
 
Kupitia hawa watu tunajifunza pia
Kuna mambo kwa akili zetu hatuwezi kuyang'amua yote.

Unaweza kuta anapinga hapa ili apate kitu fulani cha kujifunza. Lakini pia anaweza kuwa ni muumini mzuri sana tena mtiifu kwa Mungu kuliko wale wanaooneka kusali sana kumbe ni wanafiki wakubwa
Unaposema "kuna mambo akili yetu hatuwezi kuyang'amua yote" unaelewa kwamba inawezekana watu wamemtunga Mungu na kumsukumia hayo mambo ambayo akili zao haziwezi kuyang'amua, ili tuwe na jibu jepesi, wakati huyo Mungu wala hayupo, tumemuumba awe chaka letu la kutupia mambo yote ambayo hatuyaelewi vizuri, tuendelee na maisha kwa urahisi tu, wakati huyo Mungu hata hayupo?

Na kadiri tunavyojiongeza na kupata majibu, kuhusu magonjwa, sayansi, elimu etc, ndivyo tunavyoona huyo Mungu anapungukia na kazi, tunaanza kujua sababu za mambo bila kuhitaji dhana ya Mungu?

Thibitisha Mungu yupo, acha kunipachika imani ambazo mimi sina kwa kupenyeza habari za "unaweza kuta".

Mimi sitaki kukupachika wewe kuwa huamini Mungu yupo kama hujasema hivyo.

Hiyo ni dalili ya kushindwa hoja na kulazimisha mambo.

Tukiendekeza habari za speculations za "unaweza kuta" kila mtu ataweka anachotaka kwa lazima, bila kuzingatia hoja, na mazungumzo yakawa hayana maana.

Yani wewe utasema "unaweza kuta Kiranga muumini mzuri" na mimi nikasema "Unaweza kuta Von Bismarck ni atheist mzuri" tukaua mjadala kwa habari za "unaweza kuta".
 
Sawa.

Kanuni gani? Umezitaja wapi tuzichambue?

Mimi nimekupa kanuni za kimantiki.

Kwamba, kimantiki, Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote kuumba ulimwengu ambao unaruhusu mabaya kuwepo kuna contradiction.

Contradiction hiyo inaonesha Mungu huyo hayupo.

Naweza kuonesha hilo kimantiki kama ninavyoweza kukuonesha kwamba wewe mwanamme mwenyewe miaka 30 leo huna mama mzazi ambaye ana miezi 6 leo, kwa sababu wewe kuwa na mama mzazi huyo inaleta contradiction kwenye timeline.

Sasa mimi nakwambia hivyo (Mungu huyo hayupo, binti wa miezi 6 ambaye ni mama yako hayupo) wewe unaniuliza chanzo cha binadamu ni nini (unaniuliza kama huyo binti si mama yako, mama yako nani?).

Mimi sijawahi kusema najua chanzo cha binadamu ni nini. Nimesema huyo Mungu hayupo.

Mimi sijawahi kusema namjua mama yako mzazi ni nani. Nimekwambia tu kuwa huyo binti wa miezi 6 hawezi kuwa mama yako mzazi wewe mwanamme mwenye miaka 30.
tunasema Mungu yupo kupitia uumbaji (hakuna mtu anaweza kuumba isipokuwa yeye) kama yupo sema

Hana mwanzo wala mwisho. Huo pia ni ushahidi wa kudhihirika kuwa Mungu yupo na hawezi kuelezeka.
 
tunasema Mungu yupo kupitia uumbaji (hakuna mtu anaweza kuumba isipokuwa yeye) kama yupo sema

Mungu yupo katika roho na sio mwili.
Roho haifi
Hapo hujatoa kanuni, umetoa kauli ya imani.

Tofautisha kanuni na kauli ya imani.

Hujaweza kuthibitisha kwamba huo unaouita "uumbaji" umetokana na Mungu.

Yani ni hivi, umeona vitu viko, hujui vimekuwaje hivyo, ukaweka hitimisho tu kwamba vipo hivyo kwa sababu Mungu kaviumba.

Hapa umeunganisha mambo ambayo hayana uhusiano. Ni kweli, vitu vipo, lakini hakuna ushahidi wala uthibitisho kwamba vitu vipo kwa sababu ya kuumbwa na Mungu. Hii ni kauli ya imani tu.

Zaidi, mimi nimekuonesha kuwa, Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, kuumba ulimwengu ambao unaweza kuwa na mabaya kama huu ni contradiction.

The problem of evil. The Epicurean Paradox. Sijui hata kama umeielea hii point, naona hujaijibu kabisa.

Unasema Mungu yupo katika roho, na si mwili.

Hiyo roho yenyewe ni nini? Unaweza kuthibitisha ipo?

Maana isije kuwa nakuuliza kuthibitisha Mungu yupo, huwezi, unakimbilia kuongelea roho, habari nyingine ambayo pia huwezi kuithibitisha.
 
Hapo hujatoa kanuni, umetoa kauli ya imani.

Tofautisha kanuni na kauli ya imani.

Hujaweza kuthibitisha kwamba huo unaouita "uumbaji" umetokana na Mungu.

Yani ni hivi, umeona vitu viko, hujui vimekuwaje hivyo, ukaweka hitimisho tu kwamba vipo hivyo kwa sababu Mungu kaviumba.

Hapa umeunganisha mambo ambayo hayana uhusiano. Ni kweli, vitu vipo, lakini hakuna ushahidi wala uthibitisho kwamba vitu vipo kwa sababu ya kuumbwa na Mungu. Hii ni kauli ya imani tu.

Zaidi, mimi nimekuonesha kuwa, Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, kuumba ulimwengu ambao unaweza kuwa na mabaya kama huu ni contradiction.

The problem of evil. The Epicurean Paradox. Sijui hata kama umeielea hii point, naona hujaijibu kabisa.

Unasema Mungu yupo katika roho, na si mwili.

Hiyo roho yenyewe ni nini? Unaweza kuthibitisha ipo?

Maana isije kuwa nakuuliza kuthibitisha Mungu yupo, huwezi, unakimbilia kuongelea roho, habari nyingine ambayo pia huwezi kuithibitisha.
Unachotaka wewe ni kumuelezea Mungu kama tunavyoweza kuulezea chakula kilicho pikwa? Kwa Mungu hakuko hivyo.

Unataka ushahidi wa kuona ndipo usadiki?
Au ugumu wako unaupata kupitia Jina Mungu?

Mungu sio mtu.
Yeye anasimama katika nafsi yake. Ujuzi, uwezo, ukamilifu.
 
Hapo hujatoa kanuni, umetoa kauli ya imani.

Tofautisha kanuni na kauli ya imani.

Hujaweza kuthibitisha kwamba huo unaouita "uumbaji" umetokana na Mungu.

Yani ni hivi, umeona vitu viko, hujui vimekuwaje hivyo, ukaweka hitimisho tu kwamba vipo hivyo kwa sababu Mungu kaviumba.

Hapa umeunganisha mambo ambayo hayana uhusiano. Ni kweli, vitu vipo, lakini hakuna ushahidi wala uthibitisho kwamba vitu vipo kwa sababu ya kuumbwa na Mungu. Hii ni kauli ya imani tu.

Zaidi, mimi nimekuonesha kuwa, Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, kuumba ulimwengu ambao unaweza kuwa na mabaya kama huu ni contradiction.

The problem of evil. The Epicurean Paradox. Sijui hata kama umeielea hii point, naona hujaijibu kabisa.

Unasema Mungu yupo katika roho, na si mwili.

Hiyo roho yenyewe ni nini? Unaweza kuthibitisha ipo?

Maana isije kuwa nakuuliza kuthibitisha Mungu yupo, huwezi, unakimbilia kuongelea roho, habari nyingine ambayo pia huwezi kuithibitisha.
Hana hoja.. he's just bluffing
 
Unachotaka wewe ni kumuelezea Mungu kama tunavyoweza kuulezea chakula kilicho pikwa? Kwa Mungu hakuko hivyo.

Unataka ushahidi wa kuona ndipo usadiki?
Au ugumu wako unaupata kupitia Jina Mungu?

Mungu sio mtu.
Yeye anasimama katika nafsi yake. Ujuzi, uwezo, ukamilifu.
Wapi nimesema nataka ushahidi wa kuona?

Unarudi kulekule kunipandikizia vitu ambavyo sijavitaja.

Unaweza kunipa mstari mmoja nilipotaka ushahidi wa kuona?

Tutaweza vipi kuelewana ikiwa hujaelewa hata sababu yangu ya kukataa uwepo wa Mungu ni nini?

Unaelewa kwamba mpaka sasa hujaelewa sababu yangu ya kukataa uwepo wa Mungu, na zaidi, ninaanza kupata shaka kama una uwezo wa kuelewa?
 
Hana hoja.. he's just bluffing
Kuna watu unaanza kujibizana nao kwa kuwapa "the benefit of the doubt".

Halafu kadiri unavyozidi kujibizana nao, unagundua kwamba si tu hawakuelewi.

Ingekuwa shida hawakuelewi tu, hapo ni jambo la kueleweshana.

Unagundua tatizo mtu si hakuelewi tu, unagundua mtu pengine hana uwezo wa kukuelewa.

Yani, unamueleza mtu mara kadhaa kwamba, my objection is philosophical, abstract, logical.

Halafu unakuta mtu bado anarudi kukuambia "wewe tatizo lako unataka Mungu umuone, Mungu haonekani".

Unaelewa kwamba huyu mtu hata hajui tofauti ya abstract/ logical objection na objection ya physical evidence.

Yani unajitahidi kuandika the problem of evil, unajitahidi kuandika Epicurean Paradox.
zote hizo, super abstract, logical, philosophical.

Unajitahidi kuandika square root ya mbili haiwezi kuwa kubwa kuliko mbili. Abstract mathematical logic tupu.

Mwenzako hata haelewi tofauti ya abstract/ logical argument na kutaka kuthibitisha Mungu kwa kumuona ni nini.

Unaenda super abstract, super logical.

Halafu mwenzako anakwambia "tatizo lako unataka umuone Mungu umshike, Mungu hayuko hivyo".

Mpaka hapo unachoka kabisa, unaona huyu mtu tupo katika levels tofauti kabisa, yani hata kuelewa abstract/ logical argument ni nini, na tofauti yake na kutaka ushahidi physical ni ipi, huyu mtu hana uwezo wa kutenganisha viwili hivyo.

Unagundua kwamba hamuwezi kufanya mjadala wa maana, kwa sababu hamuelewani katika vitu basic sana, mwenzako hajui hata abstract thinking ni nini, na wewe objection yako ni abstract!
 
Kupitia hawa watu tunajifunza pia
Kuna mambo kwa akili zetu hatuwezi kuyang'amua yote.

Unaweza kuta anapinga hapa ili apate kitu fulani cha kujifunza. Lakini pia anaweza kuwa ni muumini mzuri sana tena mtiifu kwa Mungu kuliko wale wanaooneka kusali sana kumbe ni wanafiki wakubwa
Wewe sasa hapa unajichanganya, yani muumini mzuri wa Mungu na mtiifu kwa Mungu anaweza vipi kuthubutu kumkana Mungu wake hadharani?
 
Kwanza huyo Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Pili Mungu huyo, kimantiki, akiwapo, huhitaji kumuomba chochote, atakupa kizuri na kukuepusha na kibaya kutokana na sifa zake hizo.

Ukijikuta unamuomba Mungu huyo chochote, hicho kitendo cha kuomba ni kitendo cha kukubali huyo Mungu hayupo.

Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote utamuomba nini?

Kwani yeye hajui unachohitaji?
Wakala wa Satan pole sana
Kila kitu kitapita lakini neno la Mungu halitapita
 
Wakala wa Satan pole sana
Kila kitu kitapita lakini neno la Mungu halitapita
Hujathibitisha Mungu yupo, na huyo Shetani naye ambaye ni derivative ya Mungu hujathibitisha yupo.

Unaleta kauli za imani tu.

Weka uthibitisho kwamba Mungu yupo tuuchambue kimantiki.

Kauli za imani tupu hata kichaa anaweza kuweka hapa.
 
Wapi nimesema nataka ushahidi wa kuona?

Unarudi kulekule kunipandikizia vitu ambavyo sijavitaja.

Unaweza kunipa mstari mmoja nilipotaka ushahidi wa kuona?

Tutaweza vipi kuelewana ikiwa hujaelewa hata sababu yangu ya kukataa uwepo wa Mungu ni nini?

Unaelewa kwamba mpaka sasa hujaelewa sababu yangu ya kukataa uwepo wa Mungu, na zaidi, ninaanza kupata shaka kama una uwezo wa kuelewa

Mungu alikuwepo, yupo na ataendelea kuwepo kwa kuwa tulikuwepo tupo na tutaendelea kuwepo! Nyakati tatu zote zinadhibitisha uwepo wa Mungu.

Mungu aliweza yote, anaweza yote na ataweza yote. Ukamilifu wake unathibitisha Mungu yupo na nimkamilifu.

wewe kukataa kwamba Mungu yupo bila hoja thabiti zaidi ya kutoka mifano mfu ambayo haiendani kabisa kunaoneaha hujui hata kile unapinga.

unapojaribu kutoa mifano jitahidi sana ihusiane kimantiki na kile tunajadili hatuwezi kuzungumzia Mungu unatoa mifano ya mtoto na mama n.k.
 
Soma maandiko....humu watakupotosha tu,labda kama huulizi Kwa Nia ya dhati
 
SSitaki ku comment katika Mambo ambayo sina hakika.
Lakini ninavyofahamu hizi open - air meetings hazifanywi na Kanisa Katoliki. Na hiyo sala ya "Nifute kwenye kitabu cha kuzimu..."ni sala ya Waprotestanti au ya watu ambao sio Wakatoliki.
Hakuna Kitabu chochote. Mtu akifa,anaenda kwenye hukumu halafu anapata anachostahili.
 
Soma maandiko....humu watakupotosha tu,labda kama huulizi Kwa Nia ya dhati
Maandiko ndio yanaweza kukuchanganya zaidi.

Mpaka sasa watu wengi kila wakisoma kitabu cha Ufunuo wa Yohana wanazidi kuchanganyikiwa.

Caiser Nero ameandikwa kwa jina la mafumbo anaitwa joka, halafu sasa kitabu kinazungumzia mambo yajayo wakati kimsingi ni mambo yaliyopita tayari, huoni hapa ndio utazidi kuchanganyikiwa?
 
Maandiko ndio yanaweza kukuchanganya zaidi.

Mpaka sasa watu wengi kila wakisoma kitabu cha Ufunuo wa Yohana wanazidi kuchanganyikiwa.

Caiser Nero ameandikwa kwa jina la mafumbo anaitwa joka, halafu sasa kitabu kinazungumzia mambo yajayo wakati kimsingi ni mambo yaliyopita tayari, huoni hapa ndio utazidi kuchanganyikiwa?
Maandiko ndio yanaweza kukuchanganya zaidi.

Mpaka sasa watu wengi kila wakisoma kitabu cha Ufunuo wa Yohana wanazidi kuchanganyikiwa.

Caiser Nero ameandikwa kwa jina la mafumbo anaitwa joka, halafu sasa kitabu kinazungumzia mambo yajayo wakati kimsingi ni mambo yaliyopita tayari, huoni hapa ndio utazidi kuchanganyikiwa?
Caesars Nero,the anti-christ.
Maandiko yanahitaji utulivu wa akili
 
Mungu alikuwepo, yupo na ataendelea kuwepo kwa kuwa tulikuwepo tupo na tutaendelea kuwepo! Nyakati tatu zote zinadhibitisha uwepo wa Mungu.

Mungu aliweza yote, anaweza yote na ataweza yote. Ukamilifu wake unathibitisha Mungu yupo na nimkamilifu.

wewe kukataa kwamba Mungu yupo bila hoja thabiti zaidi ya kutoka mifano mfu ambayo haiendani kabisa kunaoneaha hujui hata kile unapinga.

unapojaribu kutoa mifano jitahidi sana ihusiane kimantiki na kile tunajadili hatuwezi kuzungumzia Mungu unatoa mifano ya mtoto na mama n.k.

Mpaka sasa unatoa kauli za imani tu, hujathibitisha Mungu yupo.

Nimekupa mfano wa kimantiki unaoonesha Mungu hayupo. Nimekuambia kuhusu The Problem of Evil/ The Epicurean Paradox.

Inaonekana huelewi, huna utashi wa kuelewa na pengine huna uwezo wa kuelewa the problem of evil/ Epicurean Paradox ni nini.

Ndiyo maana mpaka sasa hujaweza hata kutueleza tu kuwa umeelewa ninapoandika "the problem of evil" au "the Epicurean Paradox" ninamaanisha nini.

Sembuse kujibu hizo hoja.

Unaishia kurusha maneno tu kama "mantiki" wakati nikikuwekea hoja za kimantiki huwezi kuziona.

Siyo huwezi kuzijibu, maana nikisema mtu hawezi kuzijibu inawezekana akaziona, akazielewa, akashindwa kuzijibu. Yani angalau amezielewa na anaweza kuzirudia lakini hawezi kuzijibu.

Wewe hoja zangu huwezi kuziona kabisaa, huzielewi kabisaaaa.

Bisha.

Nieleze umeelewa nini nilivyokueleza pingamizi langu la the problem of evil, na unapangua vipi pingamizi langu hilo?

Hujui ninachoandika ni nini!

Unanipinga kwa kauli za imani tu badala ya kujibu hoja zangu.

Hoja huzielewi, hata huzioni.
 
Back
Top Bottom