Nikiona binadamu anazikwa nachanganyikiwa mno

Nikiona binadamu anazikwa nachanganyikiwa mno

Naona tunaendelea kutishana sasa kaka mshana kila mara nawambia siri ya mtungi aijuaye kata

Mtu akishakufa mwili auelewi kitu chochote ndio mana wenzetu wahindi wanauchoma moto

Tuzungumzie roho hapo sawa walakini roho nayo aikai humo chini kaburini
Tunatofautiana maarifa na uelewa... Natamani wengi tutoke kwenye box la mazoea la imani zetu hizi mbili tungeyafahamu mengi zaidi in deep

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni bora kuamini kuwa Mungu yupo kuliko kutokuamini halafu mwisho wa siku unakutana na Mungu.
Kwa nini kuamini ni muhimu kuliko kujua?

Nikikwambia mimi ni Mungu, nipe hela zako zote ili upate uzima wa milele.

Ni bora uamini mimi ni Mungu na kunipa hela zako zote kuliko kutoniamini halafu ukute umenikatalia wakati mimi ni Mungu, utanipa hela zako zote?
 
Kwa nini kuamini ni muhimu kuliko kujua?

Nikikwambia mimi ni Mungu, nipe hela zako zote ili upate uzima wa milele.

Ni bora uamini mimi ni Mungu na kunipa hela zako zote kuliko kutoniamini halafu ukute umenikatalia wakati mimi ni Mungu, utanipa hela zako zote?
Tumwachie Mungu.
 
Ni bora kuamini kuwa Mungu yupo kuliko kutokuamini halafu mwisho wa siku unakutana na Mungu.
Kwahio hapo kosa la mtu litakuwa ni kutokuamini ? (Yaani za Kuambiwa amechanganya na za kwake) Huoni kwamba mtu kama huyo kuhukumiwa / kuteswa atakuwa ameonewa ukizingatia kwamba huyo huyo aliyempa akili ndio atamudhibu kwa kutumia akili zake
 
Kwa Wakatoliki, mwili ukisha shushwa kaburini padri anachukua udongo kwenye mkono wake kisha anautupa ndani ya kaburi huku akisema "fulani bin fulan, wewe ni mavumbi na mavumbini utarudi", udongo huwa unalipiga lile jeneza kiasi cha kutoa sauti...

Hiyo moment haijawahi kuwaacha waombolezaji kwa amani...
 
Hata mimi huwa naamini hivyo, kifo ni usingizi usio na ndoto. Hauhisi chochote kama ulipokuwa haujazaliwa.
Yes, hata Biblia inathibitisha kuwa kifo ni usingizi mzito.
Ayu 18:17 Kumbukumbu lake litakoma katika nchi, Wala hatakuwa na jina mashambani.

Yohana 11:11
11 Kisha Yesu akasema, “Rafiki yetu Lazaro sasa amelala, lakini nitakwenda ili nimwamshe.”

Kwahiyo tumaini Pekee na mwenye nguvu ya kumwamsha mtu aliyelala ni Kristo Pekee. Mtumaini yeye maana ujapo kufa utakuwa bado unaishi.
 
Kwahio hapo kosa la mtu litakuwa ni kutokuamini ? (Yaani za Kuambiwa amechanganya na za kwake) Huoni kwamba mtu kama huyo kuhukumiwa / kuteswa atakuwa ameonewa ukizingatia kwamba huyo huyo aliyempa akili ndio atamudhibu kwa kutumia akili zake
Tumwachie Mungu.
 
Tumwachie Mungu.
Tutumie tu Natural Justice..., Kosa la mtu kutokuamini ni lipi ? Iwapo katumia akili na ufahamu uleule ambao wewe unaamini amepewa ili aweze kufanya upembuzi yakinifu sasa kama jawabu amepata tofauti na aliyempa huo uwezo kosa ni aliyepewa uwozo tofauti au mtoa uwezo ?

Hapo utaona logically it does not add up....
 
Mara nyingi mtu anayefikiria dhumuni na maana ya maisha na kifo ni eidha ni masikini, ana msongo wa mawazo, shida na changamoto nyingi za maisha na upweke.
Lakini kamwe huwezi kukuta mtu mwenye maisha safi akifikiria kifo sababu muda wote atakuwa busy na kazi na kuenjoy maisha yake, matokeo yake anasahau hata kama kuna kifo.

Kufa kila mtu atakufa tu, hivyo hakuna cha kuogopa. Bali cha msingi ni nini unakiacha nyuma? Unawaachia nini kizazi na vizazi vyako? Unaacha picha gani familia yako? Kwa watoto, wajukuu na vitukuu vyako?

Kuna Familia za matajiri, zenyewe ni matajiri tu kwa mamia ya miaka kazi ni kurithishana na kuendeleza, sababu waliotangulia walitambua umuhimu wa kuacha kitu kwa ajili ya wanaokuja nao waendeleze na sio kuwa wabinafsi na kujijari mwenyewe tu kama wengi wenu humu mnaosema ("kula bata maisha mafupi haya utakufa tu mara sijui tumia pesa ikuzoee" ubinafsi wa hali ya juu)
Sasa imagine babu yako angewarithisha na angewaachia utajiri wa company za migodi na viwanda vya kufulia vyuma na kuchimba mafuta, je ungekuwa unahangaika sasa hivi? big NO.

Kifo ni inevitable.
Mimi najua kufa nitakufa tu lakini siwezi kujiachia kufanya kila uchafu na kila starehe kisa sababu nitakufa tu, hapana.
Bali nitafanya kila ninachokiweza sio kwa ajili yangu tu bali na vizazi vyangu vijavyo waje kuendeleza, sitaki kuona wanangu na wajukuu zangu wanakuwa watu wasio na umuhimu wowote popote pale au waishi kama sio chochote kazi kufuata mkumbo hapana hicho kitu sitoruhusu. labda nife sasa hivi hapa. Lakini Point ni kuacha kitu kikubwa au chochote bora nyuma kwa ajili ya vizazi vyako vitakavyo warahisishia maisha na kuwaletea fursa.

Kama babu wa babu zenu wangekuwa wapambanaji basi bila shaka msingekuwepo kwenye huu uzi.
Wengine wangekuwa maCEO, wanasiasa wakubwa, wakiwemo wa mchongo na connection mkikimbizana na mama samia, wengine mngekuwa mnagombania urithi na wengine mngekuwa nje mkisoma kwenye vyuo vikubwa kama Harvard na Oxford kwa pesa za babu au sababu babu ni mtu mkubwa mtu wa watu mwenye watu wake.
Lakini hapana mpo hapa sababu babu zenu walikuwa kama nyinyi tu. Au unadhani MO, Bakhresa na watoto wao wanafikiria kifo? big NO.

Hell, hata mimi nisingekuwepo kwenye huu uzi.
Break the cycle.
 
Kwamba wangefanya vice versa wasingekufa ? All in all ushauri wangu kwa yoyote enjoy life, do what your heart desires. Kifo ni Inevitable na unafanya mema sio sababu kwamba kesho utakufa bali sababu its the right thing to do (according to your conscious), ila kama conscious yako haikusuti na kukitembeza kwa mademu ndio furaha yako basi do what your heart desires life is short
Mjukuu wako anasoma hii comment mwaka 2095, namuona akibubujikwa na machozi na kupigapiga miguu chini huku akirusharusha mikono na kukulaumu kwa kupayuka kwamba "kama babu asingekuwa mbinafsi na mlevi na angekuwa mpambanaji basi nisingengekuwa nashindia miguu na vichwa vya kuku."

Kila mtu akifanya kila anachokitaka kisa tu atakufa bila kujali italeta effect gani kwa wengine, basi dunia itakuwa chafu mara mbili.
Kwa mantiki yako wale wauaji, wezi na majambazi bila kuacha wale wanaojilipua, wote wako sahihi kufanya wanayoyafanya?
 
Maiti anapokuwa amekufa anaisi anaota kuwa amekufa yani yeye anaona kama ndoto ila pale anapoingizwa kaburini na kufukiwa mwenyezi mungu umrudishia roho yake na ndipo apo anazinduka na kujua kuwa kile alichokuwa anakiota siyo ndoto ni kweli kuwa amekufa upata furaha pale anapowaona wote mliokuja kumzika uhamini kuwa amtokubali kumuacha peke yake na ndipo atakapoanza kuwaita bila sauti yake inasikika na viumbe vyote kasoro binadamu na majini apo ndio atagundua kuwa hana msaada mwingine isipokuwa kwake mwenyezi mungu. niishie apo ni adithi ndefu

Sent using Jamii Forums mobile app
Alikwambia nani hizi story?
 
Back
Top Bottom