Nikiwa na 1.5-2M naweza pata sound gani kali ya nyumbani ya heshima

Nikiwa na 1.5-2M naweza pata sound gani kali ya nyumbani ya heshima

Imagine having a sound ambayo unaeza i modify muda wowote unaeza itune utakavyo...

Kitu sipend kwenye mziki ulio complete ni kwamba kuna baadh ya vitu huezi fanya afu kumfanya mtu aridhike ni ngumu sana ...kama kwenye market naona some hi-fi zenye bufa ake system ya watts 750 LG naona ka spika za saut zina watts za kutosha but wamekubana kwenye bass kuwa na spika midrange inch 6.5 afu bass inch saba saba hata watts hasijatofautiana sana

Ila huu upande mwngine kuna mambo unaeza fanya eg kuamua kila spika icheze frequency zipi yan i base pale ..mfano hizi sub zetu za kichina unakuta au nyingi mpaka theatre kale ka sub unakuta kana system kanacheza as low as 40hz or 20hz to 250hz where milio yote mizito inasikika pale na tunajua gitaa pia linaeza piga as low as 50hz means milio pia ya gitaa itasikika kwenye spika la bass manake kuna mingurumo ya kila saa isio na tija kwenye spika la bass....milio ya gitaa haisaund vizuri sana

Ila huku pengine naeza set sub icheze dundo zito tu eg 20hz to 50hz tu where above hapo zitasikika kwenye spika za midrange ambazo zitabeba saut nene nene eg milio ya gitaa ngoma ambazo si nzito za kawaida

Ukiset hivo ukasikiliza nyimbo ya malaika band Ile umeondokaa huku nyuma hali yangu sio shwari uliniahd hatochel3wa atarudi 😁 nimesahau jina lake ..ila ile nyimbo jinsi ilivopigwa na kila kitu ukisikiliza kwenye mziki wa kawaida sub litakuwa linanguruma kila saa ila kwa setting hiyo unaeza kaa sekunde 50 sub imenyamaza unaeza jua waya umekatika kumbe muda huo zinapokezana midrange na full range speakers kutoa sauti za hiyo nyimbo ila inafika a point where mid haitoweza play frequency ndogo vile basi ndo hapo sub kubwa la nch 12 peak ya 1400w or 2000w linapokea linanguruma kama simba deep bass had unaisikia kwenye mishipa ya fahamu daaa asiwaambie mtu

Setting kama hiyo hakuna nyimbo utaichukia kila ukitaka futa afu usikilize hapo unaona aaa hapana acha iwepo....

Faida ingne unaeza nunua chombo kimoja kimoja pia unaeza fanya upgrade kirahisi sana leo unaeza kuja kwangu ukakuta nina nina mziki wa watts 800 kesho ukaja ukakuta nimeongeza sub moja na full range mbil tayar system imeongezeka...

Mfano complete system ya mutek iwe milion mfano huwez nunua labda spika mbil za saut na bass moja afu vingne siku ingne NO lazima ununue yote

Kingne ni kwamba kila kampuni iko fresh kwenye upande flan mfano me napenda sony component spika najua wanazo za sauti nzuri sana but kwenye bass wako nyuma sana hvo hapo ndo natafuta kampuni ingine mfano jbl,JL audio, pioneer, polks ama alpine wako njema sana

Nakadhalika
Huu ni mpango mzuri kwa nchi ambazo vyote vinapatikana in real-time...Kibongo bongo utalazimika kutumia hela nyingi sana kukamilisha hio custom system hasa ukitaka high-end components.
 
Eti nimeona hii ya LG LHD756W
1200W 5.1Ch. DVD-HTS LHD756W
LG Home Theatre Systems LHD756W 1
Vipi ina sound kubwa ya kutosha kumiliki sitting room yangu? Wataamu nisaidieni


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Huu ni mpango mzuri kwa nchi ambazo vyote vinapatikana in real-time...Kibongo bongo utalazimika kutumia hela nyingi sana kukamilisha hio custom system hasa ukitaka high-end components.

Unaongelea inchi?? Vyte nilivotaja bongo vipo inategemea na ww upo mkoa gani kama arusha au dar huwez kosa ...

Kuhusu pesa kama unataka kitu cha maana sio pesa nyingi

Kama unaweza tumia 2M kununua radio unashindwa fanya set up ya hvyo wako watu wanafanya 2.1ch nzuri kabisa kwa laki nane au saba

Hapo radio,cross over, amplifiers, speakers, power supply nk we inabaki kuchomeka kwa umeme wa nyumban kawaida and sound ni amazing
 

Attachments

  • 18921125_1964354530511912_9113992212769090165_o.jpg
    18921125_1964354530511912_9113992212769090165_o.jpg
    53.8 KB · Views: 12
Eti nimeona hii ya LG LHD756W
1200W 5.1Ch. DVD-HTS LHD756W
LG Home Theatre Systems LHD756W 1
Vipi ina sound kubwa ya kutosha kumiliki sitting room yangu? Wataamu nisaidieni


Sent from my iPhone using JamiiForums
LG hana mziki wa kujaa mkuu, Sony anamkalisha mchana kweupe.
LG mziki wake mwepesi sana.
 
Mkuu extrovert sisi wa 600k twaweza pata home theatre gan nzuri(sony).Maana mziki twapenda ila duh hyo sony N9200 bei yake mkasi mno.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nilikuta jamaa ana lg watt 1000 kanunua 750k.haikuniridhisha uwezo wake.labda utafute mtumba zenji kwa bei hiyo unaweza pata kitu chenye afadhali inhawa tech nayo haitakuwa rafiki.lakini madukani hapo utaambulia kitabu cha user manual tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom