Nikiweza kutoboa hadi mwezi wa pili 2024 basi itakuwa ni kwa neema ya Mungu

Nikiweza kutoboa hadi mwezi wa pili 2024 basi itakuwa ni kwa neema ya Mungu

yaani kiujumla ni hivyo tu kuanzia mwezi wa kwanza ni makadirio ya kupata mtoto wa pili mungu akipenda lakini mpaka sasa bado sijasevu hata 100 ndani leo ndo nimepunguza miezi miwili ya kudaiwa kodi toka miezi minne.

Eeeh Mwenyezi Mungu tupunguzie hii mizigo na changamoto tunazozipitia wengi wetu tunaotegemea tutoke kila siku ndo tupeleke tonge mdomoni

AMEN.
Imani, shukrani na tumaini ni muhimu sana wakati huu; si wakati wa kulalama! Familia nyingi za kitanzania zimepitia mazingira haya, pamoja na kwamba mwanzo ulionekana kuwa mgumu ila mwisho ulikuwa mzuri sana....Ni maombi yangu Mungu akupe kibali Cha mpenyo wa kifedha kipindi hiki ambacho unasubiri baraka ya watoto mapacha.
Jana nimetoka kuzungumza na Mtu ambaye alipitia Changamoto kama yako na alivuka salama Kwa misingi ya Imani, shukrani na tumaini...tena ameniambia baada ya kupata uzao wake wa pili wa watoto mapacha Kila kitu kwake ni bambam! Kuna namna Mungu atafanya njia Kwa ajili yako...Pambana ndugu yangu na karibu Kwa mrejesho siku za usoni!
 
  • Thanks
Reactions: LA7
Endelea Kupambana, usisahau maombi pia, Mungu atafanya njia pasipo na njia.
 
Back
Top Bottom