Niko njia panda msaada

Niko njia panda msaada

Yani we ni mjinga ndo maana hata mwanamke kaweza kukuletea mchepuko nyumbani kwako kashakuona ni Fala huna maamuzi yoyote mbele yake.

Kwa tukio hilo ulitakiwa uwe tayari umeshachukua maamuzi ya kuachana nae kuomba ushauri ni kama vile unatafuta suluhisho ili uendelee kuishi nae acha ufala we jamaa, na hiyo safari unayomsindikiza kwao akajifungue bado tu unaiongelea na wakati mimba siyo yako?

Acha undezi acha udhaifu wa kiduanzi unampa mwanamke umuhimu kuliko hata nafsi yako? Kiazi kweli
 
Pole mkuu... usikute mkeo anatokea kanda ya kati.
 
Pole sana kiongozi, hakika Una busara na hekima ya Hali ya juu. Tafuta ushahidi wa kutosha. Mpeleke akajifungue, baada ya wiki nenda kwao na ushahidi wote Kisha mchakato wa talaka uanze. Huyu huwezi kuishi nae kama mke tena kwenye ulimwengu huu.
 
kama unampenda mchane ukweli na uwe tayari kusamehe,, kama ulishashtuka kitambo kuwa ulishikiwa akili kumuoa piga chini,, ni bora kuanza moja
 
NJIAPANDA: Mke wangu alileta mchepuko wake kwangu wiki mbili wakitafuta mtoto, sasa anakaribia kujifungua!

Sina kawaida ya kushika simu ya mke wangu kwani nilikuwa namuamini kiasi kwamba sijawahi hata kufikiria kama atakuja kunisaliti. Nimeoa na ndoa yangu ina miaka 3 sasa, na Mungu ametujalia mtoto mmoja. Sasa hivi mke wangu ni mjamzito na ana mapacha wawili tumboni.

Wiki mbili zilizopita niliona kama mke wangu amebadilika. Alikuwa hana raha na kila nikitaka kuongea naye, anakuwa mkali, na hata kunifokea hadi kunitukana mbele za watu. Mimi nilijua ni ujauzito kwani ana mimba ya miezi nane, hivyo nilijishusha na kukaa kimya.

Lakini kuna kitu kilinichanganya, alikuwa karibu sana na simu yake. Alikuwa bize nayo kiasi kwamba hata chakula alikuwa hali. Ilionekana kama kuna mtu anachati naye. Kilichonishtua zaidi ni kwamba hakutaka mtu kugusa simu yake, hata mtoto akigusa simu, anakuwa mkali, anatukana hadi basi.

Mimi password yake nilijua muda mrefu, ila sikujisumbua naye kwani alijua siijui. Nilipoona mabadiliko, nikaamua kufuatilia kujua ni nini. Nikakuta analalamika kwenye meseji nyingi tu anazotuma kwa mtu mmoja, ambaye hajahifadhiwa kwenye simu. Mwanzoni, meseji zilikuwa zinazungumzia mambo ya ujauzito, baadhi zilikuwa zimefutwa, lakini ni kama alikuwa anamwambia kuhusu watoto wake na mambo kibao, ikionyesha kuwa yeye ndiye baba wa watoto na walionysha kuwa vizuri sana.

Baadaye nikaona Mke wangu alikuwa analalamika, "Utambarikije ndoa na mke wako wakati uliniambia umemuacha? Kwanini uliniambia nibebe mimba kama ulikua na mpango wa kumuacha huyo mwanamke?" Mwanaume alikuwa hajibu, hivyo anatuma meseji tu zaidi ya mia mbili analalamika ila hajajibiwa.

Kwa kweli nilipaniki, nikaamua kufuatilia, nikagundua kuwa hata kadi ya kliniki sijaandikwa mimi kama baba wa mtoto, amemuandika huyo mtu ambaye nilipofuatilia ni mtu namjua. Alishawahi kuja mpaka kwangu kipindi fulani, akaniambia ni baba wa rafiki yake. Aliniomba huyo baba aje kulala kwangu kwa sababu alikuja yuko kwenye matibabu, mpaka rafiki ayke ananipigia simu kunishukuru, akakaa kwangu wiki mbili. Najua alikuwa anaenda hospitalini Muhimbili kumbe ndiyo walikuwa wanatafuta mtoto.

Kwa maana kuwa kumbe walishangaika kupata mtoto kwa muda mrefu kwa sababu mwanaume yuko mkoani. Mke wangu ndiye aliamua kumkaribisha nyumbani ili iwe rahisi kwake kubeba mimba, kwamba wakati mimi niko kazini wao wanahangaika kupata mtoto. Na kwa kweli nilipoangalia tarehe, zinalingana na kipindia licjhobeba mimba.

Sijamuuliza mke wangu kitu chochote, bado nipo kimya. Wiki ijayo ndiyo nampeleka kwao kwa ajili ya kujifungua kwani alisisitiza sana kuhusu mimi kumpeleka. Sasa najiuliza nifanye nini? Sina amani, sina raha, bado nimeshangaa. Hii mimba imenisumbua sana, amenitukana sana na kunidhalilisha sana, nilijua ni kisirani cha mimba kumbe hata si mimba yangu. Naomba ushauri, nifanye nini?
Katoe nakala ya hiyo kadi ya kiliniki,mpeleke kwao,usimpe matumizi wala usimfuate.
Ataliamsha yeye na baadae wewe piga kimya.
 
1. Mimi ningeshauri kwa sasa ungekaa kimya na umpeleke kwao kama anavyodai.
2. Baada ya kujifungua, akishapata nguvu, ongea naye na onyesha kwamba una mashaka na uhusiano wenu, hasa kwamba una hakika anachepuka na mtu unayemfahamu.
3. Ona mwenyewe kama unaweza kuvumilia hali hiyo (mtu mwingine asikuingizie mawazo yake).
4. Kama unampenda, samehe na endelea kuishi naye kama mkeo.
5. Katika masuala kama haya, kama hatua ya kwanza, usimhusishe mtu mwingine/ndugu/wazazi - kufanya vikao etc - jadilini mkiwa wawili tu.
5. Pole sana kwa yote.
Umemshauri vizuri Sana hakika
 
Mbaya sana hii.
Huyo si mke tena,ona njia sahihi ya kumumtaliki.
Tunza ushahidi!
 
1. Mimi ningeshauri kwa sasa ungekaa kimya na umpeleke kwao kama anavyodai.
2. Baada ya kujifungua, akishapata nguvu, ongea naye na onyesha kwamba una mashaka na uhusiano wenu, hasa kwamba una hakika anachepuka na mtu unayemfahamu.
3. Ona mwenyewe kama unaweza kuvumilia hali hiyo (mtu mwingine asikuingizie mawazo yake).
4. Kama unampenda, samehe na endelea kuishi naye kama mkeo.
5. Katika masuala kama haya, kama hatua ya kwanza, usimhusishe mtu mwingine/ndugu/wazazi - kufanya vikao etc - jadilini mkiwa wawili tu.
5. Pole sana kwa yote.
Hivi kweli,ikiwa ni wewe. Namba 4 hapo. Unaweza? Hiyo ni zaidi ya dhalau. Bora achepuke tu utasamehe,japo kauli kupenda,haipo. Huko ni kujitia uzuzu bure tu. Mpaka anamzalia mtu,ni ile unaambiwa,nipo kwake kimwili tu. Sasa,huyo wa nini?

Hii simpo. Mpaka anajifungua,bado siku chache sana. Hizo zivumilie. Kikubwa tunza hiyo namba.
Kwao,ikifika siku,mpeleke tu. Nauli toa,lakini usimuache na chochote. Na hapo hapo,kama wazazi wapo,ongea nao,na ushahidi uliopo wape. Akizaa poa. Akijifungua,sawa. Kadi ya kliniki haipo mbali,ukitaka ipige kopi,uende nayo ukweni. Mwambie atoe origino. Akigoma,toa kopi.
Mahakama ina uwezo wa kuziomba kampuni za mitandao kutoa mawasiliano ya mtu na mtu. Wambie hilo wasiwe na wasiwasi,utaghalamia. Ye mwenyewe ataamua.

Akikataa,thibitisha. Akikubali,achana nae. Ukute ulikuwa unaogea taulo alilojifutia mwenzio.
 
NJIAPANDA: Mke wangu alileta mchepuko wake kwangu wiki mbili wakitafuta mtoto, sasa anakaribia kujifungua!

Sina kawaida ya kushika simu ya mke wangu kwani nilikuwa namuamini kiasi kwamba sijawahi hata kufikiria kama atakuja kunisaliti. Nimeoa na ndoa yangu ina miaka 3 sasa, na Mungu ametujalia mtoto mmoja. Sasa hivi mke wangu ni mjamzito na ana mapacha wawili tumboni.

Wiki mbili zilizopita niliona kama mke wangu amebadilika. Alikuwa hana raha na kila nikitaka kuongea naye, anakuwa mkali, na hata kunifokea hadi kunitukana mbele za watu. Mimi nilijua ni ujauzito kwani ana mimba ya miezi nane, hivyo nilijishusha na kukaa kimya.

Lakini kuna kitu kilinichanganya, alikuwa karibu sana na simu yake. Alikuwa bize nayo kiasi kwamba hata chakula alikuwa hali. Ilionekana kama kuna mtu anachati naye. Kilichonishtua zaidi ni kwamba hakutaka mtu kugusa simu yake, hata mtoto akigusa simu, anakuwa mkali, anatukana hadi basi.

Mimi password yake nilijua muda mrefu, ila sikujisumbua naye kwani alijua siijui. Nilipoona mabadiliko, nikaamua kufuatilia kujua ni nini. Nikakuta analalamika kwenye meseji nyingi tu anazotuma kwa mtu mmoja, ambaye hajahifadhiwa kwenye simu. Mwanzoni, meseji zilikuwa zinazungumzia mambo ya ujauzito, baadhi zilikuwa zimefutwa, lakini ni kama alikuwa anamwambia kuhusu watoto wake na mambo kibao, ikionyesha kuwa yeye ndiye baba wa watoto na walionysha kuwa vizuri sana.

Baadaye nikaona Mke wangu alikuwa analalamika, "Utambarikije ndoa na mke wako wakati uliniambia umemuacha? Kwanini uliniambia nibebe mimba kama ulikua na mpango wa kumuacha huyo mwanamke?" Mwanaume alikuwa hajibu, hivyo anatuma meseji tu zaidi ya mia mbili analalamika ila hajajibiwa.

Kwa kweli nilipaniki, nikaamua kufuatilia, nikagundua kuwa hata kadi ya kliniki sijaandikwa mimi kama baba wa mtoto, amemuandika huyo mtu ambaye nilipofuatilia ni mtu namjua. Alishawahi kuja mpaka kwangu kipindi fulani, akaniambia ni baba wa rafiki yake. Aliniomba huyo baba aje kulala kwangu kwa sababu alikuja yuko kwenye matibabu, mpaka rafiki ayke ananipigia simu kunishukuru, akakaa kwangu wiki mbili. Najua alikuwa anaenda hospitalini Muhimbili kumbe ndiyo walikuwa wanatafuta mtoto.

Kwa maana kuwa kumbe walishangaika kupata mtoto kwa muda mrefu kwa sababu mwanaume yuko mkoani. Mke wangu ndiye aliamua kumkaribisha nyumbani ili iwe rahisi kwake kubeba mimba, kwamba wakati mimi niko kazini wao wanahangaika kupata mtoto. Na kwa kweli nilipoangalia tarehe, zinalingana na kipindia licjhobeba mimba.

Sijamuuliza mke wangu kitu chochote, bado nipo kimya. Wiki ijayo ndiyo nampeleka kwao kwa ajili ya kujifungua kwani alisisitiza sana kuhusu mimi kumpeleka. Sasa najiuliza nifanye nini? Sina amani, sina raha, bado nimeshangaa. Hii mimba imenisumbua sana, amenitukana sana na kunidhalilisha sana, nilijua ni kisirani cha mimba kumbe hata si mimba yangu. Naomba ushauri, nifanye nini?
Daa!! Kuna wanaume aise mna roho hili nalo ni jambo la kuja kuuliza huku aise,,, chukua maamuz ww,, na hiyo ndo tkert yake huko hom kwao,, kwanza piga pcha hiyo card ya mtt Ili uwe na ushahid,, peleka kwao siku akitaka kulud mwambie aende Kwa mme wake wa watt hao,, wambie na wazaz wake hapo hapo
 
MTU Kama analeta fiction story ili apate attention ya watu anakuwa anakosea.

MTU unatumia akili yako na muda ili kutoa ushauri kumbe MTU hayupo serious anadai hii story ya kutunga.

Hii ndo sababu MTU anaamua kukaa kimya hata kwa mwenye uhitaji wa kweli.

Guys we need to be serious na tuitumie hii platform in building each other .
 
Back
Top Bottom