Niliacha kushabikia mpira nilipobaini Mpira unageuza Watu Wachawi!

Niliacha kushabikia mpira nilipobaini Mpira unageuza Watu Wachawi!

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Asalamu alyekum!

Niliacha kushabikia mpira miaka 10 iliyopita Baada ya kugundua kuwa Mpira unanigeuza kuwa wanga, mchawi na mwenye Roho ya husda.

Nilikuwa Mshabiki wa Simba Kwa timu za ndani, Huko Ulimwenguni nilikuwa Mshabiki wa Liverpool. Lakini nikaja kugundua kila timu pinzani(namaanisha Yanga) ikishinda Roho inaniuma Sana, Kwa kweli Ile hali haikunivutia kama kijana mdogo enzi zile.
Haiwezekani Mafanikio ya mwingine ATI roho iniume, inafikia hatua ninaomba kabisa Wasishinde na wasiende Mbele.

Haiwezekani Yanga akishindwa ati ninafurahi, ninachekelea na Kupata Amani ya Moyo. Tayari niliona ugeni Mpya katika moyo wangu ambao nilipojitathmini niliamua kuwa ni lazima nichukue hatua ya kuondokana na Uchawi(kutofurahia Mafanikio ya wengine)
Nikaamua kuachana na kushabikia mipira, haikuwa kazi rahisi Kutokana na mazoea lakini niliweza.

Nilikuwa Huru, sio mchawi tena. Simba ashinde au Yanga ashinde kwangu ni pouwa! Ninaangalia Mpira kama burudani na sio kama Mshabiki.

Yanini Kujiumiza? Yanini kuwa Mchawi na umri huu. Kiufupi Mpira haunisumbui asilani. Ninaweza kulala Kwa raha na wala sio mtu wa kufuatilia mipira kabisa, yapo mambo ya kuninyima usingizi, yapo mambo ya kuutesa moyo wangu. Lakini Kwa Mpira nilikataa.
Yaani mwingine afanikiwe Mimi nitumie, hiyo nilikataa.

Nimemaliza,
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Hahaha,una moyo mdogo wewe.Haufai kuwa shabiki.Mashabiki tuna roho ngumu.

Alafu nilikuwa sina bahati, kila nitakapokaa kuangalia Mpira hasa Ile ya saa nne, kipindi kile Liverpool inahali mbali, lazima ifungwe.

Sipendi presha za burebure, yaani unakimuhemuhe, Roho jujuu ...aaah.. hapanaa bhana!
😂😂

Nina Roho nyepesi,
Sasa hivi naenjoi yeyote atakayefungwa mimi kazi yangu ni kumtania😂😂. Lazima nichukiwe hapo😊
 
Ukishafikia hatua hiyo ya ushabiki wa Yanga kufungwa we unafurahi ujue ni ngumu kuacha, kuacha kwake ni mpaka ufe.

Raha ya mpira haitegemeani na wewe timu yako kufanya vizuri, unaweza ukapata furaha kwakuona tu watani zako wanafungwa.
 
Kipindi hiki kwa wanasimba mpira ni haram

Yanga na mara chache tim nyingine zitabeba hadi 2030, Simba kuja kubeba kombe ni hadi msimu wa 2031 baada ya Samia kumaliza muda wake
Tokapa
 
Alafu nilikuwa sina bahati, kila nitakapokaa kuangalia Mpira hasa Ile ya saa nne, kipindi kile Liverpool inahali mbali, lazima ifungwe.

Sipendi presha za burebure, yaani unakimuhemuhe, Roho jujuu ...aaah.. hapanaa bhana!
😂😂

Nina Roho nyepesi,
Sasa hivi naenjoi yeyote atakayefungwa mimi kazi yangu ni kumtania😂😂. Lazima nichukiwe hapo😊
Umefanya uamuzi mzuri ,maana michezo ambayo kuna kushindanishwa ni katili sana.Lazima upande mmoja utasikitika na mwingine utalia. Sasa ukiwa upande uliopoteza hapo imekula kwako,inabidi ujue tu kuwa ni mchezo tu,kusikitika yes,ila kusichukue furaha yako.Kuna maisha zaidi ya ushabiki.Kwanza pia Ushabiki hata team ikishinda haufaidiki lolote kimaslahi.
 
Ukishafikia hatua hiyo ya ushabiki wa Yanga kufungwa we unafurahi ujue ni ngumu kuacha, kuacha kwake ni mpaka ufe.

Raha ya mpira haitegemeani na wewe timu yako kufanya vizuri, unaweza ukapata furaha kwakuona tu watani zako wanafungwa.

Sasa hapo Kwa kufurahi Watani wanafungwa ndio nikaona pagumu. Alafu wakiwa wanafanikiwa Roho inachemka😂😂 najihisi kukereka, natamani ningekuwa na uwezo wa kinabii niwapunguze nguvu. Kwa kweli ushabiki wa Mpira sio mchezo.

Naonaga kama makocha kazi Yao ni ngumu zaidi kuliko
 
Sasa hapo Kwa kufurahi Watani wanafungwa ndio nikaona pagumu. Alafu wakiwa wanafanikiwa Roho inachemka😂😂 najihisi kukereka, natamani ningekuwa na uwezo wa kinabii niwapunguze nguvu. Kwa kweli ushabiki wa Mpira sio mchezo.

Naonaga kama makocha kazi Yao ni ngumu zaidi kuliko
Raha ya shamba ni kugombaniana mipaka
 
Back
Top Bottom