Mvinyo mpya
JF-Expert Member
- Aug 24, 2013
- 1,052
- 2,866
HahahaKipi haujelewa hapo , Elimu iliyotolewa hapo ni muhimu Sana hizo typing errors ni jambo la kawaida
Mada Kama imekuzidi uzito Unasoma then Una mute
Jf hakuna MTU anajifunza Kusoma
WTF
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
HahahaKipi haujelewa hapo , Elimu iliyotolewa hapo ni muhimu Sana hizo typing errors ni jambo la kawaida
Mada Kama imekuzidi uzito Unasoma then Una mute
Jf hakuna MTU anajifunza Kusoma
WTF
Mh atakama sawaEeh ukipiga hesabu kama kila lisaa limoja utatembea kwa 80kph basi ndani ya masaa 12 utakuwa umetembea 960kms. Chukulia ulipumzika mahali hata kwa lisaa maana yake utakuwa ume cover 850kms tayari.
Yap hapa mwenyewe unaona kuwa Kuna sehemu ulipita zilikuwa hazina rami....Mimi niliteleza kwenye mkeka mwanzo Hadi mwishoMie Juma mosi iliyopita nimetoka Dodoma saa 7 na SunLG kitako cha mbuzi hadi Kondoa 160KM kwa rami,nikatoka kondoa to Kateshi 95 KM rough road nilifika saa 7 usiku hiko Kateshi.Mafuta nilitumia 30K.
Kesho yake nikatoka Kateshi saa 4 asubuhi-Singida Mjini 90KM kwa mafuta ya 10K,nikampuzika kidogo kisha nikaanza safari ya Singida -Dodoma 240KM kwa mafuta ya 20K.
So,kwa ujumla safari nzima nilitembea 590KM kwa mafuta ya 60K,ambapo nilitumia masaa 13.
KAKA KAMA WEWE ULITOKA DAR TO SHY 990KM kwa masaa 12 hongera.
Ningetumia masaa machache zaidi haki vileKama boxer umetumia masaa 12, vipi ingekuwa chuma snoray cc 250Max na ina rejeta n masaa mangap?
Alafu Kwa speed 80ACHA UONGO
Utoke Dar to Shinyanga Kwa Boxer utumie saa 12?
Wengi wanaoponda usafiri wa pikipiki ni wanaume/wavulana wa dar.Wa mikoani anaanzaje kuponda huo usafiri ikiwa wa baiskeli tu ni kawaida kutumia km 80?Mwaka Jana nilijaribu kwenda masafa marefu na piki piki ilikuwa BOXER 125 nilienda shinyanga nilitumia masaa zaidi ya 12 maana nilitoka dar es salaam alfajiri nikafika shinyanga jioni kwenye saa 1 hivi kasoro...! Boxer kidogo barabarani ilikuwa inayumba Nategemea kwenda Shinyanga kwa pikipiki aina ya Boxer, CC 125
View attachment 3135103
Mwaka huu hivi karibuni nikaamua kubadilisha usafiri nikatumia Tvs hizi toleo jibya wanaziita TVS HLX 5G hizi pikipiki nilikuwa sizielewi ila kwakweli mfumo wake ni mzuri japo kwa mbali ukikosea kuzipanga gia vizuri Ina mtetemo ila ni kwa mbali sana...na gia ukizipatia kuingiza inatulia inakuwa kama baiskel vile...Ina kuwa nyepesi na haiyumbi au kupepesuka barabarani.
View attachment 3135112
Angalizo ukiwa unataka kutumia usafiri wa piki piki kwa masafa marefu...
Mwaga oil Kuwa na spana za akiba. Mafuta hayana shida sana maana shell zipo Kila Kona. Ila ukibebab kidumu Cha mafuta walau Cha lita 5 chenye mafuta ya imagance sio mbaya. Beba balbu ya taa ya mbele. Usithubutu kusafiri na piki piki jioni...mwisho wa kusafiri na piki piki ni saa 12 jioni. Kigiza kikianza kuingia barabara kubwa inakuwa hatari sana...madereva wasio na akili Wana washa headlight itakavyo kufanya upoteze uelekeo.View attachment 3135121hivyo ni Bora ukathitisha safari Giza likiingia. Vaa sulualu zaidi ya Moja barabarani Kuna bari sana. Vaa hata jinzi Tatu. Vaa masharti ya mikono mirefu hata mawili pamoja na jaketi zito la ngozi. Vaa viatu haswa mabuti yatakayo kufanya uibane suluali. Badilisha oil Yako mwanzo wa safari...! Usilazimishe ku over take mabasi Nenda mwendo wa kawaida tu speed 80...ila kama uoni wako ni mzuri unaweza kwenda zaidi ya speed hiyo ila kwa uangalifu mkubwa.View attachment 3135133kwakweli sijutii kabisa kusafiria Pikipiki nilikuwa naogopa sana kutumia pikipiki zenye cc mdogo ila sio hatari kama Wanavyo dai...nili enjoy sana safari za pikipiki.
passo yenye cc900 kwa uzito wake hauwezi kufanana na passo yenye cc 1300?tuanzie hapo kwanza unadhani kwanini?Pikipiki ya cc 125 - 150 inaenda Dar hadi Shinyanga kwa kuanzia asubuhi mpaka jioni bila kuchemsha?
Kama ni kweli inawezekana wanaosema Passo ya cc 990 haiwezi wanakua wanamaanisha passo mbovu
Jini Kisiranii
Mbona vi carry vya it tushawahi ongozana navyo toka moro hadi boda ya kasumulu na Vina cc hiyo?kibebeshe mzigo unaowiana na hiyo injini uone kama kitachemsha sio unakibebesha mzigo wa dyna.Passo cc990 inatoboa Shinyanga na popote bila kuchemsha.
Ugomvi ni gari ya cc660, hii hata Moro hutoboi!!
wewe mwlm?imagance ni nini maama yake?? emmergence ni dharura hiyo yako ulimaanisha nini naneno sulualu ni kitu gani au misemo mipya mjini
Sijakuelewapasso yenye cc900 kwa uzito wake hauwezi kufanana na passo yenye cc 1300?tuanzie hapo kwanza unadhani kwanini?
Mbona kawaida sana, mimi nilisafiri toka mafinga hadi masasi kwa haojue escort 150cc, nili enjoy sana,
Harley sio mchezo aisee. Wale jamaa wana pikipiki haswa.Nakuunga mkono, kuna watumiaji wa piki piki wako makundi matano 5.
1. Kundi la kwanza ni The Poor & the destitutes.
Hili ndilo kundi kubwa. Kufuatia hali ya umasikini, watu wengi haswa vijijini wanaishi kwenye lindi la umasikini uliotopea ambapo hawana usafiri mwingine
Wowote tegemeo zaidi
pikipiki hawa ni wale wanao lazimika kutumia usafiri wa piki piki kama usafiri, tuu, wanatumia kusafiri mbali kwa sababu ya shida tuu, dharura na hakuna usafiri mwingine affordable.
2. The Mishe Mishe Men. Kuna watu wa mishe mishe za mambo yao fulani fulani za kukwepa mandata mabararani, hivyo hutumia piki piki kupitia njia za panya road ili wasidakwe.
3. The Hurry Men. Kuna watumiaji wa pikipiki hutumia ili kuwahi sehemu, usually maeneo ya mijini yenye foleni kila kona, usafiri wa pikipiki ndio usafiri pekee wa kuwahi.
4. The Ordinary Preference
Kuna watu usafiri wa pikipiki kwao ni preference, kuna usafiri mwingine mwingi, public transport, daladala, uba na bolt, taxi, magari, mabasi, treni na ndege lakini wanachagua kutumia usafiri wa pikipiki just for preference.
5. The Hobby Group both the rich and the ordinary.
Hili ni kundi la watumiaji wa piki piki kwa hobby, usually wanaendesha wenyewe, hawa wanatumia pikipiki as hobby, hawa wanakwenda na pikipiki popote kwasababu wanapenda and it is fun kwao. Ukifanya kitu unachokipenda na una enjoy, huchoki, na mapenzi yakizidi unakuwa blinded unacheza michezo ya hatari bila kugopo.
Kundi hili lina bike.loves wa kawaida na the rich and the famous. Hili ndilo kundi langu.
Nilikuwa namiliki piki piki 5 kwa matumizi mbalimbali.
1. Batavus ya 50 cc ya kuendea dukani hapo jirani.
2. Honda VT 250cc ya kuendea kazini daily
3. Beta 350 off road ya kuchezea michezo ya piki piki pale Kawe kila Jumapili.
4. Buel 1,200 cc for fun ride, hii ni racing bike, the only one in Tanzania by then, niliinulia US and it costed me a hell.
5. Harley Davidson 1.800 cc custom made for long safari.
Hii Harley bongo ni tuu na wazungu. Hii ndio ilinifanya vibaya na ikaripotiwa humu Pascal Mayalla apata ajali..... na nilipopona nikatoa shikrani humu Waraka wa Pascal Mayalla - Asanteni Sana!
P
Mwongo mkubwa huyu... Dar - Shinyanga ni kilometa ngapi? Tena anasema kwa mwendo wa kawaida... Hizi ni stori za kijiweni za wanabodaboda,ACHA UONGO
Utoke Dar to Shinyanga Kwa Boxer utumie saa 12?
Unapinga nini sasa? Mimi nilitoka Mwanza To Tarime kwa Tvs 150 na spidi niliweka 80 hakuna basi ambalo lilinitangulia mbele nilipitwa na Ford 1 tu.Nilitumia masaa 4 tu kumbuka hiyo ni km 338Mwongo mkubwa huyu... Dar - Shinyanga ni kilometa ngapi? Tena anasema kwa mwendo wa kawaida... Hizi ni stori za kijiweni za wanabodaboda,
Kuna mmoja alisema alitoka Dar - Mwanza kwa bodaboda.... ACHENI kutufanya wajinga.
Angesema alikuwa na Honda ya kuanzia cc 250 (mf. Baja) na kuendelea, labda angeeleweka