Nilichokiona usiku wa leo, msaada wenu wanaJF

Bro kufikiza usiku kabla ya kulala kdg inatia wasiwasi ,lkn kusoma hizo sura ni vema kabisa as muislamu, kufungua au kulala na Quraan ikasoma ni vizuri special surat Baqara lkn zaidi unguefungua Ruqya shariya hizo zipo tofauti kuzikiliza .Ubani ni vyema kuchoma wakati wa aljafiri au hata haba soda na kuwachia madirisha wazi inatoa mambo mengi au kufikiza kabla ya Maghribi .Sijui ni viumbe gani lkn si viumbe wabaya kutokna na mavazi yao kwa time hiyo waliokuja naona kama ni time ya kujitayarisha kusali ,kama unasali kama husali basi jitahidi usali sala ya asubuhi .
NOTE Wakristo musibeze Dini yetu Tafadhalini mukipata matatizo ya kiroho naona munakimbilia kwa waislamu wawasomee .Heshima kitu cha bureeeee.
 
H

hiyo playlist gives out who u r.
1. At least over 35
2. U sound like male but the playlist suggest that u r ke.
😂 mziki hutoa picha ndio lkn sio mara zote! Very wrong!
 
Shukran JazakhaAllahu Khaira... Asante ushauri mzuri..
 
Wenyewe wanaita majini wema hadi wanawachomea sijuwi madude gani eti ubani.Lengo ni kuwavutia hao viumbe na wamerusiwa
Acha ujinga ww nani kakwambia majini wanaitwa kwa Quran alafu nani kasema kawaida kuwa na adabu na uheshimu iman za watu acha upotofu wapi tunasema hivyo
 
Asante kwa ushauri na mawazo yako ninayaheshimu.. lakini sio sheria
 
Mwana kulitaka mwana kulipata
Ndo mavitu unayoyaombeaga kila sku
 

Ulichokipata ni jambo la kawaida kwa wataalamu wa somo la usingizi. Kuna hatua mbalimbali za usingizi na mambo mbalombali hutokea kwenye kila hatua.

Kuna njozi hutokea wakati unapokuwa unasinzia au wakati unaelekea kuamka toka usingizini(soma kuhusu: sleeping stages and hypnagogic vs hypnopompic hallucinations).

Njozi wakati unaamka huusisha zaidi mambo yahusuyo: kuona, sauti au vitu kugusa mwili/ngozi. Mfano: ni kuona watu au wanyama kwenye chumba kimoja, karibu au chini ya kitanda. Hali hii huongezeka zaidi kwa watu wanaopata usingizi na ku-paralaizi(sleep paralysis).
 
Hatari sana
 
Kisayansi ni sahihi ukichokisema kutokana na sayansi.
ILA KATIKA ULIMWENGU WA KIROHO ukiachana na elimu ya sayansi ambayo haiwezi kuelezea mambo ya imani au ya kiroho,maelezo yake ndiyo hayo.Mana sayansi haiamini katika Mungu wala shetani ,haiamini katika uumbaji wq Mungu,haiamini mambo ya kuzimu na mbinguni,haiamini USHIRIKINA.
Ukienda hospitali dakatari atakwambia ni tatizo la kawaida kutokana na sleep cycles stages mambo ya sleep paralysis na ni sahihi kwa upande wa sayansi.
Ila ukitaka maelezo ya ulimwengu wa kiroho ndiyo hayo tuliyoyasema hapo juu.
 
Soma mambo uliyoandika na utafakari ni nini ulitaka kueleza.

Kwa maelezo yako, "Daktari anakwambia ni sleeping cycle stages", hapa daktari anatumia nini kueleza hili/reference) na "si sahihi kwa upande wa sayansi", sayansi ipi?. Unaposoma usingizi na hatua zake inakuwa ni nini? Mtu anaposoma sleep mechanism, circadian rhythm and homeostasis anafanya kitu gani?

Upande wa kiroho ndo unajimilikisha kutoa maelezo sahihi kuhusu hili(kwa sabstancial evidence zipi?).

Ni vyema kuelezea vyema unachokifahamu wewe kwa usahihi wake na si kusema huku haiwezekani au kule inawezekana.
 
ulichokieleza kisayansi ni sahihi na wala sijakupinga.
Maelezo niliyomueleza mimi ni ya KIROHO ulimwengu wa Roho naujua unavyotenda kazi,na sayansi niliyoisoma mimi haiwezi ku proove yaliyo katika ulimwengu wa Roho wala imani za kiroho.
TUNAISHI KATIKA ULIMWENGU ZOTE MBILI,ULIMWENGU WA ROHO NA ULIMWENGU HUU PHYSICAL NYAMA.
Pamoja na kwamba sisi ni wanasayansi ila pia tuna imani ,ndio mana tupo tunaomuamini Mungu ,tupo tunaoamini binadamu sisi tumeumbwa na Mungu ijapokuwa sayansi inatuambia tume evolve kutoka kwa nyani.Hivyo ni HAKI yetu sote kikatiba na tuna uhuru wa kutoa maoni yetu ,uhuru wa kuamini imani tunazoziamini.
NINACHOTAKA KUELEZA
Muhusika aliyeuliza ameelewa ,mimi sijaelezea kisayansi nimeelezea KIROHO japo sayansi pia naijua ila nimechagua kuelezea kiroho.
 

Ukipenda kueleza kiroho au kisayansi jikite na kulinganana mtizamo wowote unaoona unafaa kumsaidia mhusika.

Ukitaka kueleza vyote eleza hivyo.
Hoja yangu ilikuwa ni mkanganyiko ulioutoa kuhusu: kisayansi vs kidaktari vs kiimani. Ukisoma hoja yako ulivyoitoa mwanzo utaelewa kuwa kuna mambo yanasigana.

Daktari anaongea kwa reference ya kisayansi, mwisho unasema sayansi haiyakubali?? Ni vyema tukubali kuwa kuna mstari kati ya mambo ya kisayansi na kiroho na kati ya hivi hakuna mwenye kusema anaweza ku-mprove wrong mwenzie kwa 100%. Haya ni mapokeo na tuishi nayo kwa kiasi.
 
umenena vyema chief,upo sahihi sana..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…