Nilifadhaika sana kupata watoto wa kike tu

Nilifadhaika sana kupata watoto wa kike tu

sisi tulizaliwa watano wote wakiume ni familia yenye amani sana hakuna drama japokuwa tulikuwa tunapigana sana kipindi cha utotoni, hivi sasa namuonea mother huruma kama yupo mpweke hivi japokuwa anawakamwana wakutosha ,[emoji23]
 
haya mambo ya watoto, mali n.k ni kushukuru tu kile mlichojaliwa, vinginevyo utaishi kwa mfadhaiko mpk uione dunia chungu
Mungu alisema tushukuru kwa kila jambo lakini pia amesema tuombe jambo lolote tutapewa.

Yohana 14:13-14​

Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya
 
Mola ana maajabu yake sana,anakujaalia watoto wa kike kisha anakupa na mapenzi ya dhati kwao.

Huwa tunasema hivi unaweza kuchukia jambo kumbe lina kheri na wewe na unaweza kupenda jambo likawa na shari na wewe.

Watoto wakike ukijaaliwa ni neema kubwa sana,hasa ukiwalea katika malezi ya dini.

Nina mengi sana ya kusema juu ya fadhila/ubora wa kuruzukiwa watoto wa kike.

Nakomea hapa.
Mungu Ni Mwema Wakati Wote
 
Huyo Mototo ametokea just kama coincidence of nature haina mahusiano yoyote na maombi yako kwa Mungu.unataka kisema watu walio katika ndoa hapa duniwni waliopitia mazingira kama yako kwa kufanya maombi wenyewe Mungu hawasikii-unataka kusema Mungu ana upendeleo??
Ni coincidence kwa watu wasiomwamini Mungu na ahadi zake. Mungu amenipa mambo mengi sana baada ya kumuomba. Sio hilo tu la mtoto wa kiume. Muda haunitoshi kuyashuhudia mambo yote humu.

Watu wanaoomba lakini hawapati haimaanishi Mungu hawasikii. Ukisoma Biblia utagundua kuwa majibu ya maombi wakati mwingine huwa yanazuiliwa au kucheleweshwa. Katika hali hiyo kinachotakiwa ni kuendelea kungojea majibu bila kukata tamaa na kumpinga Ibilisi anayezuia.

Na wakati mwingine Mungu anasikia lakini anajibu "no" kama tunaomba vibaya. Soma Biblia ndugu, utaelewa.
 
Nilivyomuelewa mleta mada hajasema jinsia fulani ni bora

Nimeelewa alipata watoto watatu jinsia moja akatamani kupata jinsia tofauti...ambacho ni kawaida
Kweli kabisa, mkuu
 
Nakuhakikishia kuwa huyo mtoto wa kiume anakuja kuwa zigo na utajuta kumzaa!
Mimi yalinikuta [emoji24][emoji24]
Mke wangu Alisali na Kufunga ili apate mtoto wa Kiume!
Mungu Akampa!
Kilicho Tokea Ukawa Mwiba ukatuchoma mimi, mke wangu, na Jamii kwa ujumla wake [emoji24][emoji24]
Anacho Tupa Mungu Tupokee kwa Shukrani
 
Dah! mtoto ni mtoto tu, kama vipi tafuta njemba ambayo inafyatua midume tu ikusaidie angalau wife afyatue vitoto vitatu vya kiume. Kuna dingi mdogo yeye kati ya watoto 10 kafyatua 9 wa kiume, kama vepe nikuunganishe naye...
 
Mimi yalinikuta [emoji24][emoji24]
Mke wangu Alisali na Kufunga ili apate mtoto wa Kiume!
Mungu Akampa!
Kilicho Tokea Ukawa Mwiba ukatuchoma mimi, mke wangu, na Jamii kwa ujumla wake [emoji24][emoji24]
Anacho Tupa Mungu Tupokee kwa Shukrani
Huyo kijana alivyobadilika na kuwa mwiba, mke wako hakupaswa kukata tamaa, angesali na kufunga tena ili Mungu ambadilishe awe mwema. Mungu anaweza yote. Anaweza kuwabadilisha majambazi wakawa Wainjilisti.
 
Mimi yalinikuta [emoji24][emoji24]
Mke wangu Alisali na Kufunga ili apate mtoto wa Kiume!
Mungu Akampa!
Kilicho Tokea Ukawa Mwiba ukatuchoma mimi, mke wangu, na Jamii kwa ujumla wake [emoji24][emoji24]
Anacho Tupa Mungu Tupokee kwa Shukrani
Unapo omba usipende kuishia kuomba Mungu akipe unacho taka, jitaidi kuomba pia Mungu akuonyeshe mwisho wa hicho kitu unachokitaka utakuweje
 
Hali hii hutokea katika ndoa nyingi. Mke anazaa watoto wa jinsia moja tu mfululizo, ama wa kike au wa kiume tu. Wazazi wengi huwa wanapenda wapate watoto wa jinsia zote. Kwa sababu hiyo inapotokea wanapata watoto wa kiume tu au wa kike tu huanza kutafuta njia ya kutatua 'tatizo' hilo. Wengine huenda kwa madaktari kutafuta ushauri wa kisayansi na kufanikiwa kupata mtoto wanayemtaka; lakini wengine ushauri wa kisayansi bado hauwasaidii kupata mtoto wa kiume au wa kike.

Wazazi wanapofikia hali hiyo wengine huenda kwa waganga wa kienyeji na huko huishia kuchanganyikiwa tu kutokana na masharti magumu wanayoambiwa na mganga. Jaribu kuwaza mtu anaambiwa apeleke kwa mganga kinyesi "fresh" cha tembo ndio apate dawa!

Nakumbuka mme fulani alisababisha mgogoro katika ndoa yake baada ya kumgombeza mke wake kwanini anazaa watoto wa kike tu. Na waume wengine huamua kuwaacha wake zao au kuoa mke wa pili ili wajaribu kama watapata watoto wanaowataka kwa njia hiyo. Njia zote hizo zinaposhindikana hubaki na huzuni isiyokoma.

Mimi pia nimepitia hali hiyo. Mara ya kwanza mke wangu alipata mtoto wa kike. Mara ya pili akajifungua tena mtoto wa kike. Tulikuwa tunajitahidi angalau tupate mtoto kila baada ya miaka miwili. Mara ya tatu mke wangu akazaa tena mtoto wa kike. Hee nikaanza kufadhaika, maana nilitamani na mimi niwe na mtoto wa kiume. Sikumlaumu wala kumgombeza mke wangu kwanini anazaa watoto wa kike tu kwa sababu najua kisayansi mwanaume ndiye anayehusika zaidi kufanya mtoto wa jinsia ipi azaliwe.

Katika kutafakari nifanyeje nikakumbuka yale maneno ya Mungu yasemayo "Ombeni nanyi mtapewa" Nikakumbuka pia habari za mama mmoja katika Biblia aliyekuwa hapati kabisa watoto lakini baada ya kumwomba Mungu akapata.

Kwa sababu hiyo na mimi nikaanza kumwomba Mungu kwa juhudi kwamba mke wangu atakapojifungua mtoto wa nne, awe wa kiume. Ndugu zangu, Mungu hana upendeleo, alisikia maombi yangu na kutupatia mtoto wa kiume. Kinachotakiwa tu ni kuhakikisha mahusiano yetu na Mungu ni mazuri na kuomba kwa imani, pasipo shaka. Yote yawezekana kwake aaminiye(Mk 9:23).
7uv
 
Unapo omba usipende kuishia kuomba Mungu akipe unacho taka, jitaidi kuomba pia Mungu akuonyeshe mwisho wa hicho kitu unachokitaka utakuweje
Nimesha Omba Toba na Rehema kwangu kama Kichwa cha Nyumba Mungu Akaturehemu na Kumkarabati kijana!
Pia Imekuwa FUNDISHO kwa walio na mawazo kama Mimi!
Amen!
 
Huyo kijana alivyobadilika na kuwa mwiba, mke wako hakupaswa kukata tamaa, angesali na kufunga tena ili Mungu ambadilishe awe mwema. Mungu anaweza yote. Anaweza kuwabadilisha majambazi wakawa Wainjilisti.
Hilo Jukumu Nilichukua Mimi kama Kichwa cha Nyumba!
 
Ni coincidence kwa watu wasiomwamini Mungu na ahadi zake. Mungu amenipa mambo mengi sana baada ya kumuomba. Sio hilo tu la mtoto wa kiume. Muda haunitoshi kuyashuhudia mambo yote humu.

Watu wanaoomba lakini hawapati haimaanishi Mungu hawasikii. Ukisoma Biblia utagundua kuwa majibu ya maombi wakati mwingine huwa yanazuiliwa au kucheleweshwa. Katika hali hiyo kinachotakiwa ni kuendelea kungojea majibu bila kukata tamaa na kumpinga Ibilisi anayezuia.

Na wakati mwingine Mungu anasikia lakini anajibu "no" kama tunaomba vibaya. Soma Biblia ndugu, utaelewa.
Wewe ni jinga tu

Kuomba vibaya ndio kupi? Kwani wasiopata watoto hawaombi?

Acha kubagua jinsia
 
Mimi yalinikuta [emoji24][emoji24]
Mke wangu Alisali na Kufunga ili apate mtoto wa Kiume!
Mungu Akampa!
Kilicho Tokea Ukawa Mwiba ukatuchoma mimi, mke wangu, na Jamii kwa ujumla wake [emoji24][emoji24]
Anacho Tupa Mungu Tupokee kwa Shukrani
Waambie hao
 
Na mwanaume hupenda kuchagua kwa sababu hajui shida apatayo mwanamke kuanzia kubeba tumbo mpaka kujifungua.Kuweni na utu kidogo
Sio wanaume wote, mbona mimi nimeridhika na wa kike lakini mwanamke ndo anataka wa kiume
 
Mkuu umesoma heading anasema alifedheheka kupata wa kike tu. Meaning Watoto wakike kwake si Bora furaha yake ingekamilishwa Kama angepata wa kiume.
Kiswahili kigumu: Fadhaika=Fedheheka??
 
Back
Top Bottom