Nilifanya kosa ndio lakini mwenzangu amegoma kunisamehe, nifanyaje?

Nilifanya kosa ndio lakini mwenzangu amegoma kunisamehe, nifanyaje?

kyagata

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2016
Posts
10,406
Reaction score
19,892
Ndugu zangu hamjambo?

Jamani nina mpenzi tumedumu muda sana tu na tumepitia vipindi tofauti yani ups and down.

Kuna kipindi tulikosana na mimi nikajitahidi kumuelewesha lakini akawa hataki hata kunisikia ila nikamchunguza nikagundua pia hana mtu.
Sasa nikaamua kuwashirikisha ndugu zake ili watuweke sawa lakini mwenzangu akawa kakasirika zaidi eti kwanini ndugu zake nimewaambia.

Mimi nimekua nikimjibu tu ni mapenzi yako kwako na siko tayari kukupoteza, ndugu zake wametusuhulisha lakini mwenzangu kila tukipishana kauli basi anaanza kunikumbushia kuhusu hiyo ishu ya kuwaambia ndugu zake anaenda mbali mpaka anasema mimi nimejipeleka kwao. Nashindwa kumuelewa ana tatizo gani kwani ndugu wakijua kuwa tunadate ni kosa kubwa la hadi mtu kuliweka moyoni.

Naomba mawazo yenu nifanyeje na huyu mtu jamani sababu imekua too much.
 
kwa nn husemi km wewe ni me au ke?!!
anyway cha msingi tulia mpe mda fanya mambo yako kwanza usimfuatilie,
baadae mfuatilitilie tena,ukiona km haeleweki bado, potea kbs!! ujue hakupendi.
 
Mmedumu muda sana, hebu taja huo muda kwanza.

Miaka mingapi?
 
Hivi wanawake wote hawa,we unahangaika na kinuka mkojo mmoja?
 
Ulimkosea nini? Huenda kitendo ulichomfanyia kilimuuma sana na huenda akagundua ulifanya makusudi. Sasa ikiwa ni hivyo ujuwe mwenzio anahitaji muda ili ajiridhishe kuwa umemaanisha kuomba huo msamaha.
 
Mkuu hiyo kyagata ni kiagata au kama ni kiagata na uko maeneo haya nishtue maana naweza kukushauri moja kwa moja
 
Afu usipende sana kuomba samahani kwa kila jambo mengine unachukilia poa ili usilipe uzito jambo na huwa yanaisha unaweza tumia lugha nyingine ila sio kila jambo samahani sio poa kabisa
 
kwa nn husemi km wewe ni me au ke?!!
anyway cha msingi tulia mpe mda fanya mambo yako kwanza usimfuatilie,
baadae mfuatilitilie tena,ukiona km haeleweki bado, potea kbs!! ujue hakupendi.
mimi ni mwanaume.
 
Mkuu hiyo kyagata ni kiagata au kama ni kiagata na uko maeneo haya nishtue maana naweza kukushauri moja kwa moja
hiyo ni kiagata ya huko musoma lkn kwa sasa siko pande hizo master
 
Back
Top Bottom