Nilifunga ndoa na mtu nisie mpenda

Nilifunga ndoa na mtu nisie mpenda

Mwachiluwi

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2022
Posts
25,258
Reaction score
48,589
Katika Maisha, kila mmoja anakuwa na ndoto kubwa yenye kumpa furaha Maishani mwake,hata wewe una ndoto ambayo siku moja ikitimia utakuwa ni mwenye kufurahi sana.Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Robson, alisoma, alipata kazi nzuri iliyomuingizia pesa nyingi, alikuwa na muonekano mzuri, mtanashati lakini alikuwa na ndoto ambayo alitamani kuiona siku moja ikitimia, ndoto yake kubwa ilikuwa ni kumuoa Sylvia.

Ndoto ya Robson ilitimia, Sylvia aliridhia kuolewa na Robson, maandalizi yote yalienda sawa na ndicho ambacho Robson alikuwa akikitaka, nafsi ya Robson ilikunjuka akawa mwingi wa furaha, si kazini hata nyumbani kwake alikuwa mwingi wa kutabasamu

“Hakika Robson unaenda kutimiza ndoto zako za muda mrefu Kaka” Alisema rafiki yake Robson aliyeitwa Mark

“Zaidi ya Sylvia sijaiona furaha nyingine Mark, kumuoa yeye ni jambo linaloenda kunipa furaha sana” Alisema Robson wakiwa wanapata chakula cha mchana nje ya ofisi yao

“Mna mpango wa Fungate?” Aliuliza Mark

“Ndiyo! Nimepanga kumpeleka Kilimanjaro Kaka, tena tukaishi karibu na Mlima kwa wiki mbili za mwanzo kisha tukamalizie Mwanza kula sato” Alisema Robson kisha walicheka kwa pamoja

“Umetisha sana, Unyama mwingi Rob!!”

Tukiachana na upande wa Robson, Nyumbani kwao Sylvia hali haikuwa hivyo kabisa, Sylvia hakuhitaji kabisa kuolewa na Robson, alikubali kwasababu Baba yake alimlazimisha kufanya hivyo, Sylvia aliwaambia Wazazi wake kuwa ana Mwanaume anayempenda sana hivyo ataolewa na huyo na siyo Robson

“Hili linaenda kufanyika Silvia, unaolewa na Robson, Kijana Mtanashati, mchapakazi..” alisema Baba yake Sylvia siku mbili kabla ya ndoa ya Robson na Sylvia, hakukuwa na mjadala tena.

Usiku wa kuamkia siku ya ndoa, Sylvia alimwambia Mama yake kuwa waliangalie upya jambo walilolitaka yeye alifanye

“Mama naolewana Mtu ambaye hayupo ndani ya moyo wangu” alisema Sylvia

“Usiseme hivyo Mwanangu, mbona Robson ni Kijana mpole, mzuri na anaonekana anakupenda sana”

“Mama, suala siyo Robson kunipenda bali ni Mimi kumpenda yeye, hii itakuwa ndoa ya upande mmoja Mama, naomba tafadhali tusitishe hii ndoa Mama yangu” alisema Sylvia, alimpa wakati mgumu Mama yake wakati mipango yote ilipangwa na maandalizi yalishafanyika

“Hadi hapa tulipofikia Sylvia hakuna namna tunaweza rudi nyuma, huna budi kuingia kwenye ndoa, nina imani Utampenda Robson” Alisema Mama yake Sylvia kisha aliondoka chumbani na kumuacha Sylvia akilia

“Kwakuwa mmenilazimisha, nitamfanya Robson ajutie kuniowa”

Alijisemea Sylvia kwa hasira kubwa sana.Siku iliyofuata ndiyo ilikuwa siku ya ndoa ya Robson na

Sylvia, Robson alikuwa mwenye kufurahi sana wakati Sylvia akiwa mwenye kuchukizwa lakini mbele za Watu alionesha tabasamu, Sylvia alikumbuka jinsi alivyokutana na Robson kwa mara ya kwanza.

Alikutana naye chuoni Udom, wote walikuwa wakisomea masuala ya fedha. Walijenga urafiki kwa zaidi ya miaka miwili, Mwaka wa tatu Robson alimueleza Sylvia kuwa anampenda, kutokana na urafiki wao Sylvia alimwambia Robson

“Siwezi kuwa na mahusiano na wewe sababu sisi ni marafiki, pia unajuwa kuwa nina Mtu wangu Robson” Alisema Sylvia

“Mtu wako amekutelekeza yupo nje ya Nchi kwa zaidi ya mwaka bila mawasiliano na wewe, unaweza vipi kujihesabu kuwa upo naye? Alafu kuhusu urafiki wetu nina imani tukiwa wapenzi tutazidi kupendana” Alisema Robson

“Hilo haliwezekani Robson, nakuchukulia kama rafiki yangu, nakupenda kama rafiki na si vinginevyo”

“Sylvia ninayosema yanatoka ndani ya moyo wangu, tafadhali kubali kuwa wangu” Alisema Robson, Sylvia alimtazama Robson kisha alimuuliza

“Itakuwaje kama Brahama atarudi Tanzania?”

“Kama atarudi nipo tayari kukuacha uendelee naye Sylvia”

Alisema Robson, kutokana na sharti hilo Sylvia alikubali kuwa na Robson, Mapenzi yao yalikuwa ya kuvutana sana sababu bado Sylvia alikuwa akimuwaza sana Brahama ambaye alikuwa ndiye Mwanaume wake wa kwanza.

Zilikuwa ni kumbukumbu za Sylvia akiwa anajiandaa kuelekea kanisani, alishika simu yake akajaribu kuipiga namba ya Brahama lakini haikupatikana, kisha akamtumia meseji Robson akamuuliza

“Tunaenda kuwa Mke na Mume, unaikumbuka ahadi yako?” Baada ya kutuma ujumbe, Sylvia aliendelea kuvalia gauni la harusi, mara ujumbe uliingia

“Nakumbuka si kuhusu Brahama?”

“Ndiyo, kama atarudi kwa ajili yangu itakuwaje utakubali Matokeo?” Aliuliza Sylvia lakini ujumbe wake haukujibiwa na Robson hadi muda ambao alikuwa tayari amemaliza kujiandaa

Gari lilipofika waliingia kwenye gari, familia ya Sylvia ilienda kanisani Magomeni, muda wote Sylvia alikuwa akijaribu kumpigia Brahama lakini simu haikupatikana, Mama yake Sylvia aligundua kuwa Mwanaye hana furaha kabisa, alimshika na kumwambia

“Tuliza akili yako Sylvia kwani unaenda kupiga hatua kubwa sana katika Maisha yako” Alisema Mama yake Sylvia baada ya kugundua Mwanaye hayupo sawa , Robson na familia yake walikuwa wa kwanza kufika kanisani, hakika alipendeza sana kwa nje lakini ndani ya moyo wake alianza kuwa na mashaka kutokana na zile meseji ambazo alitumiwa na Sylvia muda mchache kabla ya kuingia kanisani.

Shangwe na vigeregere viliibuka kanisani baada ya Familia ya Sylvia kuingia kanisani, waliopiga vigeregere hawakujuwa mioyo ya Sylvia na Robson ilikuwa kwenye msuguano mzito sana, wao walifurahia kuona Robson anamuowa Sylvia, taratibu zilifanyika kikamilifu.
 
Endelea

SEHEMU YA PILI-02

Padre alifungisha ndoa hiyo, ndoa ilifungwa siku ya Jumanne, saa nane Mchana, Padre aliwatangazia kuwa Wao ni Mume na Mke hivyo wanapaswa kuvumiliana kwa shida na raha, Sylvia alimsogelea Robson kama anataka kumbusu kisha alimnong’oneza kuwa

“Tumeshakuwa Mke na Mume” Alisema Sylvia kisha alitabasamu.

Waliondoka kanisani, sherehe nyingi zilifanyika ili kufurahia ndoa hiyo iliyojaa mpasuko ndani yake

“Sylvia! Nilipanga kukupeleka fungate Kilimanjaro na Mwanza”

Alisema Robson wakiwa chumbani usiku wa ndoa yao

“Mh! Kwanini umechagua Kilimanjaro?”

“Kwasababu ni sehemu niipendayo, naamini pia utaipenda sana, itatufanya tuzike tofauti zote na tujione kama tumezaliwa upya ili tule matunda ya ndoa yetu” Alisema Robson, Sylvia alikuwa akisoma kitabu akamjibu Robson

“Sawa”

Robson alimpenda sana Sylvia, alijiapiza kuwa atafanya kila awezalo ili Sylvia amsahau Brahama. Siku iliyofuata waliondoka Dar kwa ndege ya shirika la Air Tanzania hadi Kilimanjaro, ilikuwa ni safari iliyofanya vichwa vyao vijione vinaenda kuwa sawa!

“Karibuni Kilimanjaro, tunaweza tukawatembeza mbugani kwa gharama nafuu sana” Alisema Mwanamke mmoja aliyeonekana kuwa wakala wa kampuni ya Utalii, Robson alimtazama Sylvia akamwambia

“Unaonaje?”

“Ni sawa tu” Alijibu Sylvia

“Samahani tulikuwa tunahitaji Chumba karibu na Mlima Kilimanjaro na hiyo huduma ya utalii, kwa siku tano itakuwa shilingi ngapi?” Aliuliza Robson, ilikuwa ni mara yake ya kwanza kufanya safari ya Kwenda mlima Kilimanjaro

“Gharama ya chumba inategemea na aina ya huduma mzitakazo, zipo za laki tano kwa siku hadi milioni mbili kwa siku, kuwatembeza ni gharma ndogo tu hivyo msiumize kichwa” Alisema Mwanamke huyo

Robson na Sylivia waliridhia kuambataba na Kampuni hiyo hadi Mlima Kilimanjaro, walipata Hoteli nzuri ambayo iliwapa urahisi wa kuuona Mlima Kilimanjaro kwa ukaribu zaidi, nyuso zao zilitabasamu sana kama ambavyo Robson alisema huwenda safari hiyo ikazika tofauti zao, ndani ya siku moja ya kuwa

hapo ilionekana wazi Fungate inaenda kuimarisha ndoa yao.

“Umeona palivyo pazuri?” Aliuliza Robson wakiwa wamekaa baada ya hekaheka za safari kwisha

“Ndiyo pazuri sana nimefurahi” Alijibu Sylvia huku akiwa mwenye kutabasamu, mabusu na mahaba moto moto yalifuatia kuonesha ni jinsi gani tofauti zao zilivyozikwa na safari hiyo.

“Sijutii kukuooa Sylvia, unanifanya niwe mwenye furaha zaidi tokea mara ya kwanza nilipokuona chuo” Alisema Robson, Sylvia alimtazama Robson, mara nyingi hakupendelea kukumbuka mambo ya chuo sababu humkumbusha kuhusu Brahama ambaye yupo nje ya Nchi, Mwanaume aliyempenda kuliko Wanaume wote Duniani, Sura ya Sylvia ilibadilika akawa mnyonge ghafla

“Dear kuna tatizo?” Aliuliza Robson

“Sipendi kukumbushwa kuhusu Chuo Robson, nakumbuka mengi hivyo sihitaji kuyakumbuka yote yanayoumiza moyo wangu”

Alisema Sylvia

“Pole Mke wangu” Alisema Robson kisha alimkumbatia Sylvia mithili ya Kuku anavyokumbatia kifaranga chake.Fungate yao ilienda vizuri wakiwa Kilimanjaro, walitembea mbugani kuzunguka Mlima Kilimanjaro, ilikuwa ndiyo mara ya kwanza kwao kuona wanyama hasa Twiga ambao hupendezesha mandhari ya Mlima Kilimanjaro, Baada ya siku tano waliondoka wakaenda Mwanza kumalizia fungate yao.

Huko walikuwa na marafiki waliosoma wote, walipanga kwenye apartment kwa siku tano za kuishi Mwanza. Siku moja Sylvia alitoka kwenda kununua matunda kwenye moja ya masoko huko Mwanza, alimuacha Robson akiwa na rafiki yake.

Alipofika huko Sylvia alikutana na rafiki yake wa muda mrefu waliyesoma wote chuo

“Eeeeh siamini Mage kama nimekuona tena jamani” Alisema Sylvia

“Haaa Usijali Bwana, Milima pekee ndiyo haiwezi kukutana, kwanza ukutane nami kwa lipi Sylvia wakati umeamua kutukimbia” Alisema Mage, Sylvia alishusha pumzi zake kisha akamvuta Mage pembeni

“Unamaanisha nini Mage?” Aliuliza Sylvia

“Brahama ndiye aliyetufanya tukajuwana, nimesikia umeolewa na Rafiki yako Robson, ina maana mmekuja kuishi Mwanza?” Aliuliza Mage, Sylvia aliposikia kuhusu Brahama alipoa kidogo, alionekana kuwa mnyonge sana

“Hapana tunaishi Dar Mage, ningefanya nini Mage wakati Brahama alinipotezea, alipoondoka kwenda Ulaya kwa wazazi wake hakupatikana kwa zaidi ya Mwaka mzima, ikabidi niingie kwenye mahusiano na Robson” Alisema Sylvia akiwa analengwa na mchozi

“Mbona unaniambia stori nyingine na Brahama anasema stori nyingine?”

“Kwani unawasiliana na Brahama?” Aliuliza Sylvia

“Ndiyo!! Brahama yupo hapa Mwanza kwa zaidi ya wiki mbili, alisikia kuhusu wewe kuolewa” Alisema Mage

“Unasemaje? Brahama yupo Tanzania?”

“Siyo Tanzania tu bali ni hapa hapa Mwanza ambapo nyie mmekuja” Alisema Mage, moyo wa Sylvia ulianza kuweweseka kwa jinsi alivyompenda Mwanaume huyo.

“Mungu wangu kwanini hakunitafuta?”

“Angekutafuta vipi Sylvia na tayari wewe ni Mke wa Mtu, yaani ulishindwa hata kunipa taarifa juu ya wewe kufunga ndoa na Robson?” Alisema Mage kisha alijishika kiuno

“Nisamehe kwa hilo Mage, ndoa yenyewe aaaah!!!”

“Aaah!! Nini?”

“Tuachane na hilo basi mwambie Brahama kuwa namfikiria sana Mage, naomba namba yako basi” Alisema Sylvia kisha alimpatia simu Mage

“Sylvia Mtoe kabisa Brahama kwenye fikra zako sababu wewe ni Mke wa Mtu, hata hivyo mimi siwezi kumwambia kama. Nimekutana na wewe Sylvia, sitaki kuwa sababu ya kuvuruga ndoa yenu changa” Alisema Mage

“Mageee!!! Unasema nini sasa aaaah!!”

“Sylvia naomba niende tutaongea” Alisema Mage akiwa mwenye haraka kisha aliondoka zake

“Mageeee!! Mageee!!”

“Tutaongea Sylvia” Alisema Mage kwa sauti ya kuondoka, alimuacha Sylvia akiwa mwenye mawazo sana Kichwani pake, aliitazama pete ya ndoa kisha aliendelea kununua alivyovihitaji katika soko hilo, kisha alirudi Hotelini ambako alimuacha Robson akiwa na rafiki yakeSylvia alipita bila kumsemesha chochote Robson wala rafiki yake Robson kitu ambacho kilimshangaza Robson, alimuona Sylvia akiwa mnyonge mno tena mwenye maumivu ya ndani

“Hebu subiria niongee naye!!” Alisema Robson kisha alielekea jikoni ambako Sylvia alienda

“Mke wangu una nini?” Aliuliza Robson

“Siko sawa Rob!! Naomba tu uniache nipate muda wa kupumzika”

Alisema Sylvia kisha alielekea chumbani, Robson alimfuata Sylvia huko huko Chumbani

“Huwezi kuniambia?”

“Nikwambie nini Robson?”

“Ooooh! Shit….sawa akili yako ikitulia utaniambia” Alisema Robson kisha alirudi sebleni alipokuwa amekaa na rafiki yake.

Sylvia akiwa chumbani alijikuta akikumbuka mambo mengi sana kuhusu Udom, hasa alimkumbuka sana Brahama Mwanaume ambaye nafsi yake haiwezi kukana kuwa anampenda sana, alipekua simu yake akaitafuta namba ya Mage ambaye ndiye aliyempa taarifa za Brahama kule sokoni kisha akamtumia meseji

“Mambo Mage ni Mimi Sylvia” Aliutuma kwa Mage lakini haukujibiwa, Sylvia alijikuta akiwa katika nyakati ngumu sana katika maisha yake.

Aliporudi sebleni Robson alionekana naye kutokuwa sawa, mchana ulikuwa umeingia akamwambia rafiki yake

“Tutaonana wakati mwingine” alisema akiwa amekunja sura yake huku mikono yake ikipikicha sura hiyo pana iliyo na ngozi laini

“Kwani shemeji amepatwa na nini Kiongozi?” Aliuliza rafiki yake Robson

“Nimekwambia nenda tutaonana Bwana, Mimi ni Mume wa Mtu siyo mshikaji tena hivyo siwezi kufunguka kuhusu ndoa yangu”

Alisema Robson akionekana kumbadilikia rafiki yake, haikuwa mara ya kwanza kwa Robson kuwa hivyo kwani mara kadhaa amekuwa akiwa mwenye hasira pindi anapokuwa hayupo kwenye maelewano mazuri na Sylvia

“Si tutaonana jioni?” Aliuliza rafiki yake huyo

“Hivi huwezi kumsoma Mtu kiutu uzima Mzee, nenda basi” alikereka zaidi Robson, alimpa upenyo rafiki yake kutimka hapo kisha Robson alituliza akili yake akajiuliza

“Nini kimemvuruga Sylvia, amekutana na nini huko sokoni, yaani kama kuna Mtu amemkwaza nipo tayari kutoa roho ya Mtu”

Alijisema Robson ndani ya Nafsi yake kisha alishushia na maji kisha alijiegemeza kochini, kabla hajapata utulivu alioukusudia, Sylvia aliingia hapo Sebleni akiwa mwenye kumtazama Robson kwa jicho lenye ukakasi kidogoRobson alijiweka sawa akamuuliza Sylvia

“Una nini Mke wangu?” Alihoji kwa utaratibu kama siyo yeye aliyemfokea rafiki yake muda mchache uliopita, Sylvia aliketi bila kusema chochote huku ndani yake akiwa kwenye vita kubwa, alijiuliza amweleze Robson kuwa Brahama amerejea Nchini au akae kimya, alijiwazia kwa sekunde kadhaa kabla ya kupata jibu


 
SEHEMU YA TATU – 03

“Sikwambii chochote hadi nizungumze na Brahama niusikie msimamo wake juu yangu” Alisema Sylvia ndani ya moyo wake kisha alikunjua tabasamu wakati huo simu yake ikiingia ujumbe, alichungulia akaona ni Mage, pale kwa juu aliusoma ujumbe uliosomeka

“NIMEONGEA NA BRAHAMA AMESEMA KESHO MNAWEZA ONANA” Meseji hiyo iliongeza Bashasha kwa Sylvia ambaye alimtazama Robson

“Ghafla tu umekunjua nafsi yako, umesoma nini?” Aliuliza Robson

“Aaah! Hamna nilikuwa nawasiliana na Fifi ameniambia nikirudi atanipa ofa ya kusuka bure” Alisema Uwongo Sylvia

“Oooh kumbe, sasa ni jambo gani lililokufanya ukawa mnyonge, au kuna Mtu amekukwaza huko sokoni?” Aliuliza Robson, Sylvia alitikisa kichwa kwa ishara ya kukataa kuwa hakuna aliyemkwaza

“Sema ukweli Mke wangu yaani kwa ajili yako nipo tayari kwa lolote lile” Alisema Robson na kumfanya Sylvia atabasamu.

“Ngoja nipike basi” Sylvia aliaga kisha akaelekea jikoni, alimuacha Robson akiwa mwenye furaha sana, alijitanua kochini kama tajiri fulani, aliithamini sana furaha ya Sylvia kuliko chochote kile katika Maisha yake.

Alipofika jikoni Sylvia alimtumia ujumbe Mage kisha simu akaiweka Sailenti ili Robson asisikie chochote kile

SYLVIA: Unasema kweli Mage?

MAGE: Wallah sikuongopei, tulipoachana alinipigia Brahama nikaona ni bora nimweleze

SYLVIA: Alifurahi eeeh?

MAGE: Mtaongea wenyewe Bwana!

Jumbe hizi ziliacha tabasamu zito sana kwa Sylvia.Usiku ulipoingia Brahama alimpigia simu Mage wakapanga kuonana ili wazungumze kuhusu Sylvia, walikutana kwenye Baa moja wakaagiza vinywaji ili wazungumze

“Brahama hivi unajuwa Sylvia anakupenda kufa kabisa?” Alisema Mage akiwa anafungua kinywaji, Brahama alicheka kisha alizungumza

“Kwanini unasema hivyo, angekuwa ananipenda ndiyo angeolewa na Robson. Yaani nyie Wanawake sijui mkoje, nakumbuka Tulipokuwa chuo Siyvia alisema Robson ni rafiki yake tu na hawana mahusiano, kumbe alikuwa ananizuga Mimi” Alisema

Brahama akiwa anagida unywaji

“Hayo ni mawazo yako tu, hebu fikiria umeenda ulaya umekaa bila kumtafuta Sylvia lakini Mtoto wa Watu anakupenda hadi hivi leo tena kachanganikiwa kusikia umerudi Tanzania, na kuhusu Robson kwa jinsi alivyonisimulia ni kuwa walianzisha mahusiano baada ya wewe kumtelekeza”

“Hana lolote si angenisubiria sasa kwanini kaolewa, mbona Mimi sijaowa?”

“Ha!ha!ha! Najuwa unamfikiria Sylvia ndiyo maana hujaowa”

Alisema kwa utani Mage wakiwa wanakula sato aliyekaangwa

“Labda lakini sijui, mimi nilipoondoka sikujuwa kama ningerudi hivyo niliona mapenzi ya mbali siyo mapenzi ya kuyategemea” Alisema Brahama aliyekuwa na nywele nyingi kama Muarabu wa Msiri

“Tuachane na hilo, nimemwambia Sylvia kuwa unahitaji kuonana naye kesho hivyo ujiandae”

“Eeeh yaani wewe mbona unafanya mambo kwa kukurupuka hivyo Mage, yule ni Mke wa Mtu alafu wapo kwenye fungate ujuwe”

“Tatizo lako nini Brahama wakati Mtoto anakuzimia?”

“Mh! Haya Dada wa mipango”

Walizungumza mengi, walikula na kunywa. Usiku ulipokuwa mwingi waliondoka wakiwa wamelewa sana. Brahama alienda kumwacha Mage nyumbani kwake kisha yeye akalekea kwake usiku huo.

Upande wa pili, Fungate iliingia mdudu, Usiku kucha Sylvia alikuwa akifikiria namna itakavyokuwa atakavyoonana na Brahama kwa mara ya kwanza baada ya mwaka kupita, alikesha akiwa anamsikia Robson akikoroma hadi kulipo pambazuka.

“Kesho tunarudi Dar Mke wangu, mchana nitafwatilia tiketi ya ndege” alisena Robson akiwa amejilaza

“Eeh mbona ghafla?” Aliuliza Sylvia

“Kuna mambo ya kufwatilia kazini, hata hivyo Tulienjoi sana Kilimanjaro, huku Mwanza hata sijaona kipya” Alisema Robson, moyoni Sylvia alichukia hakupenda kabisa kuondoka Mwanza tena alitamani hata wangehamia Mwanza kabisa ili awe karibu na Brahama

“Sawa Mume wangu, kama ni hivyo itabidi nifanye maandalizi” alisema Sylvia, Robson alimvuta Sylvia akamlaza kifuani kisha akamwambia

“Wewe ndiyo furaha yangu Sylvia usije ukaenda mbali na Mimi sababu nitakuwa tayari kufanya chochote kile” Alisema Maneno ambayo yalimfanya Sylvia atabasamu tu bila kusema chochote kile.

Mchana ulipofika Robson alimuaga Sylvia kuwa anaenda kushughulia tiketi ya ndege pia kuna baadhi ya vitu akanunue kama zawadi watakaporejea Dar, hakujuwa nyuma yake Sylvia alijiandaa haraka sana akampigia simu Mage kuwa yupo tayari kuonana na Brahama

“Haya uje Kongwa House, ukifika hapo utaona nyumba inauzio wa ukuta mrefu wa bluu” Alisema Mage

“Enhee baada ya hapo?”

“Ndiyo hapo utanikuta”

“Haya powa Mage natoka sasa hivi sababu Robson ameenda kukata tiketi ya ndege ili kesho turudi Dar hivyo ni muhimu nionane na Brahama leo hii” alisistiza Sylvia

“Haya poa” Alijibu Mage kisha Sylvia alikata simu hiyo, haraka alitoka akachukua tax kuelekea alipoelekezwa huku akiwa anawasiliana na Robson kujuwa amefikia wapi

“Ndiyo naelekea ofisi zao” alisema Robson kwa njia simu. Ilimpa amani Sylvia kuwa atawahi kurudi kabla ya Robson kurudi

“Dereva unaweza kutafuta njia ya mkato maana umesema ni mbali na leo ni Jumatatu si kutakuwa na foleni?” Aliuliza Sylvia

“Foleni? Unazungumzia Mwanza hii au Mwanza gani? Hapa siyo Dar Dada yangu….” Alisema dereva huyo ambaye alionekana kujiamini sanaa

“Ha!ha!ha! Sawa ila ni muhimu nifike mapema” Alisistiza Sylvia, dereva wa Tax alimuondoa Sylvia wasiwasi kabisa, kweli Dereva alikanyaga mafuta kwa kasi kuelekea huko alipoambiwa na Sylvia

Walipofika karibu na njia panda iliyogawa barabara tatu, moja ya kuelekea Kongwa House ambapo walikuwa wakienda, walisimamishwa na askari wa Barabarani

“Ooooh yaani hawa askari wa Mwanza” Alisema Dereva akiwa anashuka ili azungumze na askari huyo, muda ulizidi kwenda,

Mage alikuwa akimpigia sana simu Sylvia kuwa mbona hafiki

“Tumekamatwa na askari wa Barabarani hapa njia panda Mage, ila nakuja” Alisema Sylvia kisha alikata simu ya Mage, akawa anaangalia saa na kumwangalia yule dereva aliyekuwa akiongea na polisi, aligundua huwenda wakachukua muda mrefu, alimuita yule dereva

“Samahani Kaka nina haraka sana hivyo naenda” Alisema Sylvia kisha alimpatia yule dereva pesa kidogo ya kumtoa Hotelini hadi hapo waliposimamishwa

“Si ungesubiria kidogo Dada yangu, muda siyo mrefu namalizana na yule askari”

“Hapana nitachelewa”

“Haya sawa!!” Alisema Stlvia kisha alianza kutembea kutafuta Bodaboda, mara simu yake iliita, alijuwa ni Mage ndiye aliyekuwa akimpigia, aliipokea bila hata kuangalia ni Nani aliyekuwa akipiga sababu kilikuwa kisimu kidogo alafu alikuwa barabarani

“Mage nakuja nipo hapa Njia panda, mnisubirie” Alisema Siyvia kisha alikata simu, kumbe aliyekuwa amempigia Sylvia hakuwa Mage bali alikuwa ni Robson, ilimchanganya sana Robson akajiuliza Mke wake anaenda wapi wakati Mwanza wao ni wageni,

Robson alichukua pikipiki bahati nzuri alikuwa ameshamaliza kukata tiketi, alirudi Hotelini huku akipiganisha akili Mke wake ameenda wapi, alimpigia simu lakini Sylvia hakupokea simu ya Robson.

“Mage! Mage! Ni Mage yupi huku Mwanza?” Alijiuliza Robson huku akizunguka sebleni, alipotuliza akili akamkumbuka Mage rafiki yake Brahama ambaye walisoma naye, yeye pekee ndiye aliyekuwa akiishi Mwanza, Sasa akajiuliza

“Ina maana Brahama yupo Tanzania, kwanini amesema mnisubirie kama anaenda kuonana na Mtu mmoja angesema nisubirie na sio mnisubirie, basi itakuwa anaenda kuonana na Brahama” Alijisema Robson, mawazo yake yalienda sawa kabisa na jinsi alivyofikiria

Muda huo Sylvia alikuwa ameshafika Kongwe House, alifuata maelekezo hadi alifika nyumbani anakoishi Brahama, Mage alifungua geti

“Waoooo karibu sana Sylvia” Alisema Mage akiwa anamkubatia

Sylvia, tabasamu zilitanda kwenye nyuso zao

“Asante Mage kumbe unaishi hapa?”

“Hapana hapa ni kwa Brahama”

“Oooh Mungu wangu moyo unanienda mbio Mage” Alisema Sylvia

akionekana mwenye hofu ya kumwona Brahama

“Usijali Sylvia, Brahama yupo ndani anakusubiria wewe tu”

Alisema Mage, basi waliongozana taratibu hadi ndani.

Sylvia alifanikiwa kunwona Brahama kwa mara ya kwanza baada ya Mwaka mmoja wa kutokuwa na mawasiliano naye, mwili wa Sylvia ulitokwa na jasho, jinsi alivyokuwa akimpenda Brahama alijikuta akidondosha chozi, Mage aliondoka ili awaache wawili hao wapate kuzungumza, Brahama alimkumbatia Sylvia ili amtulize maana aligundua Mwanamke huyo alikuwa na furaha sana kuliko hata maelezo.
 
SEHEMU YA NNE -04

“Sylvia” Aliita Brahama

“Brahama ni wewe?” Alihoji Sylvia huku chozi likiendelea kumbubujika

“Ndiyo ni Mimi, nisamehe kwa kukata mawasiliano, sikutaka uumie sababu nilienda mbali na sikujuwa kama ningerudi Tanzania” Alisema Brahama akiwa anachezea nywele za Sylvia

“Unajuwa ni jinsi gani nimekusubiria Brahama hadi nikakata tamaa?”

“Najuwa Sylvia ndiyo maana ulichaguwa kuolewa na rafiki yako, nimesikia yote, hata hivyo sikutegemea kama ningekuona tena” Alisema Brahama kisha waliachana, wote waliketi.

“Bado unanipenda Sylvia?” Aliuliza Brahama swali ambalo lilijaa mtego akiwa anatambuwa fika kuwa Sylvia anampenda sana ndiyo maana alikubali kuja kuonana naye, chozi lilikuwa likiendelea kumbubujika Sylvia ambaye alishindwa amjibu nini Brahama kwani bado moyo wake ulikuwa ukimpenda sana Mwanaume huyo.

Sylvia alifuata chozi lake lililobubujika kisha alisikia simu ikiita, haraka alifungua pochi na kuangalia ni nani aliyekuwa akimpigia

“Mungu wangu!” Alisema Sylvia baada ya kuona Robson ndiye aliyekuwa akimpigia, aliiacha iite hadi ilipokata

“Nani anakupigia?” Aliuliza Brahama huku akiwa anautazama uzuri wa Sylvia

“Ni Robson, Brahama naenda” alisema Sylvia

“Sawa ushakuwa Mke wa Mtu sasa hivi” alisema Brahama, Sylvia alinyanyuka huku akiendelea kuiangalia simu yake, aliona Missed Calls zaidi ya tatu za Robson, hofu yake ikawa huwenda

Robson atakuwa amerudi, ilikuwa hivyo hivyo Robson alikuwa amesharudi.

Alipofika nje alimpigia Robson

“Mume wangu!!” Alisema Sylvia

“Naam!!”

“Samahani kwa kutopokea simu sababu ilikuwa mbali na nilikuwa na kazi kidogo” Alisema Sylvia, Robson hakutaka Sylvia ahisi chochote kile

“Oooh nimefanikiwa kupata tiketi mbili za kurejea Dar kesho”

“Oooh pole kwa pilika”

“Sawa!! Niandalie chakula basi” Alisema Robson

“Haya ndiyo nipo Jikoni hapa” Alisema Sylvia

“Haya nakuja” Alisema Robson,,Simu ilipokatika haraka haraka Sylvia aliita Bodaboda ili arejee Hotelini, Robson alidondosha chozi, akapiga moyo konde kisha alitoka Hotelini, aliacha funguo mapokezi.

Kwasababu Sylvia alichukua pikipiki wala hakuchelewa sana aliingia Hotelini, alichukua funguo kisha aliingia kwenye Apartment yao, alifanya haraka akabadilisha nguo kisha akaenda jikoni kuandaa chakula akiamini Robson alikuwa hajarudi kumbe Robson alikuwa amesharudi,

Baada ya kutoka hapo Robson alienda kwa rafiki yake akiwa mwenye msongo wa mawazo

“Mzee unapitia jambo gani? Japo ulisema sipaswi kukuingilia sababu wewe ni Mume wa Mtu ila hauonekani kuwa sawa kabisa” Alisema Rafiki yake Robson ambaye alikuwa akiishi Mwanza

“Acha Richard, hivi Mage anaishi hapa Mwanza?” Aliuliza Robson ili apate uhakika wa kile alichokisikia

“Mage yupi?”

“Yule demu mrefu ambaye alikuwaga na Mashauzi chuo?”

“Anhaaa yule Twiga” alisema Richard kisha alicheka

“Kwanini unacheka?”

“Samahani, yule ndiyo anaishi hapa Mwanza” Alisema Richard kisha alimuuliza Robson

“Ulikuwa una shida naye?”

“Hapana, ndiyo, sijui hata nikupe jibu gani lakini usijali Ahsante” Alisema Robson kisha aliondoka hapo akimwacha Richard akiwa haelewi ni kwanini Robson alimuulizia Mage.

Robson alirejea Hotelini akionekana kuwa mwenye furaha sana, alimkuta Sylvia akiwa anapika, alisimama mlango wa jikoni akamtazama Mke wake ambaye alikuwa hana habari kama Robson alikuwa amerudi, alisogea akamkumbatia kwa nyuma

“Oooh umenishtua” Alisema Sylvia akionekana kujawa na furaha isiyo pimika

“Pole Mke wangu, unapika nini?” Aliuliza Robson

“Makange ya samaki, naamini utayafurahia. Pole kwa uchovu, basi ungeenda kupumzika wakati namalizia hapa” Alisema Sylvia

“Haya sawa kuwa Muangalifu”

“Nawe pia Baby” Alijibu Sylvia, Robson aliingia chumbani, Jinamizi la Maswali na mawazo lilirudi tena kwake.

“Ina maana Brahama yupo Tanzania?” Alijiuliza Sana Robson, aliamini kurejeaa kwa Mwanaume huyo Tanzania kunaweza kusababisha ndoa yake kuharibika, alikumbuka ahadi ambayo aliitoa kwa Sylvia kuwa endapo Brahama atarejea basi yupo tayari kumwachia Sylvia, hilo lilimuumiza sana.

Akapata wazo la kukagua simu ya Mke wake ili ajiridhishe kuwa alikuwa akiwasiliana na Brahama, aliposhika simu aligundua iliwekwa namba za siri kitu ambacho hakikuwahi kutokea kabla, akajaribu simu kubwa nayo akakuta ina namba za siri.

Alihisi moyo wake unaungua taratibu, hakupata tulizo la nafsi yake kabisa, alijilaumu kwanini alikuja Mwanza kwenye Fungate, aliamini kama asingelienda Mwanza basi Sylvia asingekutana na Mage maana alikuwa akifahamu fika kuwa Mage alikuwa na ukaribu sana na Brahama.

“Nitaipigania ndoa yangu sitajali chochote, Sylvia ni halali yangu mbele za Mungu” Alijisemea Robson huku akipanga zaidi kutaka kuujuwa ukweli kuhusu Mke wake pasipo kugundulika.

Siku iliyofuata, Robson na Sylvia walikanyaga ardhi ya Jiji lenye joto na starehe yaani Dar-es-salaam, walitumia ndege ya shirika la Air Tanzania, Sylvia alionekana kuwa mwingi wa mawazo, Robson hakutaka kumuuliza sababu alishaanza kufanya utafiti Binafsi wa kutaka kujuwa kama Brahama amesharudi Tanzania.

Maisha yaliendelea, siku moja Robson alimtafuta Mark ambaye alikuwa ni rafiki yake Mkubwa, alihitaji msaada wa kimawazo zaidi japo kuna wakati alitamani kwenda kumwona mtaalam wa masuala ya Saikolojia ili amuweke sawa lakini aliona ni bora azungumze na Mark kuhusu Sylvia, siku hiyo kulikuwa na parti ya rafiki zake Mark, Robson alimuelekeza Mark kuwa waonane mahali pengine lakini Mark alimsistiza kuwa hapo alipo hakuna shida kuna sehemu tulivu sana.

Baada ya muda wa kazi Robson alienda kuonana na Mark, aliuliza baadhi ya Watu akaoneshwa

mahali tulivu ambapo Mark alikuwepo

“Bwana harusi” aliita Mark baada ya kumuona Robson akiingia, ilikuwa ni katika hali ya utani, alitegemea Robson angeingia kwenye utani pia lakini haikuwa hivyo

“Upo sawa Rob?” Aliuliza Mark ambaye alivalia pensi na raba nyeusi

“Nipo sawa sababu bado napumua lakini kiuhalisia Kaka Mimi ni Mfu Mtu” Alisema Robson, Mark alishangaa

“Ulisema hakuna kitu kinachoweza kukupa furaha Duniani kama kufunga ndoa na Sylvia, kutokuwa sawa kunatokana na nini?” Alihoji huku Muziki kwa mbali ukiendelea kusikika

“Ni kweli Sylvia ndiye mwenye funguo ya furaha yangu lakini ndiye anaye nifanya niwe katika hali hii Mark, kwa kifupi ndoa yangu inaenda kuingia doa muda siyo mrefu” Alisema Robson

“Unamaanisha nini?”

“Nahisi Sylvia anawasiliana na Brahama”

“Unasemaje?”

“Ndiyo! Nimeligundua hili Tukiwa Fungate Mwanza, inaonesha dhahiri kuwa amerejea Tanzania”

“Mmh!! Mzee una uhakika na hilo?”

“Nimelichunguza na hisia zangu zinaniambia hivyo Mark, haikuwa kawaida lakini simu zake ameweka namba za siri kitu ambacho hakuwahi kukifanya hata tulipokuwa marafiki,

inaonesha kuna mtu wa siri anawasiliana naye, unafikiria ni nani zaidi ya Brahama?”

“Kwanini unahisi Mtu wa siri ni Brahama?”

“Kuna siku tukiwa mwanza nilimpigia wakati huo nilienda kukata tiketi, kumbe nyuma alitoka na alipopokea simu yangu pengine hakuangalia ni nani anapiga nikamsikia akisema Mage nakuja mnisubirie, niliporudi nyumbani hakuwepo, sasa nilijaribu kutafiti nikagundua Mage yule dem tuliyesoma naye

chuo anaishi Mwanza na yule dem ana ukaribu sana na Brahama”

Alielezea Robson akiwa analengwa na mchozi

“Sasa usilie Rob, cha msingi kwanza ni kuhakikisha unachokihisi lakini pili kujuwa tunafanya nini maana

tukizubaa ataitumia ile ahadi yenu kukumaliza”

“Na hilo ndilo linaloninyima Usingizi Mark, sina raha sina amani, nadondosha chozi mbele yako sababu nimefikia mahali najiona ni mfungwa wa furaha yangu” Alisema Robson, Mark alimwambia

“Hebu njoo huku utulize msongo wa mawazo” Robson alimfuata Mark, wakaingia ndani ambako palikuwa na hiyo Parti

“Unatumia kinywaji gani?” Aliuliza

“Chochote tuu”

“Haya ngoja”. Mark alienda kumchukulia Robson pombe wakatafuta mahali wakakaa wakawa wanakunywa taratibu huku wakipiga stori

“Usilifikirie hilo sana kwasbabu litapata ufumbuzi endapo tutapata uhakika thabiti kuwa Sylvia anawasiliana na Brahama”

Alisema Mark katika hali ya kumuondoa hofu Robson ambaye alikuwa mwingi wa mawazo. Siku hiyo Robson alikunywa sana pombe hadi usiku akiwa na rafiki yake Mark, alikunywa hadi alihisi matatizo yameisha.

Baadaye Sylvia alimpigia simu Robson ili kujuwa yupo wapi

“Babuuu Mkeo anapiga” Alisema Mark akiwa tungi snaa

“Mke wako ananihusu nini Mimi, wewe ndiyo Mke wako siyo Mimi”

Alijibu Robson naye akiwa tungi, vicheko vya hapa na pale viliendelea huku wakizidi kupata urabu.



Hadi Mishale ya saa tano usiku walikuwa hawajitambui kabisa, walisaidiwa kuondoka hapo na rafiki zake Mark. Usiku huo Robson alilala kwa Mark hadi asubuhi alipoamka na kujishangaa, alimwamsha Mark

“Ebwanaa ina maana nimelala hapa?” Alihoji Robson

“Ndiyo jana tulilewa sana Rob, sijui hata tulifikaje huku, nilishtuka Alfajiri.” Alisema Mark

“Oooh Mungu wangu sijui Sylvia nitamueleza nilikuwa wapi”

Alisema Robson akiwa amejishika kichwa chake, pale pale simu ya Robson iliita, aliyepiga alikuwa ni Baba yake Mzazi,

Mstaafu wa Jeshi ambaye alikuwa akiishi Kimara Stop Over

“Kulikoni Mzee Kibu anipigie asubuhi?” Alijiuliza huku akimuuliza Rafiki yake Mark, walikuwa kitandani wakiwa wameketi, bahati nzuri siku hiyo ilikuwa ni Jumamosi hivyo hakuwa na presha kuhusu kwenda kazini

“Hebu pokea Kaka huwezi juwa anataka kusema nini” alisema Mark, Robson alifikiria mara mbili mbili akaona ni bora aipokee simu hiyo, akabofya kitufe cha kupokelea na mara moja akaiweka sikioni ili kusikia Baba yake alikuwa anataka kusema nini.

“Shikamoo Baba” Alisalimia Robson kisha alipiga mhayo

“Ina maana ndiyo unaamka sasa hivi Robson?” Aliuliza Mzee kibu

“Ndiyo Baba….”

“Mkeo anaendeleaje?” Aliuliza

“Aaah….Baabaaa…Sylvia yupo vizuri tu” alisema Robson kwa sauti ya kujiuma uma

“Mshenzi mkubwa wewe, sikuzaa kituko Mimi nina heshima zangu Robson, kama ulijiona huwezi kumudu kuishi na Mke kwanini ulioa mapema..??” Alifoka Mzee kibu na kumshtua Robson

“Babaa..”

“Ujana hujaumaliza Robson. Hebuu njoo haraka nyumbani kwangu kabla ya kwenda popote” alisema Mzee Kibu akionesha wazi alikuwa na taarifa ya Robson kulala nje ya nyumba.



“Oooh jesus, nini hiki ina maana Sylvia ameenda kunishtaki kwa Baba yangu?” Alijiuliza Robson huku akimpa nafasi Mark ya kutoa mawazo yake

“Ndiyo kusema anakupenda sana, basi kama ni hivyo hachepuki nje huyo” Alisema Mark

“Hebu acha ujinga Mark, Mwanamke anaweza akabadilika dakika sifuri tu. huwenda anajitengenezea mazingira ya kunipiga tukio, kwanini leo hakupiga kabisa, jana alipiga mara tatu tuu kama ushahidi” alisema Robson huku akinyanyuka lakini alihisi kizunguzungu

Alivalia nguo zake haraka haraka kisha alimwambia Mark

“Ngoja nikamsikilize Mzee kibu, kwa jinsi alivyofoka itakuwa Sylvia amemjaza maneno sana” Robson aliondoka nyumbani kwa Mark.

Akiwa Barabarani hakuacha kujiuliza maswali mengi yaliyomzonga, akakumbuka maneno ya Mark kuwa kama Sylvia ameenda kushtaki kwa Baba yake Basi huwenda hachepuki, lakini alijikanusha mwenyewe kwa kusema”Akili ya Mwanamke hainaga msimamo thabiti”

Alikanyaga mafuta, uzuri siku hiyo hakukuwa na msongamano mkubwa wa magari, hivyo alitumia wastani wa dakika kama 55 kutoka Kurasini hadi Kimara.

Muda huu alikuwa akiegesha gari yake kwenye maegesho ya magari, aliposhuka alisimama kidogo ili kujiambia majibu ambayo atampa Baba yake, mlangoni aliona viatu vya Sylvia, haikushia hapo alihisi Pafyum ya Sylvia, ilimpa uhakika kuwa Sylvia alikuwa hapo.

Alivuta kitasa akaingia ndani, akakuta Familia ikiwa inamsubiria sebleni, alikuwepo Mama yake Robson, Baba yake na Sylvia.

“Shikamoo Mama!” Alisalimia Robson

“Marahaba!!” mama yake aliitikia

“Baba nimekuja” Alisema Robson akiwa anaketi kando ya Mke wake

“Nafikiri hakuna haja ya Sylvia kujieleza tena, harufu ya pombe inayotoka kinywani mwako ni ishara tosha kuwa simu yangu ndiyo iliyokuamsha” Alisema Baba yake Robson

“Hivi Robson unaweza ukasema ulikuwa wapi Mwanangu? Ndoa changa lakini tayari tumeshaanza kusuluhisha kweli?” Alisema Mama yake Robson

“Haina haja ya kuzungumza na huyu mshenzi kwa lugha nzuri, Robson unakumbuka ni wewe uliyesema umepata tulizo la moyo wako na unahitaji kufunga ndoa? Ulilazimishwa au kuna Mtu alikusukuma ukaoa bila ridhaa yako? Ndoa ya juzi tu tayari umeanza kulala nje?” Alisema Baba yake Robson kwa suati kali

sana, Silvia akaingilia kati

“Baba inatosha, nilikuja sababu sikutaka muone namuonea Robson, nilitaka mpate uhakika….mengine nitaongea naye…Naamini tutayamaliza” Alisema Sylvia

“Unaona jinsi ulivyopata Mke mzuri na anayejuwa nini Mama ya kuwa Mke wa Mtu? Lakini wewe ni hovyo sana Robson, hovyo kabisa” Alisema Baba yake Robson, ni wazi alichukia sana

“Baba na Mama poleni kwa usumbufu, ngoja tuwaache” Alisema Sylvia kisha alimshika mkono Robson wakatoka, walipofika kwenye gari ukimya uliendelea, hadi wanafika nyumbani kwao hakuna aliyesema na mwenzake.Robson bado alikuwa na lile wazo kuwa Sikvia anachepuka na Brahama.

“Hivi umelala wapi Robson?” Aliuliza Sylvia baada ya kuingia ndani

“Kabla sijakujibu nilikuwa wapi Sylvia nataka uniambie ni kwanini simu yako ina namba za siri anbazo Mimi sizijui” alisema Robson, hakutaka kushuka chini kabisa

“Robson tokea lini ukaanza kupekua simu yangu?” Alihoji Sylvia

“Kwasababu sikuamini Sylvia” alijibu Robson

“Oooh Nani anapaswa kutomuamini mwenzake kati yangu Mimi na wewe uliyelala nje ya nyumba bila taarifa tena unarudi unanuka pombe?”

“Sylvia usinifanye kama Mtoto mdogo, usinione mimi zezeta, najuwa kuna jambo unalonificha ila nakuapia muda siyo nrefu nitapata majibu ya hilo unalolificha” alisema Robson kisha aliingia chumbani, alimpa maswali mazito Sylvia, alijiuliza mengi akiwa amesimama lakini baadaye naye aliingia chumbani.

Doa likaingia kwenye ndoa ya Robson na Sylvia huku kila mmoja akifikiria kimpango wake, hakuna aliyetaka kujishusha sababu Sylvia alikuwa akiamini anapendwa sana na Robson hivyo hawezi kufanywa chochote wakati huo Robson akimuona Sulvia ni Msaliti, japo kulikuwa na ahadi kati yao.
 
SEHEMU YA TANO-05

Haikua utani kwa Brahama, alipomuona Sylvia alianza kumpenda upya kama zamani, tena alijilaumu kwanini aliondoka Tanzania, alijiona mjinga sana. Siku mbili aliishi kwa kumuwaza sana Sylvia, Mage alikataa kutoa namba ya Sylvia kwa kuhofia ataharibu ndoa ya Sylvia na Robson.

Mawazo yalimzonga Brahama, harufu ya huba zito ilimjaa, akamkumbuka sana Sylvia wa Chuo Udom jinsi alivyokuwa na mapenzi moto moto

“Katika vitu ambavyo Mage unaukirihisha moyo wangu ni kukataa kunipa namba ya Sylvia” Alisema Brahama jioni moja wakiwa wanapata chakula

“Sijakataa bali nina hofu na huo ukichaa wako utasababisha matatizo kwenye ndoa ya Watu”

“Matatizo yapi, Mimi nilikuwa wa kwanza kwa Sylvia, Robson amekuja baada yangu, nitakubali vipi kumuachia?”

“Usijitoe ufahamu Brahama, wamefunga ndoa wale, alafu wewe ni Kijana Handsome sana, Wanawake wengi wanakupapalikia, kwanini umg’ang’anie Sylvia?”

“Kwasababu nampenda na ananipenda!”

“Unampenda? Ungemkatia mawasiliano kwa mwaka mzima Brahama?”

Alihoji Mage, wawili hawa walishibana sana, walikuwa wakipeana siri nyingi kama ndugu waliozaliwa pamoja.

“Yalikuwa ni makosa yangu ndiyo maana nimejirudi, kwanini

niukatili moyo wangu!”

“Najuta kwanini nilikwambia kuhusu Sylvia ni bora ningekaaga kimya ikaisha hivyo” Alisema Mage,

Brahama alifanya kila namna kupata namba ya Sylvia ili awasiliane naye wakati huo Sylvia alikuwa akimwambia pia Mage ampatie namba ya Brahama, ukuta uliozuia Wawili hawa kuwasiliana alikuwa ni Mage.

Brahama akamwambia Mage

“Naenda Dar-es-salaam kuhakikisha namchukua Sylvia kutoka kwa Robson”

“Brahama hiyo ni shari tena ni vita isiyo na suluhu, Sylvia ni Mke wa Mtu nakuomba liheshimu hilo” alisema Mage lakini maneno yake yalikuwa ni sawa na machozi ya Samaki

Brahama aliondoka Mwanza kwa ndege hadi Dar-esa-salaam kwa ajili ya Sylvia.

Alfajiri alikuwa akiteremka Uwanja wa Mwalimu Julius nyerere, Licha ya kutembea barani ulaya lakini

alikuwa mgeni katika Jiji hili, alikuwa na mkakati kichwani pake nao ni kumsaka Sylvia kwa udi na uvumba maana Mage alikataa kutoa namba

Akaingia kwenye Tax bila kusema chochote akiwa amevalia koti kubwa lililomkinga na Baridi ya Alfajiri

“Unaenda wapi Boss?” Aliuliza dereva wa Tax

“Hoteli yenye hadhi ya nyota tano” alijibu Brahama

“Hoteli hizo zipo nyingi hapa Mjini Kaka au nikupeleke nzuri zaidi?”

“Itapendeza pia”

Mwendo wa saa moja na nusu walikuwa wameshafika kwenye Hoteli ya Ocean view iliyopo Masaki, ilikuwa ni Hoteli ya nyota tano, kuishi hapo haikuwa shida kwa sababu wazazi wake wanaoishi Ulaya walikuwa wakimtumia pesa nyingi za matumizi akiwa Tanzania

“Samahani unamtambua huyu?” Brahama alitoa picha ya Sylvia akamuonesha dereva wa Tax

“Kaka hili jiji lina kila aina ya Watu, ni ngumu kwangu kumjuwa kila Mtu, kama unantafuta Mtu hapa kwa picha itachukua muda mrefu sana kumpata” alisema dereva, akapatiwa pesa yake kisha Brahama akaingia Hotelini.

Tukiachana na safari ya Brahama kutoka Mwanza hadi Dar, upande wa Sylvia na mume wake Robson hakukuwa na maelewano mazuri, kichwani pa Sylvia alijaa Brahama Mtupu, hata yeye alichizika baada ya kumuona Brahama kule Mwanza.

Siku moja aliwaambia Wazazi wake kuwa

“Mlinilazimisha niolewe na Mwanaume ambaye analala nje ya nyumba yake, Mwanaume ambaye hazungumzi na Mke wake vizuri, sijui ndoa gani ya namna hii?” Alisema Sylvia.



Alikuwa ameanza kutengeneza mazingira yake mapema sana sababu alishajuwa ujio wa Brahama una lengo gani hapa Tanzania japo hakujuwa kama Brahama alikuwa Dar.

“Sylvia hupaswi kujilaumu kabisa ndoa ni jambo la baraka,

ulitaka kuolewa na nani?” Alisema Baba yake Sylvia

“Niliwaambia kuhusu Mwanaume niliyempenda lakini hamkutaka kunisikiliza matokeo yake ndiyo haya” Alisema Sylvia

“Tutakaa na Robson tutalizungumza hilo Sylvia” Alihitimisha Baba yake Brahama.

Robson alirudi kwa Mark baada ya kuonana kwa mara ya mwisho ile siku wakiwa wamelewa, bado alikuwa na msongo ambao ulisababisha ashindwe kufanya kazi ipasavyo.

“Mark hali inazidi kuwa mbaya, sylvia analitumia lile tukio la Mimi kulala nje, ananiadhibu kila kona sijui nifanyaje?”

Alisema Robson. Walikuwa wametoka kidogo ili wazungumze, walikuwa ufukwe wa Bahari Beach huku wakitazama namna Watu walivyokuwa wakipiga mbizi na kufurahia Maisha ambayo kwa Robson yalikuwa machungu sana.

“Eeh imefikia hatua hiyo Rob?”

“Hatua mbaya sana, bado nina hisia ile ile kuwa Brahama anawasiliana na Mke wangu, tufanye nini Mark hebu nishauri, nipo tayari kwa lolote” alisema Robson akiwa katika hali ya kuchanganikiwa sana

“Unaonaje tukaenda Mwanza ili tupate uhakika wa tunachofikiria?” Aliuliza Mark, alimpa nafasi Robson

kufikiria mara mbili juu ya kwenda Mwanza

“Sasa Mwanza tunaanzia wapi Mark unajuwa kuwa mbali na Sylvia nahisi kama nitakuwa naharibu kabisa ndugu yangu” alisema Robson katika hali ya kuzidi kuchanganikiwa, alikuwa katika ile hali ambayo hata kama ungempa jiwe angelipokea tu, mapenzi yalimtesa sana Robson

“Si umesema tatizo lilianzia Mwanza si ndiyo?”

“Ndiyo”

“Basi huko Mwanza ndiyo kuna suluhu la hili jambo, tutajua kinagaubaga wa hili tatizo kama ni Brahama au kuna jingine” alisema Mark akionekana wazi yupo pamoja na Robson katika nyakati hiyo

“Enhee nimekumbuka itabidi nimpigie Richard ili anipe ramani nzima ya kumpata Mage, nafikiri tukimpata Mage tutajuwa kama Brahama yupo Tanzania au bado yupo Ulaya na kama anawasiliana na Mke wangu. Maana najuwa hakuna Mwanaume anayeweza kuchanganya akili ya Sylvia zaidi ya yule Mshenzi” alisema Robson

“Ookaay!! Si unaona Robson, nilikwambia yaani tunalizima hili kitaalam, na kama umafia safari hii tutaufanya” Maneno ya Mark yalimpa tabasamu Robson ambaye alikuwa ameshikilia dafu mkononi, aliangalia saa yake kisha akamwambia Mark.

“Ngoja nirudi nikaandae mazingira ili ikiwezekana kesho kutwa twende Mwanza kwa ndege” Baada ya kauli hiyo waliagana, Mark alibaki hapo Ufukweni akisema anaangalia totozi ya kuiimbisha.

Aliingia kwenye gari yake kisha alikanyaga mafuta kurudi nyumbani, wakati huo Sylvia alikuwa akizungumza na Mage, yaani Sylvia alikuwa akilazimisha apewe namba ya Brahama lakini Mage alikuwa akikazia ila mwisho alimwambia Sylvia

“Siuoni mwisho wa hili jambo ukiwa mzuri Sylvia” Unamaanisha nini? Aliuliza Sylvia akiwa amesimama dirishani ili aweze kuona kama Robson atakuwa anarudi

“Brahama amekuja huko Dar kukutafuta wewe, kwanini msiache mambo ya zamani yakapita Sylvia, umeshaamuwa kuwa na Maisha mengine, namuonea huruma sana Robson” alisema Mage kwa sauti

iliyojaa maistizo ambayo ilimpa umakini wa kuisikiliza Sylvia

“Tatizo siyo kuendelea mbele na Maisha yangu Mage, tatizo ni kwamba moyo wangu hauwezi kufanya maamuzi, najikuta nakuwa upande wa Brahama, na kama amekuja Dar kunitafuta basi ni ishara kuwa hata yeye moyo wake hautulii kwasababu yangu.

Kingine ni kwamba hata Rob anajuwa kuwa nampenda Brahama na tulishaweka ahadi kuwa endapo Brahama atarudi basi nitarudi kwenye maisha ya Brahama” Alisema Sylvia kwa maelezo marefu yaliyomfanya Mage ashushe pumzi

“Mnanivuruga Sylvia, mmekuwa vichaa kisa penzi, unafikiria Robson atatekeleza ahadi kirahisi hivyo, eti akuache Mwanamke amabaye amekuowa mbele za Mungu tena kwa ushahidi wa ndugu wa pande zote mbili?”

“Sitojali kuhusu hilo, ninachokiangalia ni moyo wangu kupata tulizo Mage…”

“Ooooh!! Kwahiyo unataka nifanyaje?” Alihoji Mage…





“Nipe namba ya Brahama, ni rafiki yako huwezi kumwacha ateseke” Alisema Sylvia. Mage alikata simu bila kutoa jibu lolote lile kuwa anatoa namba au anaendelea kuibania.

Sakata hili lilimpa nyakati ngumu sana Mage, alishaona namna mambo yanavyoweza kuja kuwa mabaya, moyo wake ulizidi kumwambia ni bora aendelee kutokutowa namba ya Brahama kwa Sylvia, hakutaka kuwa shahidi wa kitakachoendelea maana mapenzi yana nguvu kubwa sanaa

Masaa mawili baadaye Robson alifika nyumbani kwake, alimkuta Sylvia akiwa ametulizana, baada ya kuachana na Mark alienda kwanza kazini kuomba likizo ya kuendelea na fungate kwasababu aliikatiza kwa ajili ya kurudi kazini, alikubaliwa.

Kilichobakia kilikuwa ni kumpa taarifa Sylvia ambaye alikuwa amemnunia Robson, kwanza aliketi kisha aliitupa funguo juu ya sofa akamwambia Sylvia

“Hakuna maisha upande wangu bila wewe Sylvia, hakuna thamani bila wewe Mke wangu. Mapenzi yangu yanatoka ndani ya uvungu wa moyo wangu, tafadhali kama kuna mahali nimekosea nisamehe

sipendi kuishi nawe katika hali hii” alisema Robson.

Sylvia alimtazama Robson kisha alinyanyuka na kuingia chumbani, hakumpa jibu lolote Robson kitu ambacho kilizidi kumtia uchungu na wazimu Robson

Akamtumia meseji Mark akamwmabia ajiandae asubuhi waende Mwanza, yalikuwa ni maamuzi yaliyotoka kwa hasira sana, mapenzi aliyonayo kwa Mke wake Sylvia yalimwambia kuwa alistahili kilicho bora zaidi kutoka kwa Sylvia na siyo maumivu.

Akamfuata Mke wake chumbani lakini Sylvia hakutaka hata kumtazama Robson, walilala Mzungu wa nne hadi asubuhi, tena Sylvia alilala na jinzi kabisa kuashiria kuwa hataki hata kuguswa na Robson.

Kulipopambazuka, Robson alichukua baadhi ya nguo akaandika meseji kwa Sylvia ambaye alikuwa amelala akamwambia amepata safari ya kikazi anaenda Dodoma hatochelewa atarudi.

Akamtazama Sylvia huku chozi likimtoka, akalifuta kisha akaondoka nyumbani kwake asubuhi ili kuelekea Mwanza kuutafuta ukweli wa kinachoisumbua ndoa yake changa.

Upande wa Brahama, hakutaka kuendelea kumbembeleza Mage atume namba ya Sylvia sababu aliamini angempata kwa kutumia njia zake, aliweka moyoni upendo wake kwa Sylvia

Asubuhi hiyo alijiandaa kwa ajili ya kumtafuta Sylvia lakini kabla hajatoka alisikia simu yake ikiita kutoka kwenye mfuko wa koti, alipoangalia aliona ni Mage ndiye aliyekuwa akimpigia simu, akatamani kuikata sababu alishambembeleza Sana Mage atoe namba ya Sylvia lakini alikataa, mwisho akaipokea akiwa anafunga mlango wa chumba cha Hoteli

“Mambo Brahama, naona jinsi unavyohangaika, najisikia vibaya sana. Wewe ni rafiki yangu tokea tukiwa wadogo hivyo nakutumia namba ya Sylvia lakini niahidi kuwa hautoharibu ndoa yake” Alisema Mage kwa kutiririka, Brahama alitabasamu akamjibu Mage

“Sawa nimekuelewa” Moja kwa moja simu ilikatika, dakika moja baadaye Simu ya Brahama ikaingia ujumbe mfupi kutoka kwa Mage, ilikuwa ni namba ya Sylvia ndiyo iliyotumwa, Brahama hakuamini macho yake, akajaribu kuipiga.

Mara ya kwanza haikupokelewa sababu bado Sylvia alikuwa amelala, ya pili ndiyo ilimshtua kutoka Usingizini.

“Hello?” ikasikika sauti iliyojaa usingizi ya Sylvia, Brahama hakutaka kusema chochote akakata simu baada ya kujiridhisha kuwa namba hiyo ilikuwa ya Sylvia

Alimtumia meseji Mage akamwabia

“asante sana Rafiki yangu” Brahama hakuona sababu ya kutoka tena, alisubiria hadi muda ambao atahisi Sylvia ameamka, hakutaka kumsumbua Mwanamke aliyempenda sana
 
SEHEMU YA SITA – 06

Muda huo, Robson na Mark walikuwa wakikutana Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage nyerere, ndege aina ya Boeing ilikuwa ikipakia abiria kuelekea Mwanza.

Miongoni mwa abiria ambao walipanda ndege hiyo walikuwa ni Mark na Robson ambao walikuwa na vibegi vidogo kama Watalii, walichukua siti ya Hadhi ya juu kidogo sababu Maisha yao yalikuwa ya hadhi hiyo, utawaambia nini wasomi wenye kazi nzuri lakini mmoja akiwa anateswa sana na Mapenzi

“Umemwambiaje Sylvia?” aliuliza Mark wakiwa wanakaa vizuri kwenye siti zao

“Hatuzungumzi siku hizi, nimemuandikia meseji tu nimemwambia kuwa nina safari ya kikazi” Alisema Robson akiwa anaweka simu yake Mfukoni

“Ok! punguza mawazo Mtu wangu, Mwanza inaenda kutupa ufumbuzi wa tatizo linalokusumbua, kuwa na amani japo ndoa yako ipo rehani ila tutaishinda hii vita” Alisema Mark ambaye alikuwa ndiye mshenga wa Robson

Dakika chache baadaye walianza kuliaga anga la Jiji la Dar-es-salaam, matairi ya Boeng yalikuwa yakitembea kwa kasi kutafuta spidi nzuri ya kulivamia anga zuri lisilo na mawingu huku kijua kikianza kutoka kuashiria kuwa siku ilikuwa imeanza rasmi.

Mark na Robson waliondoka Dar siku hiyo…

Sylvia alipoamka na kutuliza akili yake alikutana na ile meseji ya Robson kuwa anaenda Dodoma kikazi, hakuijali sana. Alikumbuka kuwa kuna Mtu alimpigia simu akiwa Usingizini, aliitafuta namba na kuipiga akiwa hajui kuwa alikuwa akimpigia Mwanaume aliyekuwa akimnyima Usingizi, simu ilipokelewa na sauti ya Brahama iligonga ngoma za masikio ya Sylvia ambayo yalitamani sana kuisikia sauti hiyo, kwanza alisimama kutoka kitandani alipokuwa amekaa

“Brahama?” Aliuliza Kwa mshangao uliojaa furaha, hakutaka kuyaamini masikio yake

“Naam Sylvia, ni Mimi” alisema Brahama

“Siamini kama nazungumza na wewe Brahama, nimehangaika kuitafuta namba yako, umeweza vipi kuipata yangu?” Aliuliza Sylvia akiwa katika hali ile ile ya furaha iliyoambatana na mshangao Mkuu

“Mage amenipa namba yako, alikueleza kuwa nipo Dar kwa ajili yako?” Sasa hapa ndiyo alizidi kumvuruga Sylvia, alihisi mwili wote unalowa

“Ndiyo alinieleza Brahama” alisema Sylvia akiwa katika hali ya kutaka kulia

“Nimekuja kwa ajili yako Sylvia, nimeshindwa kuhimili upweke wa kuishi mbali na wewe, natamani sana nikae nizungumze mengina wewe” alisema Brahama, Sylvia alishindwa kabisa kuongea, alikuwa akilia sana.

“Sylvia usilie, nimekuja tuongee. Najutia kukuacha ukiwa mpweke, najuwa umeolewa kwasababu uliamini nimepotelea Ulaya na siwezi kurudi tena, niliumiza moyo wako, nimerudi kuupoza”

Kila alivyozidi kuzungumza Brahama alimfanya Sylvia ashindwe kuzungumza chochote.

“Bra….hamaaa…Siamini naona kama ndoto, siamini mama ni kweli nazungumza na wewe. Nilipokuona Mwanza nilitamani kukwambia vingi Brahama, sina hata furaha na ndoa, sikuoelewa kwasababu ya mapenzi na Robson bali sikuwa na chaguo Mimi” alisema Sylvia huku akipiga kwikwi mfululizo

“Nahitaji tuonane leo”

“Wapi?”

“Ocean view Hotel” Alisema Brahama, wakakubaliana waonane hapo Ocean view Hotel ili wazungumze zaidi.

Saa 7 Mchana, Robson na Mark waliingia Jijini Mwanza tayari kuanza kazi ya kumsaka Mage, Robson akampigia Richard wakakutana kwenye Hoteli ambayo walipanga, Richard aliwapa ramani halisi ni wapi anakoishi Mage. Wakachukua tax jioni kuelekea huko

“Nyumba hiyo hapo yenye uzio wa Blue ndipo anapoishi Mage”

Alisema Richard wakiwa ndani ya Tax

“Mpigie muulize yupo wapi” Alisema Mark ambaye alionekana kuwa na haraka sana na Mage, Richard alimpigia simu Mage na kumuuliza yupo wapi, ilitumika namba ngeni ili Mage asije shtuka maana Hawakuwa na ukaribu wa kuulizana yupo wapi

“Nani wewe?” Aliuliza Mage

“Naitwa John tulisomaga wote Udom, nipo Mwanza nikaona nikutafute” alisema uwongo Richard huku akiwakonyeza akina Robson kuona kama Mtego utaenda sawa, ukimya ukawa mwingi

Mage akitafakari sauti ya Richard kisha akasema

“Oooh upo Mwanza sehemu gani, jina siyo ngeni” Wote walishusha pumzi baada ya kuona mambo yanaenda kukaa sawa

“Nyegezi hapa”

“Ooh siyo mbali nipo nyumbani ila nataka kutoka muda siyo mrefu nikitulia tutaongea” Alisema Mage, mara walimuona akifunga mlango wa nyumba, haraka Richard alikatatisha maongezi akamuaga

“Haya tutaongea” Alisema Mage kisha baada ya simu kukatika walimuona akitafakari, kisha alipuuzia akawa anasogea ili kutoka getini.

Tax iliyokuwa nje ya nyumba yake ilimuwazisha Mage, aliitazama kidogo kisha alifunga geti, Tax nyingine ikaja kumchukua.

“Fuatilia ile Tax” alisema Robson, dereva aliondoa gari kwa spidi ya taratibu ili kuifuata tax hiyo ambayo ilionekana kuelekea Mjini.

Umakini ulikuwa wa hali ya juu huku wakifanya utafiti wao ili kubaini kama Brahama yupo Tanzania,”

“Taratibu atashtukia Mzee” Alisema Mark akiwa anampa tahadhari dereva ambaye alikuwa akiifuata Tax kwa karibu zaidi.

Dar Es Salaam
Mishale ya jioni kabisa, Sylvia alimpigia Simu Brahama kuwa yupo tayari kuelekea Ocean view Hotel, alipewa maelekezo maalum, hakuwa na wasiwasi sababu alijuwa Robson yupo Dodoma kwa wakati huo.

Alitumia gari ya Robson akatoka kuelekea Hotelini, mwendo wa saa moja na nusu alikuwa katika maegesho ya magari ya Hoteli hiyo yenye hadhi ya nyota tano, moyo wa Sylvia haukutaka kuchelewa hata sekunde moja ili amuone Brahama.

Ilikuwa hivyo hata kwa Brahama ambaye alikuwa na kiu kubwa ya kuwa karibu na Sylvia, alichukua lifti ili kusonga ghorofa ya juu ambako ndiko alipokuwa Brahama.

Chumba namba 404 kilikuwa mbele ya macho yake, harufu ya pafyum ya Brahama ikapenya kwenye pua za Sylvia na kumpa taarifa kuwa Brahama alikuwa hapo, akagonga mlango ambao ulifunguliwa haraka sana kuonesha kuwa Brahama naye alikuwa akimsubiria sana Sylvia, macho yao yaligongana wakatazamana kwa sekunde kadhaa huku wakiwa kwenye hali ya kutafakariana.

Aliyekuwa wa kwanza kumvuta mwenzie alikuwa ni Brahama ambaye alimvuta sylvia na kukutanisha ndimi zao na kuanza kupigana mabusu moto moto.

Walikumbatiana kwa nguvu sanaa kuonesha ile hali kuwa kila mmoja alikuwa akimuwaza sana mwenzie, chozi lilibubujika kwenye macho ya Sylvia. Alimtazama Brahama kwa sekunde kadhaa kisha alishindwa kuzuia hisi zake, kabla ya maongezi yoyote yale, walipeana penzi moto moto la raundi tatu za nguvu kisha baadaye waliporudi kuoga ndiyo walianza kuongea.

“Nilimiss penzi lako tamu Sylvia, nimekumbuka mbali snaa baby” alisema Brahama akiwa tayari amekula penzi la Mke wa Mtu bila kujuwa kuwa Robson alikuwa Mwanza mawindoni na mlengwa kwa wakati huo alikuwa ni Mage ambaye alifahamu hii siri ya mahusiano hayo.

“Hunishindi Mimi mpenzi wangu,,nimekuwa nikikuwaza kila siku za Maisha yangu na nilikuwa tayari kukusubiria hata kama ingechukua miaka kumi, hakuna Mwanaume anayeweza kunipa furaha katika Maisha yangu zaidi yako” alisema Sylvia akiwa kwenye kifua cha Brahama

“Ndiyo maana nimerudi Tanzania Sylvia, nisamehe kwa yote najiona ni mwanaume mpumbavu kufanya jaribio la kutaka kuwa mbali na Mwanamke anayenipenda”

“Hayo si kitu kwangu kwa sasa, kwakuwa uko karibu yangu sina ujanja wowote mbele yako”

“Itakuwaje kwenye hili penzi la siri Sylvia, kila ninapofikiria kuwa ni Mke wa Robson roho yaniuma sana, natamani lirudi lile penzi letu la Udom ambalo hakukuwa nakikwazo cha sisi kuwa pamoja kama sasa ilivyo.”

“Oooh! Hata Mimi nawaza sana, ndoa ya kanisani ni lazima mmoja afe Brahama, istoshe wewe ni Muislam” Alisema Sylvia

“Oooh Shit!!” Alisema Brahama huku simu yake ikiwa inaita, aliangalia aliyekuwa anapiga akaona ni Mage.

“Nani huyo jamani” aliuliza Sylvia

“Mage!!” Alijibu Brahama

“Pokea basi”

“Aah unafikiria atasema nini Bwana”

“Pokea huwezi juwa anataka kukwambia nini” alisema Sylvia

“Sawa!!”

Brahama alipokea simu ya Mage akasikia akisema

“Kuna gari inanifuatilia huku tokea natoka nyumbani hadi jioni hii, inanipa hofu Brahama” alisema Mage

“Kuna gari inakufwatilia?”

“Ndiyo!!! Napata hisia mbaya sababu kuna Mtu amenipigia anasema tumesoma wote, ameniuliza nipo wapi, sasa nilipotoka nyumbani ndiyo nikaona hiyo Tax inanifuata kila niendapo” Alisema Mage kwa sauti ya hofu

“Upo wapi sasa?”

“Nipo Mall hapa nazuga ili nitokee mlango wa nyuma nirudi nyumbani..”

“Mmh!! Sasa ni nani anayeweza kufanya hivyo na kwanini tena” Aliuliza Brahama

“Isije kuwa Robson”

“Robson?….Mmh! Hapana kwani anajuwa mimi nipo Tanzania?”

“Aaah ngoja kwanza nitoke hapa maana naogopa sana” alisema Mage kisha alikata simu

“Nimesikia unamtaja Robson, ni huyu wangu au?” Aliuliza Sylvia, Brahama hakutaka kulipa uzito lakini Sylvia alizidi kutaka kujuwa

“Ndiyo lakini ni mawazo tu aende Mwanza kufanya nini Bwanaa” Alisema Brahama, Mage aliketi kitako akamwambia Brahama

“Robson hayupo Dar tokea asubuhi”

“Ameenda wapi?”

“Yupo Dodoma kikazi”

“Mhhh! Una hakika?”

“Ndiyo”

“Aaah lakini hawezi kuwa Mwanza sababu hajui chochote kuhusu Mimi na wewe si ndiyo?”

“Anaanzia wapi kujuwa wakati simu yangu ina namba za siri ambazo hazijui, istoshe Mimi na yeye tuna ugomvi ambaohauhusu masuala haya Bwana” alisema Sylvia akiwa ameshashusha presha yake akiamini kuwa Robson hajui chochote kile.

Waliendelea kula raha hapo Hotelini, uzuri ni kuwa walikuwa huru hata kulala pamoja sababu Robson aliaga kuwa anaenda Dodoma. Waliyafanya yote waliyokuwa wakiyafanya zamani na hata mambo mapya walioyoyajuwa kuhakikisha tu kuwa wanafurahia siku yao.

Upande wa pili, giza tayari lilikuwa limetanda jijini Mwanza, nyumba ya Mage ilikuwa giza kuanzia ndani hadi nje, Mage alikuwa ndani akisikilizia mapigo yake ya moyo.

Alipochungulia dirisha aliiyona Tax iliyokuwa ikimfwatilia kutwa nzima ikiwa kando ya nyumba yake, akakumbuka jinsi alivyowatoroka pale Mall, ilikuwa hivi…

Alipomaliza kuzungumza na Brahama ile jioni, alilichungulia lile Tax akaona linaegesha kwenye maegesho ya Magari, hakuna aliyeshuka. Aliamuwa kupitia mlango wa nyuma, akakutana na

mlinzi ambaye alimzuia kuutumia mlango huo lakini Mage alimuomba sababu kuna watu waliokuwa wakimfwatilia, Mlinzi alimruhusu ndipo Mage alipowatoroka na kurudi nyumbani kwake.

Alipomaliza kukumbuka aliiyona ile tax ikiondoka pale nje, alishusha presha yake iliyopanda kila wakati, huku akiwa anatafakari ni Nani aliyekuwa akimfwatilia kutwa nzima na alikuwa akitaka nini.

Alipata nguvu ya kumpigia tena Brahama.

“Ondoa hofu Mage huyo Mtu angekuwa anataka kukudhuru angekudhuru muda mwingi, tulipe hili jambo muda ili tuone matokeo yake” Alisema Brahama

“Sawa, lakini nina hofu sanaa na Robson sijui kwanini akili yangu inamuwaza sana” alisema Mage akiwa kitandani, sauti nzito ya Brahama ilimjibu

“Ondoa hofu Bwana, ushajuona umekosea si ndiyo, sasa anaweza vipi kuja Mwanza wakati hajui kama Mimi nipo Tanzania?”

Alisema Brahama, wakazungumza kwa zaidi ya dakika kumi huku Brahama akiwa anambembeleza Sylvia alale, Sylvia naye alikuwa akisikia raha sana kuwa na Brahama sababu alikuwa akijuwa sana mahaba ya namna hiyo ndiyo maana akili yake ilikuwa mgando kwa Mwanaume huyo mwenye asili ya Shombe shombe.

Baadaye akakata simu huku akijitupa ili apate kupumzisha akili yake ambayo siku hiyo ilitawaliwa na hofu kubwa mno.

Asubuhi ya Siku iliyofuata, Sylvia alipokea simu kutoka kwa

Baba yake Robson kuwa Wanamhitaji nyumbani kwao.

“Baby!! Umeamka poa?” Alisalimia Sylvia huku akimwangalia Brahama ambaye alikuwa na usingizi mzito sababu usiku kucha aliutumia kumbembeleza Sylvia

“Ndio Bebe…sijui wewe” alisema Brahama akiwa anapikicha macho yake huku akinyoosha mgongo wake

“Salama pia, naomba nikuache sababu nimepigiwa simu na wazazi wa Robson wananihitaji nyumbani kwao””Mh! Itakuwa wanataka kukwambia nini?”

“Sijui kwakweli ila huwenda ni masuala ya Robson na Mimi, wacha nikawasikilize” alisema Sylivia huku akitabasamu kwa jinsi ambavyo alikua mwenye furaha sana kuwa na Brahama.

“Haya mpenzi uwe makini pia utanijulisha”

“Haya! Mwaaaa..” Sylivia alimpiga busu Brahama kisha alivalia gauni lake huku akisema ndani ya nafsi yake kuwa akifika nyumbani kwake akaoge vizuri.

Akaingia kwenye gari kisha akaondoka hapo kurudi nyumbani kwao, alipofika aliona Kuna Mtu ambaye pengine alikuwa akibisha hodi hapo na alipoona mlango haufunguliwi akawa anaondoka zake, Sylivia alipiga Honi, Mtu huyu alikuwa

Mwanaume na aliyevalia shati lenye nembo ya kampuni ambayo Robson alikuwa akifanya kazi

Akashusha kioo kisha akamsalimia, Mwanaume huyo akasogea dirishani

“Samahani ulikuwa una shida gani?” Aliuliza Sylivia

“Nilikuwa na ripoti ambayo nilitaka kumpa Robson, nimempigia simu hapatikani” alisema

“Ooh sawa nikabidhi Mimi ni Mke wake”

“Sawa hii hapa” Alimkabidhi bahasha ya kaki

“Asante!!”

“Haya, Nawatakia fungate njema” Alisema Jamaa huyo kisha alitabasamu, Sylivia alishtuka kisha akamrudisha

“Umesema Fungate?”

“Ndiyo..si mnaenda kumalizia Fungate leo Mwanza?” Alisema, Sylvia alizidi kushtuka

“Oooh haya asante” alisema Sylvia kisha alimtazama jamaa huyo akiwa anaondoka, akashuka na kufungua geti kisha akaingiza gari ndani, akatulia ndani ya gari akiyatafakari maneno ya yule jamaa kuwa wanaenda kumalizia fungate

“Ina maana Robson yupo Mwanza? Kaenda kufanya nini? Kwanini kaniaga kuwa anaenda Dodoma?” Akafikiria sana, Mara simu yakeikaita, Baba Mkwe wake ndiye aliyekuwa akimpigia, akaipokea haraka sana

“Abee Baba” Alisema Sylivia baada ya kuwa ameshapokea

“Mbona hadi sasa haufiki Mwanangu?” Aliuliza Baba yake Robson

“Baba ndiyo natoka hapa nyumbani nakuja huko samahani kwa kuchelewa”

“Haya jitahidi uwahi” alisema Baba yake Robson kisha akakata simu.

Sylivia akawa na mawazo chungu nzima, kwanza kusikia kuwa Robson yupo Mwanza kulizidi kumpa mawazo akajumlisha na tukio la Mage kufwatiliwa kutwa nzima, kingine kilichompa mawazo sana ni kuitwa na Baba yake Robson, akajiuliza kuna nini?

Akatamani kumueleza Brahama lakini akaona ni bora aende kwanza kwa Baba yake Robson kisha akirudi ndiyo amueleze vyote kwa pamoja.

Akaingia ndani haraka kujiandaaa kisha akaingia tena kwenye gari akanza safari ya kwenda ukweni.

Mwanza

Asubuhi hiyo, Jijini Mwanza…Robson na Mark wakiwa Hotelini walikuwa wakipanga namna ya kuupata huo ukweli Wakajiuliza Mage aliweza vipi kuwatoroka wasimuone, wakaanza kufikiria huwenda Mage ameshtukia kuwa anafwatiliwa

“Cha kufanya hapa ni kwenda kwake na kuzungumza naye, vinginevyo tutatumia siku nyingi bila mafanikio yoyote” Alisema Mark

“Tukienda unafikiria atakubali kusema?”

“Kwanini asiseme?”

“Akikataa je?”

“Anakataaje kwa mfano?” Yalikuwa ni mazungumzo yao ya asubuhi hiyo, wakakubaliana waende moja kwa moja nyumbani kwa Mage ili kumuuliza kama Brahama amerudi japo walijuwa haitokuwa rahisi, wakapata kwanza chai huku wakizidi kupambanua mambo

“Endapo hatotoa jibu alafu akampigia Brahama itakuwaje, unajuwa sitaki Mke wangu ajuwe chochote” Alisema Robson

“Hilo niachie Mimi Robson, Yule Mwanamke atasema tu atake asitake”

Walipomaliza kunywa chai walikodi Tax hadi nyumbani kwa Mage, Wakatumia ukuta kuingilia, kisha Robson akajificha mahali, Mark akagonga mlango. Kelele za kugongwa mlango zilimshtua Mage ambaye alikuwa Usingizni, akajiuliza ni Nani anayegonga mlango wake bila kupitia getini, akajiuliza au aliacha geti wazi ila hakukubaliana na wazo hilo sababu alikumbuka kuwa alifunga milango yote kwasababu ya woga.
 
SEHEMU YA SABA-07

Alienda kuchungulia dirishani, akamwona Mark, akamkumbuka kuwa alisoma naye lakini akajiuliza Mark amefuata nini nyumbani kwake tena bila taarifa. Angalau kumwona Mtu anayemjuwa kulimfanya aondoe hofu yake, akafungua mlango akiwa amevalia Khanga tuu

“Mark!!” alisema Mage akijifanya kushtuka kumwona Mark hapo

“Mambo Mage!!”

“Powa tu, umepafahamu vipi hapa Mark, alafu umeingiaje?” aliuliza Mage

“Nimeelekezwa hapa hadi nikafika, nimekuta geti lipo wazi ndiyo nikaja kugonga hapa” Alisema Mark akiwa mwenye kutabasamu

“Kimekuleta nini hapa kwangu?”

“Mimi ni rafiki tu kwani kuna ubaya nikifika hapa?”

“Mark plzz sema kimekuleta nini hapa au ni wewe ndiye uliyekuwa ukinifwatilia kutwa nzima?” aliuliza Mage akiwa ameanza kuingiwa na hofu

“Hapana siyo Mimi, aliyekuwa anakufwatilia jana ni Robson”

Aliposikia kuwa ni Robson akataka kuufunga mlango haraka lakini Mark alimuwahi akamzuia kisha akaingia ndani kwa nguvu, Robson naye akaingia ndani, alipomuona Robson akataka kupiga simu kwa Brahama lakini wakamuwahi tena wakamnyang’anya simu, wakaona jina la Brahama kwenye kioo

“Oooh kumbe unajuwa kilichotuleta hapa si ndiyo Mage? Mimi na wewe hatukuwahi kuwa maadui wala marafiki chuoni, ulichagua kuwa upande wa Brahama” Alisema Robson akiwa ameishikilia simu ya Mage

“Hebu kaa tuzungumze Mage” Alisema tena Robson kisha aliketi, Mage aliketi pia taratibu huku akiwatazama Wanaume hao

“Hapana shaka unaishi mwenyewe hivyo kitakachotokea hapa hakitakuwa na shahidi ispokuwa Mimi na Mark” Alisema tena Robson

“Robson unataka nini kwangu?” Aliuliza Mage

“Ni kuhusu Mke wangu Sylivia, alikuja hapa siku chache zilizopita, unaweza ukaniambia alikuja kufanya nini?” Aliuliza Robson

“Robson!! Sylivia alikuja kunisalimia tu sababu tulikutana sokoni, ina maana kuna ubaya Mimi nikiwasiliana na Sylivia?”

“Siyo Ubaya wewe kuwasiliana na Sylivia kwasababu ulisoma naye lakini Ubaya unaingia aendapo wewe unaposimama kama Mtu

kati…”

“Mtu kati unamanisha nini?”

“Usijitoe ufahamu Kima wewe, hivi unajuwa ni gharama kiasi gani zimetumika kwa ajili ya ndoa ya Robson na Sylivia?” Alidakia Mark kwa hasira.

“Mbona siwaelewi Robson mnataka nini?” Alipayuka Mage Robson akampiga kofi Mage kisha akamwambia

“Ndoa yangu ipo katika mgogoro mkubwa sana kwasababu ya Brahama, najuwa yupo Tanzania” Alisema Robson huku chozi likimbubujika, Mage akakaa kimya huku akiwa anamwangalia Robson

“Unajuwa ni jinsi gani naumia? Baada ya kuja hapa Mwanza kwenye fungate ndoa yangu ilianza kupata mpasuko mkubwa sana, labda nikukumbushe kuwa kuna siku Mke wangu alikuja kwako, baada ya hapo kila jambo liliharibika, hadi hivi sasa Mimi na Sylvia hatupatani kabisa, na hakuna Mwanaume anayeweza kuvuruga kichwa cha Sylvia zaidi ya Brahama, nataka uniambie ukweli Brahama anawasiliana na Mke wangu?” Alisema Robson

Akiwa anafuta chozi, macho ya Mark yakatua kwenye uso wa Robson ambao ulipoteza nuru akajisemea moyoni

“Kumbe mapenzi yanauma kiasi hiki?” Alijisemea kisha akamshika bega Robson ili kumtuliza maana alijuwa kuwa alikuwa akipitia magumu sana, hata sura ya Mage ilijawa na majonzi mno akawa anamtazama Robson jinsi alivyokuwa akilia

“Mage kuwa katika nafasi yangu, ingia ndani yangu uone jinsi ninavyoumia. Sylivia ndiyo furaha yangu Mimi…”

“Robson ukilia haisaidii cha msingi ajibu maswali basi hakuna kitu kingine” alisema Mark akiwa anamtazama Robson

“Sielewi Mark, hujui naumia Mimi. Nimefanya kazi ngumu hadi kumuowa Sylivia, kabla hata sijala tunda la ndoa yangu…”alisema Robson akashindwa kumalizia kuongea, alijiinamia.

Chozi likambubujika Mage, akalifuta kisha kwa sauti ya upole akamwambia Robson

“Pole Robson, sijui nisimame upande upi ili unione sina hatia katika hili. Ni kweli Brahama yupo Tanzania” Alisema Mage kisha aliweka kituo baada ya Robson kunyanyua kichwa kwa mshtuko

“Unasemaje?”

“Robson, sijui hata nielezee vipi, mara zote nimekuwa nikijaribu kuongea na Brahama apotezee kuhusu Sylivia lakini….Ahhh”

“Mage niambie…. Brahama amerudiana na Mke wangu sylvia si ndiyo?” Aliuliza Robson huku mwili wake ukizidi kupata joto kali na moyo ukizidi kumuuma

“Ndiyo lakini aaah kwanini haya mambo yanatokea sasa hivi, ni bora hata angebakia huko Ulaya….lakini nisamehe Mimi Robson sababu Mimi ndiyo chanzo cha Mkeo kukutana na Brahama….Nisamehe Robson” Alisema Mage kisha akapiga goti mbele ya Robson

“Unajuwa ni jinsi gani nampenda Sylivia? Aaaah” aligumia Robson kama Mtu aliyepandwa na kichaa

“Rob Mzee, punguza jazba sababu ukitumia hasira mwisho hauwezi kuwa mzuri, kikubwa tumeshajuwa tatizo lipo wapi..”

“Ok!ok! Nifanye nini Mimi? Nifanye nini nawauliza? Kwanza Brahama yupo wapi?” Alihoji Robson akiwa kama Mbwa kichaa, kilio kilikata huku hasira ikiwa imejaa kifuani pake, akawa anahema mithiri ya Mwanariadha aliyekimbia kilomita 20 kwa dakika chache

“Robson ikibidi kuniuwa niuwe tu lakini siwezi nikakwambia alipo Brahama, kama kujuwa alipo Brahama kunatatua tatizo lako basi nitakuwa nimeshindwa kukusaidia Robson” alisema

Mage kwa ujasiri Mkubwa sana, Robson akaanza kuingia chumba kimoja badala ya kingine kumtafuta Brahama, hakunwona Brahama sababu alikuwa Dar tena alikuwa na Mke wake Sylivia

Alipomaliza kupekua kila mahali alirudi sebleni akiwa na kisu mkononi, jasho likiwa linamvuja

“Robson unataka kufanya nini?” Aliuliza Mage, Robson hakujibu chochote alikuwa kama amechanganikiwa, akawa anamsogelea Mage, Hofu ikatanda moyoni kwa Mage, hata Mark alishangaa Robson anataka kufanya nini

“Tafadhali Robson nitasema alipo Brahama, yupo Dar anamtafuta Sylivia” alisema Mage.

“Una uhakika?” Akauliza Robson

“Wallai siwezi kudanganya Robson, Brahama yupo Dar mlipotoka”

“Sasa kama utakuwa umeniongopea Mage nakuapia siwezi kukusamehe katika Maisha yangu!” Alisema Robson kisha alikitupa kisu akatoka, Mark akamwambia Mage

“Usiwe sehemu ya hili jambo sababu mwisho hautokuwa mzuri, kaa kimya hata Brahama usimweleze chochote” Alipomaliza kuchimba mkwara akaondoka zake pamoja na Robson, kilichofuata kwao ni kuanza safari ya kurudi Dar Usiku kwa ndege.

Muda huo, Jijini Dar, Mishale ya saa tano asubuhi, Sylivia alifika nyumbani kwa wakwe zake lakini cha kushangaza aliwakuta na wazazi wake wakiwa aamekaa sebleni wakiteta jambo, alishangaa maana Wazazi wake hawakumwambia kabisa kama wataenda kwa wazazi wa Robson.

“Karibu Sylvia” alikaribisha Mama yake Robson huku Baba na Mama yake wakiwa wanamtazama

“Baba na Mama hamkuniambia kama mtakuja huku!” Alisema Sylivia huku akiwa katika hali ya mshangao, alijikuta akijitupa sofani kama mzigo, akatamani sana kujuwa alichoitiwa pale.

Baada ya kuketi akamtazama Baba yake Robson kusikia atasema nini

“Sylivia Mwanangu pole kwa mshangao lakini hilo lisikupe hofu, Sisi na Wazazi wako tulikuwa tunajadili jambo kuhusu ndoa yenu na Robson” Alitanguliza kusema Mama yake Robson kisha Baba Robson akasema

“Tunajua ndoa yenu inapitia misukosuko ya hapa na pale, licha ya kujaribu kuwapatanisha lakini bado Robson amekuwa akilalamika kuwa haumfurahii, tukajaribu kuwauliza wazazi wako wakatueleza jambo lililotushangaza sana, kuwa humpendi Robson, ulikubali kuolewa na Mwanetu sababu wazazi wako walitaka ufanye hivyo, je ni kweli?” Aliuliza Baba Robson

akiwa anamtazma Sylivia kisha akawatazama wazazi wa Sylivia ambao walikuwa wameinamia chini, Sylivia hakujibu chochote kile.



Mara simu ya Sylivia ilianza kuita, haikujulikana mpigaji alikuwa ni nani lakini aliwatazama Wazazi wake kisha wazazi wa Robson, kisha akaipokea pale pale, akaisikiliza kwa mshituko mkubwa kisha akaondoka mbio mbio bila kusema chochote.

Akawafanya Wazazi wote washangae sababu hawakujuwa alipokea simu ya nini, na ameenda wapi, wakabakia wanaulizana

“Kuna nini?”

“Ile simu ina nini?”

“Ooohh haya mambo yananichosha sana kusema ukweli wazazi wenzangu” akasema Baba Sylivia

“Hupaswi kumkatia tamaa, yule ni Mtoto. Tutajuwa tu kilichomtoa hapa” Akasema Mama yake Robson, Baba Robson akawa amechukizwa sanaa na tukio hilo akawaambia wazazi wa Sylivia

“Mtoto wenu amenikosea adabu hata Mimi, kwanini atoke bila kusema chochote, huku ni kutudharau sisi”

“Mtusamehe sisi Wazazi wenzetu, hii ndiyo shida ambayo sisi Wazazi tunakumbana nayo sana, kwa kifupi ni kama tulivyowaambia, Sylivia hataki kuwa na Mtoto wenu…..Anasema yupo anayempenda” Alisema Baba Sylivia

“Sasa nasimama Kama Baba wa Robson, atake asitake ataishi na Mwanangu, hatuwezi kuingia kwenye hiyo aibu,ni bora ndoa isingepita kuliko ndoa imepita kisha yatokee haya, Mwanzo nilimuona Kijana wetu anamakosa kumbe haya yote anayetengeneza Binti yenu, sasa nitalifanyia kazi hili jambo” akasema kisha akaingia chumbani.

Hebu tumtazame Sylivia, alikuwa ndani ya gari baada ya kutoka pale kwenye kikao, alionekana kukosa umakini kabisa, alikuwa akikosea hata kuvuka barabara ambayo ilikuwa na taa nyekunde, mara kadhaa akawa anakoswa kugongwa au kusababisha ajali mbaya.

Alipiga honi kila mahali kutaka apishwe barabarani, aliongoza hadi Masaki kwenye Hoteli ya Ocean view alipo Brahama, hakuhitaji kuingiza gari ndani ya Hoteli hiyo, moja kwa moja akakimbilia kwenye lifti akaitumia kufika alipo Brahama. Akamkuta Brahama akiwa anamsubiria,,Sylivia alikuwa amechoka mwili mzima

“Brahama nimeshindwa kuendelea na kikao, simu yako imenivuruga akili mno” akasema Sylivia akiwa anaketi kitandani

“Hiyo ndiyo hali halisi, nimemwambia Mage aende polisi kutoa taarifa ya uvamizi” akasema Brahama akiwa anamtazama Sylivia

“Oooh Mungu wangu, nilitaka kukwambia hili mapema sana lakini nikaona nisubirie hadi Hatma ya kikao.”

“Kumbe nawe ulikuwa unajuwa kuwa Robson yupo Mwanza?”

“Ndiyo, nimelijuwa hilo kupitia kampuni anayoifanyia kazi”

“Ooh shit!! Kwa vyovyote atakuwa ameambiwa kuwa nipo Dar japo

Mage amekanusha kuwa hakusema ila kwa jinsi ninavyomjuwa Robson sijui”

“Sasa itakuwaje kama ameambiwa kila kitu?” Aliuliza Sylivia

“Nitakabiliana naye kwa namna yoyote ile lakini siyo kuachana na wewe Sylivia, tumetoka mbali hatuwezi achana kirahisi”

“Unamaanisha kweli Brahama?”

“Siwezi ongopa, siogopi chochote kile Sylvia”

“Sijui upande wangu itakuwaje Brahama, basi ngoja nirudi nione namna ya kumkabili najuwa atarudi na hasira zote dhidi yangu na atakutafuta wewe kila kona ya Jiji hili”

“Sylvia nimekwambia siogopi chochote hata ikibidi kujitokeza mbele yake lakini siwezi kujisaliti kwenye ahadi yangu mwenyewe”

“Haya sawa basi tutawasiliana Brahama”

“Powa Sylvia”

Wakaagana, Sylvia akarudi nyumbani kwao, lakini alipofika alikuta Wazazi wake wakiwa wanamsubiria getini, alipowaona alijuwa lazima kutakuwa na maneno makali dhidi yake, akajipanga kukabiliana nao.

“Sylivia unajuwa unatutia aibu wewe mtoto?” Alisema Baba yake Sylvia kwa hasira sana akiwa anapiga gari anayoendesha

“Baba Sylvia!!” Mama Sylvia akajatibu kutaka kumpoza BabaSylvia

“Niache…Niache…hivi wewe Mtoto unatuona sisi hatuna akili si ndiyo? Unatuona mabwenyenye ama, kipi kinachokupagawisha Mtoto wa kike kipi? Kwanini hutulii unataka uonywe na nani wewe….Haya umeamua kututukanisha si ndiyo?” Alisema kwa

Jazba kubwa, Haraka Sylvia akashuka naye akiwa amepagawa maana mambo yalianza kuharibika

“Kwahiyo ulitakaje Baba? Niishi kwa furaha kwa Mwanaume ambaye simpendi si ndiyo? Haya ni makosa yenu kwanini mniozeshe kwa Mtu ambaye hakuwa chaguo langu” Alipaza sauti Sylvia, akapigwa kofi na Baba yake

“Mshenzi wewe, kwahiyo sisi ndiyo wenye makosa si ndiyo? Hivi tulikuzaa wewe au manesi walitubadilishia?” Baba Sylvia alijawa na hasira na uchungu hasa akikumbuka maneno ya Baba Robson

“Sasa bila nyie kunilazimisha leo hii yangetokea yote haya? Nisikilizeni kwa makini sana, Siku zote punda utamlazimisha kwenda mtoni lakini kunywa maji ni hiyari yake, Punda Mimi staki kunywa Maji” Alisema Sylvia kisha akaingia kwenye gari, Baba yake akazuia kwa mbele gari ya Sylvia

“Huwendi popote Sylvia hadi tufikie muafaka wa hilo suala, kama unataka sisi tuendelee kuwa wazazi wako basi amuwa moja, kuishi kwa amani na Robson” alisema Baba Sylvia, tayari Binti yake alikuwa na hasira sana, akarudisha gari nyuma kisha akapeleka mbele kwa spidi na kufunga breki, akajikuta amemsukuma Baba yake akaangukia chini, kisha akaingiza gari ndani na kufunga geti

Baba yake akawa analalamika pale chini kuwa anaumia, Mguu ulikuwa unatoka damu lakini Sylivia hakujali kabisa.

“Sylivia umemgonga Baba yako na hujali?” Alisema Mama Sylvia, Binti yake akasimama na kugeuka akamwambia Mama yake

“Kama ambavyo nyie hamkujali kuhusu Mimi basi ndivyo ambavyo Mimi siwezi kujali tena kuhusu nyie” Alisema Sylvia kisha akaingia ndani haraka sana.

“Msaaada Jamani Mume wangu….Uwiii atakufa hapa nifanyaje Mimi” Alisema Mama Sylvia akiwa katika hali ya kuchanganikiwa sana, Bahati nzuri kulikuwa na Bajaji ambayo ilikuwa ikipita hapo, akaomba msaada wa kumwaisha Baba Sylvia Hospitali

Sylvia alishajuwa ameharibu zaidi, hakutaka kujilaumu, akafikiria afanye nini Maana Robson tayari ameshaujuwa ukweli, akakusanya mabegi yake kisha akaita Tax. Akapakiza mabegi yote akaondoka nyumbani kwa Robson.

  • ••••••
Masaa yalikatika, Hekaheka ikawa nzito kwa Baba Sylvia ambaye alikuwa amelala kitandani akitafari kilichotokea, Mguu wake ukiwa umetundikwa kwa kamba maalum za kumsaidia kupunguza maumivu. Mama Sylvia akiwa pembeni ya Mume wake akiwa amejishika tama, Mara akaingia Baba yake Robson na Mama Robson

“Jamani imekuwaje tena?” Aliuliza Baba Robson akiwa anavua miwani yake

“Hali ndiyo kama unavyoiyona, kilichotokea ndiyo kile nilichokuhadithia kwenye simu” Alisema Mama yake Sylvia

“Huyu Binti amekuwa mwenda wazimu sana, yupo wapi?” Alihoji Baba yake Robson

“Tumemuacha nyumbani kwake hakujali chochote kuhusu Baba yake” Alisema Mama Robson huku Baba Robson akiwa anaugulia maumivu ya Mguu uliopata hitilafu

“Baba Sylvia pole kwa yote, sijui kwanini yote yanatokea wakati huu, furaha imegeuka kuwa huzuni, wiki chache baada ya ndoa Hekaheka imekuwa nzito sana” Akasema Mama yake Robson

“Naumia sana sijui Binti yangu kapatwa na ukichaa gani, nini kimembadilisha ghafla hivi lakini pengine sisi tuna makosa sababu tulilazimisha aolewe na Kijana wenu” alisema Baba

Sylvia huku chozi likimbubujika

“Usiseme hivyo, mlifanya maamuzi kama Wazazi na ndiyo jukumu lenu kuhakikisha Binti yenu anaishi Maisha bora” Alisema Baba yake Robson, ilikuwa ni mishale ya jioni kigiza kikianza kuingia, Mara simu ya Baba Robson iliitaAlipoangalia aliyekuwa akipiga aliona ni Kijana wake Robson

“Eeeh Robson ndiyo anapatikana sasa hivi” Alisema Baba Robson, kila mmoja akawa makini kusikiliza lakini Baba Sylvia akasema

“Tafadhali usimwambie chochote kilichotokea hadi atakaporudi kwenye hiyo safari ya kikazi” Alisema, Hapana shaka Robson aliwaaga kama alivyomuaga Mke wake Sylvia

“Pokea Baba Robson” alisema Mama Robson, haraka Simu ikapokelewa, ikasikika sauti ya Robson ikisema

“Baba nimekamatwa na polisi Mwanza, nipo kituo cha polisi sasa hivi!!l

“Umekamatwa na polisi Mwanza? Ilikuwaje na ulienda lini huko si ulisema upo Dodoma?” Alihoji Baba Robson

“Baba hilo siyo jambo la Msingi kwasasa, kikubwa nitumie wakili kwa ajili ya hii kesi” Alisema Robson, wote walishangaa

“Kesi gani hiyo Robson mbona unaniweka kwenye funbo zito hivi?”

“Baba mtajuwa tu kikubwa aje Wakili mzuri” Alisema Robson.

“Sawa nakuja huko Usiku huu” Alisema Baba yake Robson kisha simu ilikatwa

Baba Robson alijiinamia akiwa ametingwa zaidi hakujuwa ni jambo gani ambalo lilimfanya Robson akamatwe Mwanza

“Jamani huu ni mtihani mzito sana, linaingia hili linatoka hili, kwasasa Robson anashikiliwa Mwanza, sijui alifikaje huko. Baba Sylvia ugua pole wacha nikamfwatilie Robson” alisema Baba Robson, haraka waliondoka hapo na Mama Robson

Walipofika nyumbani kwao Baba Robson alijiandaa Usiku huo huo, akawahi Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius nyerere. Bahati nzuri alipata ndege Binafsi ya askari ambao walikuwa wakienda Mwanza usiku huo hivyo ikawa rahisi kwake, alikuwa akifahamiana nao, wakamuuliza anaenda kufanya nini Mwanza akawaeleza kuwa Kijana wake anashikiliwa na jeshi la polisi huko.

“Kwanini usitumie cheo chako Mtoto akaachiwa Mzee Kibu?” Aliuliza Askari mmoja maana Baba Robson alikuwa askari Mstaafu mwenye cheo kikubwa jeshini

“Mambo kama haya ni lazima kwanza niyaelewe ndipo nifanye uamuzi japo nina imani hadi asubuhi kila kitu kitakuwa kimeisha” Alisema Baba yake Robson, waliondoka Usiku huo huo wakafika Mwanza Alfajiri.
 
Back
Top Bottom