Niliikubali sana hii hustle ya mjini

Niliikubali sana hii hustle ya mjini

Wakili wa shetani

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2022
Posts
1,726
Reaction score
3,391
Siku moja milimtembelea jamaa yangu kwenye ofisi yake ya kuuza tisheti za mtumba. Yeye huwa anafungua mabelo. Sasa anachofanya, anatoa nguo nzuri anatundika pale ofisini. Zingine zinazobaki anaweka mezani watu wachague kwa bei moja. Labda bukubuku au buku mbilimbili. Ni nguo nzuri nazo, nilikuwa napata form six nzuri tu kwa buku.

Sasa zile za mezani wanakuja mahustlers. Wanajuana na mwenye ofisi. Wanachagua nguo kadhaa labda kumi na kuondoka bila kutoa hata mia. Wanazunguka huko, jioni wakati wa kufunga wanarudi. Anahesabiwa. Labda kauza tano, basi tano zilizobaki anarudisha mezani na kumpa bosi elfu tano au elfu kumi ya alizouza.

Hapo yeye unakuta kila nguo kauza hata 5000. So unakuta ana elfu tano au kumi yake kaingiza. Mtaji mwendo.
 
Kuna jamaa namjua anapita maduka ya manukato anachukuwa chupa 5 hadi 10 kwa bei ya jumla 3,000. Yeye anarandisha kwa bei ya 8,000 jioni au siku ya pili anarudisha hela ya mwenye duka na kuchukuwa mali nyengine. Pia mwengine yeye anachukuwa raba(viatu) anafanya hivyo hivyo ila wengi wao huwa mateja sijui kwanini?.🤷‍♂️
 
Kuna jamaa namjua anapita maduka ya manukato anachukuwa chupa 5 hadi 10 kwa bei ya jumla 3,000. Yeye anarandisha kwa bei ya 8,000 jioni au siku ya pili anarudisha hela ya mwenye duka na kuchukuwa mali nyengine. Pia mwengine yeye anachukuwa raba(viatu) anafanya hivyo hivyo ila wengi wao huwa mateja sijui kwanini?.🤷‍♂️
Mjini hulali njaa. Kama ni graduate huna mchongo, unaweza acha smart yako dukani. Wanakupa mzigo, jioni unairudia.
 
Mjini hulali njaa. Kama ni graduate huna mchongo, unaweza acha smart yako dukani. Wanakupa mzigo, jioni unairudia.
Wasomi wengi hushindwa kufanya hii ishu kwa kuhofia kuonekana hawana muelekeo. Wakisahau ukitaka kufanikiwa lazima uanze chini na kupanda juu. Cheti(certificate) haikulishi wala haipo usoni mwaka, ukitaka uwe tajiri wa kweli pitia njia ngumu ya kuitafuta hela ili uijuwe samani yake. Kama dhahabu ingekuwa inapatikana kirahisi isingekuwa na thamani duniani hii leo, lakini lazima uvunje miamba ili kuifikia ndio ufanikiwe uipate.
 
Back
Top Bottom