Nilijikuta naishi maisha ambayo sikuyategemea ila sina jinsi

Nilijikuta naishi maisha ambayo sikuyategemea ila sina jinsi

Nikiwa kama katibu wa watoa pole TZ nasema pole sana bibie. Mungu yu pamoja nawe. Komaa tu na wanao ipo siku moja ya hao watoto atatokea Dimond Platnumz na utasahau yote. Sisi wanaume huwa tunazuzuka sana na mbususu mpya, jinga sana sisi.
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Jamiiforum wangeweka utaratibu wa wao kudhibitisha identify ya mtu, kisha wanaoguswa wakaweza kumsaport mtu kwa account ya jamiiforum, wengi wanapitia magumu ambayo kwa kidogo mtu alichonacho kingeleta relief.

All in all pole sana dada angu.
Wazo zuri sana mkuu
 
Ila wakati mwingine bila kutumia data za nje ambazo hatuna. Umeacha mtoto miaka miwili hujui kala nini au kanywa nini unarudia baada ya miaka miwili unataka kutoa huduma huo ni ujambazi. Miaka miwili walikufa kwa njaa utawakutia wapi?. Tuache kumlaumu mtu aliyeachiwa watoto miaka miwili bila kujua kama wanakula au wanakunywa nini. Mimi nina mfano tofauti kidogo ila unafanana. Kuna mtu alimpa mimba dada yangu miaka nane iliyopita. Amefika muda wa kwenda kujifungua akamleta nyumbani mwenyewe kwa miguu yake na kuomba wazazi ajifungue halafu atawafuata. Leo ni miaka 9 toka aache binti mjamzito na hajawahi kurudi kufuatilia kama walifia hospitalini au lah. Alienda akaoa sasa ana watoto wawili. Huyu mtu kunasiku atakuja kutulaumu tumemuibia mtoto wakati hajui anakula nini, anakunywa nini wala anafananaje? Huwa namuwaza namuona ni moumbavu. Umegombana na mama wa mtoto njoo ona kilichozaliwa. Ulimuacha kwa wazazi so inabidi ukamuone huko huko ulikomuacha. Simlaumu huyu dada. Muacheni tu maana hamjapitia bado. Miaka miwili watoto walikufa kwa njaa full stop.
 
Niliachana na aliyekuwa mume wangu miaka 5 imepita, kuachana kwetu kulikuwa kubaya sana kwa mambo mabaya yaliyopita katikati yetu. Sipendi kuyaeleza maana ni mabaya ila nilishayasahau na kuyaacha yapite.

Baada ya kuachana (aliondoka bila kuniaga na kodi ikiwa tunadaiwa miezi 5 bila kulipa) nilibaki na watoto huku nikiwa sina pa kuishi kwani mwezi 1 baadaye mwenye nyumba alinitaka kumuachia vyumba vyake, sina kazi, sina hata kitu kimoja kwa kuwa aliondoka na kila kitu hadi nguo zangu na za watoto na kwenda kusikojulikana alihama nikiwa sipo.

Kabla ya yeye kuondoka nilikuwa sijui kama tunadaiwa kodi, kwa kuwa kodi ya mwanzo ilipoisha alinambia kuwa kodi imeisha na yeye hana pesa kwa kuwa kazini kwake wamepata hasara analipwa nusu ya mshahara ambao ndio tunatumia kujikimu nyumbani.

Tukashauriana nikope pesa kwa ndugu yangu ambaye amekuwa akitusaidia kutukopesha pale tunapokwama na tunamlipa kidogokidogo, nikamtafuta na akatukopesha, nikamkabidhi 1,200,000 ambayo ndio ilikuwa kodi ya miezi 6 nikajua kalipa kumbe kampa mwenye nyumba kodi ya mwezi 1 tu na nyingine sijui alikopeleka hadi leo.

Sasa alipoondoka ndio mwenye nyumba kunitafuta kuwa nadaiwa miezi 5 hadi siku ile na nimeshaanza mwezi wa 6 ivyo ananipa wiki 1 nimuachie nyumba yake, kumbuka hapo nalala chini mimi na watoto kwa kuwa kila kitu kilishaondoka na yeye. Na nafanya kazi ndogondogo kupata chakula cha watoto.

Nikawaza kurudi nyumbani, Kilichonishangaza ni kuona ndugu zangu wote hawapokei simu zangu na wakipokea wananilaumu tu kuwa nimeyatafuta mwenyewe na nisiwasumbue na wanakata simu. Nikawaza nimeyataka yapi? Nimekosea nini? Mbona changamoto zangu pande zote wanazijua kulikoni nalaumiwa leo, nikajaribu upande wa aliyekuwa mume wangu ndio balaa zito.

Mtu 1 akaniambia unajua kuwa Unatuhumiwa kuzaa nje ya ndoa? Nikahamaki, akaendelea kusema baba fulani amewaambia ndugu zako na zake kuwa mtoto huyo mdogo sio wa kwake na ndio maana kaondoka. Nikamwambia hapana haiwezi kuwa kweli kwa kuwa sijawahi kutoka nje ya ndoa hata siku moja. Na kama kasema hayo basi ana lake jambo huenda kaamua kuficha mambo yake kwa kunitwisha mzigo maana tayari alikuwa hana pa kukwepea kutokana na mambo yake.

Basi nikatuma ujumbe mfupi kwa ndugu zangu kuwa, nashukuru kwa kuwa nimejua sababu ya nyie kunichukia ila nawaambia siyo kweli na sijawahi kufanya uchafu huo ila nipo tayari wakapime DNA nchi yoyote na ikibainika ni kweli basi wanihukumu nikazima simu ili nipate muda wa kuwa peke yangu kuwaza nini cha kufanya, nikaanza kuwaza cha kufanya nalia peke yangu.

Nikaanza safari ya kutafuta chumba japo sijui nalipa nini, nikapata mama mmoja nikamweleza hali yangu akanambia nakupa chumba ila utakuwa unanilipa mwezi mmoja mmoja sh. 60000 na mwezi huu nakupa ukae bure utaanza kunilipa mwezi ujao, nikaona chumba ni gharama ila kwangu ilikuwa ahueni maana nina mwezi mmoja wa kuanza maisha kutafuta kodi ya watu.

Nikahamia hapo, na wanangu tukaanza maisha, mwezi mmoja baadae nikapata kazi japo haina mshahara mzuri ila inaniwezesha kupata chakula na kulipa kodi ya 60000 kila mwezi, nikaanza kujibana na kununua vyombo, godoro, kitanda, nguo za watoto nk.

Miezi 7 baadaye nikaja kujua alikokwenda yule mwanaume, na kwamba alipohama alihama na mwanamke mmoja ambaye alikuwa mchepuko wake wa siku nyingi wakaanza maisha yao, nilikutana na ndugu wa huyo mwanamke ndiye aliyenipa taarifa hizo.

Baada ya miaka 2, mwanaume huyo alinipigia simu, akidai anataka kuniona kanikumbuka, nikamwambia huwezi kuniona na wala hutakaa ujue naishi wapi, kwa kuwa sikutaka hata waliokuwa wanatufahamu wajue naishi wapi pia, baada ya kumjibu ivyo akasema kwa kuwa hutaki nikuone basi nilichotaka kusema sitasema, japo nilikuwa na lengo la kuonana na wewe ili nianze kukupa hela ya matumizi ya watoto kwa kuwa umekataa na mimi sihudumii hao watoto, nikamwambia kama wameishi miaka 2 bila huduma yako, basi wataishi tu.

Akawa anaendelea kunitafuta kwa namba mbalimbali huku akifoka na kuniita nina kiburi, jeuri, sina adabu kwake, nitakuwa nimepata mwanaume ananipa kiburi nk, mara aseme nitakuwa nimewalisha watoto sumu kuwa yeye mbaya ila yeye sio mbaya anataka kuwatunza ila mimi ndio nazuia. Mwisho alikata tamaa na sasa imepita miaka 5 nikiwa naishi na wanangu.

Inaniuma sana kuishi na wanangu wakubwa sasa ndani ya chumba 1 kikiwa ndio chumba na ndio sebule kwa kuwa sina uwezo wa kulipia zaidi ya chumba 1 ukizingatia ni wa kiume ila sina jinsi najipa moyo kuna siku nitapata nafasi ya kupata walau vyumba 2 wanangu wakalala tofauti na mimi mama yao.

Nimejitahidi kuandika matukio machache kwa kuyakata sana ili nisiwacoshe
Pole sana.

Dada msamehe mmeo maisha yaendelee..binadamu hufanya makosa ili tunasamehe tu na wala hatusahau kama ulivyosema wewe..kusahau mambo mabaya huwa haiwezekani ila huwa tunasemehe na kuachilia maisha yaendelee..hao watoto wakikua ipo siku watamtafuta baba yao so ni bora uruhusu tu baba yao aanze kuwatunza..

Pia kama upo Dar jaribu kuhamia maeneo ya pembezoni mwa mji kama Chamazi,Gongolamboto,Bunju,Mbagala,Kibamba n.k huko kwa elfu 60 utapata angalau vyumba viwili vya 30 30..utatumia kimoja na watoto watatumia kimoja.


Pole sana kwa yote
 
Ndio maana Kila siku nasema, Tuanzisheni Kapu la JF , ambalo Ndani yake tutadumbukiza Mia mia tu .

Kwa ajili ya watu kama hawa, Mtoa Mada ni Mama mpambanaji sana ,mwenye uchungu na wanawe .



Niwaombe sana WanaJF wanaume Kwa Wanawake wenye Fursa nyingine za Kazi, mmfikirie , mtoa Mada alipata kazi, Kwa Uwezo mkubwa wa akili na uthubutu Alonao, Hatokaa kuomba Kodi.
I second you....

Sent from my vivo 1906 using JamiiForums mobile app
 
Niliachana na aliyekuwa mume wangu miaka 5 imepita, kuachana kwetu kulikuwa kubaya sana kwa mambo mabaya yaliyopita katikati yetu. Sipendi kuyaeleza maana ni mabaya ila nilishayasahau na kuyaacha yapite.

Baada ya kuachana (aliondoka bila kuniaga na kodi ikiwa tunadaiwa miezi 5 bila kulipa) nilibaki na watoto huku nikiwa sina pa kuishi kwani mwezi 1 baadaye mwenye nyumba alinitaka kumuachia vyumba vyake, sina kazi, sina hata kitu kimoja kwa kuwa aliondoka na kila kitu hadi nguo zangu na za watoto na kwenda kusikojulikana alihama nikiwa sipo.

Kabla ya yeye kuondoka nilikuwa sijui kama tunadaiwa kodi, kwa kuwa kodi ya mwanzo ilipoisha alinambia kuwa kodi imeisha na yeye hana pesa kwa kuwa kazini kwake wamepata hasara analipwa nusu ya mshahara ambao ndio tunatumia kujikimu nyumbani.

Tukashauriana nikope pesa kwa ndugu yangu ambaye amekuwa akitusaidia kutukopesha pale tunapokwama na tunamlipa kidogokidogo, nikamtafuta na akatukopesha, nikamkabidhi 1,200,000 ambayo ndio ilikuwa kodi ya miezi 6 nikajua kalipa kumbe kampa mwenye nyumba kodi ya mwezi 1 tu na nyingine sijui alikopeleka hadi leo.

Sasa alipoondoka ndio mwenye nyumba kunitafuta kuwa nadaiwa miezi 5 hadi siku ile na nimeshaanza mwezi wa 6 ivyo ananipa wiki 1 nimuachie nyumba yake, kumbuka hapo nalala chini mimi na watoto kwa kuwa kila kitu kilishaondoka na yeye. Na nafanya kazi ndogondogo kupata chakula cha watoto.

Nikawaza kurudi nyumbani, Kilichonishangaza ni kuona ndugu zangu wote hawapokei simu zangu na wakipokea wananilaumu tu kuwa nimeyatafuta mwenyewe na nisiwasumbue na wanakata simu. Nikawaza nimeyataka yapi? Nimekosea nini? Mbona changamoto zangu pande zote wanazijua kulikoni nalaumiwa leo, nikajaribu upande wa aliyekuwa mume wangu ndio balaa zito.

Mtu 1 akaniambia unajua kuwa Unatuhumiwa kuzaa nje ya ndoa? Nikahamaki, akaendelea kusema baba fulani amewaambia ndugu zako na zake kuwa mtoto huyo mdogo sio wa kwake na ndio maana kaondoka. Nikamwambia hapana haiwezi kuwa kweli kwa kuwa sijawahi kutoka nje ya ndoa hata siku moja. Na kama kasema hayo basi ana lake jambo huenda kaamua kuficha mambo yake kwa kunitwisha mzigo maana tayari alikuwa hana pa kukwepea kutokana na mambo yake.

Basi nikatuma ujumbe mfupi kwa ndugu zangu kuwa, nashukuru kwa kuwa nimejua sababu ya nyie kunichukia ila nawaambia siyo kweli na sijawahi kufanya uchafu huo ila nipo tayari wakapime DNA nchi yoyote na ikibainika ni kweli basi wanihukumu nikazima simu ili nipate muda wa kuwa peke yangu kuwaza nini cha kufanya, nikaanza kuwaza cha kufanya nalia peke yangu.

Nikaanza safari ya kutafuta chumba japo sijui nalipa nini, nikapata mama mmoja nikamweleza hali yangu akanambia nakupa chumba ila utakuwa unanilipa mwezi mmoja mmoja sh. 60000 na mwezi huu nakupa ukae bure utaanza kunilipa mwezi ujao, nikaona chumba ni gharama ila kwangu ilikuwa ahueni maana nina mwezi mmoja wa kuanza maisha kutafuta kodi ya watu.

Nikahamia hapo, na wanangu tukaanza maisha, mwezi mmoja baadae nikapata kazi japo haina mshahara mzuri ila inaniwezesha kupata chakula na kulipa kodi ya 60000 kila mwezi, nikaanza kujibana na kununua vyombo, godoro, kitanda, nguo za watoto nk.

Miezi 7 baadaye nikaja kujua alikokwenda yule mwanaume, na kwamba alipohama alihama na mwanamke mmoja ambaye alikuwa mchepuko wake wa siku nyingi wakaanza maisha yao, nilikutana na ndugu wa huyo mwanamke ndiye aliyenipa taarifa hizo.

Baada ya miaka 2, mwanaume huyo alinipigia simu, akidai anataka kuniona kanikumbuka, nikamwambia huwezi kuniona na wala hutakaa ujue naishi wapi, kwa kuwa sikutaka hata waliokuwa wanatufahamu wajue naishi wapi pia, baada ya kumjibu ivyo akasema kwa kuwa hutaki nikuone basi nilichotaka kusema sitasema, japo nilikuwa na lengo la kuonana na wewe ili nianze kukupa hela ya matumizi ya watoto kwa kuwa umekataa na mimi sihudumii hao watoto, nikamwambia kama wameishi miaka 2 bila huduma yako, basi wataishi tu.

Akawa anaendelea kunitafuta kwa namba mbalimbali huku akifoka na kuniita nina kiburi, jeuri, sina adabu kwake, nitakuwa nimepata mwanaume ananipa kiburi nk, mara aseme nitakuwa nimewalisha watoto sumu kuwa yeye mbaya ila yeye sio mbaya anataka kuwatunza ila mimi ndio nazuia. Mwisho alikata tamaa na sasa imepita miaka 5 nikiwa naishi na wanangu.

Inaniuma sana kuishi na wanangu wakubwa sasa ndani ya chumba 1 kikiwa ndio chumba na ndio sebule kwa kuwa sina uwezo wa kulipia zaidi ya chumba 1 ukizingatia ni wa kiume ila sina jinsi najipa moyo kuna siku nitapata nafasi ya kupata walau vyumba 2 wanangu wakalala tofauti na mimi mama yao.

Nimejitahidi kuandika matukio machache kwa kuyakata sana ili nisiwacoshe
Hii hadithi yako umeimaliza haraka bila kuihitimisha! Unataka tukusaidie nini? Inaelekea kwasasa tatizo lako ni kipato kidogo kisichokuwezesha kuwa na vyumba viwili ili wanao wapate chumba chao si ndio? Kaza buti mama ongeza kipato mradi isiwe kwenye vikoba!
 
Maisha ni safari ndefu dada. Mshukuru Mungu kwa kila jambo, ingawa ninyi wanawake mlio wengi huwa hamjitambui. Naamini kuna mwanaume anaweza kuja kwako tena ukahisi umepata tulizo kumbe unaingizwa chaka.

Nakuomba uwe makini sana, usijefanya kosa jingine tena.
 
Mimi nilikimbia mwanamke nilimuacha na watoto wawili mmoja wa kwake umri miaka mitano na mwingine miaka miwili ndio Morgan wangu huyo.

Sababu zilizofanya nimkimbie.

1. Toka mwanzo naanza naye mahusiano nilishamuweka wazi kuwa nipo mkoa ule sina furaha na kazi nayofanya na at anytime naweza kurudi nyumbani kwetu Namtumbo hapo tupo Kagera so akaamua kubeba mimba kama kunishawishi niendelee kubaki ile mimba iliharibika ilipofikisha umri wa miezi 7 tukaendelea na mahusiano kumbe kabeba mimba nyingine ndio Morgan huyo.

2. Morgan akazaliwa tukawa tunaishi lakini mimi roho yangu ilikuwa inaniuma kuona kama amenilaghai kwa gia ya mtoto ili nisiweze kurudi kwetu Namtumbo mnaweza kuhoji kwa nini nisirudi naye Namtumbo jibu ni kuwa sikuwa tayari kuwa na mwanamke pia financial sikuwa vizuri kwenda kuanza maisha Namtumbo nikiwa na familia.

3. Nilikuwa na madeni ambayo nilikataa kuyalipa nilimripoti mdeni wangu Takukuru akanambia nitakuonesha mimi na wewe nani mjanja alikuwa mtu wa Mara Chacha nikaona kabisa hapa mapanga yananihusu usalama wangu mdogo.

4. Kuongeza viugomvi vya ndani ya nyumba na stress za kuingia kwenye maisha ya ndoa bila ya kutarajia na ugumu wa maisha nikaona wakati sahihi wa kutoroka familia umewadia.

Kwa kipindi cha miaka miwili wazo nililokuwa nalo kichwani ni kurudi nyumbani nikimuangalia Morgan zile stage zake za ukuaji kama kutambaa, kutembea naona nikomae tu na huyu mwanamke lakini bado wazo la kurudi nyumbani liliponizidi nguvu.

Ilikuwa hivi siku nimerudi jioni nikamwambia nimeomba likizo naenda nyumbani jioni hii akafikiri utani akaleta chakula nikala nikachukua bag dogo nikaweka vyeti vyangu suruali kadhaa na tisheti nikamuachia hela ya matumizi nikachukua bodaboda huyo nikaanza safari ya kuitafuta Namtumbo.

Nipeni Maua yangu nimalizie hii true story.
[emoji253][emoji253][emoji253][emoji257][emoji257][emoji257][emoji257][emoji1651][emoji255]

Maua yako hayo hapo

Haya malizia story

Sent from my vivo 1906 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom