Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kumbe unajua hali halisi ya Mambo, haya mwambie aseme chanzo Cha mgogoro ni nini ?Mm nina mtoto ambae ninatoa gharama za ada tuu lakini huduma nyingine sitoi na hata hio ada nitakuja kusitisha hio huduma kutokana na tabia za mama yake kiburi na matusi,so usione namtetea huyu ukahisi labda sielewi hizi mambo,wanawake huwa wanazingua sana lkn hata baadhi ya wanaume huwa wanazingua balaa tena mwanaume ni mgeni k ndio balaa kabsa
Baba Yao kasema yupo tayari kulea watoto wake na kuwahudumia so Cha muhimu watu mlio Katika ndoa wake kwa waume tulize de libolo kwa mke mmoja mlee watoto wenu na sio kila siku mnawaza uzinzi tu mwisho mnawatesa watoto kisa ndoa zenu fake
Chanzo unajijua au ndio nyinyi wenye huruma kupitiliza huwezi kusaidia anaelia na wewe inamsaidia kwa kulia ndio unamaanisha hivyo ?Ni muda mrefu moyo wangu umekua hauhisi maumivu kwa stori yoyote ila kwa hii kweli imeniuma sana, pole kwa mtihani huu mgumu.
Ni kweli awe na kipato chake maana hamuelewekiAsilimia kubwa ya wanandoa wamepanaga bado labda umshauri awe na kipato chake maana hata mwanaume anaefurahia mke kuwa nyumbani bila kazi basi malengo ya maisha ni ngumu kufikia hasa kwa sisi wa vipato vya chini
Pole sana bi dada, usikute kuhama kwa mumeo kunachangiwa sana na huyo mchepuko wake. Kama wasemavyo wahenga kuwa adui mkubwa wa mwanamke siku zote ni mwanamke mwenzake, mchepuko akishapata mwanamme ampendaye atafanya chini juu kumroga huyo mwanamme ili amuache mkewe wa ndoa na watoto achukuliwe yeye. I guarantee you, huyu mchepuko atakuwa kafanya sayansi kimu kumchota akili huyu mumeo. Nimeshuhudia haya kwa kaka yangu binamu, alifanya haya haya aliyofanya mumeo na hakujuwa kwanini alimuacha mkewe na watoto, alipozinduliwa akili (kwa manga wa kienyeji), cha kushangaza muda huo huo akaanza kumlilia mkewe na kuomba mganga amuachie arudi kwa mkewe akamalizie dozi mbele ya mkewe. Shemeji alipojuwa hili alilia sana na kumkaribisa mumewe kwa moyo mkunjufu ila alihapa kwa Mungu kummaliza yule mwanamke endapo atampata. Sijajuwa kama alifanikiwa, ni siri yake mwenyewe shemeji. Wanawake haswa michepuko ni waharibifu sana wa ndoa.Niliachana na aliyekuwa mume wangu miaka 5 imepita, kuachana kwetu kulikuwa kubaya sana kwa mambo mabaya yaliyopita katikati yetu. Sipendi kuyaeleza maana ni mabaya ila nilishayasahau na kuyaacha yapite.
Baada ya kuachana (aliondoka bila kuniaga na kodi ikiwa tunadaiwa miezi 5 bila kulipa) nilibaki na watoto huku nikiwa sina pa kuishi kwani mwezi 1 baadaye mwenye nyumba alinitaka kumuachia vyumba vyake, sina kazi, sina hata kitu kimoja kwa kuwa aliondoka na kila kitu hadi nguo zangu na za watoto na kwenda kusikojulikana alihama nikiwa sipo.
Kabla ya yeye kuondoka nilikuwa sijui kama tunadaiwa kodi, kwa kuwa kodi ya mwanzo ilipoisha alinambia kuwa kodi imeisha na yeye hana pesa kwa kuwa kazini kwake wamepata hasara analipwa nusu ya mshahara ambao ndio tunatumia kujikimu nyumbani.
Tukashauriana nikope pesa kwa ndugu yangu ambaye amekuwa akitusaidia kutukopesha pale tunapokwama na tunamlipa kidogokidogo, nikamtafuta na akatukopesha, nikamkabidhi 1,200,000 ambayo ndio ilikuwa kodi ya miezi 6 nikajua kalipa kumbe kampa mwenye nyumba kodi ya mwezi 1 tu na nyingine sijui alikopeleka hadi leo.
Sasa alipoondoka ndio mwenye nyumba kunitafuta kuwa nadaiwa miezi 5 hadi siku ile na nimeshaanza mwezi wa 6 ivyo ananipa wiki 1 nimuachie nyumba yake, kumbuka hapo nalala chini mimi na watoto kwa kuwa kila kitu kilishaondoka na yeye. Na nafanya kazi ndogondogo kupata chakula cha watoto.
Nikawaza kurudi nyumbani, Kilichonishangaza ni kuona ndugu zangu wote hawapokei simu zangu na wakipokea wananilaumu tu kuwa nimeyatafuta mwenyewe na nisiwasumbue na wanakata simu. Nikawaza nimeyataka yapi? Nimekosea nini? Mbona changamoto zangu pande zote wanazijua kulikoni nalaumiwa leo, nikajaribu upande wa aliyekuwa mume wangu ndio balaa zito.
Mtu 1 akaniambia unajua kuwa Unatuhumiwa kuzaa nje ya ndoa? Nikahamaki, akaendelea kusema baba fulani amewaambia ndugu zako na zake kuwa mtoto huyo mdogo sio wa kwake na ndio maana kaondoka. Nikamwambia hapana haiwezi kuwa kweli kwa kuwa sijawahi kutoka nje ya ndoa hata siku moja. Na kama kasema hayo basi ana lake jambo huenda kaamua kuficha mambo yake kwa kunitwisha mzigo maana tayari alikuwa hana pa kukwepea kutokana na mambo yake.
Basi nikatuma ujumbe mfupi kwa ndugu zangu kuwa, nashukuru kwa kuwa nimejua sababu ya nyie kunichukia ila nawaambia siyo kweli na sijawahi kufanya uchafu huo ila nipo tayari wakapime DNA nchi yoyote na ikibainika ni kweli basi wanihukumu nikazima simu ili nipate muda wa kuwa peke yangu kuwaza nini cha kufanya, nikaanza kuwaza cha kufanya nalia peke yangu.
Nikaanza safari ya kutafuta chumba japo sijui nalipa nini, nikapata mama mmoja nikamweleza hali yangu akanambia nakupa chumba ila utakuwa unanilipa mwezi mmoja mmoja sh. 60000 na mwezi huu nakupa ukae bure utaanza kunilipa mwezi ujao, nikaona chumba ni gharama ila kwangu ilikuwa ahueni maana nina mwezi mmoja wa kuanza maisha kutafuta kodi ya watu.
Nikahamia hapo, na wanangu tukaanza maisha, mwezi mmoja baadae nikapata kazi japo haina mshahara mzuri ila inaniwezesha kupata chakula na kulipa kodi ya 60000 kila mwezi, nikaanza kujibana na kununua vyombo, godoro, kitanda, nguo za watoto nk.
Miezi 7 baadaye nikaja kujua alikokwenda yule mwanaume, na kwamba alipohama alihama na mwanamke mmoja ambaye alikuwa mchepuko wake wa siku nyingi wakaanza maisha yao, nilikutana na ndugu wa huyo mwanamke ndiye aliyenipa taarifa hizo.
Baada ya miaka 2, mwanaume huyo alinipigia simu, akidai anataka kuniona kanikumbuka, nikamwambia huwezi kuniona na wala hutakaa ujue naishi wapi, kwa kuwa sikutaka hata waliokuwa wanatufahamu wajue naishi wapi pia, baada ya kumjibu ivyo akasema kwa kuwa hutaki nikuone basi nilichotaka kusema sitasema, japo nilikuwa na lengo la kuonana na wewe ili nianze kukupa hela ya matumizi ya watoto kwa kuwa umekataa na mimi sihudumii hao watoto, nikamwambia kama wameishi miaka 2 bila huduma yako, basi wataishi tu.
Akawa anaendelea kunitafuta kwa namba mbalimbali huku akifoka na kuniita nina kiburi, jeuri, sina adabu kwake, nitakuwa nimepata mwanaume ananipa kiburi nk, mara aseme nitakuwa nimewalisha watoto sumu kuwa yeye mbaya ila yeye sio mbaya anataka kuwatunza ila mimi ndio nazuia. Mwisho alikata tamaa na sasa imepita miaka 5 nikiwa naishi na wanangu.
Inaniuma sana kuishi na wanangu wakubwa sasa ndani ya chumba 1 kikiwa ndio chumba na ndio sebule kwa kuwa sina uwezo wa kulipia zaidi ya chumba 1 ukizingatia ni wa kiume ila sina jinsi najipa moyo kuna siku nitapata nafasi ya kupata walau vyumba 2 wanangu wakalala tofauti na mimi mama yao.
Nimejitahidi kuandika matukio machache kwa kuyakata sana ili nisiwacoshe
Lea watoto wako mkuu kwanini uforce kupewa kyuma, wacheni ujinga wakutesa watoto nyie k kanunue Kwa Malaya hukoHapana Mimi nasimama upande wa mumewe mpaka akisema chanzo Cha yeye kukimbiwa ni nini ? Kwanini anaficha chanzo we hutatoaje hukumu bila kujua chanzo Cha tukio lenyewe husika, huyu anajua alichokosea tho kwenye mgogoro kila mtu anakua na % zake za ukosefu yeye hawezi akayaanika mabaya yake hapa kuelezea kua alimkosea nini hadi akamkimbia sababu hataki kuusema ukweli usipolijua hilo ni ngumu kung'amua ukweli, Ila nimebaini hasemi ukweli km anaficha chanzo Cha tatizo,
Hata wewe ukiniuzia sio vibaya nainunua si unaiuza Bei nafuu ? Kikubwa maelewano vipi unataka tuyajenge ?Lea watoto wako mkuu kwanini uforce kupewa kyuma, wacheni ujinga wakutesa watoto nyie k kanunue Kwa Malaya huko
Huyo ni mwanamke sio mwanaume,Ni kweli awe na kipato chake maana hamueleweki
Yes mwanamkeHuyo ni mwanamke sio mwanaume,
Sahihi kabisaNi kweli awe na kipato chake maana hamueleweki
Yes ila asimuhusishe mume Kwa maana mume ni muharibifu yupo kama nyani atammalizia mahindi shambani awe kimya tu kikinuka kama hiki anaenda kwake kashajenga siku mingi??Sahihi kabisa
Cha msingi ajipange hayo mengine ni ziada tuYes ila asimuhusishe mume Kwa maana mume ni muharibifu yupo kama nyani atammalizia mahindi shambani awe kimya tu kikinuka kama hiki anaenda kwake kashajenga siku mingi??
Ushauri wangu kama baba kakubali kuhudumia watoto usiweke ukuta kati ya baba na watoto acha watoto wapate huduma mengine mungu atahukumuPole. Napata somo kwamba, ukiwa kwenye ndoa, heshimu ndoa yako.
Bogus wwHapana hicho sio chanzo hio ni hearsay akisikia kwa watu wakisema nataka aseme chanzo na anakijua Ila hataki kusema ukweli na ukisoma huko juu amesema hatoniambia au hatotuambia chanzo au source ya huyo Mwanaume kumkimbia ukiondoa hio hearsay aliyoisikia kwa watu wakisema, yeye chanzo halisi anakijua