Hismastersvoice
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 21,741
- 26,735
Ijumaa tarehe 20 saa 1:15 asubuhi haikuwa siku njema kwangu, nilifika stesheni ya SGR nikiwa na furaha ya kuanza safari ya kuelekea Dar es Salaam, baada ya kukaguliwa tikiti yangu nikaambiwa niweke begi kwenye mtambo wa ukaguzi kisha nikaenda upande wa pili wa mtambo kulipokea begi.
Nilipofika upande wa pili nikasikia askari akitaka kumjua mwenye begi ambalo ni langu, nikajitokeza, kwa mshituko nikajikuta nipo kati ya askari watatu kijasho kilanitoka, nikaambiwa ndani ya begi kuna chupa ya maji, nikatakiwa niitoe, nikaitoa. Nikawaambia hayo ni maji yangu ya kunywa endapo nitahitaji kama ikitokea, wakati huo watu wameacha mazungumzo yao wakishuhudia kukamatwa kwa msafirishaji wa maji ya kunywa mil.500!
Kitendo cha kunihoji kijinai kilitaka kunifanya nivunje safari yangu ya SGR, baada ya mahojiano niliamriwa hiyo chupa ya maji mil.500 niiache kwenye kaunta yao alipo askari! Ndugu zangu hapo ndipo nilipojua si lazima uwe mwizi ili uende jela, mmoja wa askari aliniambia kosa hilo endapo ningeingia nayo ndani ya treni ni faini ya shilingi 500,000/=! Ninajuta kupanda SGR.
Nilipofika upande wa pili nikasikia askari akitaka kumjua mwenye begi ambalo ni langu, nikajitokeza, kwa mshituko nikajikuta nipo kati ya askari watatu kijasho kilanitoka, nikaambiwa ndani ya begi kuna chupa ya maji, nikatakiwa niitoe, nikaitoa. Nikawaambia hayo ni maji yangu ya kunywa endapo nitahitaji kama ikitokea, wakati huo watu wameacha mazungumzo yao wakishuhudia kukamatwa kwa msafirishaji wa maji ya kunywa mil.500!
Kitendo cha kunihoji kijinai kilitaka kunifanya nivunje safari yangu ya SGR, baada ya mahojiano niliamriwa hiyo chupa ya maji mil.500 niiache kwenye kaunta yao alipo askari! Ndugu zangu hapo ndipo nilipojua si lazima uwe mwizi ili uende jela, mmoja wa askari aliniambia kosa hilo endapo ningeingia nayo ndani ya treni ni faini ya shilingi 500,000/=! Ninajuta kupanda SGR.