Nilikamatwa Morogoro stesheni ya SGR nikituhumiwa kusafirisha chupa ya mil.500 ya maji ya kunywa!

Nilikamatwa Morogoro stesheni ya SGR nikituhumiwa kusafirisha chupa ya mil.500 ya maji ya kunywa!

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
21,741
Reaction score
26,735
Ijumaa tarehe 20 saa 1:15 asubuhi haikuwa siku njema kwangu, nilifika stesheni ya SGR nikiwa na furaha ya kuanza safari ya kuelekea Dar es Salaam, baada ya kukaguliwa tikiti yangu nikaambiwa niweke begi kwenye mtambo wa ukaguzi kisha nikaenda upande wa pili wa mtambo kulipokea begi.

Nilipofika upande wa pili nikasikia askari akitaka kumjua mwenye begi ambalo ni langu, nikajitokeza, kwa mshituko nikajikuta nipo kati ya askari watatu kijasho kilanitoka, nikaambiwa ndani ya begi kuna chupa ya maji, nikatakiwa niitoe, nikaitoa. Nikawaambia hayo ni maji yangu ya kunywa endapo nitahitaji kama ikitokea, wakati huo watu wameacha mazungumzo yao wakishuhudia kukamatwa kwa msafirishaji wa maji ya kunywa mil.500!

Kitendo cha kunihoji kijinai kilitaka kunifanya nivunje safari yangu ya SGR, baada ya mahojiano niliamriwa hiyo chupa ya maji mil.500 niiache kwenye kaunta yao alipo askari! Ndugu zangu hapo ndipo nilipojua si lazima uwe mwizi ili uende jela, mmoja wa askari aliniambia kosa hilo endapo ningeingia nayo ndani ya treni ni faini ya shilingi 500,000/=! Ninajuta kupanda SGR.
 
Ijumaa tarehe 20 saa 1:15 asubuhi haikuwa siku njema kwangu, nilifika stesheni ya SGR nikiwa na furaha ya kuanza safari ya kuelekea Dar es Salaam, baada ya kukaguliwa tikiti yangu nikaambiwa niweke begi kwenye mtambo wa ukaguzi kisha nikaenda upande wa pili wa mtambo kulipokea begi. Nilipo fika upande wa pili nikasikia askari akitaka kumjua mwenye begi ambalo ni langu, nikajitokeza, kwa mshituko nikajikuta nipo kati ya askari watatu kijasho kilanitoka, nikaambiwa ndani ya begi kuna chupa ya maji, nikatakiwa niitoe, nikaitoa. Nikawaambia hayo ni maji yangu ya kunywa endapo nitahitaji kama ikitokea, wakati huo watu wameacha mazungumzo yao wakishuhudia kukamatwa kwa msafirishaji wa maji ya kunywa mil.500!
Kitendo cha kunihoji kijinai kilitaka kunifanya nivunje safari yangu ya SGR, baada ya mahojiano niliamriwa hiyo chupa ya maji mil.500 niiache kwenye kaunta yao alipo askari! Ndugu zangu hapo ndipo nilipojua si lazima uwe mwizi ili uende jela, mmoja wa askari aliniambia kosa hilo endapo ningeingia nayo ndani ya treni ni faini ya shilingi 500,000/=! Ninajuta kupanda SGR.
Muwe mnasoma masharti,

Sgr inakataza kupanda na vyakula na vinywaji, wew unapanda nayo, ukipigwa fine hata Million ni uzembe hutakiwi kulalamika,

Btw, hizo sheria ni za kipuuzi, ila ndio hivyo zipo inabidi tuzifuate
 
Muwe mnasoma masharti,

Sgr inakataza kupanda na vyakula na vinywaji, wew unapanda nayo, ukipigwa fine hata Million ni uzembe hutakiwi kulalamika,

Btw, hizo sheria ni za kipuuzi, ila ndio hivyo zipo inabidi tuzifuate
Maji ya si sehemu ya vinywaji, kila kiumbe kinachoishi kina maji ndani yake, kasoro viumbe visivyo hai, hata hivyo staili ya ukamataji ni ya unyanyasaji. Wenye mabasi wanajua umuhimu wa maji ndiyo sababu wanatupa bila kutuuzia.
 
Ijumaa tarehe 20 saa 1:15 asubuhi haikuwa siku njema kwangu, nilifika stesheni ya SGR nikiwa na furaha ya kuanza safari ya kuelekea Dar es Salaam, baada ya kukaguliwa tikiti yangu nikaambiwa niweke begi kwenye mtambo wa ukaguzi kisha nikaenda upande wa pili wa mtambo kulipokea begi.

Nilipofika upande wa pili nikasikia askari akitaka kumjua mwenye begi ambalo ni langu, nikajitokeza, kwa mshituko nikajikuta nipo kati ya askari watatu kijasho kilanitoka, nikaambiwa ndani ya begi kuna chupa ya maji, nikatakiwa niitoe, nikaitoa. Nikawaambia hayo ni maji yangu ya kunywa endapo nitahitaji kama ikitokea, wakati huo watu wameacha mazungumzo yao wakishuhudia kukamatwa kwa msafirishaji wa maji ya kunywa mil.500!

Kitendo cha kunihoji kijinai kilitaka kunifanya nivunje safari yangu ya SGR, baada ya mahojiano niliamriwa hiyo chupa ya maji mil.500 niiache kwenye kaunta yao alipo askari! Ndugu zangu hapo ndipo nilipojua si lazima uwe mwizi ili uende jela, mmoja wa askari aliniambia kosa hilo endapo ningeingia nayo ndani ya treni ni faini ya shilingi 500,000/=! Ninajuta kupanda SGR.
Walikuona mlugaluga. Walitakiwa wakuambie uyaache tu hayo maji usipande nayo treni. Hao walinzi hawana common sense. Wao wako kama Bobby akiambiwa shika anashika.
 
Muwe mnasoma masharti,

Sgr inakataza kupanda na vyakula na vinywaji, wew unapanda nayo, ukipigwa fine hata Million ni uzembe hutakiwi kulalamika,

Btw, hizo sheria ni za kipuuzi, ila ndio hivyo zipo inabidi tuzifuate
Hapa ndipo CCM ilipofikisha watanzania? Kuna kosa gani la mtu kusafiri na maji ya kunywa? Kubeba maji imekuwa marufuku siku hizi? Lengo ni ili wanunuwe bidhaa za ndani ya treni ili vigogo waliojiwekea miradi yao wafaidike? Kweli Tanzania ni nchi yenye wananchi makondoo lakini ole wa hawa watawala. Kna siku watapata wanachokitafuta.
 
Ni utaratibu wa kawaida wa kuzia watu wasiingie na vitu ambavyo ni hatarishi kwa sgr, ili kuilinda sgr .

Kumbukeni hautakiwa kupanda na vyakula au vinywaji vyovyote vile kwenye sgr.

Vinywaji na vitafunwa utavikuta humohumo ndani ya sgr.
Pole kwa usumbufu ankoli.
Inaelekea unawaogopa sana police
 
Hapa ndipo CCM ilipofikisha watanzania? Kuna kosa gani la mtu kusafiri na maji ya kunywa? Kubeba maji imekuwa marufuku siku hizi? Lengo ni ili wanunuwe bidhaa za ndani ya treni ili vigogo waliojiwekea miradi yao wafaidike? Kweli Tanzania ni nchi yenye wananchi makondoo lakini ole wa hawa watawala. Kna siku watapata wanachokitafuta.
Mkuu, hizo ni sheria kwenye biashara, hata kwenye ndege hupandi na maji, uwe ulaya au bongo,
Na huko ni CCM ?
 
Back
Top Bottom