Nilikamatwa Morogoro stesheni ya SGR nikituhumiwa kusafirisha chupa ya mil.500 ya maji ya kunywa!

Nilikamatwa Morogoro stesheni ya SGR nikituhumiwa kusafirisha chupa ya mil.500 ya maji ya kunywa!

Mkuu, hizo ni sheria kwenye biashara, hata kwenye ndege hupandi na maji, uwe ulaya au bongo,
Na huko ni CCM ?
Unajua sababu ya kutokupanda na maji kwenye ndege?. Hizi treni ziko ulaya kitambo sana na hawana huu ujinga.
 
Muda wote maji ni dawa tosha na haihitaji kumuuliza mtu kama anakunywa maji au la, siku ikikutokea dharula ya kuishiwa maji mwilini ndipo utakapojua kuwa ni lazima muda wote uwe na chupa ya maji.
Ndani ya treni yapo yakutosha sana gentleman 🤣

kuna wanaoingia na visungura 🐒
 
Ijumaa tarehe 20 saa 1:15 asubuhi haikuwa siku njema kwangu, nilifika stesheni ya SGR nikiwa na furaha ya kuanza safari ya kuelekea Dar es Salaam, baada ya kukaguliwa tikiti yangu nikaambiwa niweke begi kwenye mtambo wa ukaguzi kisha nikaenda upande wa pili wa mtambo kulipokea begi.

Nilipofika upande wa pili nikasikia askari akitaka kumjua mwenye begi ambalo ni langu, nikajitokeza, kwa mshituko nikajikuta nipo kati ya askari watatu kijasho kilanitoka, nikaambiwa ndani ya begi kuna chupa ya maji, nikatakiwa niitoe, nikaitoa. Nikawaambia hayo ni maji yangu ya kunywa endapo nitahitaji kama ikitokea, wakati huo watu wameacha mazungumzo yao wakishuhudia kukamatwa kwa msafirishaji wa maji ya kunywa mil.500!

Kitendo cha kunihoji kijinai kilitaka kunifanya nivunje safari yangu ya SGR, baada ya mahojiano niliamriwa hiyo chupa ya maji mil.500 niiache kwenye kaunta yao alipo askari! Ndugu zangu hapo ndipo nilipojua si lazima uwe mwizi ili uende jela, mmoja wa askari aliniambia kosa hilo endapo ningeingia nayo ndani ya treni ni faini ya shilingi 500,000/=! Ninajuta kupanda SGR.
Afadhali hayo maji. Kuna mtu alinunua asali lita moja aende nayo Dar. Kwenye kupitisha kwenye scanner wakaiona. Eti wakamwambia aiache au ainywe yote lakini hakuna kuingia nayo kwenye train!!!! Hapo ndipo niliona hawa wafanyakazi wa SGR ni mataahira!!!! Sasa walitegemea huyo mtu angekuwa analamba hiyo asali ndani ya train? Hata common sense hawana.
 
Ukitaka ujue Watanzania bado kiza ukipita Mtera dam utasikia msipige picha hapa na wanaopiga picha wanawasumbua wakati Dunia imezungukwa na satellite ambayo inaweza kuchukua picha hata ya sisimizi popote pale juu ya uso wa Dunia..
Moja ya dalili ya ujinga ni kutojua nini cha kuzuia na nini cha kutozuia. Nini hatari na nini siyo hatari. Mwishowe unaona bora uzuie vyote ili usiumize kichwa. Hapo Mtera hata wangeweka utalii watu wapige picha walipe hata 3,000. Wangepata chochote kitu.
 
Hivi hii imeletwa kama luxury au usafiri wa UMMA ili kusaidia walipa kodi ? Sababu naanza kuona badala ya Serikali kutoa huduma imegeuka kuwa Mfanyabiashara
 
Moja ya dalili ya ujinga ni kutojua nini cha kuzuia na nini cha kutozuia. Nini hatari na nini siyo hatari. Mwishowe unaona bora uzuie vyote ili usiumize kichwa. Hapo Mtera hata wangeweka utalii watu wapige picha walipe hata 3,000. Wangepata chochote kitu.
Zipo damu kubwa kuliko Mtera kama Livingstone ya Zambia au ile ya Mozambique watu tuna Enjoy hayo maeneo bila kikwazo chochote Wabongo sasa kwa uongo usipige picha hapa eti Mtera unabaki kushangaa tu.
 
Zipo damu kubwa kuliko Mtera kama Livingstone ya Zambia au ile ya Mozambique watu tuna Enjoy hayo maeneo bila kikwazo chochote Wabongo sasa kwa uongo usipige picha hapa eti Mtera unabaki kushangaa tu.
Mbona hata daraja la Salenda Dar. nalo ni marufuku kupiga picha!
 
Mbona hata daraja la Salenda Dar. nalo ni marufuku kupiga picha!
Mimi sijui mkuu hapa dzonga napiga picha popote hata Ikulu ya Ramaphosa ukitaka ukapige picha unapiga tu enzi za Mbeki ilikua unaenda mpaka juu kule kwenye ofisi zao sema baada ya September 11 wakasitisha hizo mambo..Walinzi hauwaoni ila ni sehemu ambayo unakanyaga camera bila kujijua..
 
Hapa ndipo CCM ilipofikisha watanzania? Kuna kosa gani la mtu kusafiri na maji ya kunywa? Kubeba maji imekuwa marufuku siku hizi? Lengo ni ili wanunuwe bidhaa za ndani ya treni ili vigogo waliojiwekea miradi yao wafaidike? Kweli Tanzania ni nchi yenye wananchi makondoo lakini ole wa hawa watawala. Kna siku watapata wanachokitafuta.
Inashangaza. Mtu "kayaficha" maji yake kwenye begi, labda hana mpango wa kuyatumia ndani ya treni. Lengo lake akayatumie mbele ya safari, ameathiri vipi biashara ya vinywaji/vyakula vyao?
 
Back
Top Bottom