Nilikamatwa Morogoro stesheni ya SGR nikituhumiwa kusafirisha chupa ya mil.500 ya maji ya kunywa!

Nilikamatwa Morogoro stesheni ya SGR nikituhumiwa kusafirisha chupa ya mil.500 ya maji ya kunywa!

usipaki gari hapo wewe unapaki. Tusikukamate kweli?

usipite hapa kuna mbwa wakali, wewe unapita. Mbwa wakali watakuacha kweli?

Ni muhimu kua makini na kuuliza vitu vinavyokwenda maeneo mbalimbali nchini 🐒
Maji ya kunywa hayasimamiwi na bodi ya vileo, maji ya kunywa ni haki ya kila kiumbe kilicho hai na ruhusa kunywa wakati wowote na mahali popote.
 
Ijumaa tarehe 20 saa 1:15 asubuhi haikuwa siku njema kwangu, nilifika stesheni ya SGR nikiwa na furaha ya kuanza safari ya kuelekea Dar es Salaam, baada ya kukaguliwa tikiti yangu nikaambiwa niweke begi kwenye mtambo wa ukaguzi kisha nikaenda upande wa pili wa mtambo kulipokea begi.

Nilipofika upande wa pili nikasikia askari akitaka kumjua mwenye begi ambalo ni langu, nikajitokeza, kwa mshituko nikajikuta nipo kati ya askari watatu kijasho kilanitoka, nikaambiwa ndani ya begi kuna chupa ya maji, nikatakiwa niitoe, nikaitoa. Nikawaambia hayo ni maji yangu ya kunywa endapo nitahitaji kama ikitokea, wakati huo watu wameacha mazungumzo yao wakishuhudia kukamatwa kwa msafirishaji wa maji ya kunywa mil.500!

Kitendo cha kunihoji kijinai kilitaka kunifanya nivunje safari yangu ya SGR, baada ya mahojiano niliamriwa hiyo chupa ya maji mil.500 niiache kwenye kaunta yao alipo askari! Ndugu zangu hapo ndipo nilipojua si lazima uwe mwizi ili uende jela, mmoja wa askari aliniambia kosa hilo endapo ningeingia nayo ndani ya treni ni faini ya shilingi 500,000/=! Ninajuta kupanda SGR.
Nikajua chupa ya milioni 500😄😄😄.
 
Hujatuhumiwa kusafirisha chupa mil.500 bali ulifanya kosa la kutaka kusafiri na maji ya kunywa ndani ya treni ya SGR kinyume cha sheria, na uliendelea na safari baada ya kufuata utaratibu uliopo.
 
Inaonesha haujawahi kusafiri kwa treni, ndani ya treni imo baa inauza pombe.
Hii Sgr haina buffet car, ila kila behewa linajitegemea na huduma za vinywaji na cha kula na utahudimiwa na mhudumu husika kwa behewa husika.
Halafu sio kwamba wantakataza unnywaji wa pombe ukiwa ndani ya behewa maana hata wao wanauza pombe , Trc wanataka supply ya food and bevarage iwe juu yao kwa usalama wa kiwango chao.
 
Maji ya kunywa hayasimamiwi na bodi ya vileo, maji ya kunywa ni haki ya kila kiumbe kilicho hai na ruhusa kunywa wakati wowote na mahali popote.
Maji ni uhai na kwakweli ni muhimu mno kwa kila moja.
Lakini kwenye maeneo ya mikusanyiko yana utaratibu wake ambao uko wazi kabisaa.
Na maeneo yale nadhani kuna mabango ya kutosha kuhusu kipi kinaruhusiwa na kipi hakiruhusiwi...

Hata hivyo,
ungalikua umeishikilia mkononi maji yako, wangekuuliza nawe ungejieleza labda una tatizo na kwahivyo maji kwako ni dawa, hilo tatizo halingekua kubwa kiasi hicho..

Hata hivyo,
pole sana bilashaka kuna jambo umejifunza 🐒
 
Ccm inahusikaje hapa??
Hapa ndipo CCM ilipofikisha watanzania? Kuna kosa gani la mtu kusafiri na maji ya kunywa? Kubeba maji imekuwa marufuku siku hizi? Lengo ni ili wanunuwe bidhaa za ndani ya treni ili vigogo waliojiwekea miradi yao wafaidike? Kweli Tanzania ni nchi yenye wananchi makondoo lakini ole wa hawa watawala. Kna siku watapata wanachokitafuta.
 
Muwe mnasoma masharti,

Sgr inakataza kupanda na vyakula na vinywaji, wew unapanda nayo, ukipigwa fine hata Million ni uzembe hutakiwi kulalamika,

Btw, hizo sheria ni za kipuuzi, ila ndio hivyo zipo inabidi tuzifuate

Labda masharti ya waganga wa kienyeji. Masharti mengine huwa hatusomi kabisa
 
Ijumaa tarehe 20 saa 1:15 asubuhi haikuwa siku njema kwangu, nilifika stesheni ya SGR nikiwa na furaha ya kuanza safari ya kuelekea Dar es Salaam, baada ya kukaguliwa tikiti yangu nikaambiwa niweke begi kwenye mtambo wa ukaguzi kisha nikaenda upande wa pili wa mtambo kulipokea begi.

Nilipofika upande wa pili nikasikia askari akitaka kumjua mwenye begi ambalo ni langu, nikajitokeza, kwa mshituko nikajikuta nipo kati ya askari watatu kijasho kilanitoka, nikaambiwa ndani ya begi kuna chupa ya maji, nikatakiwa niitoe, nikaitoa. Nikawaambia hayo ni maji yangu ya kunywa endapo nitahitaji kama ikitokea, wakati huo watu wameacha mazungumzo yao wakishuhudia kukamatwa kwa msafirishaji wa maji ya kunywa mil.500!

Kitendo cha kunihoji kijinai kilitaka kunifanya nivunje safari yangu ya SGR, baada ya mahojiano niliamriwa hiyo chupa ya maji mil.500 niiache kwenye kaunta yao alipo askari! Ndugu zangu hapo ndipo nilipojua si lazima uwe mwizi ili uende jela, mmoja wa askari aliniambia kosa hilo endapo ningeingia nayo ndani ya treni ni faini ya shilingi 500,000/=! Ninajuta kupanda SGR.
Mkuu soma masharti ya kupNda SGR.
Ungekuwa umesoma hayo masharti usingepata usumbufu.
 
Mil. 500 ndo nini?
Mimi baada ya kusoma nilishindwa kuelewa mil.500
Inaingiaje hapo
Ila baada ya kuzisoma comments nikaona wote wanaona sawa tu
Ningekosoa ila nikasema labda ndio lugha yenu hiyo
Mil.500 na 500ml utofauti ni mkubwa sana ila wote wameelewa naona kasoro mimi na wewe 😄 🤣 😂
Na wewe uko Brazil kama mimi 😄
 
Back
Top Bottom