MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 14,588
- 32,361
Mkopo wa miaka 8 ni uwendawazimu aisee. Huwa najiuliza watu huwa hawapigi hesabu kabla ya kuchukua mikopo? Inatia hasira sana kuona mtu anachukua 5m na kulipa kwa miaka mingi bila kujali analipa Tsh ngapiKwa mkopo wa miaka 8 yaani Ile mikopo ya unafunga ndoa unazaa mtoto yupo darasa la tatu ndo mkopo unaisha riba hio ni sawa.
Mkopo ni laana Kama sio lazima ya ugonjwa au kusoma acha na kukopa bora ujenge taratibu taratibu.
Mkopo usizidi miaka 3
Wale ndo nyonyadamu wenyewe kuna kina tujiezeke wacha kabisa hawana huruma ndoa ya kikristo life time makatoSiyo asilimia 100 tu.Ni asilimia 140!Na hapo bado haujakutana na akina Faimbweka, Bayofpigs, Platedamnit nk. Huko mikopo ukisha kopa huwa haiishi. Watakukata maisha yako yoooteeee. Damnit!😂😂😂😂
Hakuna marejesho ya miaka 10..Tusitishane jamani interest rate kwa mwaka ni Kati ya 16% mpaka 18% kwa mwaka kwa mabenki haya tunayoyafahamu. Ukizidisha hiyo Rate na let say miaka mitano ya kulipia bado haifiki hata 100%. Ukute mtoa Mada alitaka arudishe pesa ndani ya miaka kumi.
Usimuamulie mtu pesa yake mkuu..Mkopo its all about time kama ni mda mrefu inaweza fika, kukopa hakukwepeki ila tukope kwa akili tusikurupuke unakopa kwenda kununua pikipiki au gari hapana
Muongo huyuu..Ila ndo 10M kwa 24M ? riba 100%+ huu ni wizi aisee
Usibishe Kuna bima processing fee n.k unakuta hiyo processing fee ni zaidi ya laki Tano bado bimaHii chai bwana. Tanzania hakuna benki yenye riba kubwa kiasi hicho. Labda kama umeenda kwa hawa kausha damu
Umehamisha Goal WeweUmesema jicho lipi likafunguka?
😀😅😃🤣😁😄😂😆😆😂😂😂Ndio yale unakuta mwisho wa mwezi mtu anaambulia 26,000
Mwa muda gani?Ila ndo 10M kwa 24M ? riba 100%+ huu ni wizi aisee
Inakuwa Kama Wanapofika Kukopa Wanapoteza Network Wanakuwa Mjumbe Ndiyo Kwa Kila Kitu. Sehemu Nyingine Wanaweka ATM Card KabisaMkopo wa miaka 8 ni uwendawazimu aisee. Huwa najiuliza watu huwa hawapigi hesabu kabla ya kuchukua mikopo? Inatia hasira sana kuona mtu anachukua 5m na kulipa kwa miaka mingi bila kujali analipa Tsh ngapi
Hili ni fumboWala siyo kweli. Ina maana hukujaza Mkataba mpaka usubirie slip? Maana mkataba huainisha kiasi chote unachopaswa kulipa.
Na hakuna benki Tanzania inayotoza riba ya zaidi ya asilimia 100. Hakuna.
Hii ni Chai.
Q😆😆😆hiyo ilikuwa StrokeAcha kabisa aisee!
Nikiwa nimepagawa na changamoto iliyokuwa inanikabili bila kujua la kufanya, nikakimbilia benki moja kuomba mkopo. Kufika pale nikamuambia afisa mikopo kuwa nahitaji m15, akaniambia m10 ni utapata lakini si hizo ulizotaka. Nikaona kheri tu itaokoa kitu tena kwa kiasi kikubwa sana tu.
Wakati huo, simu inapigwa kila baada ya sekunde 20 kutoka huko kwenye changamoto iliyonifanya niende kukopa, nilipagawa sana. Wakati afisa mikopo ananieleza habari za makato n.k mimi hata sikuwa nasikia chochote.
Akili ilikuwa kwenye kupata pesa tu nikamalize tatizo. Siku kadhaa mbele nikafanikiwa na tatizo likaisha na akili ikarudi katika utulivu wa kawaida.
Siku zinavyoenda haraka, mwisho wa mwezi ukafika bwana! Aisee, ile naiangalia salary slip sikuamini nilichokiona. Milioni 24 nahitajika kulipa. 24M!!
Kwanza nilihisi baridi, halafu ganzi; baadae nikahisi uono wangu kama hauko sawa. Nikajiuliza imekuaje mbona sioni vizuri? Kwakuwa nilikuwa chumbani, nikasogea kwenye kioo kujiangalia. Dah, si ndo nakuta jicho moja la upande wa kushoto limejifunga, kope haitaki kupanda juu ('kukupila' watu wa pwani ya kusini wanasema).
Nikajaribu kulifunua kwa mkono, wapi! Nikiliacha linajifunga tena. Hali iliendelea hivyo kama dakika 40 au saa moja hivi. Baadae sana ndo likarejea katika hali ya kawaida. Nilishapagawa, nilijua limeparalyse!
Mikopo!!!! Ukiweza kuachana nayo iache ndg'angu!
Kumbe?Eneo hill la mikopo linaumiza watu wengi sana kwasababu shida ikikutinga mambo mengi huyazingatii pia inakuwa siri lakini ukweli upo palepale Bank zinaendeshwa Kinyonyaji na unyonyaji umejificha kwenye masharti yaliyoandikwa kwa herufi ndogo.
Tunauenzi Ubebari tulioupiga vita Sikh nyingi mfano ukiambiwa mkopo wako ni asilima 10 ya pesa unazodaiwa hata ukilipa pesa ikapungua bado wao wanakata hata pesa uliyokwisha lipia.
Mfano ukikopa 10 mil. Makato ya liba ya 10 mil yataendelea hata kama deni limebakia lakini moja.