Nilimpiga Mwalimu akahama shule

Sema akili za uanafunzi na utoto ni za kijinga sana ingawa baadae huwa kuna majuto makubwa.

Nakumbuka shule ya Msingi tulikuwa na Mwanafunzi Mwenzetu anaitwa Charles "Mapua", alikuwa amejaaliwa pua kusawasawa, Jamaa lilikuwa likubwa nadhani alichelewa kuanza shule...kuna siku Ticha alitaka kumuadhibu Jamaa akagoma...ile Mwalimu anamlazimisha akamsukuma Mwalimu akaanguka, Mwalimu kainuka Jamaa akamchimba biti "nichape uone", kwa bahati Ticha aliingia baridi akaufyata, akimuangalia Jamaa bonge la Mtu jeusiii...Jamaa likaondoka...Jamaa alisimamishwa shule ingawa hata hivyo hakuwa Mtu anayejali sana masomo...ila shuleni ikabaki bonge la gumzo.
 
Ujana maji ya fire
 
...Ongeza Sukari ! [emoji57][emoji57]
 
Kwahiyo wewe ni TISS mkuu doh....

TISS ya siku hizi imekosa ueledi
 
Hakuna TISS mpumbavu na mjinga kama hiyo kenge hapo juu
Usipende kutukana watu ovyo,unaweza ukajiona upo okay kwakuwa huko online hujulikani,ila nikitaka kukupata wewe simalizi masaa 15 nakupata,jaribu kuset mind yako usiwe unamwili mkubwa lakini akili kisude,mimi nilichokiandika hapa ni uzi wangu wewe ulipaswa kusoma au kupuuzia,ila matusi ya nini I??kila binadamu anazaliwa tofauti hayo niliyoandika yalikuwa mapito ya kunijenga ili nifike hapa nilipo maana MUNGU alikuwa ananiandaa,sasa wewe unashindwa kufikiri unatukana ovyo,ili ni tatizo kwa jamii yetu kupuuzia na kuchukulia mambo juu juu,bwana mdogo jiheshimu sio kila mtu anatukanwa,au kwakuwa unatumia fake id ndo ujulikani??be care fully
 
Achana na hao wenye jealous mwamba we lete mastory tupate ideas ,dunian ni shule ambayo kila mtu anapaswa ajifunze.

Ushaur usijib kila mtu hapa jukwaan wewe timiza lengo la kufikisha kwa jamii kwa namna ilivyokupendeza ,Kuna wengi watajifunza kitu hapa.
 
Kweli binadamu tupo tofauti sana,sawa nitaendeleza mkuu
 
πŸ™πŸ™
 
Inaendeleea..
Baada ya mambo hayo kupita,niliendelea namaisha kama kawaida,cheo changu kile cha kaka mkuu kilikuwa kigumu sana kwangu,nilitakiwa kubaki shule mpaka mda wa saa 11 jioni ndo niindoke kwenda nyumbani,nilitakiwa nihakikishe wanafunzi wote hawapo kwenye viduka wala kwa wanaouza bangi(mapusha)..

Vikao vya walimu nilikuwa nahudhuria,na kutoa changamoto zinazowakumba wanafunzi wenzangu,kuna mwanafunzi mmoja nilimsaidia mpka akawa anasoma bure,maana alikuwa hana mzazi hata mmoja wote walifariki kwa ajali siku moja,na ndugu walihaidi watamsomesha lakini hawakufanyaa hivyo,ilinibidi niongee na headmaster wamtafutie mfadhili kutoka Australia ndo mshikaji akaendelea na masomo jamaa alinishukuru sana,kwangu mimi ilikuwa ni jambo jema kurudisha furaha ya mtu tena.

Wanafunzi wale wahuni taratibu wakaanza kubadilika,na kuhudhuria shule,taratibu uhuni ukapungua shule,sasa mtaani hali ikawa tofauti maana wale mapusha waliokuwa wanawauzia wanafunzi bangi wakatengeneza bifu nami,sikujali wala nini niliendela na majukumu yangu,nilitengeneza kikosi kazi cha makamanda wa 5 ambao walikuwa wanafunzi wahuni sana,niliwapa cheo mbele ya assembly kuwa watakuwa wanafanya doria kuzunguka maeneo yote ya shule,kuhakikisha hakuna hata mwanafunzi yupo mtani mda wa masomo wanadhurura ovyo,nilifanya hivyo kwakuwa wale walikuwa wanajua machocho yote ya kujifichia wanafunzi.

Shule ikawa tulivu sana,nakumbuka siku hiyo tukiwa darasani niliitwa na mwalimu wanidhamu,baada ya kutoka nje aliniambia niende officine kwa head master, nilipofika mkuu wa shule Alinipa sifa sana kuwa nimeweza kutuliza shule,nakuwafanya wanafunzi wote wahuni kuhudhuria masomo,aliingiza mkono kwenye droo akatoa bahasha ya kaki,akaniambia hii ni zawadi yako,sikuhamini..

Nilienda chooni kuangalia kuna nini,niliifungua taratibu nikakuta pesa mabunda mawili,ilikuwa laki 2 ,nilifurahi sana maana kwangu mimi niliona hii ngekewa maana nilikwisha potea kabisa kwenye uhuni,na walimu walinichukia sana sema kwakuwa nilikuwa nafaulu sana walikuwa hawanala kuongea..

Nilitoa laki moja nikawapa wale makamanda wangu wa 5 nikawagia kila mmoja elfu 20 walifurahi sana,nilienda zangu soko la tengeru nikanunua Travolta nyeusi kwa ajili ya shule,kipindi nikiwa shule nilikuwa nadhifu sana,kiatu kiwi imekubali sana,nimechomekea sharti la mikono mirefu,huku shingoni nimevaa tai ya uongozi yenye zebra zebra,nilipendeza sana.nilikuwa sili vyakula vya shule,ugali maharage,makande,nilikula na walimu meza moja asubuhi chai ya maziwa au uji wa lishe,mchana wali au ugali wa nyama,kwangu mimi sikujua ladha ya vyakula vya shule baada ya kuwa kaka mkuu,wanafunzi walikuwa wananiambia leo makande yamewekwa mafuta ya taa,nilicheka sana..πŸ˜‚πŸ˜‚

Wanafunzi wa kike wakaanza kunisumbua sasa,nikaanza kupokea vibarua vya mapenzi kibao kutoka kwa wanafunzi wa o level mpaka advance,kwakuwa niliheshimu cheo changu niliwapotezea..

Nilitokea kupendwa na mdada mmoja wa A level kwa jina anaitwa Clara, aisee alikuwa pisi la maana yani mtoto kasimama kweli,ni mrefu,anaweusi wa kuteleza ana bonge la shepu,tuliendana maana mimi mwenyewe ni mweusi pia mrefu sana siunajua watoto wasikazini ni matall sana,(nimesherehesha kidogoπŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…)

Clara alikuwa mnzuri sana,kila wanafunzi alitaka kuwa naye pale shule,ilikuwa ni kitu cha ajabu mwanafunzi wa O level form 3 kutembea n awanafunzi A level form 5,ilikuwa ni jambo la ajabu sana,lakini Clara alinipenda sana,mapenzi yana nguvu sana.

Nakumbuka siku hiyo shule kulikuwa na graduation ya form 4,mimi na walimu ndo tulianda tukio nzima,kipindi nikiwa shule nilikuwa naandika na kuchanika sana hiphop,hata kwenye stage mbalimbali arusha nishapanda sana..
 
Kawatishe wapumbavu wenzio unajisifia ujinga hapa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…