data
JF-Expert Member
- Apr 9, 2011
- 26,858
- 23,768
Fu ck you!Sasa kazi ikaanza kama kaka mkuu wa shule,huku ndo kuna kimbembe hatari..
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Fu ck you!Sasa kazi ikaanza kama kaka mkuu wa shule,huku ndo kuna kimbembe hatari..
You to,de punta madreFu ck you!
Fu ck again!Mwingine nilichoandika hapa anaweza ona ni utani,au najisifia siko hivyo,yote ni mazoezi nayopiga kila siku
You to de punta madreeFu ck again!
Ffffff...kk😅😅😅😂🤣😂Niliendelea na cheo changu cha kaka mkuu huku nikiudhuria vipindi vyote darasani
Ushaanza kupunguza uuuuuuuFfffff...kk😅😅😅😂🤣😂
Duh!,hii adhabu ni kibokoI naendelea......
Niliishia pale walinzi waliponikamata,wakaniweka chini ya ulinzi...
Nilipokuwa pale chini ya ulinzi,ndo ilikuwa mda wa wanafunzi kwenda nyumbani,ilikuwa assembly wanafunzi wote wa shule wapo..
Academic master alipomaliza kuongea na wanafunzi,akanifuata huku ameshika fimbo kama la kuua nyoka,akaniambia simama,Academic alinichapa kinoma,yani fimbo yote ikavunjika,alafu Academic alikuwa mjeshi..
Fimbo ilipovunjika akaanza kunitandika makofi,nilikula makofi na mitama,kama ningekuwa sina mazoezi ningekuumia sana,maana makofi mengine niliyablock,sema sikutaka kumrudishia maana ningeharibu zaidi..
Nilipigwa mpaka wakaingilia wale walinzi walionishika,wakaniamua wakanipeleka kwa head master.
Nikapewa suspension ya week 2,nilipoenda nyumbani mzazi alikuwa kashapigiwa simu kutoka shule,kuwa nimempiga mwalimu akazimia.
Nilipofika nyumbani baba alinipokea kwa ngumi,mpaka mama akawa anapiga ukunga uwiiii uwiiii,ndo wakaja ndugu wakaamua huku mimi sura imezimba hatari..
Niliuguzwa siku nne,bila kutoka nnje,nilikuwa nakula kwa shida maana mdomo ulivimba sana..
Suspension ilipoisha nilienda shule na baba,akaonge na head master kwa mda mrefu mpaka nikasamehewa ila nikapewa masharti mawili..
Sharti la kwanza nikubali kuwa kaka mkuu wa shule...
Sharti la pili nipambame na wanafunzi wote wahuni,wavuta bangi,yote hayo nilikubali.
Sasa kazi ikaanza kama kaka mkuu wa shule,huku ndo kuna kimbembe hatari..
Itaendeleeea....
Ya rasta manDuh!,hii adhabu ni kiboko
Nimekumbuka chuo tuliwah kuwa na Rais mvuta bangi,watu wa mlengo huo tuliinjoy maisha sana
JamiiforumInaendeleeea......
Yule jamaa aliongea akiwa na hasira sana,huku akiwa ameshika pisi la gogo,nikajisemea moyoni 'leo litakufa jitu',ghafla nikapigwa na lile gogo la kifua mpaka chini..
Nikiwa na ugulia maumivu akaja jamaa mwingine akanipiga teke la tumbo,alinipa hasira nilikurupuka najiwe mkononi,nilimtandika mshikaji mmoja la kifua mpaka chini,ile wanatahamaki aliyekuwa mbele yangu nilimpiga ''rear leg front kick''wapembeni nikageuka na ''tornado kick'',wengine walipoona wenzao wapo chini walikimbia,nilimfuata yule jamaa aliyenipiga jiwe akiwa anasimama nikampiga ''wing chun punch ''za kifua mpaka akatapika damu,msela angu alimkimbilia mmoja aliyekimbia akampiga mtama mpaka chini.
Mwingine nilichoandika hapa anaweza ona ni utani,au najisifia siko hivyo,yote ni mazoezi nayopiga kila siku,yanayonifanya nijiamini ninapokuwa popote,hapa nimeweka video ya jinsi ya kupiga mateke tofauti tofauti,ukitaka nikufundishe mwenyewe nipo arusha kwa sasa.
View attachment 2389908
Tuendelee,mpaka wale wakurupukaji wa kubwabwaja huko mwanzoni wafiche nyuso zao matak o nIna endeleeea!!!!@
Niliishia pale nilipopambana na wale wahuni,kweli ilikuwa hatari sana kwa mtu muoga kuwekwa kati na kundi la wahuni unawajua,matukio wanayofanya mtaani ya kihuni lazima upate waiwasi,sema kilichonisaidia ni mazoezi ya taekwondo,kama ningekuwa sina uwezo wa kujua ngumi nahisi pale wangenivunja vunja,maana jamaa walikuja kuniangamiza kabisa..
Baada ya fujo zile kupita,tulihairisha kwenda kwenye maporomoko ya maji,tukaona ni bora kurudi zetu home,maana wasi wasi ulitujia labda wameenda kukusanya kundi kubwa la wahuni.
Niliendelea na cheo changu cha kaka mkuu huku nikiudhuria vipindi vyote darasani,nilipunguza uhuni sana ,nikawa nakimbiza class,walimu walinipenda sana wakanipachika jina ""mwanakondoo wa bwana""😄😄😄
Hii siku sitakuja kusahau,arusha kuna tabia ya wanafunzi kwenda picnic,nakumbuka ilikuwa jumamosi tuliandaa kwenda picnic usa River arusha kulikuwa na club huko, jina limenitoka maana ni mda sasa. tulipendaga kwenda kwenye hiyo club kuenjoy maisha.
Siku hiyo nilijiandaa vinzuri,nilivaa kama cheguevara anavovaa..
Nilipiga jinsi yangu nyeusi kali iliyonibana kwa jina arusha inaitwa mnyonyo,chini nilivaa Travolta nyeusi,juu.nikavaa sharti langu la kaki la kiscout,juunkichwani nilivaa kofia aina ya baret ya kijani,ukiniona tu mwambaaa huyoo👌😜😜,nilibeba begi langu la janssport la kijani,ndani niliweka bapa la konyagi kubwa...
Niliondoka nyumbani saa 3 asubuhi nikiwa na yule msela angu wa kitaa,tulichukua hiace mpaka usa River,tukashuka,tukatembea kwa mguu mpaka kwenye hiyo club pana umbali kiasi,tulifika saa 6 hivi.
Baada ya kufika tulikutana na shanzi kubwa la wahuni wote washule za arusha,na mademu wale wajanja wajanja wa shule za chugah,kuna wengine niliwajua wengine ndo siku ya kwanza nakutana nao,pia kulikuwa na maraia ambao walikuwa sio wanafunzi,ni wahuni tu ambao wanapenda kuudhuria club ili kuwaibia wanafunzi..
Hii story ni ndefu sana,tena inautamu sana,mbeleni ndo patamu kinoma..
Itaendeleeeea.....
Mzee watu wanajudge mtu bila kujua kuwa yalikuwa mapito tuT
Tuendelee,mpaka wale wakurupukaji wa kubwabwaja huko mwanzoni wafiche nyuso zao matak o n
Inaeeendeleeeea!!!T
Tuendelee,mpaka wale wakurupukaji wa kubwabwaja huko mwanzoni wafiche nyuso zao matak o n
🤣 🤣 🤣 🤣. Fate ya watu anapanga MUNGU.Unaweza ukakuta ni afisa mmoja serikali I…Kuna mwamba mmoja yupo Tra ila alikuwa bangi sana na itikadi kama za huyu jamaa
Kweli mkuu🤣 🤣 🤣 🤣. Fate ya watu anapanga MUNGU.
Wakuache Mkuu.Kila mtu unayemuona mtaani, awe chizi, awe tahira ila anakitu kichwani mwake, MUNGU HAkumuumba binadamu tahira, iweje wewe uniite tahira? siku zote mtu mwenye kasoro daima hutoa wenzake kasoro ili kujipa moyo
Hawaelewi,sehemu na mazingira niliyokulia pamenifanya niwe shupavu,mtu hubadilika kulingana na mazingiraWakuache Mkuu.
Madhara ya kumpiga mwalimu mpaka leo yanaonekana. Eti HIISHE. ni lugha gani hii?Subiri hadithi hiishe
[emoji23][emoji23][emoji28] Wa kawaida mno
Kuna msela kwao kulikuwaga na pesa sana,nakumbuka tulikuwa tukiwa likizo alikuwa anapenda kwenda arusha,na baadae alianzisha kuandaa matamasha na mziki picnic,tulikuwa tunakutana huko wanafunz wa shule mbalimbali wanafunz walikuwa wanakunywa pombe sana siku hiyo na mziki ulikuwa unapigwa mpaka saa mbili usiku hz mambo zilikuwa zinafanyikaga jumamosi,naona haya mambo aliyatoa huko Arusha.Inaeeendeleeeea!!!
Kweli club kulifana sana,walijaa wahuni wa kila pembe za arusha,baadhi niliyokuwa nawajua chajop,John mabala,Ebenezer,Ringo akiwa na ndugu yake mojaa,Chingori mshikaji mmoja wa ungalimited aliyekuwa fit sana kwenye kick boxer,watu walimuogopa sana pia alikuwa amefuatana na dada ake ambaye pia alikuwa fit sana kwenye ngumi..na wengine wengi wahuni,vibaka,majambazi..
Tulikunywa pombe club huku tukicheza mziki mpaka mida ya saa 11 jioni club ikafungwa,kimbembe ikawa mda wa kurudi town sasa,maana kuna umbali mpaka ufike kwenye hiace za kwenda Town ni kilomita za kushanta zisizopungua 10.kwa kukadiria..
Tulipokuwa tunatembea kuelekea kupanda gari za Town,John mabala(arusha sec) alikuwa na bifu na ebenezer(arusha sec),toka kitambo walikuwaga marafiki sana,walipozinguana wakatengeneza visasi kwa kila mmoja wao..
Basi tukiwa tunatembea huku tumelewa,tupo wengi barabarani John mabala akamfuata Ebenezer, akamwambia kama vipi leo tumalize ugomvi huku huku,mpaka tujue mbabe nani,aisee huyo John mabalaa alikuwa sio powah jamaa alikuwa fiti sana kwenye mateke,na ukicheki mshikaji wangu ni Ebenezer pia yeye alikuwa fiti sema.sio sana..
Huyo mabalaa akampiga Ebenezer round kick ya shingo,Ebenezer akaweweseka mpaka nilipokuwa nimesimama mimi,nikamzuia kwa mkono,nikamwambia kausha kausha mabalaa,mabalaa akanifuata akaniambia wewe ndo nilikuwa nakutafuta siku zote sasa nimelianzisha ili ujae,umewazingua madogo sana shuleni wakivuta kaya unawang'ang'anya,unajifanya kaka mkuu wa shule leo hii nataka kupigana na wewe,tupiganeeee aliongea kwa nguvu tena kapandisha mzuka..
Ile na tahamaki jamaa karusha right hook,nikakwepa ile nakaa sawa akanipiga wash ya usoni, nikajisemea moyoni leo hii nimekutana na jet Lee.
Kusema la kweli sikujua kama ingetokea ugomvi siku hiyo,kumbe watu walikuwa na bifu nami toka kitambo sana,kitendo cha kuwa kaka mkuu kimenitengenezea bifu kwa watu,sio wavuta bangi tu mpaka wauzaji ambao wanaogopeka mtaani.
John mabalaa akachomoa kisu,ile anataka kunichoma kisu msela angu Ebenezer akanikingia kisu akachomwa cha mbavu,akamchoma tena visu vya paja kama mara tatu,John mabalaa alikimbia baada ya kuona damu inamtoka sana Ebenezer..
Itaendeleeea nikipata mda wa kuandika tena
Sijawahi kusoma shule ikawa haina kiranja mkuu wa shule! Chuo Kuna rais wa serikali ya wanafunzi.Kulikuwa hakujawahi kuwa na kitengo hicho kabisa