Nilimruhusu msaidizi auze bidhaa zake ndogo ila zinamlipa kuzidi mshahara wake. Je, nifanye maamuzi gani?

Nilimruhusu msaidizi auze bidhaa zake ndogo ila zinamlipa kuzidi mshahara wake. Je, nifanye maamuzi gani?

Write your reply...mkuu usisahau biashara ni kipaji lakini pia unaweza kumiliki biaahara lakini usiwe na wateja au kuweza kufanya wateja waje kununua kwako kwani hujawahi kusikia kuna watu ukimwueka akuuzie biashara siku akihama au ukimuondoa basi anahama na wateja wengi au biashara haitokuwa nzuri sana kama kipindi alikuwepo yaani kuna watu wana damu ya biashara,wana kismati. .usikute hata hiyo faida unayopata ni vile tu nyota yake inang'aa kwenye biashara yako ndo hivyo faida nono inaonekana yaani mtu ana upepo wa pesa ambao unakunufaisha na ww pia ,badala umtumie vizuri kutengenesa pesa zaidi eti unataka mfukuze wakati unaweza tajirika kupitia kipawa chake kwa kutembelea upepo wake ni vile tu hujui hao watu ni lulu kiroho na ni vp unufaike nao.! haya mfukuze utapata tabu kuisimamisha tena biashara kama hutopata mtu sahihi anaendana na aina ya biashara yako kwani wengine wanapaswa kuwa wamiliki tu hawatakiwi kuwa waendeshaji au wauzaji wa biashara la sivyo itadoda au kufa kabisa sababu huendani nayo ww au muuzaji uliyemuweka.. hivyo acha kijana afanye kazi ukimtoa utaharibu
 
Hao kuku wanaokuambia roho mbaya ukute hawajawahi hata kufanya biashara...

Ngoja nikuambie, Mimi kitambo nilikua nauza duka la mtu, hivyo hivyo nikaanza kuweka bidhaa zangu kisiri siri(MALENGO), akija mteja nachukua namba, nampigia namuelekeza duka letu jingine(ROHO MBAYA), sehemu niliyokua nauza mimi kodi ilikua chini hivyo Bei ikawa ipo chini pia, ila pale kwa Boss sababu ni potential nikawa napatumia kutangaza biashara yangu ila delivery nyingi zinafanyika kupitia kwangu, (ROHO MBAYA PLUS).
Baada ya hapo mauzo yakawa yapo chini, ila kwa sababu bado ile sehemu naihitaji, lakini pia nisimzunguke 100% mtu alieniamini, bila yeye kujua nikamshauri tuweke mzigo wa jumla, ambao najua mimi sina uwezo nao..
Akazama mfukoni tukashusha Kontena,
BIASHARA IKAPANDA, akanishukuru sana kwa idea ile na Mimi nikapanda,
WIN WIN..

Wewe usihangaike na faida yake, hangaika na mauzo/faida yako, jipe muda, ukigundua inashuka sababu ya biashara yake, Mlipe kwa % au piga chini, ukiona inapanda(ilishuka kwa sababu nyingine) muache, hata akiingiza faida kama yako, kuna watu wana vismati, as long wote mnakula basi sawaaaaa..

Sasa wewe wasikilize hao ngiri eti roho mbaya, kesho ufunge biashara uje hapa wakugeuke...
Yaani nilipe kodi ya 500k, nikulipe 220k, nitoke kwenye faida ya 800k nije 300k, kwa sababu YAKO, nikuache eti kisa na wewe unatafuta? Nani asiyemtafutaji???
Kila mtu ashinde mechi zake.
Balance mambo yako twende sawa.
 
roho mbaya itaondoa baraka zako zote picha imejieleza maamuzi ya hovyo ukichukua kitakupata icho
 

Attachments

  • 1731615794672.jpg
    1731615794672.jpg
    685.1 KB · Views: 4
Uki
Uzi huu nimeweka jukwaa la biashara nategemea michango yenye tija. Tujue kutofautisha biashara na vituo vya kutoa misaada bure, msikiti, kanisa, n.k,

Kuna kaduka nilifungua, kwakuwa utumishi umenibana niliweka msaidizi anisaidie.

Biashara imeshuka lakini kibishi naendelea nayo

nikitoa gharama za frame nayolipia laki 5 kila mwezi (AISEE !!), mshahara, allowance, umeme, usafi, Tra, leseni, n.k. naingiza faida ya laki 3 hadi 4, Kabla biashara haijashuka ilikuwa ni Laki 8+

msaidizii aliwahi kuniomba aanze kuweka bdhaa zake, Nilichukulia poa kwasababu niliona bidhaa anazouza ni ndogo na ni nje ya biashara nayofanya, Nikamruhusu.

Mshahara naomlipa ni 150,000 kwa mwezi, allowance ya matumizi yake elf 70, jumla 220,000

Leo nilifika dukani hayupo kafunga, nina ufunguo wangu nikaingia, kuna kidaftari nilikiona kwenye draw.

Kapangiliaia vizuri sana hesabu zake, kila siku anafunga hesabu kwa faida ya elf 6 hadi 7, sometmes elf 8

Nilipiga picha fasta, nimefika home nimepiga hesabu, mwezi uliopita kaingiza faida 183,500

Kuna maamuzi kadhaa nataka nichukue

  • Nimwambie awe anachukua faida asilimia kadhaa kwa biashara yoyote atayoifanya dukani kwangu
  • Nisimlipe mshahara wake niwe nampa aloowance pekee, ajilipe mshahara kwenye faida
  • Nimpe miezi kadhaa auze, baada ya hapo iwe biashara yangu

Ni jambo liliilonfanya nitafakari sana, nichukue maamuz yapi.

Kwa wale ambao mnaingiza mambo ya huruma, mle mlale

Uzi huu nimeweka jukwaa la biashara nategemea michango yenye tija. Tujue kutofautisha biashara na vituo vya kutoa misaada bure, msikiti, kanisa, n.k,

Kuna kaduka nilifungua, kwakuwa utumishi umenibana niliweka msaidizi anisaidie.

Biashara imeshuka lakini kibishi naendelea nayo

nikitoa gharama za frame nayolipia laki 5 kila mwezi (AISEE !!), mshahara, allowance, umeme, usafi, Tra, leseni, n.k. naingiza faida ya laki 3 hadi 4, Kabla biashara haijashuka ilikuwa ni Laki 8+

msaidizii aliwahi kuniomba aanze kuweka bdhaa zake, Nilichukulia poa kwasababu niliona bidhaa anazouza ni ndogo na ni nje ya biashara nayofanya, Nikamruhusu.

Mshahara naomlipa ni 150,000 kwa mwezi, allowance ya matumizi yake elf 70, jumla 220,000

Leo nilifika dukani hayupo kafunga, nina ufunguo wangu nikaingia, kuna kidaftari nilikiona kwenye draw.

Kapangiliaia vizuri sana hesabu zake, kila siku anafunga hesabu kwa faida ya elf 6 hadi 7, sometmes elf 8

Nilipiga picha fasta, nimefika home nimepiga hesabu, mwezi uliopita kaingiza faida 183,500

Kuna maamuzi kadhaa nataka nichukue

  • Nimwambie awe anachukua faida asilimia kadhaa kwa biashara yoyote atayoifanya dukani kwangu
  • Nisimlipe mshahara wake niwe nampa aloowance pekee, ajilipe mshahara kwenye faida
  • Nimpe miezi kadhaa auze, baada ya hapo iwe biashara yangu

Ni jambo liliilonfanya nitafakari sana, nichukue maamuz yapi.

Kwa wale ambao mnaingiza mambo ya huruma, mle mlale
Unapopiga goti kumuomba Mungu usisahau kumuomba moyo wenye huruma na unyenyekevu
 
Muite muweke chini, umueleze kikubwa biashara yako kaiona imedrop, gharama za frem, mshahara na vitu vingine biashara haiendi, yeye anaonaje.. Msikilize kwanza.
Muulize kwake biashara ikoje, kama inalipa vizuri, umuongezee posho, mshahara muuvunje mpaka pale biashara itakapokaa sawa.

Kama kweli anapata faida atakubali.

Lakini mkuu faida ya 180k ndio ya kukutoa roho?
Hii imekaa poa kabisa jamaa aache kuendekeza tamaa atakuja kujuta mbeleni
 
Kuna wadau wanasema una roho mbaya lakini siyo roho mbaya umakini unahitajika kwenye biashara,ni kosa kuanzisha biashara ndani ya biashara ya mtu mwingine haina uaminifu,fremu unalipa wewe,mshahara na posho unamlipa,ajiongeze na hela za malipo yake mwisho wa siku aache ajira yako afungue biashara zake.

Hiyo kitu ilinifelisha kwenye biashara kuja kugundua ananirudisha nyuma,aliomba aanzishe biashara yake ndani ya kwangu mwisho wa siku anajikopesha bidhaa zangu atumie kuendesha biashara yake humo humo,mwisho wa siku hata katon ya maji ataleta ataacha yako yake itoke kwanza ndo auze yake we unashangaa mbona bidhaa hazitoki kumbe ana zake humo anazitoa kwanza. Nikajiuliza mi nikikaa kwenye biashara siku sina kazi naingiza hela kubwa kuliko siku yeye akiwa mwenyewe.
 
Hii roho yako mleta mada ndio wabongo wengi wapo hivyo,

Huruma inakuwa mwanzoni ili mtu ajihisi yupo huru kufanya chochote ili tu awe comfortable.

Najua huko kumwambia ajiongeze kwa vitu vidogo vidogo dukani kwako ilikuwa ni kumfanya awe huru na asijutue kufanya kazi kwako.

Lakini matokeo ya uhuru huo ndio wabongo wengi hawapendi na roho mbaya na chuki juu ya mtu ndio inapo anzia.

Hapo cha kufanya ni umuache aendelee na kazi yake na usimuingilie kwa chochote as long as anakufanyia kazi na anakuingizia pesa kama inavyotakiwa.

Akikuza msingi wake na akiamua kuondoka kufungua biashara yake pia unatakiwa umuache aende .
Ilitakiwa amshauri Boss wake aongeze hizo biashara ndogo ndogo Ili mapato ya Boss yaongezeke. Hili nitatizo la wabongo wakipewa ajira wanaangalia namna ya kujinufaisha wao badala yakuongeza mapato katika biashara walizo ajiriwa.
 
Kuna wadau wanasema una roho mbaya lakini siyo roho mbaya umakini unahitajika kwenye biashara,ni kosa kuanzisha biashara ndani ya biashara ya mtu mwingine haina uaminifu,fremu unalipa wewe,mshahara na posho unamlipa,ajiongeze na hela za malipo yake mwisho wa siku aache ajira yako afungue biashara zake.

Hiyo kitu ilinifelisha kwenye biashara kuja kugundua ananirudisha nyuma,aliomba aanzishe biashara yake ndani ya kwangu mwisho wa siku anajikopesha bidhaa zangu atumie kuendesha biashara yake humo humo,mwisho wa siku hata katon ya maji ataleta ataacha yako yake itoke kwanza ndo auze yake we unashangaa mbona bidhaa hazitoki kumbe ana zake humo anazitoa kwanza. Nikajiuliza mi nikikaa kwenye biashara siku sina kazi naingiza hela kubwa kuliko siku yeye akiwa mwenyewe.
Wabongo wengi hatuwezi kuajiriwa Wala kujiajiri. Mtu umepewa nafasi ya ajira, badala utumie nafasi hio kukuza biashara ya boss wako, sisi hutumia nafasi hio kuangalia namna ya kujinufaisha. Ni mpumbavu pekee anaeweza ruhusu kitu hicho. Vinginevyo awe ni mtu tajirii ambae kashajipata, ambae anataka kutoka kwenye uuzaji wa rejareja kwenda jumla.
 
Hii imekaa poa kabisa jamaa aache kuendekeza tamaa atakuja kujuta mbeleni
Hakuna tamaa hapo, yupo sawa nikosa kuanzisha biashara ndani ya biashara ya mtu mwingine. Ilitakiwa aangalie namna yakuongeza faida ya Boss wake, kwa kumshauri waongeze bidhaa hizo ndogo ndogo. Automatically na boss angefikiria kumuongeza bonas au mshahara kwa kuona kijana aliemuweka ni mbunifu. Kwa hali hii wa Tz tutaishia kuwa machinga tu.
 
Tena huyo kukuibia hawezi maana anajipambania mwenyewe pia
Nilitaka nimuambie kitu Kama hili.
Akimwambia asifanye hiyo biashara au akitaka wagawane hiyo faida ya mfanyakazi au achangie gharama za pango au umeme huyo kijana ataanza kumuibia bosi wake au ataacha kazi.
Akina mwingine hawezi kuwa Malini na muaminifu. Atahesabu hasara kila siku.
Tamaa mbaya.
 
Hakuna tamaa hapo, yupo sawa nikosa kuanzisha biashara ndani ya biashara ya mtu mwingine. Ilitakiwa aangalie namna yakuongeza faida ya Boss wake, kwa kumshauri waongeze bidhaa hizo ndogo ndogo. Automatically na boss angefikiria kumuongeza bonas au mshahara kwa kuona kijana aliemuweka na mbunifu na muaminifu.
Huo mshahara ni mdogo sana.
Mwingine angewza kumuibia bosi au kuacha kazi.
Angalau huyo kaomba hiyo nafasi ili abakie muaminifu kazini.
Hapo inatakiwa asifanye biashara ambayo inafanana bidhaa na mwenye duka.
Ikiwezekana kila anapoleta bidhaa zake mpya amjulishe mmiliki wa duka thamani na idadi yake.
Amuwekee kikomo Cha ceiling ya mtaji au ukubwa wa biashara yake huyo kijana. Ikifikia hapo wajadili partnership au aondoe au akubali iishiie kiwango hicho tu.
Amuwekee malengo ya kufikia biashara ya bosi wake. Mfano atakiwe kubuni bidhaa mpya za kufikia hayo malengo n.k.
 
Huo mshahara ni mdogo sana.
Mwingine angewza kumuibia bosi au kuacha kazi.
Angalau huyo kaomba hiyo nafasi ili abakie muaminifu kazini.
Hapo inatakiwa asifanye biashara ambayo inafanana bidhaa na mwenye duka.
Ikiwezekana kila anapoleta bidhaa zake mpya amjulishe mmiliki wa duka thamani na idadi yake.
Amuwekee kikomo Cha ceiling ya mtaji au ukubwa wa biashara yake huyo kijana. Ikifikia hapo wajadili partnership au aondoe au akubali iishiie kiwango hicho tu.
Amuwekee malengo ya kufikia biashara ya bosi wake. Mfano atakiwe kubuni bidhaa mpya za kufikia hayo malengo n.k.
Mindset za biashara nikua ukisharuhusu hicho kitu, basi kijana ataangalia biashara nyingine ambayo haipo dukani kwa boss wake ataongeza, mwisho wasiku atampoteza huyo kijana.

Kila siku tunasema wahindi wanapiga hatua kwenye biashara lkn hakuna muhindi anaweza kuruhusu uanzishe baishara ndani ya biashara yake. Kijana ilitakiwa aangalie namna yakuongeza faida ya Boss wake tu na boss akiona biashara inakua atamuongeza mshahara tu.

Mimi mahala napofanyakazi kama tukifanikiwa kuingiza faida nzuri kwa boss wetu, pindi unapo renew mkataba boss wetu anatupa bonas kulingana na performance ya mwaka huo. Kwahio Kila mtu hulazimika kufanya kazi Ili impact yake ionekane.

Mfano wakuta walipwa mil 1/2/3/4 kwa mwezi, lkn unapo renew mkataba wapewa bonas ambayo inazid accumulation ya mshahara wako wa mwaka mzima.

Tukubali kupokea mshahara tuliokubaliana, nakukuza biashara za waajiri wetu, na tukitaka kufanya biashara basi tuache kazi, tukaanzishe biashara zetu kuepuka mgongano wa maslah.
 
Mimi nazan
1:- Achangie gharama za uendeshaji wa biashara zako kwa 15_25% (TRA.KODI.UMEME. N.K ) Mshahara wake na posho zake ibakie hvyo hvyo

2. Ukate pato lake faid ya biashara yake kwa 20%

NB:- kama ulikuta biashara imefungwa na hayupo huo.sio.utaratbu ilipaswa akupe taarfa. Ukiona ana focus san na biashara yake m-pge chin ataharbu yako , au umuachishe
 
Mimi mahala napofanyakazi kama tukifanikiwa kuingiza faida nzuri kwa boss wetu, pindi unapo renew mkataba boss wetu anatupa bonas kulingana na performance ya mwaka huo. Kwahio Kila mtu hulazimika kufanya kazi Ili impact yake ionekane.
Watanzania weusi wenzetu wengi wagumu kufanya hiki kitu.
Anaona anakupa pesa yake ya bure wakati anakulipa mshahara. Hawajui motivation muhimu.
 
Mimi nadhani unakosea kwa options zote unazotaka kuchukua, hakuna hata moja imekaa poa.

Let her, wewe muache afanye kwa sababu inapunguza risks za yeye kuiba/kudokoa kwenye bidhaa zako, lakini pia unampa motisha wa kuendelea na kazi.
 
Back
Top Bottom