Nilimshirikisha mama yangu mafanikio yangu nikadhani amefurahi, baada ya muda kila nikiwasiliana naye ananiambia isijekuwa naenda kwa waganga

Nilimshirikisha mama yangu mafanikio yangu nikadhani amefurahi, baada ya muda kila nikiwasiliana naye ananiambia isijekuwa naenda kwa waganga

Ningeshangaa sana kama mama na ndg zako wengine wangeshangilia kama mazezeta ili hali zama hizi ndg wanatolewa kafara kama mbuzi
 
Ningeshangaa sana kama mama na ndg zako wengine wangeshangilia kama mazezeta ili hali zama hizi ndg wanatolewa kafara kama mbuzi
Maadamu mimi sio mtoa kafara nabebeshwa mzigo wa punda sina budi kujiondoa kwenye familia ambazo zinalipa wanafamilia wao ubaya
 
Weka mkeka tuone basi mkuu
Ndugu mambo ya hela ni sensitive sana sio ya kuanika hadharani, siwezi kuwavua nguo kampuni yangu pendwa ya betting, hata kama ni kuwatangaza nitatumia namna nyingine lakini sio kuanika hadharani
 
Mimi nikijana wa miaka 27 nilishinda betting kiasi kikubwa tu cha pesa lakini sikuwahi kumweleza mwanafamilia yeyote na wala hakuna anayefahamu, nikaamua kujenga nyumba kupitia zile pesa za betting kwahiyo nikawa na nyumba ya ghafla

Sikutaka kumshirikisha ndugu au mwanafamilia kwa haraka
Nikaanza kumshirikisha mama yangu mzazi nikajua atafurahi

Jambo la kushangaza akashtuka sana baada ya muda kidogo kila nikiongea nae ananambia kuna utajiri wa kafara isijekuwa nimejiunga nikadhani labda ameongea tu lakini kila mara anasema maeneno hayo hayo
Kwahiyo leo nagundua kuwa tayari ananiita mchawi

Kuna kaka yangu naye ni mlokole anasali kanisa la Gwajma kwa miaka yote na mwamini lakini huwezi kuamini siku anakuja kwangu alipoondoka alianza kunizungumzia habari za kafara

Naona jinsi gani familia yangu nitavunja nao uhusiano kwasababu ya kunipakazia mambo makubwa kiasi hiki
Inawezekanaje mama yako mzazi anathubutu kukutamkia maneno kama haya ni dhahiri nimezaliwa familia yenye laana ya mafanikio

Unathubutuje kumshutumu mtu kuwa ana mali za kafara wakati pesa kapata kupitia betting
Watu wengi wanasema kuzaliwa bongo ni nuksi kwakweli nimeona
Kaa chini ongea nao waonyeshe mkeka ulioshinda
 
Dah yaani kuweka kascreenshoot tujue kuwa mwenzetu sio mshirikina umeshindwa kabisa unaishia kusema eti siwezi kuianika kampuni yangu pendwa ya kubeti ? Hapana Sina Imani na wewe ,wewe sema tu ukweli mbona sisi wengi tuna Mali za ndagu na hatufichi Kaka ?
 
Asante sana mkuu, imebidi nionane na ile kampuni ya betting tumekaa chini tukaongea sana kwakweli wamesikitika sana wakanambia sina bahati ya mama, nimezaliwa familia mbaya

Nlikua nmeamini story, hadi nlivofika hapa ndio nikagundua.....nahitaji na chapati mbili.
 
Mpaka sasa sjaona mkeka wa muhindi. So kuna mawili

1. Story ni chai
2. Wewe ni mchawi kweli
Ndugu yangu unahangaikaje kuwathibitishia watu mali zako ni kuwaacha watapike wamalize, binadamu hata umfanyie wema kiasi gani bado atakusema
 
Mimi nikijana wa miaka 27 nilishinda betting kiasi kikubwa tu cha pesa lakini sikuwahi kumweleza mwanafamilia yeyote na wala hakuna anayefahamu, nikaamua kujenga nyumba kupitia zile pesa za betting kwahiyo nikawa na nyumba ya ghafla

Sikutaka kumshirikisha ndugu au mwanafamilia kwa haraka
Nikaanza kumshirikisha mama yangu mzazi nikajua atafurahi

Jambo la kushangaza akashtuka sana baada ya muda kidogo kila nikiongea nae ananambia kuna utajiri wa kafara isijekuwa nimejiunga nikadhani labda ameongea tu lakini kila mara anasema maeneno hayo hayo
Kwahiyo leo nagundua kuwa tayari ananiita mchawi

Kuna kaka yangu naye ni mlokole anasali kanisa la Gwajma kwa miaka yote na mwamini lakini huwezi kuamini siku anakuja kwangu alipoondoka alianza kunizungumzia habari za kafara

Naona jinsi gani familia yangu nitavunja nao uhusiano kwasababu ya kunipakazia mambo makubwa kiasi hiki
Inawezekanaje mama yako mzazi anathubutu kukutamkia maneno kama haya ni dhahiri nimezaliwa familia yenye laana ya mafanikio

Unathubutuje kumshutumu mtu kuwa ana mali za kafara wakati pesa kapata kupitia betting
Watu wengi wanasema kuzaliwa bongo ni nuksi kwakweli nimeona
Naona hapo ni kuwaambia tu ukweli hela umepata wapi? Umeficha wao watajuaje?

Kwa uzoefu wa wazazi wako na ndugu zako kwa mafanikio ya gafla wamefikiria hivyo, hawakuwaza betting.
 
Shukuru amehisi ni mchawi kuliko angehisi umesaliti kiumeni.

Muhimu: Betting ni kamari kama kamari zingine.
 
Shukuru amehisi ni mchawi kuliko angehisi umesaliti kiumeni.

Muhimu: Betting ni kamari kama kamari zingine.
Alitakiwa atulie nimweleze sio kuanza kunitusi mshirikina wakati hana uhakika, je ningekuwa mwizi nakashaniita mchawi nayo imekaaje, maisha ya bongo fanikiwa ndio utajua
 
Alitakiwa atulie nimweleze sio kuanza kunitusi mshirikina wakati hana uhakika, je ningekuwa mwizi nakashaniita mchawi nayo imekaaje, maisha ya bongo fanikiwa ndio utajua
Kuanza kufikiria kwamba mama yako hapendi ufanikiwe na ni mbaya kwako basi ujue akili yako haina akili.

Kwa umri uliokiwa nao unahisi mama yako atakuwa anaelewa hayo maswala ya betting au unakaza fuvu tu na kujiona tayari umefanikiwa?
 
Kuanza kufikiria kwamba mama yako hapendi ufanikiwe na ni mbaya kwako basi ujue akili yako haina akili.

Kwa umri uliokiwa nao unahisi mama yako atakuwa anaelewa hayo maswala ya betting au unakaza fuvu tu na kujiona tayari umefanikiwa?
Amepata wapi nguvu ya kuniita mchawi wakati mimi ananijua tangu ananizaa, vilevile alikuwa ananidharau kipindi sina akaona mm ni mbwa ndio maana hata kufanikiwa kwangu anathubutu kunitusi na kukataa mafanikio yangu kanakwamba mimi ni mbwa nimewezaje
 
Unapomuambia mtu kuwa una mradi basi jitahidi pia kumueleza chanzo cha fedha zako.

Haiwezekani kijana amemaliza tu chuo, alafu mwezi unaofata una nyumba tayari na gari la kutembelea.

Mzazi atakayefurahia bila ya kujua chanzo cha mapato yako, hakupendi. Na pengine wazazi wetu wa kiafrika mawazo yao yataenda huko kwenye ulozi.

Hivyo, ungepaswa kumuambia mama nilishinda mkeka. Nikapata kiasi kadhaa na nikaamua kujenga nyumba hii. Angekuwa na amani na chanzo cha mapato yako.
Ni mchoyo kupindukia alidhani watamuomba ndio maana anafanya mambo yake kimyakimya.
 
Back
Top Bottom