Nilimtelekeza mke wangu, nimerudi nimekuta rafiki yangu kamuoa

Nilimtelekeza mke wangu, nimerudi nimekuta rafiki yangu kamuoa

Achana nao wajinga hao yatawakuta makubwa pumbavu zao
 
Nakupa pole kwa yaliyokukuta na pia nakupa hongera kwa jinsi ulivyochukua maamuzi magumu.
Kwa nionavyo mimi wewe utakuwa na 83% ya ushindi na wao wana 17%. Hivyo usihofu ndugu, hizo ni chsngamoto za maisha.
 
Usimuamini mwanamke hata kama unalala nae kila siku

Muamini mama yako pekee ndie anauchungu na wewe

Kuhusu nyumba angalia asije akakugeuza kichaa maana tabia yake kama mwanga
 
Pole sana mkuu lakini mimi binafsi sioni kosa lako mwanamke hakuwa akitaka usafiri ili utafute na ukikaa home anakupa maneno ya shombo...ila miaka 5 mzazi bila kutuma hata jero? Huo nao ni ujasiri wa kipu*mbav.
iombe mahaka ivunje ndoa yako ili jamaa awe huru lakini iruhusu watoto wako uwachukue uishi nao maana wameshakuwa wakubwa mengine sahau tu
 
Pole hakika ni pito gumu! kuolewa sio tatizo tatizo ni wao kubadilisha hati! kama aliamua kuolewa tena mumewe akamtafutie nyumba waishi..
Utashinda iyo kesi ila mimi nadhan kwakuwa ushajenga nyumba nyingine! hiyo utaomba mahakamani iuzwe pesa mgawane nusu kwa nusu! then umpe talaka na kuchukua watoto wako ishi nao ktk nyumba unayoishi sasa! nao watajua pa kwenda na mumewe!
 
bobby freetown

Umekosea kwenye kumtelekeza mkeo kwa miaka mitano. Ila kuna kitu nataka nijiridhishe kabla sijahitimisha hilo kosa la kutelekeza. Umesema jamaa kamzalisha mkeo mtoto na pia mkeo ana mimba ya huyo jamaa. Huyo mtoto ana umri gani? Ulijaribu kuchunguza kwamba walifunga ndoa mwaka gani? Nikipata hizo data, zaweza nionyesha kwamba huyo rafiki yako alikuwa akitoka na mke wako hata kabla hujatimkia Angola. Ikiwa ni hivyo, hata kama ungeondoka week moja tu, ungekuta same story ila katika mode tofauti. Hivyo lawama zote ni za huyo mwanamke na wewe sioni bega la kukubebesha lawama.
 
Last edited by a moderator:
dah kumbe ni hivi


kuna dada mmoja yeye mumewe alijenga nyumba ila hati ya hiyo nyumba ipo WAZO aliweka JINA LA KAMPUNI yake

makusudi mazima sasa alimfumania mkewe na mwanaume mwingine alichofanya kaenda mahakamani kudai talaka kesi

ilisikilizwa mwanaume alimwachia mkewe samani zote za ndani kwakuwa walipanga apartment mikocheni, rent

ilivyoisha mwanaume akachukua nguo zake tu na kusepa akamwacha mkewe na watoto 2 , kwa kuwa rent iliisha mkewe

alimtaarifu kuhusu rent mumewe akamjibu mii nataka talaka siwezi kuishi na wewe na hao watoto chukua na vitu vyote

chukua , sasa dada amechanganyikiwa watoto walizoea kusoma Genesis yeye hana fedha ya kuwasomesha huko kifupi

ameshapewa talaka sasa where is justice in such a circumstance if you won't mind nimeona umejibu murua na subsection nini dah

Basically, TALAKA ikishakuwa granted by court, hufuatia IMPACT kuu 3:

(a) Kugawana mali za ndoa (distribution of matrimonial properties). Hapa mali zinazohusika ni zile tu zilizopatikana/zilizochumwa wakati wa uhai wa ndoa (jointly acquired during the marriage). Na hapa ndipo huibuka swali la je "yupi anapata kiasi gani?" (katika huo mgawanyo wa mali), hili tuliache kwanza.

(b) Custody of the Children. Uangalizi na malezi ya watoto. Generally, Sheria ya Ndoa inataka mtoto aged under 7 years, aishi kwa mama. Notably however, katika ku-grant custody ya mtoto, mahakama huzingatia sana maslahi bora ya mtoto (the best interest of the child). Kwamba ni upande upi mtoto akiishi ataenjoy na kupata haki zake zote za msingi including malezi bora, elimu, n.k. Hili limekuwa sensitively reflected kwenye Sheria ya Mtoto ya 2009.

(c) Maintenance of the children. Matunzo ya mtoto. Sheria ya ndoa inaeleza clearly kabsa kwamba jukumu la matunzo ya mtoto/watoto ni la baba (biological father. Matunzo hayo ni including basic needs kama chakula, mavazi, pia elimu, afya, n.k. Note: suala la matunzo ya mtoto liko pale pale hata kama hamkufunga ndoa, hata kama umemzalisha tu. Nadhani unakumbuka mahakama ilivyoamua ile kesi ya HOUSE GIRL Vs IGP MAHITA, juu ya matunzo ya mtoto, mpaka vipimo vya DNA vilitumika na Mahita akawa bound!! However, mama anaweza saidia matunzo ya mtoto endapo baba hajiwezi kabsa kiuchumi.

Kwaiyo, kama kuna mtoto/watoto na mali za ndoa, mahakama inatakiwa i-compromise izo inshu 3 hapo juu (a to c) in alongside with issuance of TALAKA.

So kuhusu case ya huyo mdada, kuna possible legal channels mbili: (1) Umesema walikuwa wanaishi nyumba ya kupanga, ila kuna nyumba ilijengwa na ikawa registered with Hati Miliki ya kampuni ya mwanaume. Japo hujaeleza kama nyumba hiyo ilijengwa wakati wa ndoa ama kabla ya ndoa. Now, kama ilijengwa wakati wa ndoa, possibly anaweza akapata haki yake ktk hilo, kwa ku-determine mchango wake wa hali au fedha au huduma kwa mume. Arudi mahakamani ku-establish hiyo issue ya nyumba in terms of mgawanyo wa mali za ndoa, note: kama tu ilijengwa wakati wa ndoa!
(2) Aende mahakamani kufungua kesi ya "matunzo ya watoto" dhidi ya baba wa watoto.

WITH EMPHASIS: ni jukumu la baba kuprovide full matunzo kwa watoto wake, huwezi kulikwepa hili kwa mlango wa sheria. Ila kibongo-bongo, akina mama wengi wanaachiwa watoto na kuhangaika nao pekeyao. This is due to the fact that watanzania wengi bado hatupo courageous (not aggressive) kudai haki zetu throuh legal settings zilizopo. Pia our systems for dispensation of justice bado zipo ineffective and very corrupt! So ili kuepuka legal complications plus kupoteza muda na pesa kufuatilia kesi, akina mama wengi huamua kupotezea tu na kukomaa kulea/kutunza watoto pekeyao.

Mkuu, I hope maelezo yangu yamekidhi hoja yako kwa kiasi fulani, japo mwanga wa kuanzia. Naamini wataalamu zaidi wa sheria watatoa michango yao pia. Also, my sincere apologies if my writing irritates, maana nimeandika kwa simu!

-Kaveli-
 
Ulichokosea hapa ni kutokuwa na mawasiliano na wife wako basi. Lakini kwa upande wake wife wako alichokosea ni kubadili hati ya nyumba na kuandika jina la mpenzi wake mpya. Mimi nafikiri mkeo alidhani utakuwa umefariki ndio maana akaamua kuolewa na mtu mwingine. Yeye pia ni binadamu na anahisia zake kamili, so katika hili la kuolewa mimi naoana hajafanya kosa lolote.

Naomba nikuulize swali; hivi mkuu unataka kuniambia wewe ulipoondoka miaka yote hiyo, huko ulikokuwa hukuwahi kabisa kuchepuka na mademu wa huko Angola au huko kipindi chote hicho haukuwa na mpenzi??
 
Kosa ulilofanya ni kumkimbia mkeo, sasa mkeo miaka yote hiyo akae kukusubiria wewe na wakati hajui lini warudi?

Hizo mali samehe, anza upya.
 
Zingatia alichoshauri kaveli kuna mwanga ndani ya handaki lenye giza
 
Funzo ; wanawake ni rafiki zetu wa muhimu ukiwa nao, ukitoka au akitoka aweza kuwa adui yako mkubwa sana.

Haki yako utapata mkuu, pigania hadi tone la mwisho.
 
Back
Top Bottom