Nilimtelekeza mke wangu, nimerudi nimekuta rafiki yangu kamuoa

Nilimtelekeza mke wangu, nimerudi nimekuta rafiki yangu kamuoa

Kila kitu kinatokea kwa sababu labda kutuandaa kwa level nyingine katika maisha au kutuweka karibu na Mungu Zaidi. Katika matatizo ndo unajua urafiki wa kweli na urafiki wa magumashi, katika biblia ukimtazama Ayubu kwani yeye alikimbiwa na mke. Mimi binafsi uliyoyafanya uliyafanya hakuna sababu ya kuendela kudhani kama ulikosea au hukukosea kwani yameishatokea na maisha hayarudi nyuma. Mimi sijajua umetulia kiasi gani katika maisha hapa namaanisha kujiimalisha kiuchumi. Kwani naona kama utadeal na mambo mengi kwa wakati mmoja kitu ambacho kama hujajiimalisha kiuchumi uchumi unaweza kuteteleka tena. Mimi binafsi sipendagi kudeal na watu sana napenda kuangalia mbele, kama unaweza jenga nyingine achana nao angalia mbele. Samehe yaliyopita kama nyumba utajenga nyingine kudeal na watu wa namna hio naona utapoteza muda mrefu sana, halafu hao watu ni jeuri sana. Cha msingi ukiweza samehe angalia mbele, Mungu atakupa maisha mengine mapya kabisa. Hayo maisha yanakujengea historia ya kusimulia, watu wanaopitia kwenye shida kama hizo wengi wanakuja kufanikiwa sana katika maisha halafu wanakua watu wa kutufundisha wengine. Hivyo usiwe na hofu Mungu wako hajakutupa, ukitaka maisha ya ushuhuda achana nao angalia mbele.

Angalia ayubu mwisho wake mke wake alirudi mwenyewe kwa aibu kubwa, maana ayubu mpya sio ayubu wa kale. Mungu alimuinua mpaka mke wake akasikia kua ayubu mambo yake yamekaa kwenye njia.


Salam zenu wanaume wenzangu,

Mwaka 2006 nilipata matatizo kazini, nikafukuzwa kazi tulishikwa red handed mim ina mwenzangu tukiuza mafuta ya kampuni, nilikua nafanya kazi kwenye kampuni ya mafuta Kurasini.

Kwa kweli nilikua na hela sana kutokana na kitengo nilichokuwepo, mabosi walinitumia mimi kuiba mafuta ya kampuni na mwisho tunagawana.Bahati mbaya mabosi waligombana mmoja akaamua kutuchoma, dili likabumbuluka na jumba bovu likaniangukia mimi ukawa ndio mwisho wangu hapo.

Siwezi kuwaficha wana Jf, nilikua nimeoa mwanamke mwenye matumizi makubwa sana, alipenda kula na kuishi vizuri na kuvaa kila fashion iliyoingia mjini alitaka awe nayo, na kwa kuwa ni mzuri ajabu nililazimika kutoa gharama na huduma hizo kwa kuwa hela nilikua nayo.

Sasa nilipofukuzwa kazi, alinibadilikia sana ndani, nyumba ikawa kaa la moto, niliambiwa maneno mabaya sana, hata hela ya kula ilianza kunisumbua, sikua nimesave wala kuweka mradi wowote wakati nina hela zaidi ya kujenga nyumba tuliyokua tunaishi,Marafiki wote tuliokua tukinywa bia pamoja walianza kunikimbia baada ya kuona nimekua mtu aa mizinga.

Nikapata wazo la kwenda Angola migodini, kuna mshikaji alinipa dili hilo, alikua huko siku nyingi, ila alisema ni kugumu sana, sikua na choice nikaamua kwenda, tulisafiri na basi kupitia Zambia.

Kwa kifupi nilimtoroka mke wangu na watoto wawili, nilijua wazi asingekubali mimi kwenda Angola, hata humu TZ alikua anakataa nisiende mikoani kutafuta, alikkua anadhani somehow muujiza utatokea hali ya pesa irudi tena bila fighting na hapo hapo akaendelea kunilaum sifanyi kitu kwamba nimekaa tu, hiyo ndo sababu niliamua kumtoroka na kwenda Angola kutafuta maisha.

Nimekaa Angola tangu 2009-2014 , tangu 2006 hadi 2009 nilikua bench tu.Nikiwa Angola nilisota kama miezi 8 hivi baadae nikawa napata ajira za muda katika makampuni yenye tenda kwenye migodi kama ya drilling na construction na kadhalika.

Sikutaka mawasiliano yoyote na nyumbani, si mama yangu, mke wala ndugu yoyote, walikua wamenizomea na kunicheka sana nilipokua juu ya mawe, hivyo niliamua kutafuta kimya kimya hadi nifanikiwe ndipo nirudi nyumbani.

2014 July, nikarudi Dar kwa Mara ya kwanza tangu 2009, sikurudi nikiwa tajiri, Bali nilirudi na msingi wa kuanza upya maisha, nilikusanya kiasi cha kutosha kuanza biashara na kujitegemea kiuchumi.

Surprisingly, nimekuta mke wangu ana ujauzito wa pili (ameshajifungua kwa sasa) tayari akiwa na mtoto mwingine mkubwa wa miaka 3, mbaya zaidi nikakuta rafiki yangu wa karibu anaishi na mke wangu kwangu kinyumba na ndie baba wa hiyo hiyo mimba na watoto wanadai wameshaoana kisheria kwa mkuu wa wilaya wakati hakuna talaka yoyote iliyotolewa na Mahakama yoyote ile hapa Tanzania kuvunja ndoa yetu ya awali.

Maana yeye ana claim hiyo ndio basis ya kuchukua hiyo nyumba yangu na kujimilikisha na sasa yanasomeka majina ya huyu rafiki yangu na yeye na sio majina ya watoto.

Sasa tuna kesi Mahakamani niliyoifungua mimi, nikiiomba Mahakama kubatilisha hiyo hati, iliyofanyiwa transfer kwa udanganyifu, pili mahakama itamke ndoa hiyo ni batili maana ndio iliyozaa udanganyifu wa hati.

Pia ndoa hiyo imefungwa huku kukiwa na ndoa nyingine halali ambayo wahusika waliidanganya ofisi ya mkuu wa Wilaya.
Mwisho nimeomba custody ya watoto wangu nikae nao mwenyewe maana anawakatalia pia

Wana Jf sio kwamba namuhitaji huyu mwanamke tena, bali nahitaji hiyo nyumba iwe ni mali ya watoto wangu kwa sasa imebinafsishwa na hawa wapenzi wawili.

Tangu nimerudi nimejenga nyumba yangu mivumoni tegeta ambapo nakaa, nafanya biashara zangu ni mfanyabiashara wa kipato cha kati, na napati kazi nyingi Angola ambapo huwa nakwenda Mara kwa Mara Kwa shughuli zangu, hivyo naendelea vizuri sana.

- Kuna pahala nilikosea katika haya yote?

- Naweza kubeba sehemu ya lawama kwa kitendo alichofanya huyu mama?

- Je, naweza kushinda hii kesi kwa mtazamo wenu?
 
......that's deep, welldone!

Cc; Dark City, BAK, King'asti, Asprin


Huyu baba hana kosa lolote zaidi ya kushindwa kutumia vizuri wakati alipokuwa na fweza. Na pia ni upuuzi kumwendekeza mtu eti kwa vile no mzuri au unampenda sana.

Kwa sasa aendelee na kesi na hilo kosa la kufoji linaweza kuwakutanisha na Mramba!
 
Kosa ni lako mzee
1. Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo
2. Hukumsirikisha kabisa katika mkakati wako
3. Hukujali wataishi vipi pamoja na wototo
4. Umemtekeleza kwa miaka mingi bila kujulikana uko wapi/hai
Wakulaumiwa ni wewe na si mwingine na ulichokifanya ni utoto sana
Usimalaumu rafiki yako kwani wewe ukisusa wenzako wala na vilevile amekulelea
Ningekuwa mimi ni wewe ningeachana na habari hiyo na kuanza upya
 
yani mkeo ni booonge la fwala
simlaumu kuolewa tena,hizo genye zake!
ufwala wake ni kunyang'anya watoto nyumba na kumpa basher wake!
mxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxiou!!
 
Mkuu lawama zote kwako ungempeleka hata kwenu tu yule mwanamke kabla hujasepa
 
Mkuu ulikosea kuchagua mke ila dah kupitia mkasa wako nimepata kujifunza wakati wa shida hakuna mtu atakaekupenda wala kukuthamini.
 
Mkuu ulikosea kuchagua mke ila dah kupitia mkasa wako nimepata kujifunza wakati wa shida hakuna mtu atakaekupenda wala kukuthamini.
 
ulikosea kukimbia bilahati au bila kumjulisha mkeo...pia labda hujakosea ila ulikosea kuchagua mke uliangalia uzuri sana bila kujali anapenda mali sana....
 
Jipe moyo, hiyo nyumba ni mali yako. Ila, kisheria mke mke ulimtelekeza maana sheria inasema ni miezi 6 tu. Kama alimpata mme ikiwa ni zaidi ya miezi 6 ukiwa umemuacha basi hakutenda kosa. Shughulika na nyumba ambayo ni mali yako, watoto pia ni mali yako..
 
Jamaa amemsitiri mkeo uliemtelekeza na watoto.

Ulitaka wawe machokoraa?
kwa makabila mengine hao watoto ni wako pia na huyo mke. pigania nyumba ya watoto kama kwenu hakuna kitanda hakizai haramu.
 
Pole sana mkuu, pia Hongera kwa kupambana na maisha, Kuitwa mwnaume si kazi dogo,
 
Back
Top Bottom