Nilishtuka nilipomwona mhudumu wa mortuary akihifadhi embe kwenye jokofu lenye maiti Hospitali ya Temeke

alikuwa mwafrika au mzungu??sitegemei mtu mweus anaweza kufanya hivyo
 
Mkuu mbona hushangai madaktari wanavyofanyia dissection miili na viungo vya watu waliokufa wanapokuwa kwenye mafunzo yao na wale wanaofanyia uchunguzi miili ya marehemu, au ukiwakuta utatoka nduki....hizo ni taaluma za watu wala zisikusumbue..
 
Kweli wamezoea maana hata wale wanaouza samaki wabichi nilishangaa jamaa aliweka soda haijafungwa kizibo alibakiza akaitoa kwenye jokofu lenye uvundo wa samaki akainywa fresh tu!! Ukizoea unaona kawaida.
[emoji2][emoji2][emoji2].... Hii Mimi pia nlushafanya.. ila iwe imefungwa isiwe wazi itanuka shombo ya samaki
 
Kuna jamaa yeye alikua hospitali ya Amana miaka mingi huko nyuma alikua yeye anawaingilia marehemu wazuri wazuri walioletwa mortuary huku akiwananga kwamba mnaringaga sana nyie etc etc ila jamaa alikujaga kupata ngoma ndo ikawa mwisho wa habari yake...
 

Hakuna ukatili hapo mzee ni swala la mazoea na kazi . Wahudumu wa mortuary ni vingi wanafanya vya ajabu mno.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Aisee.
 
Unashangaa maiti hiyo, mie niliona mga maji akitolewa ziwani kwa kutumia kokoro akiwa hana ngozi pamoja na macho. Watu wakawa wanasema macho yake yameliwa na samaki, kumbuka kwenye kokoro kulikiwa na samaki wengi cha ajabu nilicho kiona mimi ni namna watu walivyo kimbilia samaki na kuuacha mwili.
 
Duh, kweli hii mkuu?
 
Kisa cha miaka miwili iliyopita ndiyo umekumbuka leo??

Na hiyo siku mlipoingia mortuary ndiyo siku maiti zilipojaa sana !!!!
Huenda labda walijumuishwa na wao maiti watarajiwa.
 
Hayo majamaa sio poa.

Nakumbuka tulipeleka maiti 3 mortuary zilitoka sehemu sehemu ya ujambazi(kupigwa risasi),kufika pale tukawa tumashusha kwa staha kidogo,maana vichwa vilikuwa vimetoboka.
Jamaa moja likaja na ile trailer ya kubebea maiti,likaivuta maiti kutoka kwenye gari na kuiachia (kapaaa)kwenye lile trailer ilarusha ubongo na damu ukatua ktk suruali yangu[emoji31][emoji31][emoji31],likacheka sana,huku mimi nikiwa nimeduwaa nisijue nafanyaje pale,maana groves zote mikononi zilikuwa zimejaa damu.likaburuza ile trailer mpaka ndani likatoka na dawa na kunawia,aisee niliirowanisha nguo yote wala sikujali.

Maiti anatisha wadau[emoji16][emoji16][emoji16]
 
Nilikuwa na project fulani ya Biomedical kwa kushirikiana na Hospitali ya Mayo Clinic kule Rochester, MN. Hospitali ile iko vizuri sana kwa utafiti wa tiba; walikuwa wanataka kujua sehemu nzuri za kuweka sensor kwenye ankle na kwenye knee ili kutafiti namna ya kutibu watu wenye matatizo ya arthritis sehemu hizo. Kuna numerical models na dummies ambazo huwa tunatumia kwenye research, sasa siku hiyo wakatuonyesha mwili halisi. Jamaa alifungua freezer iliyokuwa na maiti, ila mguu wa maiti ile ulikuwa umeshakatwa kama buchani ili kutenganisha fupa la goti na kisigino. Nilitoka kule na kichefuchefu sikula nyama kwa muda mrefu sana; kwa sababu fupa lilikuwa linaonyesha nyama ya mtu utadhani ya ngombe tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…