Nilivyoingiza 17.6M ndani ya mwaka mmoja na nusu, kwa biashara ya Mgahawa kwa mtaji wa kawaida kabisa

Hata Mimi siwezi kukushauri uache kubeti !! Mimi nimekua hapo dutwa kwa muda mrefu ! Kribia hela yangu ya kuishi hapo Kama kula na kulipia chumba ilikua unatokana na beting
Dutwa sikuhizi hakuna watu wengi.
 
Hongera sana mkuu ,biashara ni upepo mi kuna kipindi nilifungua biashara ya mgahawa nikiangalia location iko poa ila hela hamna ,duh mwisho wa siku nikaacha.

Sasa miaka ya karibuni kuna biashara moja halali upepo uliniendea ndani ya miezi miwili nilipata mil 16 ,nikaenda kutoa sadaka ya shukrani mil 1.

Baada ya hapo naendelea ila upepo sio kama wa mwanzo haipipi kabisa ,mara upepo unakuja tena gafla ila sifikii hata nusu ya niliyooteaga. But pia sometimes nahisi mtu ukianza kupata hela unaweza kupunguza ufanisi kwenye kazi na faida kushuka au unawaza mambo mengine makubwa kwa wakati mmoja hadi unafeli kwenye kile ulichofanikiwa.
 
That ending [emoji4], as they say : Profit is made when you buy, not when you sale.
 
Dah,nilikuwepo Dutwa mgodi ulivyolipuka ilikuwa Ni mwendo wa Magambuti. Nimekaa namba moja na like nyomi la watu. Mishe zangu hasa nilikuwa nafanyia namba mbili Ila Pesa ilivyopotea nikaondoka.
Kule wakati wa mvua ni mwendo wa gambuti tu hata kama hutaki maana ardhi ni ya ufinyanzi, namba mbili ilikuwa na mzunguko wa pesa ila nilivyokosa nafasi nikaamua kubaki namba moja tu.

Niliuza sana kwasababu watu walikuwa wanakwepa kula namba mbili kutokana na mazingira machafu, wanakuja mgahawani kwangu.

Kwasasa uko wapi ndugu?
 
Kuna muda unaanzisha kitu fulani ukiwa na matarajio ya kawaida ila faida unayopata inakuacha mdomo wazi, mimi sikuwahi kujua kama watu wenye migahawa wanapata faida na nilikuwa naidharau sana hiyo biashara.
 
Kuna muda unaanzisha kitu fulani ukiwa na matarajio ya kawaida ila faida unayopata inakuacha mdomo wazi, mimi sikuwahi kujua kama watu wenye migahawa wanapata faida na nilikuwa naidharau sana hiyo biashara.
Hongera Kwa uthubutu, maisha muda mwingi yanataka watu watendaji kitu ambacho watu wengi hatuna.
 
To be honest nilitulia kwanza hii miezi miwili, ila kutokana na uzoefu nilioupata kwenye biashara ya Resturant tayari nimeshalipia eneo fulani potential sana (karibu na stend) huko IGOMBE na natarajia kuanza mwezi wa saba.
Hongera mkuu
Go ahead
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…